Wednesday, October 31, 2007

Maneno ya mwisho ya Diana,aliyo sema kabla kuaaga dunia ushahidi watolewa.

Mmmhh mambo bado magumu uwanja wa nyumbani.

Waasimu wawili wa jadi Liverpool na Arsenal, hivi karibuni,walitoka suruhu 1-1, hivi karibuni walipo pambana nyumbani kwenye uwanja wa Liverpool. Baadhi ya wachezaji walilizika na suruhu hiyo, kwani mpambo huu mpaka kipyenga cha mwisho ilikuwa vigumu kuamua ni nani ataibuka mshindi. Mlinzi wa Liverpool Jamie Carragher, amesema kunahaja ya timu yao kutafuta dawa kutibu, tatizo hili la kushindwa kushinda uwanja wa nyumbani, aliongeza kwa kusema wapinzani wao Arsenal walikuwa wanonekana kila kona ya uwanja, hali hii iliwauiwa vigumu kuweza kushinda mpamabano huu. Pichani hapo juu ni ma timu kochi wakiwa na sura tofauti za kuhimiza vijana wakaze kamba. Kulia ni Arsene Wenge, akitumia mikono kupiga makofi kukumbushia stahili fulanai ambayo inaelekea vijana wamesahahau, na kushoto ni bwana Rafael Benitez akichungulia kwa makini jinsi gani vijana wanavyo menyana kulinda hadhi yao uwanja wa nyumbani, kwani wageni wa Arsenal wanapamba motoooooo. Moroko kupata nguvu za Kinyuklia hivi karibuni.
Serikali ya Ufaransa imetangaza rasmi yakuwa itaanza hivi karibuni kuisaidiaserikali ya Morroko kujennga mitamabo ya kutoa nguvu za kinyuklia, kwa ajili ya kungeza ufanisi katiak nyanja za nishati na teknolojia,. Akitangaza rasmi alipo zuru hivi karibuni nchini Moroko, rais wa Ufaransa bwana Nicolas Sarkorzy, alisema ushirikano uliopo kati ya Moroko na Ufaransa ni wa kufaakuigwa ili kuleta maendeleo kijamii duniani kote. Pichania ni mfalme wa Moroko Mohamed VI akijiandaa kumpokea rais wa Ufaransa bwana Sarkorz.
Uchaguzi nchini Kenya waja kwa vishindo ya uzawa wa maeneo.
Wannchi wa Kenya , watafanya uchaguzi wao mwaka huu 2007, mwezi wa desemba tarehe 27.Matamshi yahaya yalitolewa hivi karibuni na rais wa jamuhuri ya Kenya bwana Mwai Kibaki.
Rais Kibaki, atashiriki katika kugombani akuchaguliwa kuwa rais kwa awamu ya pili, huku atachuana na wapinzani wake mkubwa, Raila Odinga, Kalonzo Musyoka, aMchungaji Pius Muiru.
Kutokana na wachunguzi wa uchaguzi huu na hasili ya mgombea ndiyo inaangaliwa sana, hasa kutokana na vyama vikuu ambavyo wanachama wake wanavutana. Bwana Kibaki akiongoza chama kijulikanacho kama Part of National Unity(PNU) na wachama wake wengi ni watu wa kabila la Kikiyu.
Bwana Odinga ataongoza chama kijulikanacho kama Orange Democrqatic Movement ( ODM), ambaye asili yake ni kutokea kabila la Waluo.
Rais Putin nitakuwa waziri mkuu, kama tukishinda.
Rais wa Rusia bwan Vladamir Putin, ametangaza ya kuwa atakuwa waziri mkuu wa Rusia baada ya kumaliza muda wake kama rais wa Rusia.
Bwana Putin alisema haya alipo kuwa akiongea kwenya mkutano wa chama,United Russia.
Aliendelea kwa kusema atakuwa mstari wa mbele katika kampeni za uchaguzi utakao fanyika hivi karibuni. Hapo juu pichani ni bwana Putin akiongea hivi karibuni.
Rais Mugabe nitaudhuria mkutano wa Ureno, wabaya wetu ni Uingereza
Rais wa Zimbabwe bwan Robert Gabriel Mugabe, amesema yakuwa atahudhuria mkutana kati ya viongozi wa bara la Afrika na Ulaya utakao fanyika Lisbon Ureno, mwishoni mwa mwaka huu.
Aliyasema haya hivi karibuni alipokuwa akiongea na waandishi wa habari, alisifu viongozi wa SADC kwa kuwa kidete kupinga shinikizo la umoja wa Ulaya ya kuwa nani awepo na nani asiwepo,pia aliongeza ya kuwa kuna mambo mengi ambayo hayapendezi kwe jamii ya kima mataifa na hakuna,siku moja wamesha shinikizwa kuchagua nani aahudhulie kwenye umoja wa mataifa.Bali utaona dunia ina kaa kimya tu.
Aliongeza kwa kusema, Zimbabwe inamatatizo na serikali ya Uigereza, kwani serikali ya Uingereza imekataa kukamilisha mikataba waliyowekeana na serikali ya Zimbabwe, kuhusu matatizo ya ardhi.Na Zimbabwe haina matatizo na Ulaya yote
Hakukuwa na mikakati imara, ya kukabiliana na mabadiliko nchini Irak.
Maneno ya waziri mkuu amstahafu wa Uingereza bwan Tony Blair, siku tano tu baada ya kuanguka kwa utawala wa Saddam Huseein, ya kuwa Irak, itakuwa pahali pa usalama na bora kwa wa Irak na eneo zima kwa ujumla. yameoneka kupingwa na wadadisi wa mambo. Hii imetokana na hali halisi iliyopo nchni Irak kwa sasa.

Kwani kuanza kwa vita vya Irak, miaka minne iliyo pita hadi sasa, ni kitu ambacho Washington ,a London, hawakutegemea ya kuwa vita hivi vinge sumbua kwamuda mrefu,haya ni maelezo ya mmoja wa wakosoaji wa vita vya Irak aliyasema hivi karibuni.Akiongezea kwa kusema ya kuwa
kuanza kwa vita, bila kufuata misingi iliyo wekwa toka enzi za Napoleon, ni makosa ambayo yalifanyika.
Kwani," Napoleon alisema usichukue hatua ya kwanza bila kujua nini kinafuata, au kupanga kukabiliana na na matokeo yake.
Msemaji huyu alisema yakuwa vita vya Irak, vilipangwa na kuvamia nchii hii, kwa kujua ya kuwa Sadam akisha toka madarakani wairak watasidia katiak kujenga nchi yao. Na hii hali iliyopo ya kuwepo na vikundi tofauti ambavyo vina hatarisha usalama wa Irak, hakikutarajiwa.
Pichani hapo juu, ni rais George Bush wa Amerika alipo tembelea UK na bwana Tony Blair wakati alipo kuwa bado waziri mkuu wa Uingereza,wakiongea na waandishi wa habari kuhusu hali halisi nchini Irak.

Maneno ya mwisho ya Diana Malkia wa Wailes kabla ya kifo chake.

Shahidi ambaye alikuwepo wakati wa ajali ya Diana na Dodi El Feyed, amesema ya kuwa wakati alipo kuwa akisaidia katika kuokoa maisha ya Diana, alisikia Diana akisema Mungu wangu Mungu wangu mara kwa mara.
Shaihidi huyu ambaye anajulikana kwa jina bwana Damian Dalby,aliyasema haya alipo kuwa akitoa ushahidi, mbele ya wachungizi wanaochunguza ajali mbaya ambayo ilisababisha kifo cha Diana na Dodi El Feyed.
Ajali hiyo ilitokea jijini Paris, 31/Agusti/1997 kwenye daraja lijulikanalo kama Pont d'Alma.
Pichani hapo juu ni picha ya gari ambayo Diana na Dodi walipata nayo jali na kusababisha vifo vyao, ambavyo mpaka sasa bado kuna utata kuhusu ajali hiyo.
Mwandishi wa habari marufu atunikiwa nishani.
Mwanadishi wa habari na mtangazaji wa cnn, bi, Christine Amanpour, ametunukiwa nishani, na Malkia wa Uingereza kutokana na kazi yake anavyo ifanya kiadirifu.Zawadi hii ambayo ilianzishwa mwaka 1917 na Mfalme George V, kwaajili ya kuwatunukia watu amabo wamesaidia kuilinda na kupigania Uingereza wakati wa vita vya kwanza vya dunia.
Bi Christine Amanpour, alikuwa na tabasamu kubwa alipo pokea nishani hii, ambayo ina rangi za blue na msalaba wa dhahabu na michirizi ya rangi nyekundu,na una motoo KWA AJILI YA MUNGU NA MFALME.
Vilevile bi Christine ni moja ya waanzilishi wa cnn london ambayo imeanzishwa hivi karibuni.
Bi, Christine Amanpourni mmoja kati wa waandishi waliokuwa wakilipoti enzi za vita vya Bosnia na Elsagovina, vilivyo tokea ulaya mashariki,na ametangaza matukio mengi amabayo ya mejili hapa duniani.
Hapo juu bi Christine Amanpour akionyesha nishani aliyo pokea kutoka kwa malkia Elizabeth.
Belguim ya waonya wanunuzi wa almasi kwa magendo.

Msemaji mmoja wa mawakili hao amesema, ununuzi huu umekuwa ukisaidia kendelea kwa matatizo na vita vya wenyewekwa wenyewe, katika bara la Afrika kwa muda mrefu, na tunatarajia kukabidhi koti kesi hizi karibuni.

Kutokana na uchunguzi uliofanywa, imegundulika hivi karibuni,serikali ya Belguim., ilitaifisha kiasi cha faranga( Fedha) zipatazo Euro million 14, ambazo zilitokana na mauzo ya almasi haramu, amabazo zinaaminika zilitokea almasi hizi zilitokea nchini Ivory Coast, moja ya nchi ambayo vita vya wenyewe kwa wenyewe bado vinaendela, kuigawa nchi hiyo kataiak sehemu kubwa mbili.

Ajiunguza baada ya kuchoka na ubaguzi.
Hivi karibuni nchini, kwenye mji wa Luxenburg nchini Belguim, mwana mama mmoja,mwenye wototo watatu, alijimwagia mafuta aina ya petrol, na kujiwasha moto, kwa madai ya kuwa ubaguzi umezidi,mjini hapo.
Mwana mama huyo alijiwasha karibu na waandishi wa habari, na kuleta mshtuko mkubwa, mjini hapo, na hasa wakati wa maandamano hayo yalioandaliwa kuelezea hali hii ya ubaguzi inavyo wakela.
Hata hivyo, hivyo wafanyakazi wa zima moto na watu wa huduma ya kwanza waliwahi kufika na kuokoa maisha ya mama huyu, aliye julikana kama Maggy.D.Mufu.
Mwana mama huyu alikimbizwa kwenye hospitali ya Bon Secours mjini Metz , ambapo anaendelea na matibabu zaidi.
Hapo juu ni mwana mama Meggy alipo kuwa amejiwasha kupinga ubaguzi, mjini Luxenburg Belguim, na hapo wanaonekana watu wakijaribu kumvua nguo zake ili moto usimzuru zaidi.

Friday, October 26, 2007

Tupo tayari kuilinda nchi yetu

Maelfu wamuaaga hayati, nyota wa muziki wa rege Luck Dube. Itakuwa siku ya kukumbukwa milele kwa wapenzi wa muziki wa rege, duniani , Afrika na Afrika ya Kusini kwa ujumla.Siku ya tarehe 28/10/07, siku amabayo dunia imemuaaga nyota ya muziki wa rege hayati Luck Dube, amabaye amelazwa leo pale kwe yenye nyumba yake ya milele. Mke wake bibi, Zanele ,watoto wake saba, Bongi,Nonkululeko,Thokozani, Laura,Siyanda,Philani,na Melokuhle , ndugu,jamaa na marafiki. walibubujikwa na mchozi pale walipo shuhudia kulazwa kwakwe. Na hasa ni nyimbo za hayati Luck Dube zilizo kuwa zikipigwa wakati wote wa maombelezi yake katika kijiji cha Ingogo km 250 kusini mashariki mwa Johannesburg . Hayati Luck Dube alitoa album 22 wakati wa huhai wake. Hayati Luck Dube mwenye miaka 43 alifariki dunia mbele ya watoto wake, baada majambazi kutaka kumpora gari lake kwa kumiga risasi,alipo kuwa ameenda kumtembelea ndugu yake. Kwa mujibu wa polisi, watu watano wamekamatwa kuhusiana na kifo cha mwanamusiki huyo. Tupo tayari kuilinda nchi yetu pindipo tukushambuliwa. Marumbano kati ya Iran na Amerika, simapya, kutokana na msemaji wa serikali ya Iran. Kuwekewa vikwazo na Amerika hakuanza leo, na vikwazo hivyo havita tuteteresha, kwani ni kama nyongeza tu. Kutokana hali hii ,hasa baada ya viongozi wa serikali ya Amerika, kuweka wazi upo uwezekano wa kutumia nguvu za kijeshi zidi ya Iran, pindipo haita kubaliana kusimamisha kuendelea kujenga mitambo ya Nyuclia. Lakini msemaji wa jeshi wa Irana alihakikisha ya kuwa jeshi lake lipo tiyari kiulinda Iran kwa wakati wowote pindipo ikishambuliwa. Hapo juu, pichani ni mmoja wa wasemaji wakuu wa serikali ya Iran,akiongea jinsi gani Iran ilivyo jiandaa na hali hii ya kivita pindipo ikitokea.

Mtuhumiwa wa Guantanamo bay, ala miaka nchini mwake.
Katika harakati za kupingana na ugaidi, serikali ya Tunisia ime muhukumu miaka mitatu jela, mmoja ya watuhumiwa wa ugaidi, ambaye alikuwa ameshikiliwa kama gaidi kwenye jela ya Guantanamo Bay Bwana Lfti Lagha ambaye amakaa Guantanamo Bay kwa kipindi cha miaka 5 kama mtuhumiwa wa kigaidi Jichani hapo ni ya baadhi ya watuhumiwa walio kamatwa na kuwekwa kwenye jela ya Guantanamo. Rais, Putin aonya kuhusu ushindani wa siraha.
Rais wa Rusia, bwana Vladimir Putin, amesema hivi karibuni ya kuwa, kitendo cha Amerika kutaka kujenga mizinga ulaya ya masharika, ni sawa na kipindi kile cha wakati wa Kyuba ilipo kuwa na mizingas ya masafa miaka ya 1960s. Bwana putin aliyasema hayo, alipo kuwa akiongea na viongozi wa Umoja wa Ulaya mjini Lisbon Ureno. Kwa kutaka kujenga rada na mizinga hiyo ndani ya jamuhuri ya Czech, kitakuwa kitendo cha kudharirisha, na kudharau Rusia kijeshi. Na kunahabari ya kuwa huenda bwana Putin akwa waziri mkuu, baada ya kumaliza kipindi chake cha urais mwaka 2008. Picha hapo juu ni rais Putin akisikiliza kwa makini swali kutoka kwa mwandishi wa habari. Wapinzani wa siasa wa zamani wa Nigeria wakutana.
Maneno haya ya methibitishwa kwa vitendo na mshindi wa zawadi wa Nobel kwa uandishi bwana Wole Soyinka.
Baada ya miaka isiyo pungua 40, mwandishi wa vitabu Wole Soyinka ambaye ni raia wa Nigeria, amerudi kujionea mwenyewe hali ilivyo eneo la Biafra, ambalo miaka 40 iliyo pita alikuwa ni eneo lililo kuwa halina usalama na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilikuwa havina muhamana, na vilifanya watu wengi kuathirika.
Mmoja ya watu hawa ailikuwa bwana Wole Soyinka, amabye alifunga miezi 22 na kazi ngumu kwa kupinga jinsi hali ilivyo kuwa ikiendeshwa na serikali ya enzi hizo. Bwana Wole alirudi kuonana na watu walio amrisha afungwe, kwa kupinga serikali nyakati zile.
Pichani hapo juu ni bwana Wole Soyinka akiwa na watu walio mfunga miaaka 40.Kushoto bwana Wole Soyinka akiwa na bwana Ojukwu aliye husika kukamatwa kwa bwana Wole na kulia pichani bwana Wole aliwa na Mej Gowon mmoja ya watawala wa enzi hizo.
Martin Jol yamkuta ya Morinho.
Kizaaza cha kuleta matokeo,aukuifanya timu ishinde, nikitu ambacho kinahitaji,bahati kwa wakati uliopo kama kocha, lakini wapenzi na wanachama pamoja na vibopa, wa timu, huwa siku zote, wanataka matokeo mazuri, na wala siyo kuhisi kitu bahati, kinahitajiika kwenye timu.
Hali hii imemkuta kocha Martin Jol,ambaye kuja kwake wapenzi wa Totenham,kulizaniwa ya kuwa atifanya Tot-ham, kurudia enzi zake za kina Poul Gascoine. Lakini bwana Jol, mambo haya kumwendea vizuri, na hivi sasa hana kazi tena.
Na sasa Tot - ham wamempa kazi kocha mwingine bwana Juan Ramos,ambaye alikuwa akifundisha Sevilla fc ya Uispania.Hii ni katika kujaribu kurudisha hadhi ya wana Tot - ham.
Pichani hapo juu kulia ni bwana Jol aamini kama kazi ndiyo hiyooo imepepea, na kushoto chini ni bwana Juan, akiangalia kwa makini nini la kufanya, kwani kiti moto cha ligi ya Uingereza, huwa kina joto lisilo la kawaida.
Rais mstaafu Joaquim Alberto Chissano avuna alicho panda.
Hivi karibuni, rais mstaafu wa Mozambiki, bwana Joaquim Alberto Chissano, amezawadiwa, donge nono la kiasi cha dolla $ 5-Million, kwa kuwa kiongozi wa kwanza wa Afrika, kufaidiaka na tuzo la Ibrahimu Mo.
Tuzo hili, lilianzishwa na bwana Mo, ili kuwapa heshima wale vingozi ambao wametumikia taifa lao,hasa kwa wakati wa matatizo ya kisiasa na kijamii, na hivyo kujaribu kufanikisha maendeleo ya nchi na wananchi kwa ujumla.
Bwana Chissano, alianza kuwa rais wa Mozambiki, baada ya kifo cha rais wa kwanza wa Mozambiki hayati Samora Machel.
Bwana Chissano alikabiliana na matatizo ya kivita vya wenyewe kwa wenye, kati ya serikali FRELIMO na wapinzani wa serikali RENAMO kwenye miaka ya 80,lakini bwana Chissano alikabiliana na haya, kwa kuleta uelewano kati ya chama chake FRELIMO, cha wapinzani RENAMO.
Namibia ya wa moto kwa Amerika baada ya siri kugundulika.
Serikali ya Namibia ime wafukunza wa amerika wawili, amabao walikuwa wapo nchi, kwa madhumuni ya kukusanya na kulaghai wanamibia kujiunga na kampuni ambayo yana fanya kazi nchini Iraki na Afghanistani.
Kutokana na msemaji wa wizara ya mabo ya ndani, amesema watu hawa ni wawakilishi wa makampuni ya ulinzi yanayo fanya kazi katika nchi za Iraki na Afghanistani na wali kuja kwa madhumuni ya kutafuta watu wa kwenda kufanya kazi za ulinzi kwenye kampuni hizo.
China ya kasilishwa na kitendo cha kumpa nishani Dalai Lama.
Uhusianao kati ya China na serikali ya Amerika, umezidi kuingia doa.
Doa hili limekuja baada ya Amerika kumzawadia kiongozi wa Budha bwana Dalai Lama, nishani ya juu ya dhahabu ya bunge la Amerika hivi karibuni.
Bwana,Dalai Lama amabye ameishi ukimbizini kwa muda usiopungua 48 baada ya jaribio la kutaka kuleta mapinduzi nchini China,hii ilitokana na kutokuelewana na wan nchi wa Tibet.
Hapo juu pichani Dalai Lama, akikaribishwa kwenye baraza la wabunge.
Libya yarudisha vitu ilivyo taifisha wakati wa mapinduzi ya kung'oa Mfalme.
Serikali ya Libya imerudisha vitu na mali zote, ambazo zititaifishwa wakati wa mapinduzi ya kuung'oa utawala wa kifalme wa hayati Idris Senussi , mapinduzi haya yalitokea mwaka 1969. Tangu hapo rais Gaddafi akachukua madaraka.
Katika mali na vitu hivyo pamoja na nyumba inatumika na ubalozi wa Uingereza, kuanzia sasa una mmiliki mpya.
Ni muda sasa serikali ya Libya tangu ianze mpango wa kurudisha vitu na mali ambazo ilizitaifisha kipindi hicho. Hii yote ilitokea wakati hule, kwa kupitishwa sheria ya kuwa serikali pekee yake ndiyo yenye uwezo wa kujenga na kumiliki vitu.
Pichani hapo juu ni kanari, na rais wa Libya bwana M. Gadaffi.
Wazawa walalamika kuhusu mali ya asili.
Kuna habari za kuaminika ya kuwa wapinzani wa serikali ya Sudani wamevamia machimbo ya mafuta, ambayo yanachimbuliwa na makampuni ya kigeni, kutoka nchi za India, China, na Malaysia.Kwa mujibu wa wa masemaji wa mapinzania hao, waliamua kuvamia maeneo hayo na kuteka wa fanyakazi wa makampuni hayo, kwa madai, fedha zinazo tolewa na makampuni haya kigeni kwa serikali ya Sudani zinatumika katika kununulia siraha ambazo zinatumika katika kuwapigia wapinzania hawa na na badala ya kuijenga nchi yao. Msemaji huyu aliongeza kwa kusema ya kuwa hii mali ( Mafuta) ya asili "Imekuwa balahaa kwetu sisi wazawa".
Pichani hapo juu ni wapinzani wa serikali ya Sudani, wakiwa katika mazungumzo.

Thursday, October 25, 2007

Luck Dube, Mungu akuweke mahali pema peponi. Amina.

Hata Beyonce naye alikuwepo,na wengine wengi tu kwenye Karne mpya. Wakati watu wengine duniani walisha adhimisha kuisha kwa karne ya kale.Lakiniwana Ethiopia walikaribisha karne mpya ya 2000th, kutokana na karenda yao ya asili hivi majuzi. Kati ya hao ni mwana dada Beyonce amabye alifanya vitu vyake kwa masaa mawili, mbele ya watazamaji wasio pungua maelfu mjini Addis Ababa, aliimba nyimbo za zake za zamani na kuimba nyimbo zake za albumu ya B'Day. Mwana dada huyu ambaye amenza maonyesho yake ya kuzunguka dunia kwa kupiga muziki wake, atatembelea nchi kama Russia, Romania,Turkey,India, Indonesia, na China. Hapo juu Beyonceeee, akimwaga vitu vyake mjini Addis Ababa - Ethiopia.

Wapendanao, Pitt na Angelina Jolie wanataka kuja na kitu kipya hewani.
Wana sanaa na wacheza sinema maharufu duniani Pitt na mama Angelina Jolie, wanaanza kuaandaa mchezo wa sinema, au (Drama), ambao utazungumzia maisha ya ndani ya wanasiasa, mashirika ya kimataifa jinsi ya vavyo toa misaada, kazi inayvyo fanywa na wafanyakazi wa mashirika haya.
Kama utakumbuka wapendanao hawa wali cheza kwe sinema ijulikana yao kama Mr and Mrs Smith, amabyo iliwapaita sifa nyingi saanaaaaa tu.
Hapo juu pichani, wapendanao hawa, wakiangaliana kwa jicho la haba, na kuku baliana kwa tabasamu. Habib na habibit Manshalahaah, hakuna kinacho haribika.
Wapenzi wa hudhulia kumwombea hayati Luck Dube kanisani.
Luck Dube Mola akuweke pahali pema peponi
Ndugu,jamaa na marafiki walihudhulia, misa ya mwisho ya kuagana na nyota ya muziki wa regge Afrika, na Afrika ya Kusini hayati Luck Dube, amabaye aliuwawa na majambazi wakati wa kijaribu kunyangaya gari lake.
Hayati Luck Dube, alikuwa akishauri kwa kupitia nyimbo zake, kwamba watu waachane na matendo ya ujangili, rushwa, ukabaji wa aina yoyote na mambo mengine mabaya, na watu wajaribu kuwa wanapendana na kukaa pamoja nchini Afrika ya Kusini.
Kwani zaidi ya watu 20,000 wamepoteza maisha yao kipindi cha miaka ya nyuma nchini humo.
Mmoja wa wapenzi wa muziki wake, alisema "Alikuwa akishauri vizuri,na kupinga vitendo vibaya, na leo hii watu wenye kutenda mabaya ndiyo wamemundoa duniani,"Jamani"
Hayati Luck Dube atazikwa 28/10/07 siku ya jumapili na ndugu na jamaa zake wa karibu, kutokan na msemaji wa familia ya marahemu.
Pichani kulia ni baadhi ya ndugu wa hayati Luck Dube walipoahudhulia maombi kanisani, na kushoto ni picha ya hayati Luck Dube na ujumbe "RESPECT"Luck Dube. Anina
Alpha Blondy, muziki wa wake ni dawa na matumaini kwa walala hoi, na wapiganaji pia.
Nchini, Ivory Coast, hasa mji mkuu Abidjani, muziki wa regge ni dawa yetu,wakati wowote, hasa tunapo kuwa tunapingania haki zetu.Haya yalisemwa na mtummoja ambaye akutaka jina lake litajwe.
Aliongeza kwa kusema hata wanajeshi na askari wana pumzika huwa wana burudika na miziki ya regge hasa ya mwana musiki wa hapa nyumbani Alpha Blondy, kwani huwa anakumbusha mambo mengi na kufundisha jinsi ya kupambana ha hali ya dunia ya sasa.
Pichani juu Alpha Blondy akifanya vitu vyake katiak moja ya maonyesho yake ya muziki wa regge.
Mashindano ya kombe la rugbi la dunia kumbe nayo yamo jamani ?
Ina kadiliwa kiasi cha watazamaji wasiopungua millioni 15 1/2 wali pata huhondo wa kuangalia mibaba yenye miraba minne imenyana ili kutafuta nani zaidi, na nani alikula lishe ya maana tangu akiwa mtoto.
Mvuto huu wa watu kukaa ka kula raha za macho kwenye runinga ( TV), ulielekezwa nchini Ufaransa, wakati wa mashindano ya kombe la dunia la rugbi. Na matokeo yake watoto kutoka bara la Afrika wakatokea kuwa washindi wa mchezo huu wa mwaka 2007
Hapo juu ni wapenzi wa rugbi wakiwa wanajiaandaa kuishangilia timu ya kupitai runinga.
Jina la "Bafana bafana" mmghg. Tafuteni jina linalo lingana na asili yetu " Rais Mbeki"
Rais wa Afrika ya kusini bwana Thabo Mbeki, ameomba timu ya mpira wa miguu ya Afrika ya Kusini, kutafuta jina jingine, badala ya ya la sasa , ninalo julikana kwa wengi ka bafana bafana(The boys the boys), rais Mbeki aliendelea kusema, ya kuwa kwa mantiki na ukweli jina hili alivutii, kwa kuzingatia ya kuwa Afrika ya Kusini ndiyo mwenyeji wa mashindano ya Dunia ya 2010. kama mna kumbuka hapo zamani timu zote za michezo zilitwa kwa jina moja Springboks, lakini sasa kila timu ina jina lake , ukinzia kriketi, na michezo mingine, hivyo haileti maana hata kidogo.
Kuzingatia hoja hii iliyotolewa na rais Mbeki, pia kocha wa zamani wa timu ya taifa ya miguu bwana Jomo Sono, amekubalina na rais, na kuongezea ina bidi itafutwe rangi rasmi ya timu za taifa za mpira wa miguu, kwani zimekuwa zikibadilishwa badilishwa kila mara.
Pichani hapo juu , ni wachezaji wa timu ya taifa ya Afrika ya kusini ndani ya ya Jezi zenye raingi tofauti ya timu ya mpira wa miguu wa taifa la Afrika ya Kusini.
Mashindano ya magari F1 yaingia utata kupatikana mshindi wa kweli. Matumaini kwa Hamilton?
Kim Raikkonen, mkimbizaji wa magari aina ya Ferraris, huenda akwanyang'anywa ushindi wake aaliyo upata havi karibuni nchini Brazil.
Hii yote inatokana na kuwepo kwa mvutano kwa kampuni anayo endesha mwingereza Lewis Hamilton, kampunu nyingine na kampuni ya mbio ya Mc Laren ambayo ndiyo iliyo mtoa mshindi wa mbio hozo mwaka huu bwana Kim.
Kabla ya kumalizika mashindano haya, Lewis Hamilton alitalajiwa kwa mshindi, lakini Hamilton, hakuweza kushinda, hasa baada ya kupoteza mashindano ya magari ya Asia bila kutarajiwa. Hata hivyo wapenzi wake Hamilton wakawa na matumaini atafanaya vizuri nchini Brazil,lakini ikaja kinyume, kwa kushindwa bwana Lewis Hamilton na mpinzani wake mkubwa bwana Kim. Pichani hapo juu, Kim Raikkonen na mwenzake Jean Todt wakipongezana, baada ya ushindi wa Brazil.

Monday, October 22, 2007

Mozambiki wataka kujua chanzo cha kifo cha rais Samora Machel.

Madiba Magics naMadiba Boys watawala dunia.

Wa na wa Uingereza kuamua kumpa heshima ya pekee Madiba kwa kuweka sanamu ya kumbukumbu walijua umuhimu wake, na nguvu za Madiba au kama wanavyo ita "Madiba Magics"
Haya yametimia hivi karibuni baada ya timu ya taifa ya (RUGBY SPRINGBOKS), kuitesa vibaya timu ya taifa ya rugbi ya Uingereza kwa mabao 15 kwa 9, kwenye fainali ya mashindano ya dunia ya rugbi, yaliyo malizika hivi majuzi mjini Paris, Ufaransa..
Hapo juu kulia, rais wa Afrika ya Kusini, Thabo Mbeki akinyanyua kombe la dunia la mpira wa rugbi
Viva Madiba viva Madiba and long live madiba magics.
Mozambiki wataka kujua chanzo cha kifo cha rais Samora Machel.
Serikalai ya Mozambiki imesisitiza, lazima ukweli upatikane nani aliye husika katika kifo cha rais wa kwanza wa Moizambiki,hayati Somora Moises Machel. Msisisito huu ulitolewa na waziri anaye shughulika wapiganaji wa zamani, msemaji huyu alisema hatuta tulia mpaka tujue ukweli na chanzo cha ajalihiyo. Rais Hayati Samora Machel alifariki dunia miaka 21 iliyo pita baada ya ajali ya ndege, kutokana na utata wa mawasialiano.
Hayati, Machel alitawala kama rais wa Mozambiki, kwa muda wa miaka isiyopungua 11 wakati wa uhahi wake. Picha hapo juu kataiaka ni hayati Samora Machel akisalimiana na hayati Oriver Tambo enzi hizo za kupingania uhuru wa kusini mwa Afrika
Ndenge ya Lufthansa ya tua kwa ghafla na dharula mjini
nairobi .
Ndege ya shilika la ndege ya Ujerumani ( Lufthansa), imetua kwa ghafla, kutokana dharula iliyo tokea kwenye ndege hiyo.
Msemaji wa polisi amesema, ndege hiyo aliyokuwa ikitokean Afrika ya Kusini, ilibidi ituwe mjini Nairobi baada ya rubani wake kugundua matatizo katika moja ya mashine zinazo saidia ndege kuruka.
Hali hii inakuja baada ya ndege ya moja ya mizigo kuanguka maeneo ya nayo kaliwa na watu mjini Kinshasa DRC ambapo zaidi ya watu 50 walipoteza maisha yao.
First lady aachana na rais wa Ufaransa kwa makubalino .
Rais wa Ufaransa, bwana Nicolas Sarkozy 52, ametangana na mke wake bi, Cecilia Sarkozy, au kwa jina kamili bi, Cecilia Maria Isabel Ciganer Albeniz.. Baada ya kuishi pamoja zaidi ya miaka kumi na mmoja.Kutengana huku kumekuwa kwa mkubaliano ya manufaa ya pande zote mbili. Wachunguzi wa mamboa wanasema makubalianao haya ni manufaa zaidi kwa rais Sarkozy, hasa kwa wakati mgumu aliyo nao na sheria mpya ya kazi, ya kutaka muda wa kufanya kazi uongezeke kiumri.
Bwana Sarkozy, ambaye alioa mara mbili, ana watoto watatu,pamoja waliompata na bibi Cecilia.

Pichani juu na wakati ule wapendanao wakiwa na tabasamu la maana kabisa walipokuwa anakula raha pamoja.

Wataka, msako wa silaha uanze mara moja, kupunguza hatari mitaani Uingereza.
Kutaokana na vitendo vyakinyama, mauaji yanayo endelea miongoni mwa vijana, shirikisho la polisi wenye asili ya kiafrika, linatarajiwa kuiomba serikali ya Uingerezam kuwaruhusu polisi, kuanza kusimamisha vijana wote, mahali popote wa na mahali walipo kwa ajili ya kukagua siraha kama visu, na bunguki ndogo( Pistols), ambazo zinachangia kuhartarisha maisha ya vijana na raia kwa ujumla.
Msemaji wa shilikisho hili, amesema vitendo vya kinyamana, mauaji yanayaotokea hayana rangi, kwani ni vijana wa tabaka zote wanao athirika na jamiii zao pia. Amesema hayo kwa kusisi tiza ya kuwa watu wenye asili ya kiafrika ndiyo wana simamishwa saana zaidi ya mara sita,kulinganishwa na watu wamatabaka mengine, hali hii inaleta mushkeri kwa raia.Lakini hakuna budi hili jambao litendeke ili kuleta usalama kwa wote.
Pichani ni baadhi ya siraha ambazo zilikamatwa na polisi hivi karibuni.
John Howard akalia kiti moto na mpinzani wake mkubwa, bwana Kevin Rudd.
Siasa ya Australia imeingia kwenye mpapambano mkali. Kwani waziri wa sasa wa Australia bwana Howard, amekutana na wakati mgumu, hasa kuzingatia hali ya kivita iliyopo Iraki,ambapo Australia inamajeshi yake kwenye inchi humo, mipango ya kiuchumi na mabadiliko ya hali ya hewa kwani bwana Howard anadaiwa kuwa anapinga makubaliano ya Kyoto kuhusu ubinjani na hali ya hewa.
Pichani, bwana Howard ,akiingia kwenye kiti moto.
Dick Cheney aitahadhalisha Iran kuhusu kujenga mtambo wa nyuklia
Makamo wa rais wa Amerika, bwana Dick Cheney, ameinya Irani ya kwamaba ataruhusiwa kujenga au kuendelea, nampango wake wakutaka kuwa nga nguvu za kinyukria . Amesema ya kuwa kama Iran itasikiliza yanayo takiwa wafanye na mataifa mengine, basi wajue hali haitakuwa nzuri kwao.Huu ni ujumbe ambao tunatuma kwa serikali ya Iran.
Onyo hili linakuja, kufuatia hotuba aliyo toa rais George Bush, kuwa nyukria ya Iran, inaweza kuzua vita vingine.
Na hivi karibuni , mzungumzaji wa kinyukria wa Iran, bwan Ali Larijni amejihudhulu, na hakuna sababu za kujiuhudhulu kwake.
Kwa upande wa serikali ya Irani, imesema mitmbo yao ni kwa aajili ya kupata nguvu za umeme na wala siyo kujenga mitamabo ya siraha. Hapo juu anaonekana bwana Cheney akiongea kuhusu swala hii la Iran hivi karibuni.
Vita vya Kongo DRC na wapinzani vyahatarisha kina mama.
Inakadiriwa kila siku wananchi 1000 wa Kongo DRC, hasa upande wa Kivu, wanahamahama kutoka, eneo moja kwenda jingine, kutafuta sehemu ambayo wanaweza kuwa na usalama kwa maisha yao.
Mapigano hayo kati ya majeshi ya serikali na wapiganaji wanao muunga mkono Gen- Lautent Nkunda, yamekuwa yakiendele sasa kwa muda mrefu, huku marumbano yakiendelea.
Kutokana mmoja wa wakimbizi hawa, anasema kila siku, huwa kukesha usikumzima na mchana wakingojea lini hali ya amani itarudi, kwani vita vinasababisha hali ngumu ya kimaisha"Mkimbizi "
Picha hapo juu aanonekana mama akiwaamebeba, mtoto na baadhi ya mizigo akikimbia vita hivyo. "Jamani vipi Afrika tuta jenga kweli?

Mamruki na askari wa kukodiwa wa Kifaransa aliye sumbua Afrika aaga Dunia.
Askari na mamruki wa kifaransa, ambaye alikuwa , na kazi yakuongoza vita zidi ya serikali za Afrika,hasa inapofika migogoro ya kisisasa, katika nchi hizi, bwana Bob Benard, amefariki dunia hivi karibuni.
Bo Benard, aliusika saana katika vita vya Kongo -Katanga, kataika miaaka ya 1960-1963, baadaye kuhusika na vita vya Komoro, Zimbabwe ( Rodesia) enzi hizo, Benin, Nigeria, na Angola. Bwana Benard alikuwa akijiita (Pirate of Republic)
Raul Castro ashika kiti cha Fidel Castro kwa makini nchini Kuba.
Kwa wa kuba wengi jina Raul Castro siyo geni. Lakini kwa waliowengi Raul Castro, amekuja fahamika baada ya kaka yake , rais wa kwanza wa Kuba , kuanza kuwa na matatizo ya kiafya. Raul Castro aliachiwa madaraka, na kaka yake Fidel Castro,ili aiendeshe nchi kwa amani, na kufuata misingi ya katiba ya Kuba. Raul Castro amekuwa akisifiwa na wachunguzi wa mambo kama anaelekea kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa kiasi. lakini hata hivyo wana siasa wanadai ni mkuba mwenye itikadi kali ya kisiasa kuliko kaka yake. Hivyo ni vigumu kumwelewa kiundani, hata hivyo Kuba bado inashamiri chini ya uongozi wake WaKuba siku zote wana sema viva la Castro,viva la Kuba.