Monday, June 29, 2009

Kamati ya uchaguzi Iran, rais,Mahmoud Ahmadinejad,badao ni mshindi.

Chaji za simu kuwa za aina moja kiviwango. Brussels, Ubeligiji - 29/06/09. Kampuni zilazo shughulikia, utengenezaji wa simu, zimekubaliana kwa pamoja kuanza kutengeneza chaji za aina moja, kwa ajili ya matumizi ya simu zote. Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya ofisi inayaoshughulikia, maswala ya mawasialiano katika nchi za jumuia ya Ulaya, zimesema ya kuwa kampuni za Nokia ,Motorola, Sumsung, Sony Ericsson., Apple,na LG, ambazo zina tengeneza simu na kutukiwa na wakazi wa Ulaya, zimekubaliana na kamati ya mawasiliano kwa kukubaliana kutengeneza chaji zitakazo tumika kwa kiwango kimoja. Kwa mujibu, wa habari hizi , kuanza kutumika kwa chaji hizi mpya, kuaanza mapema mwakani. Picha hpo juu, zimnaonekana, aina tofauti za chaji , ambazo hutumika kwa simu tofauti,na huwa zinaleta matatizo kwa watumiaji wa simu katika nchi Ulaya. Millionea ahukumiwa kwenda jera miaka 13 nchini Urussi. Moscow, Urussi, -29/06/09. Mahakama mjini Moscow, imemuhukumu, milionea Boris Berezovsky kwenda jela miaka 13, baada ya kukutwa na hatia ya kulaghai kwa kujipatia kiasi cha $million kutoka kwa kampuni ya Avtovaz. Boris Berezovsky,alihukumiwa, wakati yeyemwenyewe hakuwepo mahakamani. Mtuhumiwa huyo, Boris Berezovsky, anaishi ukimbizini nchi Uingereza. Picha hapo juu, anaonekana, Boris Berezovsky,akiingia ndani ya gari, ambapo kuonekana kwake huwa nadra saana.

Kamati ya uchaguzi Iran,rais, Mahmoud Ahmadinejad bado ni mshindi.
Tehran, Iran - 29/06/09. Kamati inayosimamia uchaguzi nchini Iran, imetoa matokeo ya kura zilizo hesabiwa upya na kusema ya kuwa rais, Mahmoud Ahmadinejad, mchaguliwa, ameshinda kwa kura nyingi na kusisitiza ya kuwa hata kura ambazo zimehesabiwa hivi sasa bado zina mpa kura nyingi rais.
Kura hizo za asilimia kumi,ambazo ndizo zilizodaiwa kuwa hazikuhesibiwa na kuleta utata.
Hata hivyo, wapinza ambao walikuwa wanagombea kiti hicho cha urais, waligomea uchaguzi kwa kudai ya kuwa kulikuwa na matatizo ya kura katika mahesabu yake.
Picha hapo juu, anaonekna rais, wa Iran, Mohmoud Ahmadinejed, akiongea katika moja ya mikutana , mara baada ya kutangazwa matokeao ya uchaguzi na kumpa ushindi mkubwa.
Picha ya pili wanaonekana, baadhi ya watu wakiandamana kupinga matokeo ya uchaguzi, kwa madai ya kuwa kura zao hazikuhesibiwa.
Rais aomba ukimbizi,baada ya mapinduzi.
Honduras,Tegucigalpa - 29/06/09.Rais mpya aliyeapishwa nchini Honduras, Roberto Micheletti, kuchukua nafasi ya rais, Manuel Zelaya, ambaye yupo ukimbizini Kosta Rica.
Kufuatiwa kupinduliwa kwa rais, Emanuel Zelaya, baada ya rais huyo, kukataa kumrudisha kazini amir jeshi mkuu, ambaye alimfukuza kazi.
Kupinduliwa kwa, rais wa Honduras, Emanuel Zelaya, kumelaniwa na umoja wa mataifa.
Picha hapo juu, anaonekana, rais Emanuel Zeyala, ambaye yupo ukimbizini Kosta Rica.
Picha ya pili, anonekana, rais mpya wa Homduras, Micheletti, akiapishwa kuwa rais wa Honduras.
Picha ya tatu,kinaonekana , kifaru cha jeshi kikiwa mbele ya ikulu,kulinda serikali mpya ya rais, Robert Michelitti.
Aliyetikisa wawekezaji kutumikia kifungo miaka 150.
New York, Amerika - 29/06/09. Mahakama ya jijini, New York , imemuhukumu miaka 150 kwenda jela,Bernard Madoff,aliyekuwa mwenyekitia wa Nasdaq soko la wawekezaji na wabadishaji lililopo jijini New York.
Hukumu hiyo, ilitolewa na jaji Danny Chin, baada ya Bernadr Madoff, kukili kosa lake, la kuwatapeli mamia ya wawekezaji, wakiwepo watu mashuhuri kutoka ,Hollywood, wastaafu,na wafanya biashara wengine.
Kutolewa kwa hukumu hiyo, kunaaminika kutajaribu kupunguza jazba au machungu waliokuwa nayo wale wote waliotapeliwa na Bernard Madoff.
Pichani hapo juu, anaonekna Bernard Madoff, akielekea mahakamani ,huku paparazzi wakiwa kazini kupata picha za kumbukumbu.

Friday, June 26, 2009

Mfalme wa Muziki wa Pop atutoka,MUNGU BABA TUNAKUOMBA UILAZE ROHO YA MICHAEL JACKSON PEPON.AMINA.

Mfalme wa Muziki wa Pop atutoka,MUNGU BABA TUNAKUOMBA UILAZE ROHO YA MICHAEL JACKSON PEPON.AMINA.

Picha ya familia ya Mzee Joseph Jaskson, akiwa na watoto wake, Jackon Five, wa kwanza kushoto ni Michael Jackson, ambaye alikuwa ndiye nyota katika kundi zima la musiki wa Jackson 5.

Michael Jackson, alikuwa na umri wa miaka 50.

Los Angeles, Amerika - 26/06/09.Wapenzi wa Muziki Duniani twapigwa na wingu zito.
Picha zilizopo hapo juu, zineleza ni jinsi gani, marehemu Michael Jackson,alivyo pendwa kutokana ma kubarikiwa kipaji na Mungu.
Mzee Joseph Jackson, baba, ya Michael Jackson, alikuwa anampenda mwanae Michael ,kwa hali na mali, hapo anaonekana kwenye picha ya tano, akiwa ameshikilia moja ya CD(Album) ambayo ina picha ya Michael Jackson na ndani ya CD hiyo kuna nyimbo za Michael jackson.
Hamas yasema taifa la Israel hapana.
Damascus, Syria 26/06/09.Kiongozi wa Hamas,Khaled Mashaal, amesema Hamas, haitalitambua taifa la Israel.
Kiongozi huyo wa Hamas, Khaled Mashaal, aliyasema haya, siku ya Alkhamisi, mbele ya wanachama na wadau katika mkutano wa Hamas nchini Syria, ambapo kunawanachama na wadau wengi wa Hamas.
Hata hivyo, kiongozi huyo alikubaliana na mpango wa kuwa na mataifa mawili, ikiwa kutazingzatiwa makubaliano ya mwaka 1967 na Jerusalem mji mkuu.
Picha hpo juu, anaonekana, kiongozi wa Hamas, Khaled Mashaal, akihutubia mamia wanachama wa Hamas siku ya Alkhamis.
Serikali ya Somali kupata msaada kutoka Amerika.
Washington, Amerika - 26/06/09.Serikali ya Somalia ina karibia kupata msaada wa kijeshi kutoka serikali ya Amerika, ili kukabiliana na makundi yanayo pingana na serikali.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana,kutoka serikali ya Amerika,zina sema ya kuwa ipo haja ya kuisaidia serikali ya Somali, inyo ongozwa na Shariff Shabab.
Ili kukabiliana na hali ya hatari iliyopo nchi Somali, hasa Mogadishu, serikali ya Somalia, imetangaza hali ya hatari siku ya jumatatu katika jiji hilo.
Picha hpo juu, anaonekana, mmoja wa wapiganaji wa kundi la Al Shabab, akishambulia moja ya mitaa mjini Mogadishu.
Uturuki ipo karibu kuanza mazungumzo na muungano wa Ulaya.
Brussels, Ubeligiji - 26/06/09. Waziri mkuu wa Uturuki,Recep Tayyip Erdogan, amesema ya kuwa nchi yake, inampango wa kuanza upya mazungunzo ya kujiunga na muungano wa Ulaya.
Waziri, Recep Tayyip Erdogan, aliyasema haya, wakati alipo kuwa nchini Ubelingiji kwa mazungumzo na viongozi wa jumuia ya muungano wa nchi za Ulaya.
Hata hivyo, Uturuki imekuwa na wakati mgumu kujiunga na jumuia ya nchi za Ulaya kwa kuto kukubali kuitambua Syipras(Cyprus) na katiba yake, nakushinda kushirikiana kikamilifu na Ugiliki katika swala zima la Cyprus.
Picha hapo juu, wanaonekana, waziri mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, akisalimiana na Olli Rehn, mkuu anaye shughulika kujiunga na Muungano wa nchi za ulaya, walipo kutana Brussels siku ya Ijumaa.
Waandamanaji na viongozi wao wawekwa karibu na kiti moto nchini Iran.
Tehran, Iran - 26/06/09.Mmoja wa viongozi wa kidini nchini Iran,Ahmad Khatami, amesema ya kuwa wale watu wote ambao wanaandamana kupinga matokeo ya uchaguzi ya juni 22, ni lazima waadhibiwe vikali.
Ayatollah, Ahmad Khatami, ambaye ni mbuge katika kamati ya wabunge teule, ameagiza kwa kusema ya kuwa viongozi waliosababisha au kusimamia maandamano lazima waadhibiwe ili wawe mfano kwa wengine.
Ayatollah, Ahmad Khatami, aliyasema hayo wakti wa swala ya Ijumaa,na kutangazwa na radio moja kwa moja.
Picha hapo juu, anaonekana, Ayatollah, Ahmad Khatami, akiwahutubia maelfu waliokusanyika katika ukumbi wa chuo kikuu cha Tehren siku ya Ijumaa baada ya swalat Ijumaah.
Picha ya pili wanaonekana , watu walioudhulia swalat Ijuma, wakishangilia na kukubaliana na Ayatollah, Ahmad Khatami kwa yale anayo yaongea.

Tuesday, June 23, 2009

Urussi yatamka kushirikiana kuhusu swala la mashariki ya Katu

Wapigania uhuru kuishitaki Uingereza.

London,Uingereza - 23/06/09.Wapigania uhuru watano wa Kenya ambao walikuwa kundi la Maumau, wamefungua kesi ya mashitaka zidi ya serikali ya Uingereza kwa kuvunja haki za binadamu wakati wa utawala wa kikoloni wa Uingereza ulipo kuwa ukitawala miaka ya 60 kurudi nyuma.
Wapigania uhuru hao ambao wanamiaka kati ta 70 na 80. wanadai ya kuwa serikali ya Uingereza inatakiwa kulipa fidia na kuomba msamahaa kwa matendo yaliyo fanywa na Uingereza wakati Inaitawala Kenya.
Msemaji wa wapigania uhuru hao, Gitu wa Kahengeri, alisema wanafanya hivyo kwa ajili ya wapigania uhuru wenzao, wa kundi la Mau mau ambao walipoteza maisha kwa ajili mya kutetea uhuru.
Hata hivyo serikali ya Uingereza, imedai ya hali halisi ilipewa serikali ya Kenya baada ya kupata uhuru.
Picha hapo juu, ni ya bendera ya Kenya, nchi ambayo ilikuwa chini ya utawala wa Uingereza hadi ilipo pata uhuru 1963.
Picha pili, wanaonekana, baadhi ya wapigania uhuru wa mau mau wakiwa chini ya ulinzi, ambao wengi wao walipoteza maisha wakati wa kutetea uhuru wa nchi yao
Urussi yatamka kushirikiana na Misri kuhusu swala la Mashariki ya Kati.
Kairo, Misri-23/06/09.Rasi wa Urussi, Dmitri Medvedev, yupo nchini Misri kwa ziara ya kiserikali. Katika ziara hiyo, rais,Medvedev, amekutana na rais wa Misri, Hosni Mubaraka, kuzungumzia swala zima la mashariki ya kati. Picha hapo juu, wanaonekana marais wa Urussi na Misri wakiwa katika mazungumzo, wakati rais,Dmitri Medvedevwa Urussi alipo kutana na rais, Hosni Mubaraka wa Misri. Israel ya mwachia kiongozi wa Hamas.
Jerusalem,Israel- 23/06/09.Serikali ya Israel imemwachia huru spika bunge wa Hamas bwana, Abdul Aziz Dweik, baada ya kukaa miaka mitatu jela kwa kuso la kujihusisha na kundi hilo ambalo linamshikilia, Gilat Shalit.
Pichani hapo juu, anaoneka bwana, Abdul Aziz Dweik, akitolewa pingu na polisi kabla ya kuwa huru.
Picha pili anaonekana,Abdul Aziz Dweik, akitabasamu kabla ya kutoka kizimbani kuelekea nyumbani.

Tuesday, June 16, 2009

Rais wa zamani wa Amerika atembelea Gaza.

Wananchi wa Niger, kupiga kura ya maoni ya hatma ya urais. Niamey, Niger 16/06/09. Maelfu ya wanchi Niger, wameandamana kudai ya kuwa rais,Mamadou Tandja, aliyepo madarakani,asibadilishe katiba, ili aweze kugombea tena kiti cha uchaguzi kwa mara ya tatu. Maandamano hayo, nayamefanywa kufatia kupangwa tarehe ya kupiga kura ya maoni 4/Agusti,ikiwa kama rais Mamadou Tandaja ataweza endelea kugombea kiti cha uraisi. Rasi, Mamadou Tandja, anatarajiwa kumaliza muda wake wakuongoza nchi hivi karibuni. Picha hapo juu, anaonekana, rais Mamadou Tandja, akiwa katika moja ya mikutano ya kimataifa.

Makamu wa rais wa Kongo DRC, afunguliwa mashitaka.
Hague, Holland - 16/06/09. Mahakama inayo shughulikia kesi za kimataifa za jinai na maafa yanayo sabaishwa na vita, imemfungulia kesi makamu wa rais wa Kongo (DRC), Jean - Pierre Bemba, ya kuhusika na vita nchini Kongo na kusababisha kuvunjwa kwa haki za binadamu wakati wa vita vilivyo tokea kati ya mwishoni mwa mwaka 2002 hadai mwanzoni mwa mwaka 2003
Kwa mujibu wa mwanasheria wa mahakama alidai ya kuwa Jean Piere Bemba, alikuwa ana fahamu yote yaliyo tokea.
Hata hivyo mwanasheria anayemtete bwana, Bemba , amesema yakuwa, mteja wake hakuhusika na wala alikuwa hajui nini kilichokuwa kinaendelea, hii ni yote ninakuja kutokana na mrindimo wa siasa.
Rais wa zamani wa Amerika,atembelea Gaza.
Gaza,Ukingo wa mto Magharibi - 16/06/09.Rais wa zamani wa Amerika, Jimmy Carter,ametembela maeneo yaliyo shambuliwa na Israel mwishoni mwa 2008 na mapema mwaka huu 2009, na kusema yakuwa imestua saana.
Bwana, Carter, alisema ya kuwa mstuko huo, unaonyesha ni jinsi gani, Wapalestina wanavyo fanywa kama siwatu, na kuagiza ya kuwa kuna haja ya Wapalestina kupata haki kama watu wengine.
Picha hapo juu, wanaonekana, rais wa zamani wa Amerika, Jimmy Carter,na kiongozi wa Hamas,Ismail Haniyeh,kulia wakitembea kuelekea ofisini, kabla ya kuongea na waandishi wa habari.
Picha ya pili, wanaonekana, rais wazamani wa Amerika, Jimmy Carter kushoto na kulia kiongozi wa Hamas, Ismail Haniayeh, wakiongea na waandishi wa habari.
Kamati yaamua kura kuhesabiwa upya.
Tehran, Iran - 16/06/09.Kamati iliyo simamia uchaguzi wa urais wa Iran,imetangaza yakuwa watatizama kiundani na kuanza kuziehesabu kura upya.
Hata hivyo, Mir Hussein Mousavi, ambaye ameshindwa katika uchaguzi huu, ametaka kura zipigwe upya, swala ambalo kamati iliyo simamia uchaguzi imelikataa.
Mvutano huo wa matokeo ya kura,yameleta wasiwasi wa kisiasa nchini Iran, jambo ambalo linaufanya uongozi wa Iran, chini ya Ayatollah Ali Khamenei kuwa na wakati mgumu.
Picha hapo juu, ni picha ya rais,Mahamoud Ahamdinejad katikati, akiwasiri nyumbani,baada ya kukatiza ziara yake ya kikazi nchini Urussi.
Picha ya pili, anaonekana, Ayatollah Ali Khamenei, ambaye uongozi mkuu wa Iran,ambaye Iran inategemea uwezo wake.

Monday, June 15, 2009

Ahmadinejad, achaguliwa tena kuwa rais,matokeo ya uchaguzi yaleta sakata Iran.

Muda si mrefu,Waingereza kupata ukweli kuhusu vita vya Irak.

London, Uingereza, 15/06/09. Waziri mkuu wa Uingereza,ametangaza ya kuwa serikali itafanya uchunguzi kwa makini kuhusu kuhusika kwa Uingereza katika vita vya Irak, vilivyo fanyi miaka sita iliyo pita.
Vita hivyo,vilivyoanza mwaka mapema 2003 na kumng'oa rais wa Irak, Saddam Hussein, vimekuwa vikileta joto ya jiwe kwa serikali ya, Gordon Brown na aliye mwachia ofisi, waziri mkuu mstaafaafu, Tony Brair.
Picha hapo juu, anaonekana,waziri mkuu wa Uingereza, Gordon Brown, ambaye amekuwa na wakati mgumu kutoka kwa wapinzani kudai kuwepo kwa uchunguzi wa Uingereza kuhusika kwa nchi hiyo katika vita vya Irak.
Picha ya pili wanaonekana, wanajeshi wa Uingereza wakiwa wakiwa katika mapambano katika kumng'oa Saddam Hussein.
Ahmadinejad,achaguliwa tena kuwa rais, matokeo ya uchaguzi yaleta sakata Iran.
Tehran, Iran - 15/06/09. Kamati inayosimamia uchaguzi wa Iran, nchini Iran imetangaza ya kuwa rais Mahamoud Ahmadinejad, kuwa mshindi kwa kupata kura kiasi cha 62% zidi ya mpinzani wake Mir Hossein Mousavi, katika kinyanganyiro cha kugombea kiti cha urais wa Iran.
Hata hivyo, baada ya matangazo ya ushindi wa rais, Mahmoud Ahamadinejad,mpinzani wake, Mir Hoeesin Mousavi, amesema yakuwa uchaguzi umekuwa batili na amekata rufaa, kutokubaliana na matokea hayo.
Kufuatia, malalamiko hayo, wasimamizi wa uchaguzi huo, wamesema wanafanya uchaguzi, watautangaza baada ya siku kumi.
Picha hapo juu, anaonekana, ras Mahmoud Ahmadinejad, ambaye amechaguliwa kuwa rais wa Iran kwa mara nyingine tena.
Picha ya pili wanaonekana,wadau wa rais Mir Hossein Mousavi, wa cha upinzani, wakiandamana kuelekea kwanye uwanja wa ukumbozi kupinga matokea ya uchaguzi huo.
Majeshi ya NATO na Amerika yapata Generalali mpya.
Kabul, Afghanistan, 15/06/09. Jeneralali Stanley Mc Chrystal,ambaye aliteuliwa kuwa wa mkuu wa majeshi ya Amerika na NATO, nchini Afghanistan,katika kupambana na kundi la Taliban.
Jeneralali, Stanley MacChrystal, amechukua nafasi ya aliyekuwa mkuu wa majeshi hayo, Generalali, David McKiernan, ambaye aliachishwa kazi, baada ya kutokea makosa ya wakati wa uongozi wake.
Picha hapo juu, anaonekana, Generalali, Stanley McChrystal, akiongea na rais, Baraka Obama,mara baada ya kuteuliwa kuwa mkuu wa majeshi hayo.
Mashariki ya kati bado fumbo kwa jumuia ya kimataifa.
Jerusalem, Israel - 15/06/09. Waziri mkuu wa Israel, Menyamin Netanyahu,amesema ya kuwa kuwepo kwa taifa la Wapalestina,ni muhimu kwa usalama na amani wa eneo zima la mashariki ya kati.
Akisisitiza mkazo wa kuwepo kwa taifa la Wapalestina,waziri mkuu wa Israel, Benyamini Netanyahu, alisema ya kuwa hii yote itafanikiwa, ikiwa Wapelestina, wataitambua Israel ni taifa, ,swala la wakimbizi,kutofanya mashambulizi kwa Wanchi wa Israel, na kuzuia au kuwapokonya siraha wale wote wanao shiriki katika ugaidi.
Hata hivyo,serikali ya Palestina,imesema yakuwa hotuba ya waziri mkuu wa I srael, Benyamini Netanyahu, ni kikwazo kikubwa cha kuleta amani na usalama katika eneo zima la Mashariki ya Kati, hawaoni kama wana mshiriki katika swala la amani na usalama wa eneo hilo.
Picha ya hapo juu anaonekana, rais wa Palestina, Mahmoud Abbas, ambaye uongozi wake umekuwa unapata ushirikiano wa karibu na serikali za Amerika na Ulaya katika swala la kuleta amani kati ya Waisrael na Wapalestina.
Picha ya pili, anaonekna waziri mkuu wa Israel , Benyamini Netanyahu, akihutubia jana taifa na jumui ya kimataifa kuhusu sera ya serikali yake katika maswala ya mambo ya nchi za nje.

Wednesday, June 10, 2009

Sudan kuzalisha mafuta kutoka kwenye mimea.

Sudan kuzalisha mafuta kutoka kwenya mimea. Khartoum, Sudan - 10/06/09. Serikali ya Sudan imezindua rasm mmea utakao tumika katika kutengenezea mafuta ya kuendeshea mitambo. Akizindua mmea huo, rais wa Sudana, Omar Al Bashir, alisema ya kuwa serikali yake itafanya kilanjia mradi huo udumu kwa utaipatia Sudan, pesa za kigeni na kuta ajira. Kwa mujibu wa uongozi wa kampuni hiyo ya Kenana, imesema ya kuwa mtambo huo utakuwa na uwezo wa kuzalisha mafuta lita 200 million , yatakayo toka kwenye mimea hiyo baada ya miaka miwili. Picha ya hapo juu, ni ya bendera ya serikali ya Sudan, nchi ambayo imegundua mimea itakayo toa zao halisi la mafuta kwa ajili ya kuendeshea mitambo. Hali halisi ya maisha kuisaida Taliban kukua. Ismabad, Pakistan - 10/06/09. Wachunguzi wa mambo ya kiusalma nchini Pakistan, wanasema ya kuwa kundi la Taliban, linazidi kukua kila mwaka. Hii inakuja kutokana na hali halisi ya eneo hili,kiimani,mila na desturi na hasa swala usalama wa wanchi waliowengi nchini Pakistan na hivyo wanchi wengi kujikuta kuingia katika kundi la Taliban kwa nguvu au kwa hiyari yao. Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya watu, ambao wamesimama khuku wakiota jua,katika kambi moja ya wakimbizi, baada ya kukimbia vita vinavyoendelea kati ya Taliban na majeshi ya serikali.

Tuesday, June 9, 2009

Familia ya, Ken Saro Wiwa, na wenzake walipwa madai yao.

Mbrazili nyota asajiliwa kwa kitita kinene. Madrid, Uispania - 09/06/09.Timu ya Real Madrid,imemsajili mchezaji nyota wa Brazil, Kaka, kwa kitita cha $ 94.05million na kuvunja rekodi ya dunia. Kaka, ambaye alikuwa mchezaji wa, AC Milan, amevunja rekodi ya iliyo wekwa na, Zinedin Zidane, aliposajiliwa na mwaka 2001. Hata kwa mujibu wa wachunguzi wa maswala ya soka, wanasema bado Zinedine Zidane, anaweka rekodi ya kuwa mchezaji aliye nunuliwa kwa Euro 73million na Kaka Euoro 63, kwa kuzingatia mzunguko wa mabadiliko ya pesa ( Fedha). Picha hapo juu anaonekana, Kaka , akiongea na waandishi wa habari, muda baada ya kumaliza kufanya uangalizi wa afya mapema jana. Jose Emanuel Barroso,achaguliwa tena kuwa rais wa Muungano wa Ulaya.

Brussel, Belgium - 09/06/09.Muungano wa Ulaya,umemchagua tena, Jose Emanuel Barroso, kwa mara nyingine kuwa rais wa muungano huo kwa kipindi kingine cha miaaka mitano.
Akiongea baada ya kuchaguliwa kwake, kuendela kuwa rais wa muungano wa Ulaya, Jose Emanuel Barroso, alisema yakuwa imekuwa ni heshima kubwa kwake kwa kuchaguliwa tena kuwa rais wa muungano huo, na kuhaidi yakuwa atajitaidi kwa kila njia kuhakikisha muungano wa Ulaya utazidi kuwa imara.
Picha ya hapo juu, ni ya Jose Emanuel Barroso,ambaye amechaguliwa tena kuwa rais wa muungano wa Ulaya kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Picha ya pili, ni ya bendera ya muungano ya Ulaya,ambao umekuwa ukizidi kuwa imara kila kukicha.
Familia ya Ken Saro Wiwa na wenzake walipwa madai yao.
Niger Delta, Nigeria - 09/06/09.Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu nchini Nigeria, wataendelea kusukuma na kusisitiza kutaka kupata haki na ukweli kuhusu kifo cha aliyekuwa kiongozi wa kuteteta mazingira, Ken Saro Wiwa, aliye uwawa mwaka 10/11/1995, licha ya kampuni ya Shell kukubali kulipa malipo ya dola za Kimarekani 15.5 million kwa familia zilizopinga kuwepo kwa Shell katika jimbo la, Niger Delta, kwa madai ya kuchafua mazingira.
Hata hivyo, kampuni ya Shell, imekuwa ikikana kuhusika na sakata hilo lililo sababisha vifo vya Ken Saro Wiwa, na wenzake wengine wanane.
Picha hapo juu, ni picha ya kuchorwa ya, Ken Saro Wiwa, ambaye alikuwa kiongozi wa wanaharakati walio pinga kuwepo kwa Shell katika eneo la Niger Delta.
Picha ya pili, ni ya maeneo ambayo mfuta huwa yanahifadhiwa tayari kwa kusafirishwa.

Monday, June 8, 2009

Rais wa Gabon hatupo nae tena.

Waandishi wahabari, 2 wa Amerika wahukumiwa kwenda jela miaaka 12 kila mtu.

Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 08/06/09. Hakama nchini Korae ya Kaskazini imewahukumu, waandishi wa habari raia wa Amerika miaka 12 jela , baada ya kuwakuta na hatia ya kosa la kuingia katika maeno ya Korea ya Kaskazini kinyume cha sheria. Waandisha hao wa habari, Laura Ling na Euna Lee, walikamatwa mnamo Machi 17/2007, ana askari wa ulinzi wa mipaka wa Korea ya Kaskazini.
Kufuatia hukumu hiyo, serikali ya Amerika ,imesema haikuridhishwa na kitendo hicho cha Korea ya Kaskazini, na itafanya kila jitihada kuhakikisha waandishi hao Laura na Euna,waachaliwe.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Korea ya Kaskazini,nchi ambayo imekuwa na mvutano mkubwa na Amerika kwa miaaka mingi tangu miaaka ya hamsini.
Picha ya pili wanaonekana, Laula Ling na Euna Lee, waandishi wa habari walio hukumiwa kifungo cha miaa 12 kila mtu na serikali ya Korea ya Kaskazini.
Rais wa Gabon hatupo naye tena.
Libreville, Gabao - 08/06/09.Serikali ya Gabon,imetangaza yakuwa rais wa Gabon Omar Bongo amefariki dunia nchi, Uispania Barcelona.
Kwa mujibu wa habari kutoka ofisi ya waziri mkuu wa Gabon, zilisema ya kuwa, alifariki jumatatu ya leo saa nane machana katika Hospital ya Quiron.
Rasi, Omar Bongo aliyekuwa na miaka 73, alikuwa anajulikana kama rais wa maisha wa Gabon. ameitawala Gabon kwa muda wa miaaka 41, na kuwa kiongozi aliyetawala kwa muda mrefu katika bara la Afrika.
Picha hapo juu anaonekana rais , Omar Bongo , enzi za uhai wake, akiwa anatafakari kwa makini.
Picha ya pili anaonekana, rais, Omar Bongo, enzi za uhai wake,akikagua gwaride la heshima nchini Ufaransa, alipo tembelea nchin hiyo.
Picha ya tatu, anaonekana rais, Omar Bongo, akiwa na rais wa Ufaransa, Nikolas Sarkozy, wakati rais wa Ufaransa alipo tembelea nchini Gabaon.
Uchaguzi wa Lebanon, waleta hafuaheni.
Beirut, Lebanon - 8/06/09. Matokeo ya uchaguzi uliofanyika nchini Lebanon,yamekipa ushindi mkubwa chama kinacho ongozwa na mtoto aliyekuwa waziri mkuu wa Lebanon, hayati Rafiki Hariri, Saad Hariri kwa kupata viti 71 kati ya viti 128 katika bunge la Lebanon.
Kushinda kwa chama hicho 14 March,kinampa uwezo, Saad Hariri na chama chake kuongoza Lebanon na.
Hata hivyo chama kilichokuwa kinaupinzani mkubwa na 14 March, cha Hezbollah, kimepata viti 57, katika bunge hilo, jambo ambalo litaleta wakati mgumu kwa chama cha 14 March kupitisha baadhi ya maamuzi katika bunge hilo.
Ushindi huo wa chama cha 14 March, umepokelewa na nchi za Ulaya na Amerika kwa unafuu mkubwa, kwani uhusiano wa nchi hizo na Hezbollah siyo mzuri.
Picha hapo juu ,ni picha ya bendera ya ya Lebanon, nchi ambayo imekuwa katika hali ya mashaka kwa muda, hasa kwa baadhi ya viongozi wa siasa kuuwawa.
Picha ya pili anaonekana mmoja ya wananchi wa Lebanon, akijipongeza mara baada ya kujua ya kuwa chama chake kipata kura bungeni.