Friday, June 27, 2008

Licha ya joto ya siasa kuwa juu nchini Zimbabwe" Siasa na Uchumi haviko sawa" Kampuni kuendela na uchimbaji madini.

Billy Gates,aamua kutumia muda mwingi kujitolea kwa jamii".

Los Angeles, US - Mwenyekiti na mwanzilishi wa kampuni inayo shughulikia mtandao duniani bwana Billy Gates, ameamua kutangaza ya kuwa atatumia muda wake mwingi , ili kuweza kusimamia na kuendesha shughuli zake za kusaidia na kutoa huduma kwa jamii kupitia shirika alilo lianzisha mapema miaka ya nyuma lijulikanalo kama Billy and Melinda Gate Foundation.
Shirika hilo ambalo Billy pamoja na mkewe Malinnda wamakuwa wakisimamia, limekuwa likitoa misaada kwa jamii kwa kiasi kikubwa sana.
Billy mwenye miaka 52, alianza shughuli za mtandao wakati akiwa na miaka 13.
Billy aliamua kuachana na masomo ya elimu ya juu katika chuo kikuu cha Harvard, na kuamia New Mexico,mahali ambapo yeye na rafiki yake Poul Allen, walianzisha mtandao wa microsoft mwaka 1975. Mwenyekiti , Billy Gates, alisema mafanikio ya microsoft yametokana na jitihada za wafanyakazi wenzake.
Picha ya kwanza anaonekana mstari wa chini kushoto anaonekana Billy Gates, akiwa na washiriki wenzake mwaka 1978.
Picha ya pili, baada ya kucha kuendelea na masomo ya juu, hivi karibuni Billy Gates kushoto, alitunikiwa shahada ya juu na na chuo kikuu cha Harvard mwaka 7/6/2007.
Picha picha ya tatu,anaonekan ni jinsi gani Billy Gates alivyo kuwa anafikilia ni nini afanye ili aweze kufanya dunia iwe sehemu ya usawa na kusaidiana.
Picha ya mwisho , Billy Gates akiwa na Malkia Elizabeth wa Uingereza, wakati alaipo mtunukia nishani mwaka 2005
Lisha ya joto ya siasa kuwa juu nchini Zimbabwe, "Siasa na Uchumi haviko sawa".Kampuni kuendelea na uchimbaji.
Harare, Zimbabwe - Kampuni kubwa duniani inayo shughulikia uchimbaji wa madini Agro American, imesema yakuwa itaendelea na mradi wake wa uchimbaji wa madini aina ya platinum nchini Zimbabwe.
Kwa mujibu wa kampuni hiyo, imesema kuwepo kwa Agro American nchini Zimbabwe tangu miaaka ya 1960 na mradi huu umekuwa ukiendelea tangu mwaka 2003 na vilevile kunainua maisha ya wafanyakazi ambao no raia wa Zimbabwe.
Inaaminika ya kuwa mradi huu utagharimu zaidi ya $US 400million na utakuwa ni wa kwamza katika nchi za kigeni.
Hata hivyo Agro American, imesema ya kuwa serikali ya Zimbabwe imnapaswa kulifikilia swala la kisiasa linavyo kwenda nchini Zimbabwe.
Picha ya kwanza hapo juu wanaonekana wafanyakazi wakiwa ndani ya ardhi wakielekea kuchimba madini.
Picha ya pili hii ni moja ya picha ya maeneo ambayo huwa yanachimwa madini.
Picha ya tatu, wanaonekanawafanyakazi wakiwa wanatumia nyenzo nzito kuchimba madini,
Vita Afriaka, vinaghalimu kiasi cha mabillioni ya US $ dola, "na wanamama wawa waathirika".
UN, New York - Kiasi cha zaidi ya mabillioni ya fedha yanatumika kufadhili vita katika nchi za bara la Afrika imeripoti shilika moja la kutoa huduma la Oxfam lililopo Uingereza.
Kwa mujibu wa ripoti iliyo tolewa na mapema mwisho wa mwaka 2007, imeonyehs aya kuwa tangu mwaka 1990 hadi kufika mwaka 2005 zaidi ya nchi zisizo pungua 23 zilizipo barani Afrika zilimekuwa navita au zilicha wahi kuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe au nchi kwa nchi na kughalimu zaidi ya $ US billioni 300.
Kwa mujibu wa ripoti hii, pesa nyingi zimekuwa zikitumika kununulia siraha, nakuagiza lazima kuwepo na sheria ya kuchunguza ni jinsi gani siraha hizi zinapatikana kutoka nje ya bara la Afrika.
Wati huo huo shirika la jingine linalo shughulikia utoaji wa misaada na huduma kwa watoto, UNICEF, limesema ya kuwa vita vinavyo endelea katika bara la Afrika vimekuwa vinaleta athali nyingi katika jamiii, hasa kwa kina mama na watoto.
UNICEF, ililipoti hivi mapema mwaka huu ya kuwa wanawake wamekuwa wakibakwa, ( kufanya mapenzi kwa kutumia nguvu bila hiyari ya mtu), hali hii imekuwa pia ikifanywa na hata raia na baadhi ya wapiganaji( wanajeshi wa vikundi vinavyo pigana).
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wanawake wakijaribu kuingia katika moja ya jengo la serikali ili kuokoa maisha yao, baada ya kutokea vurugu na mapigano ya kutumia siraha kwenye maeneo wanaoishi.
Picha ya pili wanaonekana baadhi ya wapiganaji wa moja ya vikundi, ambavyo wakati wanapo pigana na vikundi vingine huwa hali ya ubakaji wa wanawake hutokea na pengine wanawake hawa hupoteza maisha yao.
Picha tatu, anaonekana mmoja ya mwanamama akilia kwa uchungu na huku amejiinamia baada ya kumaliza kueleza yaliyo mkuta wakati wa vurugu na mapigano na pembeni ni mtoto wake akiwa ananagalia na hajui nini kimemkuta mzazi wake.
Nchini zilizopo pembe ya Afrika mashakani"Huenda zikakumbwa na vita".
Bruseli, Belgium - Shirika moja linalo shugulika na kutathmini matatizo na majanga dunia, limesema yakuwa hali ya ilivyo hivi sasa pembezoni mwa pembe ya bara la Afrika huenda ikakumbwa na janga la kuibuka vita kati ya nchi ya Ethiopi na Eritrea.
Shirika hilo ambalo silo la kiserikali, limesema ya kuwa, mbele ya balaza la umoja wa Mataifa, linalo shugulikia usalama, ya kuwa umoja wa mataifa hauangalii kiundani na kutilia mkazo jinsi ya kusuruhisha mgogoro ulipo kati ya nchini hizi mbili.
Hata hivyo shirika hilo , liliagiza ya kuwa ule mkataba wa amani ulikubaliwa mwaka 2000, utekelezwe na nchi hizo mbili zikae na kujadili ni jinsi gani zitatatua mgogoro huo.
Picha hapo juu wanaonekana kijana mmoja akiwa ameshikila pisto ambayo ailikuta imeachwa njiani,katika moja ya maeneo yanayo zungumziwa na shirika linalo shughulika matatizo na kutathmini hali ya majanga duniani.
Picha ya pili inaonyesha ni jinsi gani vita vinapo piganwa katika nchi yoyote, basi watoto na wakina mama ndiyo huwa wanahathirika na hali hii, hapo juu anaonekana mtoto mmoja ambaye afya yake ni dhofu kwa kukosa lishe na matibabu, kwa sasbabu vita bado vinaendelea katika eneo la pembe ya Afrika.
Korea ya Kusini ya onyesha matumaini kwenye jumuia ya Kimataifa.
Pyongyang, Korea ya Kusini - Serikali ya Korea ya Kusini,leo tarehe 27/06/2007, imevunja na kubomoa sehemu moja ya kiwanda kilicho kuwa kikitumika kutengenezea nguvu za kinyuklia.
Mlipuko mkubwa, ulisikika mbele ya waangalizi na wakaguzi wa nguvu za nyuklia wa kimataifa na huku baadhi ya waandishi wa habari wakishuhudia uvunjwaji huo, ilikuiakikishia jumuia ya kimataifa ya kuwa Korea ya Kusini, ipo mbioni kutekeleza azma yake ya kuacha kabisa kuendelea na harakati za kujenga nguvu hizo za kinyuklia.
Kitendo hicho cha serikali ya Korea ya Kusini, kimekaribishwa na jumuia ya kimataifa ikiwemo waasimu wake wasikunyingi ambayo ni serikali ya Amerika.
Picha hapo juu linaonekana moja ya kinu kilicho kuwaa kikitumika kuendeshea mitambo ya nguvu za kinyuklia kiporomoka.
Picha ya pili wanaonekana baadhi ya wafanyakazi wa serikali ya Korea ya Kusini, wakiwa kazini katika moja ya idara zinazo shughulika nguvu za mitambo ya kinyuklia.
Picha ya tatu. serikali ya Korea ya kusini ikionyesha moja ya siraha zake za kivita katika moja ya siku za sherehe za kimataifa.

Tuesday, June 24, 2008

Jumuia ya waandishi wa habari yapata msiba mkubwa" Tim Russert atupo naye tena"

Hali ya afya ya nyota ya muziki nchini Uingereza yaleta mashaka kwa wapenzi wamuziki wake.

London- Uingereza - Mwanamusiki maarufu nchini Uingereza Amy Winehouse, ameruhusiwakutoka hospital hivi karibuni, baada ya kupata matibabu ya mapafu na tiba nyingine za mwili. Amy Winehouse, ambaye inasemekana amekuwa akiishi maisha yasiyo ya kwaida kwa kujihusihsa saana na vilevi vingi na uvutaji wasigara ndivyo vinasadikiwa vina athiri afya yake. Pichani hapo juu anaonekana bi Amy Winehouse akiwa anatumbwiza wapenzi wake hivi karibuni kabla ya kupelekwa hospitali. Picha ya pili anaonekana bi, Amy Winehouse, akivuta sigara, punde tu alipotoka hospitali kwa matibabu.
Jumuia ya waandishi wa habari yapata msiba mkubwa"Tim atupo naye tena".
Washington, Amerika - Mkubwa wa shirika la utangazaji la NBC lililopo jiji Washington, bwana Tim Russert, alifariki dunia siku ya ijumaa iliyopita kwa ugonjwa wa moyo.
Hayati, Tim Russert aliajisikia vibaya wakati alipo kuwa kazini tayari kuanda kipindi kijulikacho kama 'meet Press' na baadaye kukimbiziwa hospitali ambapo alizidiwa na kuaaga dunia.
Hayati Tim Russert, atakumbukwa kwa umaili wake wakuuliza maswali na umakini wa kuelewa nini la kufanya katika fani hii ya uandishi wa habari.
Picha hapo juu ni picha ya familia ya ya hayati Tim Russert, kati ni picha ya mjane bi, Maureen Orth na kushoto ni mtoto wao Luke Russert.
Chini wanaonekana baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wakilipokea jeneza la hayati Tim Russert wakati walipo kwenda kumwaaga kwa mara ya mwisho.
Picha ya tatu, anaonekana hayati Tim Russert, akizungumza na papa Benedict XVI, wakati alipotembelea nchini Amerika hivi karibuni.
Picha ya mwisho, anaonekana hayati Tim Russert, alipokuwa kazini enzi za uhai wake.
Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amin.
Hali ya watu wanao penda kuishi kwa jinsia moja ni moto wa mbali nchini Uganda.
Kampala, Uganda - Serikali ya Uganda imewafungulia mashitaka waandamanaji watatu ambao walikuwa wakiandamana hivi karibuni wakati wa kuadhimisha siku ya mkutano wa unaozungumzia ugonjwa wa ukimwi.
Watu hao watatu ambao waliooshutumiwa kwa kupita na kufika maeneo yaliyo zuiliwa kuingia.
Watu hao watatu, walikuwa wakifanya hivyo kwa kutaka uongozi wa serikali ya Uganda kuwakubali watu wainao penda kuishi kijamii moja kama mke na mume au ushoga.
Kwa mujibu wa masemaji mmoja wa watu hao, alisema yakuwa ni muhimu watu wawatambue na kuwakubali watu waina hii wanao pendelea mashoga.
Hata hivyo serikali ya Uganda hairusu ushoga na ni kosa la kisheria katika jamii.
Picha hapo juu ni picha ya bendera ya Uganda.
Picha ya pili na ya tatu ni picha ya baadhi ya watu wanao penda kuishi kijinsia moja huruhusiwa hasa katika nchi za magharibi kisheria.
Kanisa lapiga marufuku kutumia kanisa kupiga picha za sinema.
Rome, Itali - Uongozi wa kanisa Katoliki mjini Rome, umepinga na kukataa kuruhusu upigaji wa picha za sinema zinazo zungumzia habari kuhusi kitabu kijulikanacho Da Vinci Code.
Hadithi za kitabu hiki ambacho kinapingwa vikali na uongozi wa kanisa la jumia ya Kikatoliki kwa kupotoshwa maadili ya Kanisa zima la Katoliki.
Picha za sinema zilitakiwa kupigwa katika makanisa ya Santa Maria del Popolo na Santa Maria della Vittoria ambayo yapo kataika jiji la Rome.
Picha hapo juu inaonesha moja ya sehemu ambazo wapigapicha wanahitaji kutumia katika kupiga picha ya sinema ya Da Vinci Code.
Picha ya pili inaonyesha picha ya kitabu ambacho maandishi yaliyomo yalitakiwa kuwekwa katika wa sinema(film).
Picha ya tatu anonekana mmoja wa wacheza sinema ya Da Vinci Code, akiwa kazini anafanya vitu vyake.
Ajali ya meli yaleta msiba mkubwa nchini Philippinzi.
Cebu, Philippinzi - Wazamiaji ambao wapo mbioni kutafuta miili ya watu ambao waliokuwemo kwenye meli yenye uzito upatao tani 23,824 ,ambayo ilipinduka ilipo kuwa ikifanya safari zake zakawaida.
Meli hii imesadikiwa ya kuwa ilikuwa imechukua (beba) zaidi ya wapatao 8000.
Ajali hiyo ilitokea hivi karibuni, wakati wa machafuko ya hali ya hewa yaliyo tokea hivi karibuni nchini Philippinzi.
Hata hivyo msemaji mmoja wa serikali, alisema yakuwa watu wapatao 43, walipona kutokana na janga la ajali hii ya meli.
Picha hapo juu ni picha ya meli ambayo imepinduka hivi karibuni na inasadikiwa kupoteza maisha ya watu wengi kwa wakati mmoja.
Picha ya pili, wanaonekana baadhi ya ndugu na jamaa wa watu waliosafiri na meli hii iliyo pinduka, wakibandika picha za ndugu zao kwenye ofisi ya shirika la meli ambayo ndiyo mmiliki.
Abu Hamza Al Masri ashindwa" Huenda akapelekwa Amerika kujibu mashitaka".
London - Uingereza - Mahakama kuu ya Uingereza imeidhinisha kupelekwa kwa Abu Hamza Al Masri nchini Amerika kujibu mashitaka ya dhidi ya ugaidi.
Abu Hamza Al Masri, ambaye anatumika kifungo cha miaka saba kwa kosa la kushawishi ugaidi nchini Uingereza.
Abu Hamza Al Marsi 51, ambaye alidai yakuwa alipoteza jicho lake na mkono wake alipo kuwa nchini Afghanistan, anakabiliwa na mashitaka yapatayo 11 ikiwemo kuhusika kwake katika utekaji nyara wa watalii mwaka 1998 nchini Yamen.
Picha hapo juu ya bwana ,Abu Hamza Al Masri anayetuhumiwa kuhusika na makosa ya ugaidi.

Wednesday, June 18, 2008

Viongozi waasimu wawili wa nchi jirani kukutana kwenye mkutano"Asema waziri wa mambo ya nje".

Mfalme wa mtindo wa samba afariki dunia. Rio De Jenairo, Brazil - Aliyekuwa bingwa wa kuimba na kucheza mtindo wa samba nchini Brazil, bwana Jose Bispo Clementino aliye kuwa na miaka 95, amefariki dunia hivi karibuni. Mwana muziki huyu ambaye ametamba katika mtindo huu wa samba zaidi ya miongo mitano alifariki katika hospitali ya Rio. Jose Bispo Clementino, alizaliwa mjini Rio De Jenairo 1913, atakumbukwa kwa maneno yake matamu matamu ya kuwa anapenda miziki na vimwana kwake sio kazi kubwa kuvinjari nao. Pichani hapo juu anaonekana hayati Jose Bispo Clementino, alipo kuwa akifanya vitu vyake enzi ya uai wake.Mungu ailaza mahari pema peponi roho yake Amin. Mtuhumiwa aliyetaka kuongoza mapinduzi ya kupindua serikali ya Ekwetoria Guinea angoja nini pitalato atasema.

Malabo, Ekwetoria Guinea - Aliyekuwa mmoja ya watuhumiwa ambao walihusika katika jaribio la kutaka kumpindua serikali ya Ekwetoria Guinea huenda akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela.
Mtuhumiwa huyu bwana, Simon Mann, ambaye inasadikiwa alikuwa ni mmoja wa watu waliokuwa mstari wa mbele kutaka kuongoza mapinduzi ya kuingoa serikali ya Ekwetoira Guinea.
Bwana Simon Mann, aliye kamatwa nchini Zimbabwe, alikili kwa kukubali makosa haya wakati alaipo kamatwa 2004, muda baada ya kabla ya mapinduzi haya kutokea na alidai ya kuwa hakuwa peke yake wapo wakubwa wake.
Hata hivyo viongozi wa serikali ya Ekwetoria Guinea, walidai ya kuwa bwana, Simon Mann, alikuwa kama chambo lakini wahusika wakuu wapo.
Kesi hiyo ambayo ina muhusisha bwana Mark Thatcher, mtoto wa waziri mkuu wa zamani wa Uingereza,bi Magreth Thatcher,ambaye inasemekana ndiye aliye kuwa mfadhili mkuu,na bwana Mark Thacher, alihukumiwa kwa kutozwa fini na kifungo cha nje.
Picha hapo juu ni picha ya bwana Simon Mann, akielekea mahakamani kusikiliza kesi yake.
Picha ya pili ni picha ya Mark Tharcher, ambaye inasemekana alikuwa mfadhili mkubwa wa mapinduzi yaliyo taka kutokea nchini Ekwetoria Guinea.
Picha ya chini anaonekana Mark na mama yake bi Magreth Tharcher wakati walipo kuwa wakielekea kwenye moja ya sherehe za kiserikali.
Viongozi maasimu wawili wa nchi jirani kukutana kwenye mkutano" Asema waziri wa mambo ya nje".
Paris, Ufaransa - Viongozi wa nchi mbili maasimu na majirani wa kihistoria wa rais wa Syiria bwana Bashir Al Assad na waziri mkuu wa Israel, bwana Ehud Olmert, huenda wakakutana ana kwa ana wakati wa mkutano utakao fanyika mjini Paris hivi karibuni.
Akisema hayo , waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ufaransa, bwana Bernard Kouchner, alisema haya mbele ya bunge.
Alisema ya kuwa katika mkutano huo, ambao utajumuisha nchi zilizopo kwenye ukanda wa Medeteranian, viongozi hawa watakaa meza moja.
Hapo juu ni picha ya rais wa Syiria , bwana Bashar Al Assad ambaye huenda akaudhulia mkutano wa Paris.
Picha ya chini, anaonekana, waziri mkuu wa Israel, bwna Ehud Olmert, anaonekana akifikilia kwa makini nini jinsi gani amani itapatikana kwenye eneo la masharika ya kati.
Rais, George Bush, afanya ziara ya mwisho Ulaya , akiwa kama rais wa Amerika.
London, Uingereza - Rais wa Amerika , bwana, George Bush alikuwa ziarani katika nchi za Ulaya Magharibi hivi karibuni.
Ziara hii itakuwa ya mwisho kwa rais Bush akiwa kama rais wa Amerika.
Kataika ziara yake aliweza tembelea nchi za Ufaransa pamoja na Uingereza, ambapo alikutana na viongozi wa nchi hizo na kujadili maswala mbalimbali ya nayo ikabiri dunia kwa sasa.
Katika mazungumzo hayo na viongozi wa wa nchi hizo, walisisitiza jinsi ya kutokomeza ugaidi duniani na swala la nchi ya Iran kupa nguvu za kinyulia.
Pichani hapo juu anaonekana rai, George Bush akiwa na Malkia wa Uingereza, wakati alipo kwenda kumtembelea Malkia.
Ziara ya rais George Bush, ilikuja na maandamano makubwa yaliyo fanywa nchini Uingereza, kwa kupinga kuja kwa rais Bush nchini humo.
Chini wanaonekana rais George Bush , akiwa na mkewe Laura, wakiwaaga wananchi wa Uingereza kabla ya kuanza safari ya kulekea nyumbani.
Rais wa zamini Kuba, Fidel Castro aonekana mzima wa afya mbele ya wa Kuba.
Havana, Kuba - Rais wazamani wa Kuba , bwana Fidel Castro, ameonekana kwa mara ya kwanza kwenye runinga ya Kuba baada ya kufanyiwa upasuaji kipindi cha miezi sita iliyo pita.
Rais huyo wa zamani wa Kuba bwana Fidel Castro pamoja na mdogo wake Raul Castro, walionekana akiongea na rais wa Venezuela bwana Hugo Charvez.
Pichani wanaqonekana rais wa zamani wa Kuba , bwana Fidel Castro katikati, kulia Raul Castro na kushoto ni rais wa Venezuela bwana Hugo Charvez walipo kutana hivi karibuni.
Picha ya chini anaonekana rais wa zamani wa Kuba bwana, Fidel Castro, akisikiliza kwa makini nini kinaongelewa wakati walipo kutana na rais wa Venezuela.

Tuesday, June 10, 2008

Rais Gaddafi akataa makubaliano ya Mediterranian" Utavuruga na kuvunja nguvu za uhusiano wetu"

Nani kuwa bingwa wa soka 2008 , "Homa ya panda tena kwa wapenzi wa soka Ulaya".

Viena, Uswis - Mashindano ya kugombea ubingwa wa mataifa ya Ulaya kwa kwenye mchezo wa soka, kabumbu au mpira wa miguu yameanza rasmi siku ya jumamaosi suku ya ya tarehe 7/06/2008.
Mashindano haya ambayo yanazikutanisha timu ambazo zilifaulu kupita mthiani wa kugombania nafasi hii wakati wa awamu ya mwanzo.
Nchi ambazo zinashiriki kinyang'anyiro hiki ,i mabingaw watetezi, Ugiriki , German, Ureno, Sweden, Spania, Uhollanzi,Itali,Uturuki, Urusi, Swisi , Ausrtria,Romania,Cratia, Poland, Ufarannsa na Jamuhuri ya Czech.
Picha hapo juu, wanaonekana baadhi ta wachezaji maarufu duniani katika picha moja, wengine wakiwa na majonzi baada ya kukosa kikombe hiki cha ubingwa wa Ulaya wakati nchi zao zilipo shindwa kunyakua kikombe hiki, na wachezaji wengine wakiwa wamenyaua kikombe cha ubingwa wa Ulaya, wakati nchi zao zilipo fanikiwa kuwa mabingwa wa kikombe hicho.
Chini ni moja ya viwanja ambavyo nyasi za uwanja wake zitakuwa na kazi ngumi kikabili vishindo vya wanaume walioshiba tayari kuonyeshana nani atanyakua kikombe hiki cha Ulaya 2008 hadi 2012.
Picha hapo ya mwisho ni picha ya mrembo ambaye alikuwepo wakati wa ufunguzi wa mashindano ya kugombea ubingfwa wa kombe la Ulaya 2008 nchini Uswisi.
Rais Gaddafi akataa makubaliano ya Mediterranian, Utavuruga na kuvunja nguvu za uhusiano wetu.
Tripol, Libya - Rais Libya, Muhamar Gaddafi, amekataa kuku baliana na mpango wa kuanzisha umoja wa ushirikiano katika nchi zilizopo kaskazini mwa Afrika amabo ungejulikana kama muungano wa Umoja wa Mediteranian.
Rais, Gaddafi alisema yakuwa nchi zilizo udhulia mkutano huu ni wanachama wa jumuia ua muungano wa Afrika na muungano wa Urabuni, na aliongega na kusema muungano wa mediteraniani utaleta madhara katika jumuia ya muungano wa Afrika(AU).
Akiongeza kwa kwa kusisitiza kupinga mswada huu, rais Gaddafi alisema yakuwa Nchi za Ulaya zinazidi imarika kwa kuwa pamoja na kama zinataka kushirikana na si , basi zitashirikiana na muungano wa jumuia hizi AU- African Union na AL- Arab League.
Mkutano huu ulihudhuliwa na nchi za Algeria, Mauritania, Morocco, Siria -Syria na Tunisia.
Picha hapo juu ni picha ya rais Gaddafi, alipo kuwa akiwasili kwenye moja ya mikutano hivi karibuni.
Chini anaonkekana rais, Gaddafi, akiongea katika mkutano hivi karibuni.
Hipo haja ya kuanza kuongea na Lebanoni' Waziri mkuu wa Israel".
Tel Aviv, Israel - Wazri mkuu wa Israel bwana, Ehud Olmert, ameshauri ya kuwa mazungumzo ya amani yanabidi yaanzishwe na Lebanoni, baada ya kurudia mazungumzo na serikali ya Siria(Syria).
Bwana, Olmert, alisema ikiwa tumeanza mazungumzo na Siria, kunauwezekano wa kuanza mazungumzo na Lebanoni, aliyaongea haya alipo kuwa akiongea viongozi wa serikali ya Israel.
Wakati huo huo mmoja wa wanajeshi wa jeshi la Israel korpo Gilad Shalit , aliyekamatwa mwaka 2006, ameandika barua kwa famiia yake na kuomba jitihada zifanyike ili aweze kuachiwa.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Israel,barua hiyo ilipitia kwenye ofisi ya mradi unao simamiwa na bwana Jimmy Carter, aliyekuwa rais wa zamani wa Amerika.
Hata hivyo baba ya Gilad, bwana Noam Shalit, alisema ya kuwa mwanae, hayuko katika mazingira bora na anhitaji kurudi nyumbani salama.
Na hii inaonyesha ya kuwa kopro Gilad Shalit bado ni mzima, na msemaji mmoja wa Hamas, alisema yakuwa hii ni kutokana na juhudi zilizo fanywa na rais wa zamani wa Amerika bwana Jimmy Carter.
Picha hapo anaonekana waziri mkuu wa Israel bwana, Ehud Olmert lipo kuwa akiongea hivi karibuni nchi Amerika katika mkutano wa ushirikiano kati ya Amerika na Israel.
Picha ya pili wanaonekana wanajeshi wa Israel , wakati wa mapambano na kundi la Hezbollah mapema mwaka 2006 mapambano amabayo yalichukua zaid ya siku wiki nne.
Picha ya chini ni picha ya mwanajeshi wa Israel, bwana Gilad Shalit, kabla ya kukamatwa kwake na kundi la wapiganaji kwenye maeneo ya Wapalestina.
Walio husika katika ukamatwaji wa raia wa Kijerumani watakiwa kujibu mashitaka.
Munich, Ujerumani - Kundi la kutetea haki za binadamu nchini Ujerumani, limeishitaki serikali ya Ujerumani kwa kushirikiana shirika la makachero la Amerika (CIA).
Kesi hiyo imefunguliwa kwa kuitaka serikali ya Ujerumani kuwaleta wafanyakazi 13 wa CIA, waliousika katika ukamatwaji husio kihalali wa raia wa Ujerumani bwana, Khaled Al Masri na Wolfgang Kalek hapo miaka ya nyuma.
Msemaji mmoja wa mahakama mjini Munich, alisema yakuwa kesi hiyo imefunguliwa , lakini hakusema ni lini itaanza kusikilizwa.
Bwana, Al Masri , aliachiwa huru mei 2004, na alikamatwa kimakosa.
Hata hivyo serikali ya Amerika imekataa kuzungumzia swala hilo, lakini viongozi wa serikali ya Ujerumani walikubali yakuwa kuna makosa yalifanyika.
Picha hapo juu ni nembo ya CIA.
Picha ya pili ni picha ya bwana Khaled Al Masri, ambaye alikamatwa wakati alipo kuwa mpakani mwa nchi za Serbia na Macedonia, na baadaye aliwekwa chini ya ulinzi kwa kipindi kileferu nchini Afghanistan.
Chini wanaonekana mmoja ya watu waliopo chnini ya ulinzi katika moja ya vizuizi ya watu wanaoshukiwa ni hatari kwa jamii ya kimataifa.
Kiongozi wa kidini wa kabila la rais wa zamani wa Irak, auwawa.
Tirkit, Iraq - Aliyekuwa kiongozi wa kidini wa kabila la aliyekuwa rais wa Irak Saddaam Hussein, Sheikh Ali Al Neda's amefariki dunia siku ya jumannne 9/06/2008, baada ya gari aliyoy kuwa akisafiria kulipuliwa na bomu.
Kiongozi huyo wa kabila la Al Bu Nasir lenye watu wengi jamii ya Sunni na ni moja ya kabila ambalo alilotokea rais wa zamani wa Irak, Saddam Hussein.
Sheikh Ali Al Neda's, alikuwa mwanzilishi wa kampeni ya ya kuwapinga wapiganaji wa Kisuni, ambao wanaopigana na jeshi la Amerika.
Pichani anaonekana mama akilia kwa uchungu baada ya kupoteza mmoja ya ndugu zake kutokana na machafuko na ukosefu wa uturivu nchini Irak.
Katikati ni bendera ya Irak.
Chini ni picha za watu ambao wamepoteza maisha yao, kutokana na hali yakutokuwa na amani nchini Irak.
Iran yawa na mtazamo tofauti na Iraq, "Mkataba na Amerika siyo muafaka" Wairan
Teheran, Iran - Kiongozi mkuu wa Kidini nchini Iran, Ayatollah Ali Khamenei,ameshauri ya kuwa serikali ya Iraki ya kuwa hapendelei mkataba ambao wa serikali ya Irak inafikilia kukubaliana na serikali ya Amerika(US).
Mkataba huo ambao hupo njiani kufikiwa, unahusu kwa jeshi la Amerika kukaa zaidi nchini Iraq, kwa kipindi cha miaka mingi baada ya ya mwaka 2008.
Kiongozi huu mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, alisema haya wakati alipo kutana na waziri mkuu wa Iraq bwana, Nuri Al Maliki ya kuwa wanamatumaini wananchi wa Irak, watakuwa na amani na maisha ya kawaida hapo baadaye , lakini siyo ndoto ya Kiamerika itakayo wawezesha kufikia amani hiyo.
Hata hivyo waziri mkuu wa Irak, bwana Nuri Al Maliki, alisema yakuwa, nchi yake kamwe haitatumika kama, kiwanja cha kuchambualia Irana na nchi majirani zake.
Hata hivyo.
Picha ya hapo juu wanaonekana, viongozi wa serikali ya Iran na serikali ya Iraki,wakati walipo kutana hivi karibuni.
Chini ni picha ya wana mama wakiwa mafunzoni tayari kujianda kulinda nchi yao Iraki.
Mkataba wa amani ya Somalia wawa mashakani, UN bado wanamatumaini.
Mogadishu , Somalia - Kiongozi wa kundi kubwa linali pingana ns serikali ya Somali, Sheikh Dahir Aweys , amekataa kuku bali mkataba wa makubaliano ya kuleta amani nchini Somalia.
Sheikh Dahir Aweys, alisema mkataba huo ni mkataba ambao utawapa nafasi upande wa serikali kujikusanyaia nguvu zaidi za kijeshi.
Akiongea kwa njia ya simu na moja ya mashirika ya habari, Sheikh Aweys, alisema ya kuwa tuna wapa moyo wapiganaji wote na tutajitahidi mpaka hapo tutakapo mshinda adui.
Jeshi la Somalia likisaidiana na jeshi la Ethiopia wanapigana na vita na makundi mbali mbali yaliopo nchini Somalia kwa kipndi kisicho pungua mwaka sasa.
Hata hivyo msemaji wa Umoja wa Mataifa,bwana Ould Abdallah, alisema yakuwa wamekubaliana kimsimgi kuhusu mktaba huo, na wakati huo huo. katubu mkuu wa umoja wa Mataifa, bwana Ban Ki Moon, ameyakaruibishwa makubalianao hayo, na kuagiza ya kuwa hata yele makundi binafsi yatakubaliana na mkataba huu.
Picha hapo juu anaonekana mpiganaji wa moja ya makundi yanayo pingana na jeshi la serikali,akiwa ameshikialia bunduki tayari kupambana na jeshi la serikali.
Picha ya kati wanaonekana, wapiganaji wa kundi la AlShabaab wakipokea mafunzo ya na mbinu zakupigana vita dhidi ya wanajeshi wa serikali.
Picha ya chini ni mmoja wa viongozi wa vyama/ makundi ambayo yamekataa kuukubali mkataba wa amani.