Sunday, December 27, 2009

Ulinzi waongezwa kwenye viwanja vya ndege.

Maelfu wakumbuka waliopoteaza maisha wakati wa Tsunami. Aceh, Sri Lanka - 27/12/09. Maelfu ywa watu diniani wamekusanyika kwenye nchi ambazo zilipata maafa makubwa kutokana na Tsunami yaliyo tokea mnamo mwaka 2004. Maafa hayo ta Tsunami yalipoteza maisha ya watu wapato 226,000 na watu wengine kuachwa bila makazi na kuleta uaribifu mkubwa katika jamii. Kwa mujibu wa shirika linalo shughulikia utoaji wa misaada la umoja wa Matifa Red Cross, limesema maafa ya Tsunami bado yapo katika maeneo yote na hasa kwa familia zilizo athirika na na janga hili. Picha hapo juu ni picha ya boti, ambayo ilibakizwa baada ya janga la Tsunami,na anaonekana mama mmoja akiangalia kwa uchungu janga lililoletwa na Tsunami katika eneo lao.

Gaza waadhimisha mwaka mmoja tangu kuisha vita.
Gaza, Palestina-27/12/09. Wapalestina wakazi wa Gaza wameandamana kukumbuka siku ya kuanza kwa mashambulizi yaliyo fanywa na jeshi la Izrael kwa muda wa siku 22.
Mashambulizi hayo ambayo yalisababisha vifo vya watu 1600 na uaribifu mkubwa wa makazi ya Wapalestina.
Vita hivyo ambavyo vilileta maafa katika eneo la Gaza, vilikuwa kati ya Hamas na jeshi la Izrael.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya waandamanaji wakiwa wakiaandamana kuadhimisha siku ya kuanza kwa vita vya Gaza.
Ulinzi waongezwa kwenye viwanja vya ndege.
Michigan, Amerika- 27/12/09. Raia wa Nigeria ameshitakiwa kwa kosa la kutaka kulipua ndege ya abiria iliyo kuwa ikitokea Schiphol Asterdam.
Hakimu alimsomea kesi mshitakiwa akiwa hospital katika hospitali ya Ann Arbor iliyopo Michigan.
Mshitakiwa huyo kwa jina Umar Abdulmutallab 23, alianzia safari yake nchini Nigeria siku moja kabla ya siku ya tukio.
"Kufuatia tukio hilo , ulinzi umeongezwa katika viwanja vya ndege vyote nchin Amerika" alisema msemaji wa mwaswala ya ualama wa anga wa taifa nchin Amerika.
Picha hapo juu wanaonekana maafisa wa usalama wa moja ya kiwanja cha ndege wakiangali kwa makini wasafiri wanavyo jiandaa kukaguliwa.
Siku ya Ashura yaingia dosari nchini Iran.
Tehran, Iran - 27/12/09. Wapinzani wa serikali nchini Iran, wamepambana na polisi wa serikali wakati wa kusherekea kumbulumbu ya siku ya Ashura na watu kupoteza maisha na wengi kujeruhiwa.
Siku hii ilikuwa ni kwa ajili ya kumbukumbu ya kifo cha mjuukuu wa Mtume Muhammad, Ashura, kilichotokea karne ya 7th
Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Iran, watu wanne walipoteza maisha katika maandamano hayo.
Msaidizi wa jeshi la polisi la Iran,Ahmad Reza Radan, alisema " watu wapatao 300,walikamatwa kwa kusababisha vurugu wakati wa sherhe ya kumbukumbu ya Ashura.
Hata hivyo, viongozi wa vyam vya upinzani walisema kun zaid ya watu wanne waliopoteza maisha yao.
Picha hapo juu, anaonekana mmoja ya mwanadamaji akisaidiwa na wenzake mara maada ya kujeruhiwa vibaya na moto.

Friday, December 25, 2009

Ulinzi wa Papa waingia dosali.

Ulinzi wa Papa waingia dosali Vatican city, Vatican - 25/12/09. Waumini wa madhehebu ya Kikatoriki waliokuja kuhudhuria misa ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu katika kanisa kuu la Vatikani,walishikwa na mshituko baada ya mmoja ya waumini wa kike kuruka kizuizi na kumkaba Papa Benedikt wa XVI na kuanguka nae chini. Mwanamke huyo jina limehifadhiwa, anaulaia wa Itali na Swis,alikamatwa na walinzi wa Papa na baadaye kuwekwa chini ya ulinzi kwa mahojiano. Hata hivyo, Papa , 83 aliweza kuendelea na misa ya usiku wa Krismas, baada ya kuthibitisha hakupat madhara ya aina yoyote. Picha hapo juu anaonekana Papa Benedikt wa XVI akiwasalimia na kuwabaliki waumini waliokuja kuudhulia misa ya Krismas. Waathirika wa nguvu za kinyuklia kulipwa fidia. Paris, Ufaransa - 25/12/09. Serikali ya Ufaransa imekubali kulipa fidia kwa wanachi wa Algeria walio athirika kutokana na mazara ya kujaribiwa nguvu za kinyuklia mnamo kati ya miaka ya 1960-67. Kukubali kwa serikali kumekuja baada ya bunge la Ufaransa kupitisha mswada huo wa malipo kwa waathirika wa nguvu hizo za nyuklia. Hata hivto malipo yatalipwa kutokana na kesi ya kila mwathirika atakapo wakilisha kesi yake. Waziri wa ulinzi wa Ufaransa, Herve Morin alisema " Kupitishwa kwa seria hiyo kumeleta usawa." Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wafanyakazi wa moja ya mitambo inayoongoza nguvu za kinyuklia wakiwa wanaangalia kwa makini mitambo hiyo.

Mwanjeshi aliye kamatwa na Taliban bado yuhai.

Kabul, Afghanistan - 25/12/09. Viongozi wa jeshi la NATO lililopo Afghanistan limethibitisha ya kuwa picha ya video ya mmoja ya mwanajeshi wa Kiamerika aliyekamtwa miezi mitano iliyo pita na kundi la Taliban.

Mwanajeshi huyo, Bowe Bergdahl alitekwa nyara mara baada ya kuwasili Afghanistan katika moja kambi moja ya kijeshi iliyopo Paktika.

Video hiyo ilionyeshwa kwa dakika 36, huku mwanajeshi huyo, akiongea ya kuwa kuwepo kwa majeshi ya NATO nchini Afghanistan ni kimyume cha wananchi wa Afghanistan.

Katika video hiyo, kiongozi mmoja wa Taliban,Zabihullah Mujahid, alisema "Itabidi kuwepo na kubadilishana wafungwa ikiwa NATO inataka Bowe Bergdahl aachiwe na kundi hilo."

Picha hapo juu ni ya Bowe Bergdahl, akiongea katika picha ya video iliyo tolewa na kundi la Taliban hivi karibubi.

Thursday, December 24, 2009

Wakristu duniani wakumbuka kuzaliwa kwa Mkombozi.

Wakristu duniani wakumbuka kuzaliwa kwa Mkombozi. Usiku wa Krismas- 24/12/09. Mamilion ya waumini wa dini ya Kikristu duniani leo usiku wanasherekea siku ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu,akiongea kwa furaha, mmoja wa waumini wa dini ya kikristu alisema "Sisi wakristu tunaamini ya kuwa alikuja kuikomboa dunia na kupitia yeye kila mtu atakombolewa akimfuata Yesu Kristu. icha hapo juu, wanaonekana waumini wa dini ya Kikristu, wakiwa kanisani kuhudhulia misa ikiwa ni siku muhimu ya kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu Kristu.

Iretrea yawekewa vikwazo na UN.
New York, Amerika - 24/12/09.Kamati ya usalama ya umoja wa Matifa, imeiwekea vikwazo serikali ya Iritrea kwa kushirikiana na kuwasaidia magaidi wa Kisomalia wa Al Shabaab na kukataa kutoa jeshi lake karibu na mpaka na Djibuti. Azimio hilo lilipitishwa kwa pamoja kwa kura 13,lakini China na Libya hazikupiga kura. Hata hivyo serikali ya Iritrea, imekuwa ikikanusha ya kuwa inashirikiana na kundi la Al Shabaab ambalo lina pigana na jeshi la serikali ya Somalia. Picha hapo juu anaonekana mmoja wa mwanajeshi wa Iritrea,akiwa kazini kulinda mpaka kati yake Iretrea na Djibuti. Mwana sayansi akubali kutolewa kwa viungo vya mwili.
Tel-Aviv, Izrael- 24/12/09.Mwanasayansi na mchiunguzi wa miili ya binadamu, Jehud Hiss amekubali yakuwa Izrael ilikuwa ikitoa baadhi ya viungo vya binadamu bila ruhusa ya watu walio aga dunia au ruhusa za ndugu zao.
Jehud Hiss, ambaye alikuwa akifanya kazi katika moja ya maabara ambazo zilikuwa zikitumika katika kupima na kuangalia nini nyanzo vya vifo vya watu hao.
Jehus Hiss alisema "viungo kama mioyo ngozi na baadhi ya mifupa ilikuwa ikitolewa kwa ajili ya matumizi binafsi na viungo hivyo vilikuwa vikitolewa katika miili ya wafanyakazi wageni na Wapalestina."
Kukubali kwa habari hizo kunakuja baada ya moja ya gazeti la nchini Sweden, kutoa habari yakuwa Izrael ilikuwa ikitoa baadhi ya viungo vya miili kwa watu walioag dunia bila makubaliano ya watu hao au ndugu zao, habari ambayo Izrael ilikanusha.
Picha hapo juu ni moyo kiungo muhimu katika mwili wa binadamu.
Urussi kuimarisha nguvu zake za kinyuklia.
Moscow, Urussi - 24/12/09. Rais wa Urussi, Dmitry Medveded, amesema Urussi itaendeleza nguvu zake za kinyuklia kufuatina na wakati.
Akiongea na waandishi wa habari, rais Medvedev alisema" Ili kulinda nchi yetu ni lazima kuendeleza na kufanyia marekebisho siraha zetu za kinyuklia na Amerika wanaelewa swala hilo."
Rais Medvedev, aliongezea kwa kusema ya kuwa kukua kwa uchumi wa Urussi, umeanza na utachukua muda kufikia hali nzuri.
Picha hapo juu, anaonekana mmoja ya raia wa Urussi, akiangali runinga,wakati rais wa Russia , Dmitry Medvedev akiongea na waandishi wa habari.
Volkano yatishia maisha ya wakazi.
Mlima Mayon, Philipinsi- 24/12/09 . Hali ya hatari imetangazwa kwa wakazi wanao kaa karibu mlima Mayon kufuatia mlipuko wa volkano uliotokea katika mlima huo.
Akionga kwa msisitizo, mkurugenzi wa maswala ya sayansi ya volkano, Renato Solidu malisema"Mlipuko huo ulionza mwamzoni mwa wiki iliyo pita na hadi kufikia sasa unaelekea kuleta madhara makubwa kwa jamii na mzingira ya karibu na mlima huo." Majivu ya moto yaliotokana na mlipuko huo, yalionekana kuruka kuelekea hewani kiasi cha umbali wa zaidi ya mita miatano.
Picha hapo juu, majivu ya moto yanaonekana yakiruka juu, hali ambayo wakazi karibu na maeneo hayo wamekuwa na wasiwasi mkubwa.
Urussi yafungua mpaka na Georgia.
Moscow,Urussi- 24/12/09 . Serikali ya Georgia na Urussi, zimekubaliana kufungua mpaka nchi zao, tangu kusimama kwa vita vilivtotokea mwaka mmoja uliopita.
Kwa mujinu wa wasemaji wa serikali zote mbili, ufunguzi wa mipaka hiyo utawasaidia wanachi wa Georgia kusafirisha mizigo yao.
Urussi, ilifunga mpaka na Georgia tangu mwaka 2006,kutokana na mvutano wa kisiasa uliotokea kati ya nchi hizo.
Picha hapo juu, kinaonekana moja ya kifaru cha kijeshi kikiwa katika ulinzi wa mpaka kati ya Urussi na Georgia.

Saturday, December 19, 2009

Uchumi wa China kuonyesha mabadiliko.

Uchumi wa China kuonyesha mabadiliko. Beijing,China - 19/12/09. Serikali ya China, imetangaza ya kuwa uchumi wa umekuwa kwa kiasi cha asilimia 0.6 hadi kufikia mwisho wa mwezi wa Novembea. Kwa mujibu wa habari zilizo tolewa na serikali ya China, zinasema kukua huku kwa uchumi kwa kipindi cha miezi kumi iliyo pita , kuanatokana na kuongezeka na ununuzi na uzalishaji na kuwekwezwa kwa vitega uchumi kuliko ongezeka. Picha hapo juu ni bendera ya China nchi ambayo uchumi wake umeanza kuku kwa kulinganisha na nchi zinanzo endelea dunia.

Taliban yawa na mbinu mpya za mashambulizi.
Kabul Afghanistan - 19/12/09. Kiongozi mmoja wa kundi la Taliban,amesema ya kuwa kundi la Taliban litabigana na jeshi la Amerika na NATO hadi mtu wa mwisho, hata kama wakileta zaidi ya wanajeshi 200,000.
Kwa mujibu wa maelezo ya wataalamu wa mambo ya kivita wamesema ya kuwa Taliban, wamebadilisha mbinu ya kupigana hasa kwa kipindi cha baridi, wameongeza mashambulizi tofauti na miaka ya nyuma.
Picha hapo juu wanaonekana wapiganaji wa Taliban, wakiwa mafichoni tayari kwa kuanza mashambulizi.
Jibu la kutunza na kulinda mazingira bado kitendawili kwa jumuia za kimataifa.

Copenhagen,Denmark-19/12/09.Umoja wa mataifa umekubaliana kimsingi uamuzi uliochukuliwa nchini Denmark na viongozi na marais walioudhulia mkutano wa kujadili jinsi ya kukabiliana kuaribika kwa maziangira na hali ya hewa.

Akiongea mbele ya waandishi wa habari katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban ki Moon, alisema" Nchi zote zimekubaliana kimsingi kukubaliana ni kwa jinsi gani zitashiriki kupunguza uharibufu wa masingira na hali ya hewa, muda muafaka utakapo fika miswaada iliyo kubalika itakuwa sheria."

Hata hivyo Amerika, Brazil, China na Afrika ya Kusini, zimekubaliana kwa kiwango kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa kutokana na nchi hizo kuwa na viwanda vingi.

Picha hapo juu, wanaonekana baadhi ya wanachama wa chama cha Kijana na wananchi wengine wakiwa wanapinga na kusema ni aibu kwa uamuzi uliofanywa wa kutokuwa kubaliana kwa pamoja kupambana na uharibifu wa mazingira.

Picha ya pili wanaonekana waandamaji wakiwa wamebeba maelezo yenye ujumbe kwa wajumbe walioudhulia mkutano wa kukabiliana na uharibifu wa mazingiza jijini Copenhagen Denmark.

Monday, December 14, 2009

Evo Morales aongoza kwa kura nchini Bolivia.

Evo Morales, aongoza kwa kura nchini Bolivia.. La Paz, Bolivia - 14/12/09. Matokeo ya uchaguzi uliofanyika nchini Bolivia, yanaonyesha rais wa sasa wa nchi hiyo Evo Morales, ameshinda kwa asilimia 60%. Kwa mujibu wa ripoti za kamati inayo simamia uchaguzi, mpinzani wa Evo, Manfred Reyes Villa, inasemekana amepata kura kwa asilimia 23%. Hata hivyo matokeo ya uchaguzi yanatarajiwa kutangazwa wiki hii rasmi. Picha hapo juu anaonekana, rais wa Bolivia, Evo Morales,akihutubia kwa makini wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Bolivia. Rais wa Kuba Raul Castro, ailaumu Amerika. Havana, KUba 14/12/09. Rais wa Kuba ,Raul Castro, ameilaumu serikali ya Amerika kwa kuunga mkono uchaguzi wa Honduras, ambao hakuwa wa haki na inastahili rais wa zamani Manuel Zelaya arudishwe madarakani. Rais, Raul Castro, aliyasema haya wakati wa mkutano unao zikutanisha nchi za Latini Amerika Hata hivyo msemaji wa serikali ya Amerika, alisema " Raul Castro inabidi aanze demokrasi nchini mwake, kwani wakati wakuchaguliwa kwakwe kura zilikuwa za mtu mmoja." Picha hapo juu anaonekana rais wa Kuba,Raul Castro akiongea wakati wa mkutano wa viongozi wa Latini Amerika uliofanyika jijini Havana nchini Kuba kujadili maendeleo ya nchi zao kiuchumi na kijamii na kutafuta njia ya kukuza uchumi. Waandamanaji wakumbana na nguvu za dola. Copenhagen,Denmark - 14/012/09.Watu zaid ya 200, wamekamtwa na polisi wakati wa maandamano ya kupinga kuongezeka kwa machafuzi ya hali ya hwe na mazingira. Waaanamanaji hao, wanaanandamana kuwataka viongozi wa dunia ambao wapo kwenye mkutano nchini Denmark kujadili kila njia ya kupunguza machafuzi na kuharibu hali ya hewa duniani. Kufuatia maandamano hayo, polisi wamekuwa wanasimamisha watu na kuwakagua kama wana zana za hatari. Picha hapo juu anaonekana mmoja ya waaandamaji akikabiriana na polisi wanao linda mkutanao huo unaoendelea. Waziri mkuu wa Itali ashambuliwa. Roma. Itali - 14/12/09.Waziri mkuu wa Itali, Silvio Berlusconi,amejeruhiwa kwenye paji la uso baada ya mtu mmoja kumrushia kigae usoni. Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, alisema "Mtu mmoja 42 ambaye anamatatizo ya akili ndiye aliyemrushia kigae hicho", mtu huyo alikamatwa na polisi mara moja. Waziri mkuu, Berlusconi, alijeruhiwa pua na baadhi ya meno kukuvunjika. Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Itali, Silvio Berlusconi, akiwa njiani kuelekea hospitali, baaada ya kushambuliwa na kigae.

Thursday, December 3, 2009

NATO kuongeza wapiganaji Afgahinstan.

NATO kuongeza wanajeshi Afghanistan.

Washington, Amerika - 03/12/09. Rais wa Amerika Baraka Obama, ametanganza ya kuwa wanajeshi wapatao 30,000 watakwanda nchini Afghanistan.
Akiongea mbele ya wanajeshi waliomaliza mafunzo ya kijeshi, rais Obama alisema "Vita hivi ni kwajili ya usalama na ulinzi wa Amerika na nchi wanachama wa NATO".
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana zinamsema kabla ya kutangaza hatua hiyo, rais Obama, aliwasiliana na viongozi wa bara la Ulaya wanachama wa NATO,ili kuzihimiza nchi hizo kushirikiana kikamilifu kushinda vita dhidi ya Taliban na kundi la Alqaeda.
Picha hapo juu anaonekana rai wa Amerika, Baraka Obama, akihutubia mbele ya viongozi wa serikali na wanajeshi,kuhusu kuongeza idadi ya wanajeshi watakaokwnda nchini Afghanistan.
Picha ya pili, wanaonekana wanajeshi wakiwa katika doria nchini Afghanistan, katika harakati za kupambana na Taliban na Alqaeda.
Rwanda mwamachama mpya wa Commonwealth.
Kigali, Rwanda - 03/12/09 . Jumuiya ya nchi wanachama wa ambazo zilitawaliwa na Mwingereza - Commonwealth group- zimeikaribisha rasmi nchi ya Rwanda kuwa manachama wa 54. Kwa mujibu wa waziri wa habari wa Rwanda, Louise Mushikiwabo, aliseama nchi yake imepiga hatua kubwa kimaendeleo tangu kutokea vita vya kikabila vya mwaka 1994.
Picha hapo juu, anaonekana rais wa Rwanda, Paul Kagame, ambaye tangu kuwa kiongozi wa Rwanda, nchi yake imeendelea kiuchumi na kijamii kwa kiasi kikubwa.
Picha ya pili, ni ya rais wa Ufaransa, Nikolas Sarkozy, ambye nchi yake imekuwa mtawala wa Rwanda wakati wa kipindi cha ukoloni, na sasa Rwanda imejiunga na jumuia ya nchi zinazo sema kiingereza.

Saturday, November 28, 2009

Mvutano wa kisiasa nchini Pakistan kurudia tene ?

Mvutanao wa kisiasa nchini Pakistan kurudia tena? Karachi. Pakistan - 28/11/09. Mswada wa kisheria ambao ulikuwa umewekwa kwa ajili ya kumlinda rais wa Pakistan kufuatia shutuma za rushwa umekweisha hivi karibuni. Kwa mujibu wa habari zilizo patikana kutoka Pakistan, zinasema rais, Asif Ali Zardari huenda akawa na wakati mgumu wa kisiasa katika uongozi wake. Wachunguzi wa mambo ya siasa za Pakistan, wanasema huenda Pakistan, ikakumbwa na mzozo wa kisiasa ambao ulikuwepo wakati wa rais Pervez Musharraf. Picha hapo juu anaonekana, rais wa Pakistan, Asif Ali Zardari akiongea hivi karibuni na waandishi wa habari.

Saturday, November 14, 2009

Waumini wa dini ya Kislaam kuelekea Mecca Kuhijji

Waumini wa dini ya Kislaam kuelekea Mecca Kuhijji. Mecca, Saudi Arabia - 14/11/09. Mamilion ya waumini wa dini ya Kislaam wameanza kuelekea nchini Saudi Arabi, kwa ajili ya Kuhiji na kujiswafi nia zao na kufuata maagizo ambayo Mungu aliyaagiza kupitia Mtume Muhammad SW. Kwa mujibu wa serikali ya Saudi Arabia, hali ya usalama ipo katika hali nzuri na hakuna haja ya Waumini wa kuwa na wasiwasi. Picha hapo juu, wanaonekana waumini wa dini ya Kislaam wakiwa katika Hijja, kwa kujiswafi. Syria na Izrael huenda wakaanza mazungumzo ya amani. Paris,Ufaransa - 14/11/09. Rais wa Syria, Bashar Al Assad,amesema amekutana na rais wa Ufaransa,Nikolas Sarkozy, wakati alipo tembelea Ufaransa kwa ziara ya kiserikali. Katika ziara hiyo, marais hao walizungumzia, ni kwa jinsi gani wataanzisha mazungumzo ya kuleta amani kati ya Izrael na Syria. Hata hivyo, rais wa Siyria, aliseama yakuwa "hatafanya mazungumzo na waziri mkuu wa Izrael moja kwa moja, itabidi Izrael kutuma ujmbe wake na Syria itatuma wajumbe wake na hapo mazungumzo yanaweza kufanyika." Picha hapo juu anaonekana rais wa Syria, Bashar al Assad, akisalimiana na rais wa Ufaransa, Nikalas Sarkozy,wakati walipo kutana nchini Ufaransa.

Rais,Baraka Obama, kuudhulia mkutano wa viongozi wa Asia.
Paya Lebar, Singapore - 14/11/09. Rais wa America, Baraka Obama, amewasili Singapore, kuudhulia mkutano wa iongozi wa Asia na Pacific, ambao unatalajiwa kuaanza siku ya Jumapli.
Akiwa ziarani kwenye bara la Asia, rais Baraka Obama, alianza kutembelea nchini Japan, na kuahaidi yakuwa Amerika itashirikiana na nchi za Asia kwa ukaribu.
Picha hapo juu, anaonekana rais, Baraka Obama, akisalimia kabla ya kuelekea nchini Singapore kwenye mkutano.

Tuesday, November 10, 2009

Serikali ya China kuisaidia Afrika.

Serikali ya China kuisaidia Afrika. Sharm El Sheikh, Misri - 10/11/09. Serikali ya china imesema itazipatia nchi za Afrika billions 10 za dollah ya Kiamerika kwa ajili ya kuinia na kujenga jamii zao nchi zao na kuziwezesha nchi hizo kufanya biashara na China. Akiongea hayo mbele ya viongozi wa Afrika waliohudhulia mkutano uliofanyaka nchi Misri, waziri mkuu wa China, Wen Jiabao,alisema wale wanao ikosoa na kuilaumu serikali ya China, waangalie kwani China inawataaalamu zaidi ya 15,000 katika bara la Afrika, ambao wanasaidia katika nyanja mbalimbali na China haitajihusisha na maswala ya ndani ya nchi yoyote. Serikali ya nchini imeseini mikataba ya kibiashara na nchi nyingi za Kiafrika na kufikia kiwango cha asilimia 33% ya kibiashara kwa mwaka. Picha hapo juu, amnaonekana, waziri mkuu wa China, Wen Jiabao, akiongea mbele ya viongozi na marais wa Afrika walioudhulia katika mkutano uliofanyaka katika mji wa Sharm El Sheikh nchini Misri. Charles Taylor, azilaumu nchi za Ulaya Mgharibi na Amerika. The Hague, Uhollanzi - 10/11/09. Aliyekuwa rais wa Liberial, Cherles Taylor, ameiambia mahakama ya kuwa kuondolewa kwake madarakani ulikuwa mpango wa serikali ya Amerika na nchi za Ulaya Magharibi ili ziweze kutawala upatikanaji wa mali ya asili iliyopo katiak eneo hilo. Akiongea kuelezea kukamatwa kwakwe, Charles Taylor, alisema hakuwa anaotoroka au kikimbia kutoka Nigeria,bali serikali ya Nigeria, ilishindwa kutimiza makubaliano yaliyo wekwa na rais wa wakati ule Olusegun Obasanjo yakuwa hakutakuwa na kesi zidi yake ikiwa atatoka madarakani lakini ikawa kinyume cha makubaliano yaliyowekwa. Uamuzi wa kesi hiyo huenda ikatolewa mwaka 2010 baada ya pande zote kutoa ushahidi wa kutosha mbele ya mahakama. Picha anaonekana rais wa zamani wa Liberia, Charles Taylor akiwa mahakamani tayari kusikiliza kesi ambazo zinamkabili. Korea ya kaskazini na Kora ya Kusini zatupiana risasi. Seoul,Korea - 10/11/09. Korea ya Kaskazini na Korea ya Kusini, zimelaumia baada ya wanajeshi wa nchi hizo mbili kutupiana risasi kwenye mpaka ulipo katika bahari Manjano. Mapambano hayo ambayo yalitokea 11:28 kwa saa za maeno hayo. Hata hivyo kwa mujibu wa masemaji wa serikali ya Korea ya Kusini , alisema, " Hakukua na majeruhi yoyote." Picha hapo juu, nimoj ya meli ya kivita ambayo inaaminika ilitumika kushambuliana katika ya nchi ya Korea ya Kusini na Korea ya kaskazini.

Monday, November 9, 2009

Hatimaye Lebanon kupata serikali.

Wanaharakati na Wapalestina wavunja ukuta. Qalandiya, Palestina - 09/11/09. Wapalestina hukun wakishirikiana na wanaharakati wa kigeni wamebomoa ukuta uliojengwa kutenganisha Wapalestina na Waizrael katika eneo la mji wa Qalandiya. Wanaharakati hao na wapalestina walitumia roli na kuvuta ukuta kwa umbali wa mita mbili, kabla ya polisi wa Izrael, kuja kuwazuia. Mmoja wa wanana harakati hao, Abdullah Abu Rahma, alisema wanaona ukuta huo ni sawa ule wa Berlin, "na ikiwa leo wanaadhimisha miaka 20 tangu kuvunjwa kwa ukuta wa Berlin, basi waliona ni bora kuvunja ukuta huo kwa kuadhimisha sherehe hiyo." Picha hapo juu wanaonekana, baadhi ya wanaharakatina Wapalestina wakiwa juu ya ukuta unaotenganisha Izrael na Palestina. Hatimaye Lebanon kupata serikali. Beiruti, Lebanon - 09/11/09. Waziri mkuu wa Lebanon , Saad Hariri, amkabidhi majina ya mawaziri amabo wataunda serikali ya Lebanon kwa rais wa nchi hiyo Michel Sleiman. Kuteuliwa kwa mawaziri hawa kumekuja baada ya mazungumzo marefu yaliochukuwa miezi kadhaa, kujadiliana na vyama vya upinzani ambavyo vilikataa uteuzi uliofanyaka mara ya kwanza. Serikali hiyo itakuwa na mawaziri 30,ambapo chama cha Hezbollah kimepata wizara 10. Picha hapo juu wanaonekana viongozi wa vyama tofauti wakiwa katika mazungumzo ya kuunda serikali ya Lebanon itakayo apishwa kuongoza serikali. Rais wa Afghanistan Hamid Karzai ,azitaka nchi za Kislaam kuisaidia nchi yake. Istambul,Turkey- 09/11/09. Rais wa Afghanistan, Hamid Karzai, amezitaka nchi wanachama shirikisho la nchi za Kiislaam kuisaidi Afghanistan kiuchumi na kijamii. Akiongea hayo , rais wa Hamid Karzai, alisema wananchi wa Afghanistan, wanaitaji msaada mkubwa kwa sasa, kutokana na hali halisi ya nchi hiyo, ambapo imekuwa na matatizo ya kivita kwa muda mrefu. Picha hapo juuanaonekana, rais wa Afghanistan, Hamid Karzai, alipo wasili katika jiji Istambul. Maaelfu washangilia miaka 20 tangu kuvujwa kwa ukuta wa Berlin. Berlin, Ujerumani - 09/11/09. Wanachi wa Ujerumani pamoja na viongozi mbali mbali duniani wameungana kwa pamoja kushangilia miaka 20 ya kuvunjwa kwa ukuta wa Berlin. Wakiongozwa na , Kanselar, Angela Markel na rais wa Ujerumani,Horst Koehler,na huku mvua kubwa ikinyesha viongozi hao na wananchi wali tembelea eneo ambalo ukuta wa ulikuwa umejengwa. Baadhi ya watu waliokuwepo kipindi hicho cha kuvunjwa kwa ukuta wa Berlin, wamekuwa wakisikika wakisema "hawaamiani kama sasa ni miaka 20 imepita tangu kuvunjwa kwa ukuta huo na kuifanya nchi ya Ujerumani kuwa moja." Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya watu wakiwa juu ya ukuta wa Berlini, huku wakishangilia kuvunjwa kwa ukuta huo mwaka 1989.

Thursday, November 5, 2009

Rais wa Wapalestina atangaza kutogombea urais mwakani.

Rais wa Wapalestina, atangaza kutogombea urais mwakani. Ramal, Palestina 05/11/09 - Rais wa Palestina, Mahmoud Abbas, ametangaza rasmi yakuwa hatagombea uchaguzi wa rais ambao unatarajiwa kufanyika mapema mwaka ujao 2010. Akitangaza mbele ya waandishi wa habari, alisema ameamua hivi kufuatia vikwazo ambavyo vinakwamisha kuwepo kwa amani kati ya Waizrael na Wapalestina. Picha hapo juu, anaonekana rais wa Wapalestina, Mahmoud Abbas, akijianda kuongea mbele tya waandishi wa habari kuhusu uamuzi wake wa kutogombea kiti cha urais . Wafanyakazi umoja wa mataifa nchini Afghanistan matatani. Afghanistan, Kabul - 05/11/09. Umoja wa Matifa,umetangaza ya kuwa wafanyakazi wake wote waliopo nchini Afghanistan waondoke nchini humo kutokana na hali ya usalama kuwa tata. Uamuzi huo unakuja baada ya wafanyakazi watano wa umoja wa mataifa kuuwawa hivi karibuni. Hata hivyo mwakilishi wa umoj wa matifa Kai Eide,alisema yakuwa haina maana umoja wa matifa utasimamisha misaada yake kwa Afghanistan. Picha hapo ju ni moja ya gari la umoja wa matifa, ambalo lilishabuliwa hivi karibuni.

Monday, November 2, 2009

Umoja wa Matifa waismamisha misaada ya kijeshi nchini Kongo DRC.

Umoja wa Mataifa kusimamisha misaada ya kijeshi nchi Kongo DRC.

Kinshasa, DRC - 02/11/09. Umoja wa Mataifa umesimamisha misada iliyokuwa inatoa kulisaidia jeshi la Kongo (DRC) kwa kudai yakuwa kuan baadhi ya wanajeshi wa jeshi hilo la serikali wanakwenda kinyume na sheria za kijeshi kwa kuhusika na kutesa , kunyanya na hata kuua raia.
Akiongea, msemaji wa UN, anayeshughulikia maswala ya amani, Alain Le Roy, amesema yakuwa raia wamekuwa hawapati kulindwa na jeshi hilo, na badala yake jeshi limekuwa likienda kinyume.
"ata hivyo serikali ya Kongo DRC, imesema imekuwa inafanya uchunguzi wa kesi hisi,na haitakuwa jambo la busara kwa UN kusimamisha kulisaidia keshi la Kongo kwani kutafanya hali ya usalama kuwa mbaya"alisema waziri wa habari wa wa Kongo DRC, Lambert Mende.
Picha hapo juu, ni bendera ya Umoja wa mataifa, ambapo UN, imetangaza kusimamisha kuisaidia Kongo DRC kijeshi.
Picha ya pili, anaonekana rais wa Kongo DRC, Joseph Kabila, ambye serikali yake imekuwa inawakati mgimu wa kuijenga upya Kongo DRC,na kupambana na makundi ya wapinzani wanao pigani malia ya asili ya Kongo DRC.
Korea ya Kaskazini na Amerika bado zavutana.
Pyong Yang, Korea ya Kaskazini - 02/11/09. Serikali Korea ya kaskazini,imeitaka serikali ya Amerika kufikiara kutoa uamuzi wa haraka kama itakubali mazungumzo ya nchi hizo mbili kufanyika.
Habari kutoka wizara ya mambo ya nje ya Korea ya kaskazini,zilisema ya kuwa Korea ya Kaskazini imeweka bayana ya kuwa inataka kuzungumza na serikali ya Amerika moja kwa moja, na kama haitafanyika haraka, basi korea ya Kaskazini itaamua ni nini la kufanya.
Hata hivyo serikali ya Amerika, imekuwa inasisitiza mazungumzo yafanyike kuwa kuhusisha nchi za China, Urussi, Japan,Korea ya Kaskazini na Korea ya Kusini.
Picha hapo juu, wanaonekana wanajeshi wa Korea ya kaskazini wakiwa wanakula kwata katika moja ya sherehe za kimataifa za nchi hiyo.
Hamid Karzai kuwa rais wa Afghanistan.
Kabul Afghanistan - 02/11/09. Kamati ya uchaguzi wa Afghanistan, imetangaza rasmi ya kuwa Hamid Karzai kuwa mshindi wakiti cha urais kutokana na uchaguzi wa uliofanyika mapema mwezi wanene tarehe 20, ambapo matokeo ya uchaguzi huo yalionekana yakuwa kulikuwa na ukiukwaji wa sheria za uchaguzi.
Uamuzi wa kumtangaza Hamid Karzai kuwa rais wa Afghanistan, kumekuja , baada ya mpinzani wake Dr Abdullah Abdullah kujitoa katika uchaguzi wa marudio ulikuwa umepangwa kufanyika tarehe 07/11/09 kwa kudai yakuwa hautakuwa wa haki, kutokana na baadhi ya mahsrti waliyo taka kutotimizwa.
Picha hapo juu, ni ya bendera nchi ya Afghanistan, nchi ambayo hali ya kisiasa imekua katika mutata kwa muda mrefu sasa.
Picha ya pili ni kushoto, Dr Abdullah Abdullah,ambaye amejitoa katika uchaguzi wa rais na kumpa nafasi ya kutangazwa Hamid Karzai kulia kuwa rais wa Afghanistan.
Iran yataka mkataba wa nyuklia utazamwe upya.
Tehran, Iran - 03/11/09. Serikali ya Iran imetaka shirika linalo shughulikia maswala ya nguvu za kinyuklia kutizamwa upya.
Akiongea na waandishi wa habari, waziri wa mabo ya nje wa Iran, Monouchehr Mottaki, alisema ya kuwa Iran,imelitizama kiundani swala la kuitaka Iran, kupeleka nje madini yanayo tumika kutengenezea nguvu za nyuklia nje ya Iran, ili kuihakishia dunia yakuwa aina mpango wa kutengeneza bomu la nyuklia.
hata hivyo Iran, imekuwa ikisisiti yakuwa haina mpango wa kutengeneza mabomu ya nyuklia.
Picha hapo ju ni moja ya kiwanda cha kutengenezea na kuchuja madini ambayo yanatumika kutengeneza nguvu za nyuklia.

Sunday, November 1, 2009

Uchaguzi wa Afghanistan waingia doa, mpinzani ajitoa kushiriki uchaguzi.

Waasi wa Nigeria watishia kuvunjika kwa makubaliano ya amani. Niger Delta, Nigeria - 01/11/09. Msemaji wa kundi MEND Henry Okah ambalo linapinga kuwepo kwa makampuni ya kigeni ambayo yanachimba mafuta katika eneo hilo limesema linataka makampuni yote yaliopo eneo hilo yaondoke. Akuiongea, Henry Okah, alisema yakuwa serikali ya Nigeria imekuwa haitimizi matakwa ya wanachi na wakazi wa Niger Delta, basi haitachukua muda hali itakuwa mbaya katika eneo hilo. Picha ya kwanza hapo juu wanaonekana wapiganaji wanaotete haki zao katika eneo la Niger Delta wakiwa wamshikilia siraha na wanatishia kuvunjika kwa makubaliano ya amani yaliyopo. Picha hapo juu, ni ya bendera ya Nigeria ya Nigeria, nchi ambayo eneo la Niger Delta linaleta kichwa kuuma kwa serikali ya Nigeria. Raia wa Afrika ya Kusini kuchunguzwa. Johannesburg, Afrika ya Kusini - 01/11/09. Serikali ya Afrika ya Kusini, inafanya uchunguzi ili kujua ni raia gani wa Afrika ya Kusini walishiriki katika vita vya Wapalestina na Waizrael mapema mwisho wa mwaka 2008. Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema yakuwa ikiwa kuna raia wa Afrika ya Kusini alishiriki,hatachukuliwa hatua za kisheria, kwani serikali ya Afrika ya Kusini hairuhusu raia wake kushiriki vita bila ruhusa ya serikali. Picha hapo juu, wanaonekana, wapiganaji wakiwa wamepiga picha pamoja. Uchaguzi wa Afghanistan waingia doa, mpinzani ajitoa kushiriki uchaguzi. Kabul, Afghanistan - 01/11/09. Mgombe uchaguzi wa urais wa Afghanistan ,Dr Abdullah Abdullah, amesema hatashiriki katika marudio ya uchaguzi yanayo tarajiwa kufanyika tarehe 07/11/09. Uamuzi wa mgombea huyo, Abdullah Abdullah, alisema ameamua kutoshiriki, kwa uchaguzi huo hautakuwa wa haki. Hata hivyo, uamuzi huo, umekuja baada ya serikali kukataa kuwafukuza kazi baadhi ya viongozi ambao chama cha Dr, Abdullah Abdullah kiliwataka viongozi hao wafukuzwe kazi, kwa kukosa imani nao. Akiongea, mbele ya wadau na waandishi wa habari, alishangiliwa na baadaye kujibu maswali baadaye. Picha hapo juu, anaonekana, Dr, Abdullah Abdullah akiongea mbele ya waandishi wa habari kutoshiriki kwakwe katika uchaguzi mkuu wa rais utakaofanyika 07/11/09. Amerika bado kupata jibu la Wapalestina na Waizrael kuwa na amani.

Jerusalem,Izrael - 01/11/09.Waziri wa mambo ya nje wa Amerika Bi, Hillary Clinton, amemaliza ziara yake mashariki ya kati bila yakuwa na mafanikio makubwa ya kuleta amani kati ya Wapalestina na Waizrael.
Hali hii inakuja baada ya viongozi wa Palestina na Izrael kuzidi kuvutana kufuatia madai tofauti ya kila upande, ambayo yamefanya hali ya amani katika eneo hilo kuwa na utata.
Picha hapo juu, anaonekana kushoto Bi, Hillary Clinton, na kulia ni rais wa Palestina, Mahmoud Abbas wakati walipo kuta mapema jana.
Picha ya pili anaonekana, waziri mkuu wa Izrael, Binyamin Netanyahu kushoto akiwa na Bi, Hillary Clinton wakati walipo kuwa wanaongea na waandishi wa habari.