Monday, June 30, 2014

Waasi wa Irak wajitangazia utawala.

Wataalamu wasema Oscar Pistorius ni mzima wa akili.

Pretoria, Afrika ya Kusini - 30/06/2014. Ripoti ya upimaji wa akili ya mwanariadha  maafuru wa Afrika ya Kusini  imetolewa na kukabidhiwa jaji anaye sikiliza kesi hiyo tayari kwa kesi kuendelea.


Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na wataalamu wa kupima akili na utashi, wamesema kuwa " Pitorius ni mzima wa akili."

Akiongea kuhusu ripoti hiyo, jaji anaye sikiliza kesi hiyo, Jaji  Thokozile Masipa amesema, " nimepata ripoti hii leo Jumatatu hasubuhi na bado sijaisoma."

Jaji Masipa, alitoa ruksa kupimwa akili kwa Pistorius, baada ya mwanasheria wake, kudai kuwa mteja wake anamatatizo ya akili kutokana na historia ya maisha yake.

Ripoti hiyo ambayo ina muhusu mwanariadha Osca Pistorius 27,  ambaye alipelekwa kwenye nyumba ya kuangalia mwenendo wa tabia na akili yake ili ilikuweza kufahamu kuwa wakati alipo kuwa akifanya kitendo cha mauaji alikuwa hali ya uzima wa akili au la.
 
Oscar Pistorius akikutwa na hatia ya kuua, huenda hakaukumiwa kwende jela si chini ya miaka 15 au kifungo cha maiasha.

Waasi wa Irak wajitangazia utawala.


Diyala , Irak - 30/06/2014. Kundi linalo julikana kama ISIS lilipo nchini Irak, limetangaza kuwa maeneo ambayo imefanikiwa kuyatwaa yatabadilishwa majina na kuitwa kwa ujumla  kama  majimbo ya nchi za Kiislaam.

Likitoa uthibitisho wa kubadilishwa kwa majina haya, kundi hili lilisema " kuanzia sasa, maeneo ya Diyala  na  jombo la Aleppo yataitwa  kwa pamoja nchi ya Kiislaam na yataongozwa Kiislaam."

Pia kundi hilo liliongeza kuwa " Abu Bakar al Baghdad, ndiye kiongozi wa kundi hilo kwenye eneo hilo zima."
Kundi la ISIS limetangaza hivyo, baada ya miaka kumi kupita tangu jeshi la Marekani na washiriki wake kuiangusha  serikali ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Saadam Hussein.

Kundi hilo limeshutumiwa hivi karibuni kwa kufanya mauaji ya kinyama ambayo yamelaaniwa na mashirika ya haki za binadamu na ya kutetea haki za binadamu, kwa kusema kuwa lazima hatua za kisheria zichukuliwe mapema ili kuhakikisha kuwa mauaji kama hayo yasitokee tena.

Kufuatia kuwa na nguvu kwa kundi hilo ISIS na kufanikiwa kutwaa maeneo inayo yashikilia, waziri mkuu wa Irak Nour al Marik kuomba msaada katika kupambana na kundi hilo, ambalo kwa sasa jeshi la serikali ya Irak linapambana na kundi hilo katika jimbo la Tikrit, ambapo ndiko aliko zaliwa Saadam Hussein.  

Friday, June 13, 2014

Mashindano ya kombe la dunia yaanza kwa vishindo.

Mashindano ya kombe la dunia yaanza kwa vishindo.

Sao Paulo, Brazil - 13/06/2014. Mashindano ya kugombea kombe la dunia kwa mchezo wa soka  yameeanza rasmi huku timu wenyeji kiondoka na ushindi.

Wenyeji Brazili ilibidi wafanye kazi ya ziaada na huku bahati kuwaangukia kwa kushinda magoli matutu kwa moja zidi ya timu ya Croatia katika mechi ya ufunguzi wa mashindano hayo. Magoli ya Brazili yalifungwa na Neymar aliye pachika mabao mawili, moja la penati na Oscar alifunga bao la tatu na Croatia walipata goli baada ya beki wa Brazil Marcelo kujifunga katika harakati za kuokoa mpira usiingie golini

Mashindano ya kombe la dunia yanazishirikisha timu 32 kutoka mabara yote yaliyopo duniani na yanafanyika kwa mara ya ishirini tangu kuanzishwa mwaka 1930.

Mashindano ya kombe la dunia kwa mchezo wa kandanda yanatarajiwa kuwa na msisimko mkubwa na huku baadhi ya washabiki wakitoa matumanini kwa timu mwenyeji Brazil kuibuka na ushindi kwa kubeba kombe hilo tena kwa mara ya sita.


Sunday, June 8, 2014

Viongozi wa Wapalestina na Izrael wakutana Vatican.

 Viongozi wa Wapalestina na Izrael wakutana Vatican.

Vatican City, Vatican - 08/06/2014. Papa Fransis ameongoza ibada ya misa ya amani ambayo iliudhuriwa na viongozi wa juu wa Izrael na Palestina.

Ibada hiyo ambayo ilikuwa na nia ya kuombea amani kati ya Waizrael na Wapalestina, ilidhuriwa na rais wa Izrael Shimon Peres na kiongozi wa Wapalestina Mahamoud Abbas.

Kukutana huko kwa viongozi wa juuu wa jijini Vatican  kumekuja baada ya mwaliko uliofanywa na Papa Fransis baadanya kufanya ziara katika  eneo la nchi za Mashariki ya Kati za Izreal na maeneo ya Wapalestina ilikutafuta njiaa ya kuleta amani katika eneo hilo.

Akiongea baada ya ibada ya misa na kukutana kwa viongozi hao wa kuu wa Wapalestina na Waizrael, Padri Pierbattista Pizzaballa ambaye ni mkuu wa kitengo kinacho simamia masuala ya amani ya Mashariki ya Kati alisema "hatuwezi jidanganya kuwa amani ya Mashariki ya Kati italetwa bila mazungumzo, na ndoyo maaana Papa Fransis ameweka mkakati katika suala hili, na kwa sara na maombi basi mafanikiyo yataonekana."

Viongozi hao wa Palesestina, Izrael na ongozi wa Vatican kwa pamoja walikaa na kuongea ili kutafuta suruhu ya amani katika eneo zima la Mashariki ya kati na kuwa na ujumbe kuwa eneo la Ardhi takatifu lazima liwe na amani.

Hatimaye  Wamisri wapata rais.

Kairo, Misri - 08/06/2014.  Aliyekuwa  wa majeshi ya Misri, Abdel Fattah al Sisi ameapishwa rasmi kuwa rais wa nchi ya M,isri mwaka mmoja baada ya kuongoza mapinduzi ya kuipindua serikali ya kiongozi wa Muslim Brotherhoods Mohammed Mosri

Akiongea mara baada ya kuapishwa kuwa rias Abdel Fattah Sisi alisema" mafanikio ya Wamisri ya po wazi, hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunajenga Misri bora ambayo inaweza zalisha makate, yenye kufuata sheria na haki za binadamu ambazo  zinafuata haki"

Hata hivyo wapinzani wa Sisi, wameeleza wasiwasi wao kuwa "huenda rais  huyu mpya wa Misri akafuata nyayo Hosni Mubaraka"

Rais Abdel  Fattah al Sisi aliapishwa kwenye jengo ambalo aliapishiwa rais  aliyempindua Mohammed Mosri na kuudhuliwa na badhi ya viongozi wa serikali na huku watu wanao mmuunga mkono wakishangilia kwa kupeperusha bendera ya Misri.

Abdel Fattah al Sisi amekuwa rais wa nne kutoka kuwa mkuu wa jeshi hadi kushika nafasi ya uongozi wa juu wa  kiti cha urais.

Uongozi wa Kifalme nchi Uhispania wakubwa na mthiani.

Madrid, Uhispania - 08/06/2014. Mamia ya watu wameaandamana katika jiji la Madrid kwa madai ya kuupinga utawala wa kifalme siku chache baada ya mfalme wa sasa wa Uhispania Juan Carlos 74 kutangaza kuwa anamwachia  kiti cha ufalme mwanae wa kiume Prince Filipe
.
 Maandamano hayo ambayo yalikuwa na nia ya kutaka Uhispania kuwa na serikali ya Jamuhuri, badala ya sasa ambayo inatawaliwa na mfalme.

Mmoja wa waandaaji wa maandamano hayo ana amabaye pia ni mkuu wa chama cha Pademos Pablo Igresias amesema " tunataka suala hili likabidhiwe kwa wananchi, tunaka kura ya maoni ipigwe, na siyo tatizo kama Waispania wakipewa nafasi ya kuamua kwa aajili ya maisha ya baadae ya kila Mspania."

Maandamano hayo yamefanyika ikiwa zimebakia siku 11 kabla ya  mwana wa mfalme Prince Filipe kuapishwa rasmi ili kukabidhiwa kiti cha ufalme wa Uispania.

Uongozi wa kifalme unaungwa na chama kilichopo madarakani  na baadhi ya vyama vikuu vya upinzani,  na Prince Filipe anatarajiwa kukukabidhiwa kiti cha Ufalme Juni 19- 2014 ambapo sherehe hiyo itakuwa ikiendena na shughuli za kibunge katika siku hiyo ya kuapishwa kwa mwana huyo wa mfalme.




Thursday, June 5, 2014

Wakuu wa G7 vichwa kuuma juu ya Urusi.

Rais Bashar al Assad ashinda tena uchaguzi mkuu nchini Syria.

Damascus, Syria - 05/06/2014. Matokeo ya uchaguzi mkuu wa urais  uliyofanyika 03/06/2014 nchi  Syria umempa ushindi mkuu rais wa sasa wa Syria kwa asilimia kubwa.

Bashar al Assad ambaye ndiye rais wa sasa wa Syria na ambaye alikuwa akigombea kiti hicho kwa mara nyingine ameshida uchaguzi huo kwa mara ya tatu kwa asilimia zaidi ya 90 kutoka kwa wapiga kura milioni 10.

 Hata hivyo matokeo ya ushindi  wa kura wa rais Bashar al Assad, umepingwa vikali na serikali za Marekani na washiriki wake kwa kudai ya kuwa " Uchaguzi huo haukuwa wa maana na hakuwa wa halali na ni uchaguzi sifuri."

Hata hivyo Iran ambayo ni mshiriki mkuu wa serikali ya Syria imesema
"kitendo cha kuchaguliwa tena rais  Bashar Hafez al Assad ni pigo kwa wapinzani wa watu wa  Syria, na hasa ni kitendo cha aibu kwa Marekani na washiriki wake kwani hawapo kwa aajili faida ya watu wa Syria bali wanacho angalia ni maslahi yao"

Syria imekumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya wale wanao unga mkono serikali ya rais Bashar al Assad na wapinzania wake jambo ambalo limesababisha maelfu ya Wasyria kukimbia nje ya  nchi na mamia kupoteza maisha yao.

Rais Bashar al Assad, ameshinda uchaguzi huo ambao ulikuwa wa vyama vingi na anatarajiwa kushika utawala wa kiti hicho cha urais kwa muda wa miaka saba ijayo.

Rais  Vladmir Putini ataka ushahidi uonyeshwe hazarani.

Paris, Ufaransa - 05/06/2014. Rais wa Urusi amezitaka Marekani na washiriki wake kuonyesha ushaidi kwa jumuiya ya kimataifa kuwa majeshi ya Urusi yapo nchi Ukraine.

Rais Vladmir Putin aliyasema hayo wakati alipo kuwa akiongea na waandishi wahabari jijini Paris, ambapo amewasili nchini Ufaransa kwa ajili ya sherehe za kumbukumbu ya miaka 70 ya vita vya pili vya dunia.

Akiongea rais Putini alisema " ni jambo la kushangaza, ikiwa kuna wanajeshi wa Urusi nchini Ukraine mbona mpaka sasa hawajaonyesha ushahidi"

" Dunia nzima inakumbuka wakati Marekani ilipo toa ushaidi kuwa Irak ina siraha za sumu, kuwa kuonyesha, malori na chupa zilizo kuwa na unga aina ya poda ambazo walidai sumu na ni za Saddam Hussein, na kwa kigezo hicho wakavamia Irak na baadaye Saddam Hussein alinyongwa, muda haukupita ikajulikana kuwa Irak haikuwa na siraha za sumu."

" Na ushahidi kuhusu Irak, ulitolewa mbele ya kamati ya usalama ya Umoja wa Mataifa, hivyo napenda kukumbusha kuwa, kuongea ni vyepesi na kutoa ushaidi wa huhakika ni hali nyingine."
 
Akisisitiza rais Putini alisema "baada ya mapinduzi ya serikali nchini Ukraine Februari mwaka huu,  Urusi iliunga mkono na kusimamia kura ya maoni ya jimbo Cremia kutaka kujiunga na Urusi, kwani hii niuamuzi wa watu wa Cremia na hii ipo katika kifungu cha 1 cha katiba ya Umoja wa mataifa."

Maelezo hayo ya rais  Putin yamekuja baada ya Marekani na washirika wake kudai kuwa Urusi ndiyo chanzo cha vurugu zinazo endelea nchi Ukraine.

Hata hivyo, rais Putin alisema kuwa yupo tiyari kukutana na kiongozi yoyote kuongea naye kuhusu  masuala ya kimataifa ikiwemo ya Ukraine wakati atakapo kuwa nchini Ufaransa, na kama rais wa Marekani yupo tiyari, basi yeye hanakipingamizi.

Wakuu wa G7 vichwa kuuma juu ya Urusi.

Brussels, Ubeligiji - 05/06/2014. Viongozi wa nchi za G7 au nchi zenye maendeleo ya kiuchumi wameionya Urusi kuwa huenda ikakumbwa na vikwazo zaidi ikiwa haita badili mwenendo wake kwa nchi ya Ukraine.

Onyo hilo lilitolewa na rais wa Marekani Baraka Obama , mara baada ya mkutano wa pamoja na viongozi wenzake wa G7 na uongozi wa jumuiya ya nchi za umoja wa Ulaya.

Rais Obama alisema " dunia inategemea uchumi shirikishi unaokuwa kwa pamoja, leo Urusi inajikuta haipo katika kuinuua uchumi wake, kwa ajili ya uchaguzi potofu unaofanywa na uongozi wa Urusi."

" Hivyo ipo haja ya Putin kuitambua serikali ya rais Petro Poroshenko na pia kusimamisha upelekeji wa siraha kwa wapinzani wa serikali ya Ukraine."

"Putin ananafasi ya kufuata sheria za kimataifa" Aliongezea rais Obama.

Mkutano wa wakuu wa G7, imefanyika baada ya ule mkutano  uliyokuwa ufanyike wa nchi za G8  kwenye mji wa Sochi Urusi kugomewa na Marekani na washiriki wake, kwa madai kuwa Urusi imejiingiza katika masuala ya Ukraine.


Wednesday, June 4, 2014

Marekani yahaidi kuwa karibu na Ukraine.

John Kerry afanya ziara ya kustukiza nchini Lebanoni.


Beiruti, Lebanoni - 04/06/2014. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani amewasili nchi Lebanoni ili kujua ni kwakiasi gani Marekani itasaidiana na viongozi wa Lebanoni ili kutatua suala la wakimbizi.

Akiongea mara baada ya kufika Lebanoni na kujionea mwenyewe ni kwa jinsi gani serikali ya Lebanoni inavyo kabiliana na  hali ya wingi wa wakimbizi, waziri John Kerry alisema '' nimuhimu kwa serikali ya Lebanoni ikasaidiwa katika swala zima la kusaidia wakimbizi kwani hili nijukumu la kimataifa''

Kufatia zira hiyo ya John Kerry, Lebanoni inatarajiwa kupata msaada wa dola $51million ili kuweza kukabiliana na wimbi la wakimbizi wanaoingia nchi humo toka Syria ambapo bado vita vya kutaka kuing'oa serikali ya rais bashar al Assad.

Lebanon imekuwa katika myumbo wa kisiasa kwa muda mrefu, na tatizo la ongezeko la wakimbizi kukimbilia nchini humo limefanya jamii ya Walebanoni kuwa na upinzani mkubwa kwa kuwepo kwa wakimbizi wanao ingia nchini humo wengi wao kutoka Syria.

Marekani yahaidi kuwa karibu na Ukraine.

Warsaw, Poland - 04/06/2014. Serikali ya Marekani imehaidi kuongeza misaada kwa serikali ya Ukraine, ili kuweza kupambana na wapinzani wanaotaka kuigawa nchi hiyo.

Haadi hiyo ilitolewa na rais wa Marekani Baraka Obama wakati alipo kutana na rais wa Ukraine Petro Poroshenko jiji Warsaw.

Rais Obama alisema '' kitendo cha wanachi wa Ukraine kumchagua Petro Poroshenko ni cha busara kwani  ni mtu atakaye waongoza kwa bora zaidi.''

'' Na serikali ya Marekani itatoa pesa kiasi cha dola billion 5$ ili kusaidia Uikraine kutokana na hali iliyopo ili kulinda usalama wake''  Tangu mwezi Machi serikali ya Marekani imesha toa dola $23million kwa Ukraine.

Kabla ya kuchaguliwa kuwa rais katika uchaguzi uliyofanyika May 25, Petro Poroshenko, alikuwa mfanya biashara ambaye alikuwa akishughulika na uuzaji wa vyakula hasa chololati na bidhaa zinazo endana na mikate na kupewa jina la Mfalme Chokolati.

Tuesday, June 3, 2014

Abdul Fattah al Sisi ashinda uchaguzi wa Urais nchini Misri.

Rais Obama atangaza msaada kwa NATO.

Warsaw, Poland - 03/06/2014. Serikali ya Marekani imetangaza kutoa pesa ili kusaidia   kuikuza NATO kiulinzi kwenye bara la Ulaya.

Hayo yalisemwa na rais Baraka Obama wakati alipo kuwa akihutubia jiji Warsaw, Poland wakati wa alipokutana na wanajeshi wa Kimarekani waliopo nchini humo.

Rais Obama alisema "tukiwa marafiki na washirika wakubwa ni jukumu letu kujilinda kwa pamoja, na naomba wabunge wa kongresi waunge mkono wito wakukubali kutoa dola billion moja ilikuweza kufanikisha lengo hili kwani usalama wa washiriki na marafiki zetu ni usalama kwetu pia."

 |April mwaka huu wanajeshi 150 wa Kimarekani waliwasili nchini Poland, baada ya hali ya machafuko kuongezeka nchini Ukraine.

Rais Baraka  Obama alipokelewa na mwenyeji wake rais Poland Bronislaw Komorowsiki kwenye uwanja wa Kijeshi ambapo ndipo waliongea na kutoa hotuba kwa pamoja.

Baada ya kumaliza ziara yake nchi Poland rais Obama atatembelea  nchi Ubeligiji na baadaye pia kuwasili Ufansa ili kuhudhuria sherehe ya miaka 70 tangu kuisha vita vya pili vya dunia.

 Waziri mkuu wa Uturuki akemea CNN.


Istambul, Uturuki - 03/06/2014. Waziri mkuu wa Uturuki ameyalaumu mashirika ya habari ya nchi za magharibi kwa kutangaza habari kwa kupendelea na pia kuwa kama makampuni ya makachero.

Waziri mkuu  Recep Tayyip Erdogan aliyasema hayo wakati alipo kuwa akihutubia katika mkutano wa wanachama wake wa chama cha AK  na kutoa mfano kuwa  CNN ni moja ya shirika la habari ambalo limekuwa likifanya kazi yake kama ofisi ya kikachero.

Akiongea waziri mkuu Erdogan alisema "CNN ilitumia masaa nane wakati wa siku ya kumbu kumbu ya Gezi, na mwaka huu wamekamatwa na kuonyesha kuwa hawafati maadili ya uandishi na kazi yake ni kuchangia kuvuruga nchini."

"Ni jukumu langu kuhakikisha Uturuki inakuwa salama kwa kila mtu, na polisi wanatakiwa kufanya kazi yao bila kuingiliwa ili kuleta usalama na nitawalinda kwa hali na mali."

"Mbona hawaonyeshi yanayo fanywa na polisi nchini Marekani au Uingereza?" 

Waziri mkuu Tayyip Erdogan, alilitaja shirika la habari la CNN kuwa katika ripoti yake ya vurugu zilizo tokea mwaka 2013 katika kiwanja cha Taskim, ilikuwa ni kwa ajili ya manufaa ya nchi za kigeni na mpaka sasa bado mashirika hayo yanania ya kukuza mvugo wa amani nchini Uturuki. 

Kuongea huko kwa waziri Erdogan umekuja baada ya mmoja wa waandishi wa habari wa CNN kukamatwa wakati wa maandamano na baadaye kuachiwa  huru baada ya kuwekwa chini ya ulinzi kwa muda wa zaidi ya dakika 45.

Abdul Fattah al Sisi ashinda uchaguzi wa Urais nchini Misri.



Kairo, Misri - 03/06/2014. Matokea ya uchaguzi nchini Misri yamempa ushindi mkubwa Abdul Fattah al Sisi ambaye alikuwa anagombania kiti cha urais.

Sisi ambaye alikuwa mkuu wa majeshi na kuachia magwanda Machi 26 2014, ameshinda kwa wingi wa kura za asilimia 96.91 katika uchaguzi mkuu uliyo fanyika Misri.

Ushindi huo wa Sisi, umekuja miezi tisa tu, baada ya kuhusika katika mapinduzi ya serikali ya rais Mohammed Morsi  na  ambaye alimchagua Sisi kuwa mkuu wa majaeshi. 

Tangu kuangushwa kwa serikali ya Hosni Mubara mwaka February 11/ 2011, Misri imekuwa na misukosuko ya kisiasa na kupelekea kuvuruga  nchini humo, jambo ambalo Sisi amehaidi kulipatia jibu na pia kusema "itachukua miaka 25 ili kuleta demokrasi kamili nchi Misri."

Abdul Fattah al Sisi anatarajiwa kuapishwa kuwa rais siku ya Jumapili wiki hii.

Mwizi wa kimtandao atafutwa kwauvumba na ubani.


Washington, Marekeni - 03/06/2014. Marekani inamsaka raia wa Urusi ambaye alifanikiwa kuingia katika mfumo mzima wa kimtandao na kuiba mamilioni ya pesa katika mabenki tofauti duniani.

Evgenivy Bagacgev 30 ambaye ametajwa kama mtuhumiwa wa wizi wa kimitandao, anatakiwa kujibu mashitaka ya kuhusika na kutengeneza mfumo wa kimtandao ambao uliweza kutengua mfumo mama wa kiulinzi wa kibenki na kuweza kupenyeza na kuiba pesa tangu 2006. 

Akiongea mara baada ya kutoa wajihi wa mtuhumiwa, mmoja  wa mkuu wa kitengo cha usalama wa mitanndao wa  Marekani Leslie Caldwell  alisema "mfumo aliyotengeneza Bagacgev ni wa hali ya juu na ilikuwa vigumu kuugundua, na hii tuliweza kugundua kwa kushirikiana na nchi 10 ambazo zilikumbwa na matatizo haya na hivyo lazima atafutwe kwa uvumba na ubani"

Evegenivy Bagacgev anasemekana kwa mara ya mwisho alionekana katika maeneo ya Black See kwenye kitongoji cha Anapa akijiliwaza .

 Wapalestina wapata serikali mpya.


Ramallah, Palestina - 03/06/2014. Wapelestina wamepata serikali ya muungano, ambayo itakuwa na kazi kubwa ya kuuanda matayarisho ya uchaguzi mkuu wa rais na wabunge.

Serikali hiyo ambayo imeunganisha vikundi vya Hamas na Fatah, itakuwa na viongozi 17 kutoka pande zote. 

Kuundwa huko kwa serikali ya muungano, kumekuja baada ya majadiliano yaliyo chukua wiki tano na kufanikiwa kufikia tamati kwa makubaliano ambayo yalifanyika April 23 mwaka huu.

Akiongea mara baada ya kuundwa na kula viapo kwa viongozi wapya wa Kipalestina, rais wa Wapelestina Mahamoud Abbas alisema "serikali hii itakuwa ya mpito, na maswala ya ukombozi wa Wapalestina katika majadiliano ya amani na Izrael yapo chini ya PLO - Palestina Liberation Organasation, na serikali hii kama serikali zilizo pita, itafuata na kutii sheria zilizo sainiwa hapo awali."

Hata hivyo kitendo cha Fatah na Hamas kuungana na kuunda serikali, kimepingwa vikali na Izrael, na kuitaka Marekani kutounga mkono serikali hoyo.

Uchaguzi mkuu wa kuchagua viongozi kwa Wapalestina unatarajiwa kufnyika mwaka 2015

Mfalme wa Uispania kuachia madaraka.

Madrid, Uispania - 03/07/2014.Mfalme wa Juan Carlos Uispania ametangaza kuachia kiti cha ufalme, baada ya kukikalia kwa miaka arobaini.

Akiongea kumwakilisha Mfalme Juan Carlos, waziri mkuu wa Uspania Mariano Rajoy alisema " Mfalme Juan Carlos ameamua kuachia uongozi wa kifalme, ili kutoa nafasi kwa kizazi kipya na pia nakuwa na matumaini katika kurekebisha makosa ambayo yametokea katika harakati za  kuijenga na kuimarisha Uispania"

Mfalme Juan Carlos, amependekeza kuachia kiti hicho kwa mwanae 46 Prince Phillipe, ambaye anatazamiwa kuwa mfalme wa kizazi cha kisasa na kuwa na majukumu  magumu ya kuimarisha ufalme, kutokaa na baadhi ya kashfa kuzuka katika ufalme huo.
 Na vile vile kutokea upinzani wa hapa na pale  wakupinga uongozi wa Kimfalme nchi Uispania