Thursday, April 30, 2009

Jeshi la Uingereza kuanza kurudi nyumbani kuanzia leo.

Rais, Baraka Obama, kafanikiwa alimia 65% kwa muda wa siku 100, ofisini. Washington, Amerika - 30/04/09. Rais wa Amerika, Baraka Obama, ametimiza siku 100,tangu kuwa rais wa Amerika. Kwa mujibu wa wachunguzi wa mabo ya kisiasa na kiuchumi, wanasema rais, Baraka Obama, amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa kukamilisha kwa asilimia zaidai ya 65% kwa ya le yote aliyo yasema wakati wakampeni za uchaguzi wa rais mapema mwaka jana. Moja ya mamba ambayo rais , Obama ameyatimiza, ni kufungwa kwa jela, ya Guantanamo Bay,kutia sahii kuzuia kuteswa kwa wafungwa au mtuu yoyote kinyume na sheria za haki za binadamu,kusaidia kuyakwamua kifedha makampuni makubwa ya magari kama GM(General Motors) nchini Amerika na kurudisha uhusiano mzuri na nchi nyingi ikiwemo, Venezuela. Picha hapo juu anaonekna, rais wa Amerika Baraka Obama,akionyasha vidole ya kuwa mambo ni kuelekea mbele, kabla ya kuanza kuongea na waandishi wa habari na kujibu maswali. Jeshi la Uingereza kuanza kurudi nyumbani kuanzia leo. Basra,Irak - 30/04/09.Jeshi la Uingereza limemaliza muda wake wakuu kaa nchini Irak, kama jeshi la ulinzi na kulinda amani. Hii ina fuatia , baada ya ya waziri mkuu wa Uingereza, Gordon Brown,kusema haya siku ya alkhamisi wiki hii wakati alipo kutana na waziri mkuu wa Irak,Nour al Maliki, ya kuwa jeshi la Uingereza litajea nyumbani. Jeshi hilo la Uingereza limekuwa nchini Irak kwa kipindi cha miaka sita (6). Kwa mujibu wa habari kutoka kwenye jeshi la Uingereza, zina sema ni wanajeshi 400 watakao baki, kwa ajilii ya kutoa mafunzo kwa Wairak. Picha hapo juu wanaonekana, wanajeshi wa jeshi la Uingereza wakiwa wanatoa heshima zao kwa wanajeshi wenzao waliopoteza maisha katika vita nchini Irak, vilivyo anza mwaka 2003.

Kesi ya mauaji ya waziri kuu wa Lebanoni watuuhumiwa bado kupatikana.
Beiruti,Lebanoni - 30/04/09. Wakuu wa nne wa jeshi la LebanoniMustafa Hamdan,Jamil al Sayyed,Ali al Hajji na Raymond Azar , waliachiwa huru jana, baada ya mahakama ya Umoja wa mataifa inayo shughulikia kesi za vita na mauaji kusema kuwa hakukua na ushahidi wa kutosha ya kuwa wakuu hao wa kijeshi walihusika katika mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu wa Lebanoni, Rafiki Hariri.
Akiongea hayo, Jaji Daniel Franseen, akisoma mbele ya mahamaka mjini Beiruti, kutangazwa kuachiwa huru kwa wakuu hao wa kijeshi,moja kwa moja kwa njia ya runinga (TV), kuliamsha msisimko tofauti kati ya Walebanoni.
Waziri mkuu, Rafiki Hariri, aliuwawa na mabomu tarehe, 22/04/05, na kuleta mvulugano wa kisiasa na kulazimisha kuondoka kwa jeshi la Syria, ambalo lilikuwa nchini humo kwa muda wa miaka 29.
Picha hapo juu, inaonekana picha ya waziri mkuu wa Lebanoni, Rafiki Harii, ikiwa imetundikwa ukutani wakati wa shererhe ya kukumbuka siku ya kifo chake.
Picha ya pili zianaonekana, picha za wakuu wa kijeshi ambao walikuwa wanashitakiwa kwa kuhusika na mauaji ya waziri mkuu, Rafiki Hariri, wameachiwa huru baada ya mahakama kukosa ushaidi kalimi.

Monday, April 27, 2009

Mafua ya nguruwe yaiweka dunia njia panda.

Mafua ya nguruwe yaiweka dunia njia panda.

Mexico City,Mexico 27/04/09.Mlipuko wa ugonjwa wa mafua ya nguruwe, umeiweka dunia katikahali ya taadhali, baada ya watu wapatao 149 kufariki dunia kutokana na ugonjwa huo, na wengine kwa mamia kuugua kutokana na ugonjwa huo.
Kwa mujibu wa waziri wa afya wa Mexico, Jose Angel Cordova, serikali ya Mexico kwa kushirikiana na shirika la afya ulimwenguni WHO, zinajitahidi kuzuia ugonjwa huo usienee na tiba yake inatolewa mara moja pindipo atakapo patikana mgonjwa.
Picha hapo juu wanaonekana abiria wakiwa katika treni, anaonekana mmoja ya askari akigawa dhana za kukingia mdomo kwa abiria waliomo ndani ya treni.
Picha ya pili, wanaonekana, askari wakiwa katika kwata , huku wakiwa wamevaa midononi na puani dhana za kukinga ugonjwa usiwakumbe wakati wakiwa kazini.
Mashindano ya siraha,huenda yaka anza Mashariki ya Kati.
Dubai, UAE - 27/04/09. Serikali ya UAE, imeongeza uwezo wake wa kijeshi,kwa kununua zana za kijeshi ili kuongeaz uwezo wake wa kijeshi, kufuatana na wakati.
Kwa mujibu wa ripoti zilizo tolewa na shirika la kimataifa linalo shughulikia, maswala ya amani na zana za kivita (SIPRI - Stockholm International Peace Research), limesema ya kuwa UAE, kwa muda wa miaaka isiyo pungua kumi, UAE imepanda kuwa nchi ya 15 duniani kwa kununu siraha na teknolojia za kivita.
Kufuatia hali hii, shirika hilo, linasema kunaweza kuleta mashindano ya zana za kivita katika eneo la Mashariki ya Kati.
Picha hapo juu, ni moja ya gwaride la wanajeshi wa UAE, wakiwa katika moja ya sherehe za kitaifa,na kwa upande wa kushoto ni moja ya siraha ambazo UAE, inazo katika himaya yake.
Picha ya pili, linaoneka bomu likiwa linatoka kwenya mtutu, kuelekea lilipo lengewa wakati wa mazoezi ya kivita.
ANC ya pata ushindi kwa mara nyingine tena "Tayari kuongoza serikali".
Johannesburg,Afrika ya Kusini - 27/07/09. Matokeo ya uchaguzi mkuu, ulifanyika Afrika ya Kusini, kumeipa chama tawala cha ANC ushindi kwa mara ya tatu tangu kukomeshwa kwa utawala wa wazungu wachache.
Ingawaje katika uchaguzi huo, chama cha ANC, hakikuweza kupata vingi wa viti katika bunge ambavyo vingewezesha ANC kuweza kubadilisha katiba ya nchi.
Katika uchaguzi huo,ANC ilipata 65% sawa na viti katika bunge 264 kati ya viti 400,vilivyopo katika bunge.
Picha hapo juu, inaonekana bendera ya Afrika ya Kusini, nchi ambayo ilikuwa chini ya utawala wa wazungu wachache kwa kipindi kirefu.
Picha ya pili,ni ya chama tawala ANC,chama ambacho kilikuwa mstari wa mbele, katika kupinga ubaguzi wa rangi na kupigania haki za Waafrika wa Kusini waliokuwa wakikandamizwa na serikali ya makabulu.

Thursday, April 23, 2009

Hali ya ukame nchini Kenya huenda ikaleta maafa kwa jamii"UN"

Aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Amerika lawamani. Washington, Amerika 23/04/09.Aliyekuwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, Bi Condoleezza Rice,inesemekana ndiye aliyetia sahii kuanza kutumika kwa njia ambazo zilikwenda kinyume na haki za binadamu wakati watuhumiwa waliokamatwa kama wahujumu na watu hatari kwa Amerika wakati wa mahijiano katika gereza la Guantanamo Bay. Kwa mujibu wa habari zilizo patikana, zinasema Bi Rice, alitia sahii ruhusa hiyo mwaka 2002, wakati akiwa mshauri wa waziri wa mambo ya ndani ya nchi Picha hpo juu, anaonekana, Bi Condeelezza Rice, akiongea katika moja ya vikao wakati alipo kuwa akifanya kazi katika ofisi ya mambo ya ndani ya Amerika. Wahisani wakubali kuisaidia Somalia. Brussels, Ubeligiji - 23/04/09. Kundi la waihisani wamekubaliana kwa pamoja watachanga kiasi cha US$250 million, ili kuisadia Somalia kujenga na kurudisha hali ya kiusalama nchini humo. Wahisani hao walikubali kwa pamoja kutoa mchango huo,kwa kufuatia ombi la Umoja wa Mataifa kuitisha mkutano kuzungumzia hali halisi ya Somalia, hasa kufuatia kuku kwa uharamia. Picha hapo juu wanaonekana, rais wa Somalia, Sheikh Sharif Ahmed ,na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, wakati wa mkutano huo uliofanyika nchini Ubeligiji na wahisani na Umoja wa Mataifa. Uhusiano wa Amerika na Venezuela kuanza upya. Caracas, Venezuela - 19/04/09. Serikali ya Venezuela, imesema ya kuwa itafungua ofisi zake za kibalozi nchini Amerika, ikiwa ni ishara ya kuonyesha yakuwa Venezuela inahitaji kushirikiana na Amerika. Hayo yalizungumzwa na rais wa Venezuela , Hugo Chavez, wakati alipo kutana na rais wa Amerika, Baraka Obama,kwenye mkutano, ulio zishirikisha nchi zililizopo katika bara la Amerika nchi Trinidad na Tobago. Uhusiano wa Venezuela, haukuwa mzuri wakati wa kipindi cha utawala wa rais George Bush, hata kufikia, kufungwa kwa ofisi zote za kibalozi kati ya nchi hizi. Pcha hapo juu ,anaonekana , rais wa Amerika Baraka Obama na rais wa Venezuela, Hugo Chavez, wakiwa wameshikana mikono, wakta rais Hugo Chavez, alipo kuwa akimkabidhi rais Baraka Obama kitabu cha historia ya Watu wa Latini Amerika na maisha yao hadi hivi leo. Picha hapo juu, wanaonekana marais , Hugo Chavez kuliana rais, Baraka Obama kushoto wakiwa mwameshikana mkono wakati walipo kutana nchini Trinidad na Tobago ili kuzungumzia hali ya kiuchumi ya Amerika. Algeria yalaumiwa na Morocco kwa kutaka kuvuruga amani. Rabat, Morocco - 19/04/09. Serikali ya Morocco imeilaumu serikali ya Algeria, kwa kusaidia wapiganaji wa POLISARIO, kuingia karibu na mpaka wa Morocco na kufanya mashambulizi ambayo ayakuleta madhara. Kwa mujibu wa habari zilizo toka ofisi za mambo nchi za nje za Morocco, zilisema wapiganaji hao walipiga risasi ovyo hewani. POLISARIO, ni kundi lililopo kusini magharibi mwa Morocco linalo pigania kujitenga na Morocco. Picha hapo juu ni ramani ya Afrika ya Kaskazini Magharibi,na kusini mwa ramani hiyo, kunaonekana,eneo la Sahara ya Magharibi, ni eneo ambalo kwa muda mrefu linamvutano na mgogoro mkubwa huko kaskazini magharibi mwa bara la Afrika. Hali ya ukame nchini Kenya huenda ikaleta maafa kwa jamii."UN".

Nairobi, Kenya 18/04/09. Hali ya ukame inayo endelea nchini Kenya, imefika hali mbaya, kwa mujibu wa maseami wa shirika linalo shughulikia vyakula Duniani ( WFP - World Food Progamme), Gabrielle Menezes alisema, kufuatia ukame huo, Kenya itakabiliwa na upungufu mkubwa wa chakula,ambapo msaada wa vyakulua hutaitajika.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Kenya nchi ambayo hali ya ukame nchini humo inatishia jamii.
Picha ya pili wanaonekana wa kina mama wakiwametua kupumzika, baada ya kutembea kwa muda mrefu kutoka kutafuta ridhiki.
Wazimbabwe washerekea siku ya uhuru chini ya serikali ya muungano madarakani.

Harare, Zimbabwe - 17/04/09. Viongozi wa vyama pinzani nchini Zimbabwe,Robert Mugabe wa NAZU PF na Morgan Tsvangirai wa MDC, wamechelekea kwa pamoja siku ya uhuru wa Zimbabwe hivi karibuni, tangu kuanzishwa kwa serikali ya muungano.

Sherehe hiyo ambayo ili udhuliwa na viongozi wote wa serikali na baadhi mabalozi huwa inaadhimishwa kila tarehe 17/04/09 ya kila mwaka.

Katika sherehe hiyo, rais,Robert Mugabe , aliwataka wananchi waungane kwa pamoja, kujenga nchi na kuulunda nchi yao

Picha hapo juu ni ya bendera ya Zimbabwe, nchi ambayo ulipata uhuru wake kutoka kwa Uingereza mwaka 1980.

Sunday, April 19, 2009

Makampuni yaliyo shiriki katika ubaguzi wa rangi nchini Afrika ya Kusini yanaweza kushitakiwa.

Ukame wa waanza kusogelea Afrika ya Magharibi. Akkra, Ghana - 19/04/09.Wataalamu wa sayansi ya mazingira nchini Ghana wamesema huenda ikawa na hali ya ukame zaidi hapo mbeleni, kwa kufuatia uchunguzi wa kisayansi uliofanywa kwa kulinganisha karne ya 20 na karne tuliyo nayo sasa. Kwa mujibu wa kituo kimoja cha sayansi kilichopo nchini humu(Ghana) kinasema hii ni kutokana na utafiti uliofanywa katika ziwa Bosumtwi lililopo nchini Ghana. zimeonyasha tofauti kubwa kulingana na za karne za nyuma. Hata hivyo, wanasayansi walisema yakuwa,bado itachukua muda hali kuwa mbaya zaidi kwa kuzingatia mvua na maeneo ya kijiografia yaliopo katika nchi hizi. Picha hapo, juu ni ya ramani ya Afria ya Magharibi, eneo ambalo wanasayansi wanasema hali ya ukame inalinyemelea kwa mbali.

Mmoja ya washukiwa wa ulipuliwaji wa Msikiti mkubwa aachiwa kwa dhamana Pakistan.
Islamabad,Pakistan - 19/04/09.Mahakama nchini Pakistan, imemkubalia dhamana, kiongozi mmoja wa mlango wa kushoto wa kundi la Taliban, Maulana Abdul Aziz,baada ya kuwekwa jela kwa kipindi kisicho pungua miaka miwili,baada ya kushukiwa kuhusika na mauaji ya ulipuaji wa msikiti mkubwa uliokuwepo Red Square mwaka 2007.
Maulana Abdul Aziz,ambaye ni mmoja ya viongozi ambaye anapendelea kuwepo na sheria za kidini nchini Pakistan na kupinga kwa kuwepo kwa majeshi ya kigeni hasa ya Amerika na washiriki wake katika maeneo hayo.
Hata hivyo , baada ya kutoka jela, Maulana Abdul Aziz alihutubia mamia katika eneo la msikiti uliolipuliwa wa Red Square, alisema, atakubali tena vita vya kuwa lipua Waislaam wenzake, lakini vita bado vitakuwa vya amanim, kwani mapambano bado yanaendelea.
Picha hapo juu anaonekana, Maulana Abdul Aziz, akitoka jela ambapo alikaa kwa muda wa miaka miwili.
Picha ya pili,wanaonekna baadhi ya waumini wa kiswali huku wamelizunguka gari, lililo tobolewa kwa risasi, wakati wa mashambulizi ya mwaka 2007 ya ulipuliwajiwa msikiti wa Red Square.
Katibu mkuu mpya wa NATO, anawakati mgumu bele yake.
Kabul, Afghanistan - 19/04/09. Kundi la Taliban, lililopo nchini Afghanistan, kimesema ya kuwa katibu mkuu mpya wa NATO,Anders Fogh Rasmussen, ni adui wa Waislaam, baada ya kushindwa kuchukua hatua yoyote kwa wale wote walio husika na uchoraji wa katooni za kumkashifu Mtume Mohammed nchini mwake, akiwa kama kiongozi wa serikali.
Hata hivyo, Anders Fogh Rasmussen, ambaye alisema ya kuwa katiba haimruhusu yeye kuingilia maoni ya mtu, kwani atakuwa amekiuka haki inayo mruhusu mtu kuongea anachotaka kwani ni uhuru wa mtu kuongea anavyotaka kwa kutokana na katiba inavyosema.
Picha hapo juu, anaonekana , Anders Fogh Rasmussen, ambaye amechaguliwa kuwa katibu mkuu mpya wa NATO hivi karibuni.
Sudan yakubali kurejea kwa baadhi ya mashirika ya kigeni,"Asema , Seneta John Kerry".
Khartoum,Sudan - 19/04/09.Serikali ya Amerika imetuma ujumbe wake wa juu kabisa nchini Sudan, li kutathmini hali halisi ya nchi hiyo hasa katika eneo la Darfur.
Ujumbe huo, unao ongozwa na, Seneta, John Kerry, ulizungumza na viongozi wa serikali ya Sudan kwa undani zaidi,ili kuweza kutatua hali halisi ya mvutano kati ya serikali ya Sudan na mahakama ya kimataifa inayo shughulikia kesi za kivita na haki za binadamu iliyopo nchini Nederland kutoa hati ya kukamatwa kwa rais, wa Sudan, Omar Al Bashir na kufukuzwa kwa mashirika ya kigeni ambayo yalikuwa yanatoa misaada kwa wakazi wa eneo la Darfur.
Picha hapo juum anaonekana, Seneta, John Kerry, akiongea na makamu wa rais, wa Sudan, Ali Osman Mohammed Taha, wakati walipo kutana hivi karibuni mjini Khartuom kwa mazungumzo.
Makampuni yaliyo shiriki katika ubaguzi wa rangi nchini Afrika ya Kusini yanaweza kushitakiwa.
New York, Amerika - 19/04/09.Mahakama ya Amerika, imekubali ya kuwa watu wote walio athirika wakati wa utawala wa kibaguzi wa serikali ya Afrika ya kusini, wanaweza kuishitaki kampuni za General Motors, BMI na nyingine zilizo husika katika kushiriki kukiuka haki za kibinadamu.
Mahakama hiyo iliyopo New York, ilisema ya kuwa, General Motors ilikuwa inajua fika ya kuwa magari yake yalikuwa yanatumika wakati wa utawala wa kibaguzi nchini Afrika ya Kusini, kuwakandamiza watu waliowengi.
Vilevile mahakama ilisema ya kuwa IBM, ilikuwa inajua yakuwa mitambo yake ya mtandao, ilikuwa inatumika katika kubagua na kutenganisha weusi na weupe kwa kuweka repoti.
Uamuzi huo umekuja, baada ya mahakama kuona ya kuwa makampuni hayo yanaweza kushitakiwa, kwa kufuatia sheria ambayo inaruhusu makampuni ya Amerika kushitakiwa nje ya Amerika, ikiwa kesi hizo zitaletwa katika mahakama ya Amerika.
Picha hapo juu, ni bendera mpya Afrika ya Kusini, nchi ambayo wananchi wake wamekandamizwa na kunyanyaswa kwa muda mrefu na serikali ya kibaguzi wa Wazungu wachache , kwa kupitia au kutumia teknolojia zilizo tolewa na baadhi ya makampuni ya kimataifa zikiwemo IBM na General Motors na mengine mengi.
Rais wa Paraguay, Fedrinando Lugo, akubali yaliyosemwa na redio.
San Pedro, Paraguay - 19/04/09.Rais wa Paraguay, Ferdinando Lugo, amekili ya kuwa yeye ndiye baba ya watoto wawili,ambapo hapo mwanzo alikanusha baada ya redio moja kutangaza ya kuwa alikuwa rais Ferdinando Lugo, anawatoto wawili ambao amezaa na mwanake mwenye miaka 26,Viviana Rosalith.
Rais , Ferdinando Lugo, ambaye , hapo mwanzo alikuwa ni Askofu wa kanisa Katoliki katika jimbo la San Pedro,kwa kipindi cha miaka kumi, kabla ya kuamua kuacha kazi ya ukasisi na kuingia katika siasa.
Kwa mujibu wa redio, hiyo ilisema ya kuwa, rais Ferdinando Lugo ,alizaa na Viviana Rosalith wakati bado akiwa kama askofu wa jimbo la San Pedro.
Picha hapo juu, anaonekana, rais wa Paraguay, Ferdinando Lugo, akitoa heshima katika moja ya sherehe za kitaifa hivi karibuni.
Picha ya pili anaoneka, Ferdinando Lugo, akionekana kukusalimia, baada ya kumaliza kuapishwa kuwa rais wa Paraguay, mwezi wa nne mwaka jana.
Rais wa Bolivia, asimamisha mgomo wa kula.
La Paz, Bolivia - 19/04/09.Rasi wa Bolivia, Evo Morales,amesimamisha mgomo wake wakukataa kula hivi karibuni, baada ya bunge kupitisha sheria ya kumruhusu kugombea tena kiti cha urais unao tarajiwa kufanyika mwisho wa mwaka huu 2009.
Hata hivyo viongozi wa vyama vya upinzani walijitahidi kupinga mswada huo, kwa madai ungempa rais, Morales, nafasi nyingine ya kuiongoza nchi hivyo.
Picha hapo, juu anaonekana , rais Evo Morales, akiwa amekaa mara baada ya bunge kupitisha mswada wa kumruhusu rais, kuweza kugombea urais kwa mihula miwili.
Picha ya pili, aneonekna ,rais Evo Morales, kulia akiwa amelelala chini na baadhi ya wanchama wenzake kwenye chumba
, wakati walipo fanya mgomo wa kula chakula,ili bunge kupitisha sheria mpya ya urais.
Hatuna mpango wa kuleta machafuko au mashambulizi nchini Misri.
Beiruti,Lebanoni - 19/04/09. Kiongozi wa kundi la HezbollahHassan Nasrallah, lililopo nchini Lebanoni. amekanusha ya kuwa kundi lake halina mpango wa kuleta machafuko au mashambulizi nchini Misri.
Alikuwa akiyaongea hay hivi karibununi , baada ya serikali ya Misri kudai ya kuwa kundi la Hezbollah, lina mpango wa kushambulia nchini Misri, baada ya kuwakamata watu 49, na mmoja wao inasemekana ni wanachama wa kundi la Hezbollah
Picha hapo juu, anaonekana kiongozi wa kundi la Hezbollah,akiongea kupitia lunginga, kukanusha habari ya kuwa kundi lake lina mpango wa kuleta machafuko nchini Misri.

Thursday, April 9, 2009

Swala la nguvu za nyuklia ni kitendawili kwa Iran, Amerika na washiriki wake.

Kim Jong Il, achaguliwa kuwa rais wa Korea Kaskazini tena.

Pyongyang,Korea ya Kusini - 09/04/09.Kiongozi wa Korea ya Kaskazini,Kim Jong Il, amechaguliwa tena kuwa kiongozi na rais na bunge la nchi hiyo.
Kim Jong Il, alikuwa anashikilia madaraka yaliyo achwa na baba yake Kim Il Sung alifaliki dunia 1994, alikuwa ka rais wa mpito.
Kwa kuchaguliwa kuwa rais wa nchi hiyo, atakuwa ni kiongozi wa jeshi la Korea ya kaskazini.
Picha hapo juu, anaonekana akikagua jeshi, ambalo kwa sasa litakuwa chini yake.
Picha ya pili, wanaonekana, baadi ya wanchi wakiwa katika moja ya sherehe za kitaifa nchini Korea ya Kusini.
Swala la mguvu za nyuklia ni kitendawili kwa Iran, Amerika na washiriki wake.
Isfahan,Iran 09/04/09 - Rais wa Iran,Mahmoud Ahmadinejad, amefungua rasmi mtambo kutengenezea nguvu za kinyuklia, katika mji wa Isfahan.
Katika sherehe ya ufunguzi wa mtambo huo, rais wa Iran, alisema mazungumzo ni lazima yawe ya faida kwa pande zote mbili na siyo kwa faida ya upande mmoja tu
.
Rais, Mahmoud Ahamadinajad, alisema hayo,kuonyesha ya kuwa, maelezo yaliyo tolewa na rais wa Amerika , Baraka Obama hivi karibuni,hayakuwa kizuizi cha Iran kuendelea kiteknolojia katika nyanja za matumizi ya nguvu za nyuklia.
Huku akisisitiza, rais ,wa Iran , alisema, mazungumzo kati ya Amerika na Iran katika swala la nyuklia, yanatakiwa yawe ya kisheria za kimsingi, na siyo Amerika nchi ye nye nguvu kutumia,chombo cha kutathmini nguvu kusimamisha maendeleo ya Iran kiteknolojia.
Hata hivyo , rais wa Amerika, alionya ikiwa Iran, inatakakuwa na uhusiano mzuri na Amerika na jumuia ya kimataifa ni lazima isimamishe mpango wake wa kuendeleza kuzalisha nguvu za kinyuklia.
Picha ya hapo juu, anaonekna rais, wa Amerika , Baraka Obama, akiongea katika moja ya mkutano na wandishi wa habari, wakati wa ziara yake ya kwanza katika bara la Ulaya tangu kuwa rais wa Amerika.
Picha ya pili , ni ya rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad, akiongea mara baada ya kufungua mtambo mpya wa kuendeshea nguvu za kinyuklia katika mjin wa Isfahan.
Utata wa kisiasa nchini Georgia, waleta mshaka kwa rais.
Tiblisi, Geogria -09/04/09 - Hali ya kisiaasa nchini Georgia imeendela kuwa ya utata , baada ya mamia ya fuasi wa vyama vya upinzani na viongozi wao wameaaandamana hadi kwenya maeneo ya bunge kwa madai razima rais Mikheil Saakashvili, ajiudhulu kutaka madarakani kwa kushindwa kutekeleza ahadi alizo zihaidi kabla ya uchaguzi nakuwa na ukilitimba wa madaraka.
Akiongea hayo wakati wa maandamano hayo,Levan Gachechiladze, ambaye alikuwa mgombea mpizani wa kiti cha urais wa Georgia, alisema watakaa mbele ya bunge mpaka hapo, rais atakapo sikiliza hoja za wananchi.
Hata hivyo wakati viongozi wa vyama vya upinzani wanafanya maandamano , rais Mikheil Saakashvili alikuwa akiwahutubia wanchi wa Georgia kwa kusisitiza umoja kwa wanchi wa Geogria,katika kumbukumbu za kuazimisha tangu, Georgia ilipo kwa moja ya nchi za umoja wa shirikisho za nchi za Kirashia.
Picha hapo juu , ni ya rais wa Georgia, Mikheili Saakshvili, anaye daiwa ajiudhulu toka madarakani na vyama vya upinzani.
Picha pili, wanaonekana wanchi wa vyama vya upinzani wakiandamana kuelekea kwenya ukumbi wa bunge kwa madai ya kuwa ni razima rais ajiudhulu.
Picha ya tatu , wanaonekana mamia ya waandamanaji wakiwa mbele ya bunge la Georgia, wakidai rais ajiudhulu,ndipo watatoka katika eneo hilo.
Wafuasi wa Al Sadr,wataka majeshi ya kigeni yaondoke.
Baghdad,Irak - 09/04/09 - Maelfu ya watu wameaandamana ,kwa madai ya kuwa jeshi la Amerika na washirika wake waondoke nchini humo.
Wafuasi na mwadau wa kiongozi wa Shia Murtada al Sadr, ambaye anajulikana kupinga kuwepo kwa majeshi ya kigeni, walionekana wakiwa wameshikilia mabango ya picha ya kiongozi huyo na huku wakidai ni lazima majeshi hayo ya kigeni yaondoke.
Waandamanaji hao wakikusanyika katika mnara wa aliyekuwa rais wa Irak , hayati Saddam Hussein, ambapo mnara huo, uling'olewa na jeshi la Amerika,mara baada ya kufanikiwa kuianguha serikali ya rais Saddam Hussein.
Irak,imekuwa chini ya majeshi ya kigeni kwa kipindi cha miaaka sita, tangu kuuangushwa kwa aliyekuwa rais wa Irak, Saddam Hussein na jeshi la Amerika na washirika wake.
Picha hapo juu wanaonekana waandamanaji wakiwa wameshikilia mabango na bendera katika moja ya mtaa mjini Baghadad.

Wednesday, April 8, 2009

Rais wa zamani wa Peru aongezewa miaka 25 zaidi kukaa jela.

Tetemeko la ardhi la leta maafa nchini Itali.

Rome Itali - 08/04/09.Idadi ya watu waliokufa kutokana na maafa ya tetemoko la ardhi lililo tokea katika mji wa L'Aquila mji uliopo karibu na Rome wamefikia 260.
Kwa mujibu wa wafanyakazi wa shirika la msalaba mwekundu, kunaidadi ya watu 30,000, ambao wamepoteza makazi yao kutokana ma tetemeko hilo lililo kuwa na nguvu ya 5.6 magnitude.
Meya wa L'Aquila, alisema tetemeko hilo lilitokea usiku wa manane wakati watu wakiwa wa melala.
Picha hapo juu, yanaonekana matenti ambayo yanatoa huduma ya kwanza kwa watu walio kutwa na maafa.
Picha ya pili anaonekana, mmoja ya wahudumi wa huduma ya kwanza akijaribu kumtuliza mmoja mkazi aliyekumbwa na maafa.
Rais wa zamani wa Peru, aongezewa miaka 25 zaidi kukaa jela.
Lima,Peru - 08/04/09.Mahakama nchini Peru, imetoa adhabu ya kifungo cha miaaka 25, kwa rais wa zamani wa nchi hiyo Alberto Fujimori ambaye kwa sasa anamiaka 70.
Rais huyo wa zamani, ambaye kwa sasa,alikuwa anatumika kifungo cha miaka sita baada ya kukutwa na hatia katika kesi ya awali.
Hukumu hiyo ,ilitolewa baada ya mahakama kumkuta na hatia ya kuhusika na mauaji, utekaji nyara, na kukiuka haki za binadamu wakati alipo kuwa madarakani wakati wa miaka ya 1990s.
Hata hivyo , rais huyo wazamani amekuwa akikana mashitaka yake hayo. Picha ya hapo juu anaonekana, rais wa zamani wa Peru, akiongea enzi za utawala wake alipokuwa rais wa Peru.
Picha ya pili, anaonekana mmoja ya wapenzi na mdau wa uongozi wa rais wa zamani wa Peru,akilalamika kwa uchungu mara baada kuhukumiwa na mahakama nchini Peru.
Hali ya kisiasa nchini Thailand yaanza kuyumba tena.
Bang Kok,Thailand - 16/04/09. Waandamaji wanazidi kuandamana nchini Thailand, kudai waziri mkuu Abhisit Vejjajiva, ajiudhulu kutoka madarakani.
Waandamaji hao wapatao 300,000, waliovalia shati za rangi nyekundu, walionekana wakiwa na mabango, huku wakidai wanataka waziri wao wa zamani, Thaksi Shinawatra aliyepo ukimbizini, arudishwe madarakani.
Picha hapo juu, anaonekana mmoja wa waandamanaji anaonekana akipiga kerere kudai serikali ijiudhulu.
Picha ya pili, wanaonekana waandamaji wakielekea mjini kuandamana.

Sunday, April 5, 2009

Baraka .H.Obama atangaza kupunguzwa kwa siraha za nyuklia duniani.

Korea ya Kaskazini yarusha chombo chake angani.

Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 04/04/09.Serikali ya Korea ya Kaskazini, imetangaz rasmi yakuwa imefanikiwa kurushwa chombo chake angani saa 0029GMT na kwa sasa kinazunguka dunia.
Chombo hicho kilichorushwa katika kituo cha sayansi cha Musudan- ri, kinasemekana kilipita katika maeneo ya Japan kuelekea maeneo ya Bahari ya Pasifiki.
Kwa mujibu wa serikali ya Korea ya Kaskazini, chombo hicho nikwa ajili ya mawasiliano, na hakipo anga kwa matumizi ya kivita.
Hata hivyo, kurushwa kwa chombo hicho angani na Korea ya Kaskazini, kumeleta wasiwasi, kwa jumuiya ya kimataifa, kwani Korea ya Kaskazini, imekiuka moja ya sheria za kimataifa,kwa mujibu wa msemaji wa Umoja wa Mataifa.
Picha hapo juu wanaonekana , baadhi ya wana nchi wa Korea ya Kaskazini, wakiangali kwa makini, chombo cha anga kilicho rushwa na walaataamu wa nchi yao.
Picha ya pili, ni ya chombo, cha kurushia mitambo angani, kikiwa tayari kurusha chombo angani, ambacho kipo angani kwa sasa, kwa mujibu wana sayansi wa anga.
Baraka .H.Obama, atangaza kupunguzwa kwa siraha za nyuklia dunia.
Prague,Chech -04/04/09. Rais wa Amerika Baraka .H. Obama, amesema serikali yake itafanya kila jitihada ili kupunguza matumizi ya nguvu za kinyuklia kwa ajili ya kutengeneza siraha, ambazo zitakuja kuleta maangamizi hapo baadaye pindipo zikipitia kwenye mikono potofu.
Rais, Baraka .H. Obama,akiwahutubia maelfu, alisema ni muhimu kwa Amerika kuanza kuongoza katika swala hili la kupunguza siraha za nyuklia, kwa ilisha wahi kutumia siraha hizo, na nilazima nchi nyingine zifuate mfano huo wa Amerika wa kupunguza siraha za nyuklia.
Rais , Obama, alisema ingawaje maangamizi hayo hayatokea wakati wa uhai wake , lakini ni lazima yaanze mara moja, na atahhakikisha serikali yake, itakuwa mstari wa mbele, kwani kwa kufanya hivyo ni kwa manufaa ya vizazi vijavyo.
Picha hapo juu anaonekana, rais wa Maerika , Baraka .H.Obama, akihutubia maelfu waliokuja kumlaki na kumsikiliza, akiongea kuhusu hali halisi ya mabadiliko ambayo walimwengu wanatakiwa kuyafanya ili kuokoa dunia mna mzingira yake yasiharibike, na yatunzwe kwa kizazi kijacho.
Picha ya pili wanaonekana, maelfu waliokuja kumsikiliza rais wa Amerika, Baraka Obama, badaa ya hutuba yake anaonekana rais Baraka .H.Obama, akiwasalimia wananchi kwa kuwapungia mikono.
NATO yatimiza miaka 60 tangu kuanzishwa"Afghanistan bado kitendawili".
Strasbourg,Ufaransa - 03/04/09.Viongozi wa NATO wakiwa wanaadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa kwa NATO, wamekutana nchini Ufaransa, ili kujadili hali halisi ya Afghanistan na kutathmini, mafanikio ya demokrasi yanavyo endelea nchini humo.
Katika kikao hicho viongozi hao wote kwa pamoja walikubalina ni muhimu kujenga Afghanistan, na kuahakikisha hatakuwa tena kwenye mikono ya utawala wa Taliban,na mafanikio hayo yataletwa ikiwa nchi wanachama zitashirikiana kwa zati.
Vilie vile viongozi wa NATO walijadili ni jinsi gani watashirikiana na nchi nyingine ambazo siyo wanachama wa NATO, ili kuweza kuushinda ugaidi unaosumbua dunia.
Picha hapo juu, wanaonekana mawaziri wanchi za nje wakisaini kwa mara kwanza kukubali k,uanzishwa kwa NATO 4/04/1949.
Picha ya pili, anaonekana katibu wa sasa wa NATO, Jaap de Hoop Scheffer, akihutubia viongozi wa nchi wanchama wa NATO, kabla ya kuanza kikao rasmi.
Picha ya pili wanaonekana viongozi wa nchi wanchama wa NATO, wakiwa wamepiga picha kwa pamoja kabla ya kuanza mazungumzo na mjadara wa kuimarisha NATO, tangu miaka 60 ilipo anzishwa.
NATO yapata katibu mpya"Baada ya Uturuki kuridhika".
Brussel, Ubeligiji,03/04/09 - Waziri mkuu wa Denmark Anders Fogh Rasmussen, amechaguliwa kuwa katibu mkuu wa shirikisho la jumuia za nchi zinazo shirikiana kiulinzi na usalama wa nchi wanachama wa Amerika na Ulaya - NATO.
Anders Rasmussen, atachukua ofisi abayo hapo mwanzo ilikuwa ikiongozwa na Jaap Scheffer, ambaye muda wake wakuongoza unakwisha mwezi wa julai (Saba).
Hata hivyo kuchaguliwa kwake, kumekuja baada ya Uturuki, kukubaliana na nchi wanachama,kwani Uturuki ilikuwa ikitaka maelezo zaidi na uhakika kutoka kwa nchi wanchama yakuwa Anders Rasmussen, hatakuwa na msimamo aliyo weka wakati mmoja ya magazeti nchini mwake 2005 yalichapisha picha ta kumkashifu Mtume Muhammed,na hakuchukua hatua kali dhidi ya wahusika.
Nabaada ya nmaelezo ya kutosha ndipo Anders Fogh Rasmussen, alichaguliwa , na anatarajiwa kuanza kazi rami mwezi wa saba 2009.
Picha hapo juu , anaonekana waziri mkuu wa Den Mark, Anders Fogh Rasmussen, akiongea katika moja ya mikutano ya kimataifa ,kujadili hali ya dunia na maendeleo yake.