Wednesday, February 29, 2012

Korea ya Kaaskazini kusimamisha uzalishaji wa kinyuklia.

Korea ya Kaaskazini kusimamisha uzalishaji wa kinyuklia.

Pyong Yang, Korea ya Kaskazini - 29/02/2013. Serikali ya Korea ya Kusini imekubali kusimamisha mpango wake wakuendelea uzalishaji  wa nguvu kinyuklia.
Habari zakusimamishwa kwa uzalishaji huo wa nguvu za kinyuklia nchini Korea ya Kaskazini zilitangazwa na shirika la habari la nchi hiyo.
Hata hivyo Marekani imesifu uamuzi huo lakini kudai yakuwa bado inalitizama kwa makini.
Korea ya Kusini imekuwa ikisitasita mara kwa mara kushiriki katika mkutano wa nchi sita, Korea ya Kusini, Korea ya Kaskazini, China, Japan, Urusi na Marekani ili kujadili maswala ya kinyuklia zidi ya nchi hiyo.

Monday, February 27, 2012

Wawili wakamatwa kwa kuwa na mipango ya mauaji ya Vladmir Putin

Ujerumani yakubali kuipa pesa Ugiriki.

Born, Ujerumani - 27/02/2012. Bunge la Ujerumani limepiga kura ya ndiyo kwa wingi ambapo itaruhusu kwa serikali ya Ujerumani kutoa pesa ili kusaidia Ugiriki.
Kura 496 ziilikubaliana na azimio ilo na 90 zilipinga.
Serikali ya Ugiriki inahitaji zaidi ya euro130 billion ili kuweza kuinua uchumi wake ambao upo njiani kuporomoka.

Wawili wakamatwa kwa kuwa na mipango ya mauaji ya Vladmir Putin.


Moscow, Urusi - 27/02/2012. Watu wawili wanshikiliwa na vyombo vya uslama baada ya kupatikana kuwa na njama za kutaka kumwua waziri mkuu wa Urusi.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana kutoka katika ofisi za usalama za Urusi na Ukraini " zinasema watu hao walikuwa wapepanga kufanya mauaji hayo na mashambulizi mengine mara baada ya uchaguzi wa urais unotarajiwa kufanyika hivi karibuni.
Watu hao wawili waliomo mikononi mwa vyombo vya usalama wanaaminika walipata amri hiyo kutoka kwa kiongozi wa kundi la Chechen Doku Umarov.

Wasyria  wakubali mabadiliko ya kisiasa na bursara za Kofi Annan zasubiriwa.


Damascus - Syria - 27/02/2012. Wananchi wa Syria wamepiga kura ya ndiyo ili kufanyika kwa mabadiliko ya mfumo wa kisiasa nchini humo.
Serikali ya rais Bashar al Assad, ili tisha kura za maoni ili kutaka kujua ya kuwa kama wananchi wa Syria watakubaliana namabadiliko ya mfumo mzima wa kisiasa.
Mataokeo ya kura zilizo pigwa  nchini kote zimeleta matokeo ya kuwa asilimia 90 ya wapigakura wamekubalia na mabadiliko ya kuwa mfumo wa sasa wakisiasa wa chama kimoja ubadilishwe.
Kufuatia matokeo hayo ya kura, Syria imefikia mwisho wa kuwa na chama kimoja na milango ya vyama vingi umefunguliwa rasmi.
Huku mabadiliko ya kisiasa yakiwa yapo njiani, katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan aliteuliwa na katibu mkuu wa sasa wa umoja wa Matifa,  ilikusaidia kuleta suruhu za kisiasa nchini Syria.
Syria imekuwa katika hali ya vurugu za kisiasa kwa kipindi kirefu na kusababisha watu wengi kupoteza maisha kutokana na vurugu hizo.

Friday, February 24, 2012

Somalia bado kitendawili kwa jumuiya ya kimataifa.

Hugo Chavez kufanyiwa upasuaji nchini Kuba.

Caracas,Venezuela - 24/02/2012. Rais wa Venezuela amewasili nchini Kuba ili kufanyiwa upasuaji.
Rais, Hugo Chavez 57 ambaye hapo mwazo alifanyiwa upasuaji ili kuondoa uvimbe wa kansa nchini Kuba, aliwaambia wanchi ya kuwa " kwa mara nyingine tena nipo vitani na nitashinda na kuishi vyema"
Wataalamu wa mambo ya kisiasa nchini Venezuela wamekuwa wanaulizana  kama rais Chavez ataweza kuongoza nchi tena kama akichaguliwa katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi wa Oktoba 2012.
Somalia bado kitendawili kwa jumuiya ya kimataifa.


Dadaab, Kenya - 24/02/2012. Wakimbizi wanao tokea Somalia wapo hatarini, baada ya  misaada ya kiutu iliyo tolewa kukaribia kuisha.
Dadaab ni kambi kubwa duniani ambayo ina wakimbizi zaidi ya 500,000 kutoka Somalia na inaaminika ya kuwa kuna wakimbizi ambao wameishi hapo zaidi ya miaka 15.
Kutoka kwa habari hizo kumekuja siku moja baada ya viongozi kukutana jijini London na kuweka mikakati mikubwa ya kupambana na makundi yanayo vuruga amani nchini Somalia.

Wednesday, February 22, 2012

Rais wa Afghanistan aomba utulivu baada ya vitabu vya dini kuchomwa moto.

Rais wa Afghanistan aomba utulivu baada ya vitabu vya dini kuchomwa moto.

Kabul, Afghanistan - 22/02/2012. Rais wa Afghanistan amewataka wanachi wa Afghanistan kuwa watulivu na kutondelea na vurugu baada ya vitabu vya dini kuchomwa moto.
Rais Hamid Karzai alisema " naomba watu wausalama wasitumie nguvu, ila walinde usalama wa raia na vitu vyao."
Ombi hilo la rais wa Afghanistan limekuja baada ya kugundulika ya kuwa baadhi ya wanajeshi wa Marekani waliopo nchini Afghanistan walichoma vitabu vya dini Kiislaam - Koroani, baadaya ya kuvikusanya na kuondoka navyo kutoka kwenye jela moja  inayowashikilia wapiganaji wanahusika na kundi la Taliban wakati  waliopokuwa wakifanya uchunguzi ni mbinu gani zinatumika katika mawasiliano kati ya wapiganaji wa kundi la Taliban.
Serikali ya Marekani kupitia wakuu wa jeshi  imeomba msamaha kwa kitendo hicho kwa kusema  " tukio hilo siyo zuri na siyo msimamo wa jeshi la Marekani, kwani jeshi la Marekani linaheshimu dini zote."
Hata hivyo vuguvugu la maandamano kufuatia kuchomwa huko kwa Koroani bado linanendelea nchini Aghanistan kwa madai walio husika wawekwe mbele ya vyomba vya sheria.

Ugiriki yaopolewa na nchi wanachama.
Brussels, Ubeligiji - 22/02/2012. Jumuia ya nchi za Ulaya imekubalia kuipataia Ugiriki pesa nyingine ili kuinua uchumi.
Makubaliano hayo yalikuja baada ya Ugiriki kutimiza masharti ambayo ilitakiwa kuyatimiza.
Kufuatia kutimiza makubaliano hayo Ugiriki itapatiwa pesa kiasi cha dolla za Kimarekani $170billion ambazo zitaiwezesha serikali ya Ugiriki kuimarisha uchumi wake ambao ulikuwa umesha fikia kiwango cha kuporomoka.

Iran na IAEA zapishana mawazo.
Tehran, Iran - 22/02/2012. Wakaguzi wa maswala ya kinyuklia ambao wapo nchini Iran, wamekataliwa kutembelea eneo la kijeshi.
Mkurugenzi mkuu wa shirika linalo simamia maswala ya kinyuklia - IAEA International Atomic Energy Agency, Yukiya Amano alisema " tunasikitika ya kuwa wakaguzi wetu hawakuruhusiwa kutembelea eneo la Parchin ambalo linahusika na utaalamu wa maswala ya kijeshi."
Hata hivyo, mkuu wa maswala ya kinyuklia wa Iran, Ali Asghar Soltanieh alisema " tumeongea mambo mengi ya kujenga na natumaini tutakapo kutana tena tutaendelea kujadiliana kwa undani."
Wajumbe wa IAEA waliwasili nchi Iran kwa mara ya pili katika kipindi kisicho pungua mwezi mmoja ilikujadilia na serikali ya Iran katika maswala ya kinyuklia, jambo ambalo Iran imekuwa ikidai yakuwa inafanya maendeleo ya kinyuklia kwa ajili ya kukuza utafiti wa kisayansi.

Mji wa Baidoa nchini Somalia warudi mikononi mwa serikali.
Baidoa, Somalia - 22/02/2012. Majeshi ya Somalia na Ethiopia yamweza kuukamata mji wa Baidoa, ambao hapo mwanzo mji huo ulikuwa chini ya kundi la Al Shabab.
Baidoa mji ambao upo km 250 kutoka Mogadishu umekuwa chini ya kundi la Al Shabab na kusadikiwa kuwa kituo chao kukuu cha kupanga mikakati yao.
Masemaji wa jeshi la serikali ya Somalia Muhidin Ali alisema " majeshi ya serikali na Ethipoa yameweza kuutwaa mji wa Baidoa bila hata risasi moja kulia na maadua walikimbia mji kabla ya jeshi letu na la Ethiopia kuukamata mji huo, na watu wa mji huu wametukaribisha kwa shangwe."
Kukamatwa kwa mji wa Baidoa kumekuja  wakati Umoja wa mataifa umepitisha azimio la kuongeza msaada kwa jeshi la Umoja wa nchi za Afrika, ili kudumisha amani zaidi.

Monday, February 20, 2012

Waziri Mkuu wa Uingereza aombwa kupamabana na vilevi.

Waziri Mkuu wa Uingereza aombwa kupamabana na vilevi.
London, Uingereza - 20/02.2012. Wataamu wa afya nchi Uingereza wametahadhrisha madhara ya unywaji wa pombe katika jamii na kuonya yakua inasabaisha vifo vingi na kuhatarisha jamii.
Wataalamu hao wa afya ambao walifatilia na kufanya utafiti wa madhara ya pombe kwa jamii  walimwandikia barua Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron kutafuta mbinu mpya za kudhibiti unywaji wa pombe ambao umeongezeka katika jamii ya Waingereza.
Wakiongozwa na Profesa Ian Gilmore wataalamu hao walitoa ripoti inayosema "unywaji wa pombe umekuwa ukichangia kwa kiasi kikubwa katika magonjwa ya ini, msukumo wa damu, kupooza, magojwa ya moyo, kansa na magonjwa sugu kudumu na wanywaji wengi kuhusika na vurugu katika jamii."
Ripoti hiyo imekuja baadaya ya baadhi ya viongozi wa dini na wanasaiasa kudai serikali iangalie upya sheria za vinywaji vyenye vilevi, kwa ni idaiwa vilevi vimekua chanzo cha jamii nyingi kukosa amani.
 Waziri Mkuu wa Urussi ataka nguvu za kijeshi la nchi  ziongezwe.
Moscow, Urussi - 20/02/2012. Serikali ya Urussi imehaidi kuongeza nguvu za kijeshi, ili kuimarisha ulinzi wa nchi hiyo.
Waziri Mkuu Vladmir Putin alisema " nilazima kuimarisha nguvu za kijeshi ili kuweza kuilinda nchi yetu."
Kwamujibu wa habari zilizo patikana zinasema Urussi inatarajiwa kutumua zaidi ya £487billion ili kuimarisha maswala ya ulinzi wa nchi hiyo.
Putin ambaye anagombea kiti cha Urais wa Urussi mapema mwezi wa Machi mwaka huu alishawahi kuwa rais wa Urussi kabla ya kuchukua ka waziri mkuu wa Urussi.
China ya onya kuhusu ni ya  mashambulizi zidi ya Iran.
Beijing, China - 20/02/2012. Serikali ya China imepinga kitendo chochote cha mashambulizi zidi ya Iran na kudai yakuwa kutafanya eneo zima la Mashariki ya Kati kuwa na vurugu kumbwa.
Waziri wa mambo ya nje wa China Hong Lei alisema " gtumekuwa siku zote tunapinga vitendo vya kutishia vita  kati ya mataifa au taifa kwa taifa na huu ndoyi msimamo wetu."
Onyo hili kutoka serikali ya China,limekuja baada ya baadhi ya viongozi wa siasa nchini Marekani kudai hagtua za kijeshi itabidi zichukuliwe zidi ya Iran kwa kitendo chake cha kuendeleza mradi wa kinyuklia.
Hata hivyo serikali ya Iran imehaidi yakuwa kitendo cha nchi yoyote kuishambulia Iran basi Iran itajibu kwa nguvu zote mashambulizi hayo.

Saturday, February 18, 2012

Maelfu waamuaga Whitney Houston.

Maelfu waamuaga Whitney Houston.

New Jersey, Marekani - 18/02/2012. Zaidi ya watu 1.500, ndugu, marafiki na jamaa wameudhuria misa ya mazishi ya mwana mama nyota wa muziki wa pop Whitney  Houston  48 ambaye alifariki hivi karibuni.
Katika kumwaga mwanamuziki Whitney Houston, wanamuziki maarufu duniani  akiwepo Stevie Wonder, waliimba nyimbo tofauti ikiwa ni heshima zao za mwisho kwa mwanamuziki huyo.
Whitney Haouston alikutwa amefariki dunia wiki iliyo pita katika hotel ambayo alikuwa amefikia katika jiji la Los Angeles.
Polisi nchini Senegal wapambana na waandamanaji.


Dakar, Senegal - 18/02/2012. Polisi wa kuzuia ghasia nchini Senegal wameshambuliana na wananchi katika jiji la Dakar baada ya kupinga agizo la serikali ya kutaka wasifanye maandamano.
Mashambulizi hayo ya polisi  yalitokea mara baada ya waandamanaji kuandamana kupinga kitendo  rais wa sasa wa Senegal kugombea kiti cha urais wa nchi hiyo kwa mara ya tatu.
Vurugu hizo zimekuja ikiwa zimebakia siku chache kabla ya  kufanyika uchaguzi wa urais ambapo rais wa sasa Abdoulaye Wade anagombania kiti hicho kwa mara nyingine.
Meli ya jeshi la Iran yavuka mfereji wa Suezi kwa mara ya pili.


Tehran, Iran - 18/02/2012. Meli za kivita za  jeshi la Iran zimeonekana katika bahari ya Mediteraniana na kuvuka mfereji wa Suez.
Mkuu wa msafara huo wa meli za kijeshi za Iran Habibollah Sayari alisema " niya ya safari hii nikuonyesha nguvu za  kiamani na urafiki."
Meli hiyo ya kijeshi inayojulikana kwa jina la  Shahid Qandi imekuwa ya pili tangu Iran kufanya mapinduzi mwaka 1979.
Msafara huo ambao haukutajwa kuelekea wapi,umekuwa wa pili kufuatia ule wa kwanza uliofanywa Februari mwaka jana.
William Hague  vita vipya vya baridi huenda vikaibuka.


London, Uingereza - 18/02/2012. Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza ameeleza wasiwasi wake kuhusu maendeleo ya kinyuklia yanayo fanywa na Irani.
Willam Hague alisema " kutokana na mpango wa kinyuklia unaoendelea nchini Iran, kunaweza kuwa chanzo cha mashindano mapya ya vita baridi, na hii inazewa leta hatari katika jumuiya ya kimataifa.
"Ikiwa Iran itakuwa na uwezo wa kutengeza mabomu ya kinyuklia basi kutafanya nchi nyingine katika maeneo ya Mashariki ya Kati kujidhatiti na kuanza miradi ya kinyuklia."
Iran nchi ambao imekuwa ikitakiwa na nchi za Ulaya Magharibi na Marekani kuiachana na mpango wake wa kuendeleza maradi wa kinyukia imetangaza hivi karibuni kufanikiwa kuzalisha nguvu mpya za kinyuklia ambazo zitatumika katika utafiti wa kisayansi na kudai yakuwa haina mpango wa kutengeneza mabomu ya kinyuklia.
Nikolas Sarkozy kugombea tena kiti cha urais wa Ufaransa.
Paris, Ufaransa - 18/02/2012. Rais wa sasa wa Ufaransa ametamgaza hivi karibuni nia yake yakugombania tena kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao mwaka huu.
Nikolas Sarkozy ambaye muhula wake wa kwanza wa urais unafikia ukingoni alitangaza kwa kusema "ikiwa kama sitagombani nafasi hii ya urais itakuwa kama kususa uongozi, hivyo nitagombania tena kiti hichi ili kukamilisha yale yote ambayo hatujayakamilisha kwa sasa"
Uchaguzi huo ambao unatarajiwa kufanyika mapema wakati wa mwanzo wa kipindi cha kiangazi mwaka huu, utakuwa ni mthiani mkubwa kwa rais Nikalas Sarkozy, kwani maoni ya kura bado yanaonyesha yakuwa bado anakazi kubwa ya kuwashawishi wapiga kura kumchagaua.


Thursday, February 16, 2012

Aliyetaka kulipua ndege siku ya Krimasmas ahukumiwa kukaa maisha jela.

Aliyetaka kulipua ndege siku ya Krimasmas ahukumiwa kukaa maisha jela.
Detroit, Marekani - 16/02/2012. Mahakama nchini Marekani imetoa adhabu ya kukaa jela maisha kwa mshitakiwa ambaye alitaka kuilipua ndege iliyo kuwa ikielekea Marekani wakati wa siku ya Krismas 2009.
Mtuhumiwa huyo, Umar Farouk Abdul Mutallab ambeye alifanikiwa kuingia kwenye ndege ilikuilipua ndege hiyo ikiwa hewani kwa kutumia mabomu ambayo ailikuwa ameyavaa mwilini.
Mtuhumiwa huyo alikili kwa kusema " nilichukua mabomu ili kulipiza kisasi zidi ya serikali ya Wamarekani."
Hukumu hiyo ya kifungo cha maisha Jaji Nancy Edmunds baada ya kukutwa na hatia ya kutaka kuwauwa watu ambao walikuwepo kwenye ndege kuelekea Dertoit.

Iran yatangaza maendeleo ya kinyuklia.
Tehran, Iran - 16/02/2012. Serikali ya Iran imetangaza hivi karibuni kufanikiwa kutengeneza keki ubinjani ambayo itatumika katika kuimarisha nguvu za kufanya utafiti wa magonjwa.
Rais wa  Iran Mahmoud Hamedenejad alisema " Iran ipo tayari kushirikiana na nchi nyingine katika maswala ya kisayansi ili kupambana na magonjwa yanayo hatarisha maisha ya binadamu."
Uamuzi wa serikali ya Iran kutangaza maendeleo ya kinyuklia kumelaaniwa na nchi za Magharibi na Marekani na kudai ya kuwa "Iran haipo wazi katika maswala yake ya kinhyuklia."
Hata hivyo serikali ya Iran imekuwa ikikanusha madai hao, na kusema mpango wake wakinyuklia ni kwa aajili ya kukuza maendeleo ya kisayansi.

Umoja wa  Wajumbe wa  Umoja wa Mataifa wavutana juu ya Syria.
New York, Marekani- 16/02/2012. Mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa umelaani kwa pamoja matendo ya ukiukwaji wa haki za binadmu yanayo tokea nchini Syria na kupiga kura kupitishwa muswaada wa kutaka kusimamishwa mara moja vitendo hivyo.
Kura hizo zilizo pigwa 137 ziliaani  hasa vitendo vya serikali ya Syria chini ya rais Bashar al Assad didi ya 12 ambazo hazikubaliana na mswaada huo na kura 17 hazikupigwa.
Urusi, China na Iran zilipinga mswada huo kwa madai ya kuwa muswaada huo haukamilika kwani ulikuwa haulaani vitendo ya majeshi pinzani yanayopingana na serikali ya Syria.
Rais wa Syria Bashar al Assad amepitisha mswaada wakuundwa kwa katiba mpya itakayo husisha vyama vingi jambo ambalo vyama vya upinzani havikubaliani navyo.
Uamuzi wa kupigwa kura hiyo kumekuja baada ya mswaada mpya wa nchi za jumuiya za Kiarabu kutaka jitihada zaidi zifanyaike ili kuilazimisha serikali ya Bashar al Assad iachie madaraka na kuipisha serikali ya kidiplomasi itakayo chaguliwa na wananchi wa Syria.

Tuesday, February 14, 2012

Mkuu wa jeshi wa Urusi aonyo kuwepo mashambulizi nchini Iran .


Izrael yailaumu Iran baada ya mashambilizi nchini India, Thailand na Georgia.
Tel Aviv, Izrael - 14/02/2012. Serikali ya Izrael imeilaumu serikali ya Iran kufuatia mashambulizi ya mabomu yaliyo tokea nchini India,Georgia na Thailand.
Heud Baraka ambaye ni waziri wa ulinzi wa Izrael alisema "mashambulizi yaliyo tokea yanaonyesha yakuwa Iran inafanya vita bubu zidi ya Izrael na mashambulizi haya ni ushaidi fika.
"Iran na Hezbollah wanashirikiana katika kuvuruga amani katika eneo la Mashariki ya Kati na dunia nzima."
Hata hivyo serikali ya Iran imekanusha kuhusika na mashamulizi hayo.
Mashamulizi zidi ya maofisa wa Kiizrael waliopo nchini India, Georgia na Thailand yametokea kwa kufuatana katika nchi hizo.
Hata hivyo Iran  ilishailaaumu Izrael kuhusika na mashambulizi zidi ya wanasayansi wake wanaohusika na maswala ya kinyuklia hivi karibuni ambayo yalitokea nchi Iran.
Na serikali ya Izrael ilikataa kuhusika na mashambulizi hayo.
Mkuu wa jeshi wa Urusi aonyo kuwepo mashambulizi zidi ya Iran.


Moscow, Urusi - 14/02/2012. Mkuu wa jeshi la Urusi ameonya yakuwa kuna kunampango wa kuishambulia Iran hasa kwenye maeneo ya viwanda vya nyuklia.
Meja Generali Nikolai Makarov alisema " Urusi inaangalia kwa makini swala hilo kwani upo uwezekano Iran kushambuliwa na uamuzi wa kufanya mashambulizi unaweza fanyika wakati wa kiangazi mwaka huu."
Mashambuli nchini Iran yamekuwa yakiongelewa na hasa kwa serikali ya Marekani kusema " uamuzi wowote juu ya Iran unaweza fanyika ikiwemo wa kivita."
Hata hivyo sertikali ya Iran ilishasema " ikiwa nchi yoyote itaishambulia Iran, basi Iran itajibu na majibu yake yatakuwa hayana mfano na maadhara yake yatakuwa makubwa."
Mvutano na malumbano ya kidiplomasia kati Iran na nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani umezidi kuongezeaka baada ya serikali ya Iran kutangaza yakuwa itafunga mfereji wa Strait Hormuz ikiwa itaona vikwazo vitahathiri uchumi wa Iran, jambo ambalo limezifanya nchi za Magharibi kupeleka maadhi ya maanuali zake za kijeshi karibu na eneo hilo.
Uingereza yafanya mazungumzo kumrudisha Abu Qatada nchini Jordan.
London, |Uingereza - 14/02/2012. Serikali ya Uingereza inafanya mazungumzo na serikali ya Jordan ili kupata huakika juu ya kurudishwa kwa mshukiwa Abu Qatada.
Kwa mijibu wa hamari kutoka ofise ya  mambo ya ndani zinasema "James Brokenshire, ambaye ni amewakilisha serikali ya Uingereza yupo nchini Jordan ili kuishawishi serikali ya nchi hiyo kukubali kmpokea Abu Qatada ambaye anshukiwa kuwa mtu hatari katika jamii ya Kiingereza.
"Serikali ya Uingereza itatumia kila minzi zilizopo ili kuwezesha kurudishwa kwa Abu Qatada."
Uamuzi wa serikali ya Uingereza kufanya mazungumzo na serikali ya Jordan juu ya Abu Qatada kumekuja  baada ya mahakama ya nchi wanachama wa jumuiya ya  Ulaya kukataa ombi la serikali ya UIngereza la kutaka Abu Qatada arudishwe nchini Jordan.
Mahakama hiyo ilisema " Kufuatia hali iliyopo nchini Jordan Abu Qatada hatapata haki na kesi yake haitakuwa halali kwani ushahidi utakao tumika ulipataikana kwa mateso na minyanyaso, ambayo inakwenda kinyume cha haki za binadamu na sherika za nchi wanachama wa Ulaya."
Abu Qatada aliachiwa kutoka jela kwa dhamana baada ya kukaa jela kwa muda mrefu bila kuhukumiwa  na ambaye anashukiwa kuwa mtu muhimu kwa kundi la Alqaeda na hasa kuwa mtu wa karibu na aliyekuwa mkuu wa kundi hilo hayati Osama bin Laden .
Taliban yakataa kukutana na serikali ya Hamid Karzai.

Kandahar, Afghanistan - 14/02/2012.  Kiongozi wa kundi la Taliban amekataa ya kuwa wanaweza kushirikiana na serikali ya Aghanistan kwa madai yakuwa serikali hiyo siyo halali.
Zabiullah Mujahidi ambaye ni msemaji wa kundi la Taliban alisema " hatuwezi kukaa  na kuongea na kundi la Taliban ambayo inaongozwa na Hamid Karzai.
Na hatujawahi kuulizwa wala kualikwa kuudhuria mazungumzo na serikali ya Karzai na hakuta kuwepo na uwezekano huo kwani serikali hiyo ni ya kibaraka na nikitu ambacho hakiwezekani kuongea na serikali ya kibaraka.
"Hata hivyo tumesha pata mwaliko wa kuongea na serikali ya Marekani, lakini hata hivyo kama  serikali ya Karzai atahusishwa basi hatutashiriki."
Mswada wa kukutanisha serikali ya Afghanistan inayo ongozwa na Hamid Karzai na kundi la Taliban ambao umekuwa ukiandaliwa na serikali ya Marekani ili kujaribu kusimamisha vita nchini Afganistan, vita ambavyo vimekuwa vikipigwana kwa muda mrefu sasa kati ya kundi la Taliban na serikali ya Afghanistan.


Monday, February 13, 2012

Zambia yachukua ubigwa wa kombe la Afrika katika soka.

Zambia yachukua ubigwa wa kombe la Afrika katika soka.

Libreville, Gabon - 13/02/2012. Timu ya taifa ya Zambia imechukua ubingwa wa kombe la Afrika baada ya kuifunga Ivory Coast kwa penati 8 kwa 7.
Mechi hiyo ambayo ilichezwa huku kila timu ikitumia mbinu karibu zilizo fanana ili kutafuta ili bidi ichezwe kwa dakika 120 na baadaye kulekea kwenye penati na hatima yake Zambia kuibuka na ushindi.
Ushindi  wa Zambia nchini Gabon umekuja  na kuleta kumbukumbu kubwa kwa Wazambia kwani ufukwe wa bahari  wa nchi hiyo uliwapoteza viongozi na wachezaji wa timu taifa ya Zambia baada ya kupata ajali ya ndege.
Greeki yapiga kura kufanya mabadiriko ya  kiuchumi.

Athens, Ugiriki - 13/02/2012. Bunge la Ugiriki  limepiga kura na kupitisha mswada ambayo utaifanya serikali ya Ugiriki kubadili sheria ili kuimarisha uchumi.
Mswada huo ambao ulipitishwa utaiwezesha serikali ya Ugiriki kuweza kupata pesa kutoka  mfuko wa  jumuiya ya Ulaya.
Hata hvyo wakati wa mpango wa kupiga kura hiyo, zaidi ya watu 100,000 walikuwa mamesimama nje ya bunge hilo ili kupinga mswada huo, jambo ambalo lilisababisha vurugu kati ya waandamanaji na polisi wakuzuia ghasia.
Sudani ya Kusini na serikali ya Sudan zakubaliana makubaliano ya amani.

Adis Ababa, Ethiopia - 13/02/2012. Serikali ya Sudani ya Kusini na Serikali ya Sudan zimetiliana sahihi mkataba wa makubaliano kati ya nchi hizo  kuhusu  maeneo yaliyopo kati ya mipaka hiyo.
Mkataba huo ambao ulitiwa sahii na mkuu wa maswala ya usalama wa Sunadani ya Kusini Thomas Douth na  mkurugenzi mkuu wa usalama wa Sudan Mohamed Atta.
Mkataba wa makubaliaono hayo yalisainiwa mbele ya rasi wa zamani wa Afrika ya Kusini Thabo Mbeki ambaye ni mkuu wa majadiliano hayo.
Kwenye makubaliano ya mkataba huo wa nchi zote mbili unazitaka "Sudani ya Kusini na Sudan uheshimu mipaka ya nchi hizo mbili na kutoshabuliana kijeshi."
Kwa mujibu wa habari ziliz toka katika mkutano huo zimesisitiz aya kuwa kinacho fuata ni mazungumzo juu ya ugawaji na uzalishaji wa mafuta yaliyopo nchini humo.




Sunday, February 12, 2012

Whitney Haustone afariki dunia.

Whitney Haustone afariki dunia.


Los Angeles, Marekani -12/03/2012. Mawanamuziki maarufu na aliyekuwa mcheza sinema amekutwa amefariki dunia katika hoteli aliyo kuwa amefikia katika mji wa Los Angeles.
Mark Rose ambaye ni msemaji wa polisi alisema "polisi ilipata habari yakuwa kuna mtu anamatatizo katika hoteli aliyofikia na tulipofika tukakuta ni Whitney Hauston 48.
Hata hivyo msemaji huyo wa polisi hakutoa maelezo nini chanzo cha kifo cha mwanamuziki huyo. 

Serikali ya mpito ya Libya yaingiwa na wasiwasi na kauli mtoto Muammar Gaddafi.




Tripoli, Libya - 12/02/2012. Serikali ya Libya imeiomba serikali ya Niger kumkabidhisha mtoto wa aliye kuwa rais wa Libya Muammar Gaddafi.
Maombi hayo ya serikali ya Libya, yamekuja baada ya Saad Gaddafi ambaye ni mtoto wa tatu wa rais aliyetolewa madarakani na kuuwawa na serikali ya Libya ambayo inatawala kwa sasa.
Mohamed Hareizi ambaye ni msemaji wa serikali ya mpito ya Libya alisema "tunaomba Saad Gaddafdi na iongozi wengine waliopewa hifadhi nchini Niger waudishwe nchini Libya ili kudumusha uhusiano mzuri na serikali hiyo kwani maoni iliyotoa Saad yana tishia usalama wa taifa."
Maombi hayo yamekuja baada ya Saada Gaddafi baada ya kudai ya kuwa Libya itakuba na mvurugo wa kisiasa hivi karibuni kwani na "mawasliano na watu nchini humo na wanadai ya kuwa hali iliyopo siyonzuri."
Saada Gaddafi yupo makimbilioni nchini Niger baada ya serikali ya baba yake  Muammar Gaddafi kuangushwa na serikali ya mpito kwa msaada wa jeshi la NATO.




Thursday, February 9, 2012

Viongozi wa Urusi na Ufaransa wajadili kwa simu hali ya Syria

Al - Shabab wajiunga  rasmi na Al Qaeda.

Mogadishu, Somalia - 09/02/2012. Kiongozi wa kundi la Al-Qaeda ametangaza rasmi kuwa kundi la AlShabab lililopo nchini Somalia limejiunga rasmi katika kundi lake.
Ayman al Zawahiri ambaye ni kiongozi wa mkuu wa Al Qaeda alisema " napenda kuwatangazia ya kuwa kaka zetu katika imani Al - Shabab wamejiunga rasmi na Al-Qaeda na tutashirikiana nao kwa kila hali."
Kundoa la Al- Shabab limekuwa likiongoza mashambulizi zidi ya serikalia ya Mogadishu kwa muda mrefu na kusababisha kutokuwepo na amani katika nchi ya  Somalia

Sudani ya Kusini yatafuta mbinu mpya ili kusafirisha mafuta yake

Juba, Sudan ya Kusini - 09/02/2012. Serikali ya Sudani ya Kusini imetiliana sahihi mikataba na serikali za Ethiopia na Djibouti ili kuwezesha kujenga mabomba ya mafuta ambayo yatapitishwa katika nchi hizo.
Mikataba hiyo ni ya pili baada ya ya ule wa kwanza ambao serikali ya Sudani ya Kusini ilisini mkataba na serikali ya Kenya ili kuweza kujenga mabomba ya mafuta baada ya kutokea mgogoro na serikali ya Khartoum.
Serikali ya Sudani ya Kusini ilitangaza kusimamisha  uzalishaji wa mafuta kwa madai ya kuwa serikali ya Khartoum - Sudan kuzidisha kodi na kuiba mafuta. 
Kwa mujibu wa habari kutoka ofisi ya mawasiliano ya Sudani ya Kusini zinasema " ujenzi wa mabomba hayo utachukua miaka mitatu na kugharimu zaidi ya paundi za Kiingereza £ 3billion.

Viongozi wa Urusi na Ufaransa wajadili kwa simu hali ya Syria.
Moscow, Urusi - 09/02/2012. Rais wa Urusi amefanya mazungumzo na rais wa Ufaransa ili kujadili hali halisi ya kisiasa na machafuko yanayo endelea nchini Syria.
Katika mazungumzo hayo rais wa Urusi Dmitry Medvedev na Nikolas Sarkozy wa Ufaransa waliongea kiundani na kujadili ni kwa kiasi gani ahaadi zilizotolewa na  rais wa Syri Bashar al Assad wakati alipo kutana na waziri wa mambo ya nchi za nje wa Urusi nchini Syria.
Mazungumzo hayo yamekuja huku Urusi ikionya haitakuwa jambo la busara kwa nchi za nje kuingilia maswla ya ndani ya Syria, kwani ni ya wa Syria wenyewe.

Hali ya usalama nchini Syria yazidi kuwa tete.



Homs, Syria - 09/02/2012. Jeshi la serikali ya Syria limezidisha mashambulizi katika mji wa Homs na kusababisha maafa makubwa.
Mashambulizi hayo makubwa ambayo yameanza siku sita zilizo pita ikiwa ni moja ya nia ya serikali ya Syria kupambana na wale wote wanao leta vurugu katika mji wa Homs.
Habari zinasema " karibu maeneo ya makazi ya watu  katika mji wa Homs yamealiwa vibaya sana."
Nazo habari kutoka serikali ya Syria zinasema "Abdul Razzaq ambaye ni  mkuu wa jeshi la al Farouq jeshi ambalo lina pingana serikali ya Syria ameuwawa katika mashambulizi hayo."
Machafuko nchini Syria yalianza mwaka 2011 Machi, kufuatia upepo wa mageuzi ya kisiasa uliyo zikumba nchi za Kiarabu tangu kuanza kwa mwaka 2011.

Tuesday, February 7, 2012

Urusi kushiriki katika mpango wa kuleta amani nchini Syria.

Malkia Elizabeth atimiza miaka 60 tangu kutawazwa kuwa Malkia wa Uingereza. 

London, Uingereza - 07/02/2012. Wanchi  na Malkia wa Uingereza wameanza kusherekea miaka 60 tangu Malkia Elizabeth kutawazwa rasmi kuwa Malkia baada ya kifo cha baba yake 1952 Mfalme George VI.
Katika kuadhimisha sherehe hizo Malkia  Elizabeth 85 alisema  "nawashukuru wananchi wote na wale wote waliomwezesha mimi na Prince Philips kuweza kuwepo, natumaini ya kuwa tutazidi kuwa pamoja wakati wa kutembelea sehemu tofauti nchini na nchi za nje."
Malkia Elizabeth anatarajiwa kufanya ziara katika nchi tofauti ikiwa ni moja ya kuadhimisha sherehe ya miaka 60 tangu kutwazwa kuwa Malkia wa Uingereza.

Urusi kushiriki katika mpango wa kuleta amani nchini Syria.


Damascus, Syria - 07/02/2012. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Urusi amewasili  nchini Syria ili kuongea na rais Bashir al Assad.
Sergei Lavrov alikutana na kuongea na uongozi wa rais wa Asad katika jitihada za kuleta amani nchini Syria.
Lavrov alisema " rais  Bashar al Assad amekubali kushirikiana katika kuhakikisha yakuwa amani inarudi nchini Syria na Urusi itakuwa mmoja ya wahusika katika mazungumzo hayo kwa kuwaunganisha viongozi wa upinzani kwani hii yote ni kwa niaba na manufaa ya Wasyria."
Nazo habari kutoka ofisi ya rais Asad zinasema " Uongozi wa serikali ya Syria upo tayari na unawakaribusha watazamaji kutoka nchi za jumuiya ya nchi za Kiarabu kuteta wajumbe ili waje kuangalia hali harisi."
Kuwasili kwa waziri wa mambo ya nje wa Urusi nchini Syria kumekuja wakati Marekani na Uingereza zimetangaza kuzidisha hatua zaidi katika kuhakikisha ya kuwa utawala wa rais Bashar al Assad unakomesha mauaji na ajitoe madarakani kufuatia maombi ya nchi za jumuiya ya Kiarabu.

Fataha na Hamas wakubali kushirikiana katika uchaguzi.


Doha, Katar - 07/02/2012.Viongozi wa vyama viwili ya kisiasa  vinayongoza sehemu tofauti za Wapalestina wamekutana na kukubaliana kuunguana ili kuaandaa uchaguzi mkuu ujao.
Viongozi hao wa vyama  Hamas na Fatah walikutana nchini Kuwait Doha na kukubaliana kwa pamoja ni kwa njia gani watashirikiana katika uchaguzi unao takiwa kufanyika hivi karibuni.
Katika kikao hicho rais wa  Palestina Mahamoud Abbas amechaguliwa kuongoza vyama hivyo hadi uchaguzi utakapo fanyika.
Waziri Mkuu wa Izrael Benyamin Netanyahu alisema " kitendo cha Fatah kushirikiana na Hamas kundi ambalo ni lakigaidi ni makosa makubwa ya kuvuruga mpango wa amani."
Vyama vya Hamas na Fatah vimekuwa na vinaongoza Wapelestina kwa maeneo tofauti. Hamas wamekuwa wakiongoza na kutawala Ukanda wa Gaza na Fatah wamekuwa wakiongoza West Bank.


Baraka Obama asiini mkataba wa kuwekewa vikwazo vya kibenki Iran.


Washington, Marekani - 07/02/2012. Rais wa Marekani amekubaliana na mswada uliopitishwa wa kuiwekea vikwazo Iran.
Rais Baraka Obama alitia sahiini sheria hiyoambayo itaifanya Iran kutokuwa na uhusiano wa aina yoyote kimabenki na benki za Marekani na vitengo vyote vinavyo husika katika maswala ya kifedha ili kuzuia kuinua na kukuza maradi wa kinyuklia ambao Iran unauendeleza.
Ofisi inayohsughulikia maswala ya kigeni ya Iran ilisema "vikwazo na kampeni ya Marekani imekuwepo na imekuwa haisaidii na hazitazimamisha nia yetu ya kuendeleza nia yetu ya kukua kisayansi hasa katika mpango wa nyuklia."
Vikwazo ambavyo vimewekwa kwa nchi ya Iran, vimekuja wakati Iran na Marekani zinapigana vita vya kidiplomasia kuhusu swala kinyuklia linalo enendelea nchini Iran.