Maelfu wakumbuka waliopoteaza maisha wakati wa Tsunami. Aceh, Sri Lanka - 27/12/09. Maelfu ywa watu diniani wamekusanyika kwenye nchi ambazo zilipata maafa makubwa kutokana na Tsunami yaliyo tokea mnamo mwaka 2004. Maafa hayo ta Tsunami yalipoteza maisha ya watu wapato 226,000 na watu wengine kuachwa bila makazi na kuleta uaribifu mkubwa katika jamii. Kwa mujibu wa shirika linalo shughulikia utoaji wa misaada la umoja wa Matifa Red Cross, limesema maafa ya Tsunami bado yapo katika maeneo yote na hasa kwa familia zilizo athirika na na janga hili. Picha hapo juu ni picha ya boti, ambayo ilibakizwa baada ya janga la Tsunami,na anaonekana mama mmoja akiangalia kwa uchungu janga lililoletwa na Tsunami katika eneo lao.
Sunday, December 27, 2009
Ulinzi waongezwa kwenye viwanja vya ndege.
Posted by Kibatala at Sunday, December 27, 2009 0 comments
Friday, December 25, 2009
Ulinzi wa Papa waingia dosali.
Ulinzi wa Papa waingia dosali Vatican city, Vatican - 25/12/09. Waumini wa madhehebu ya Kikatoriki waliokuja kuhudhuria misa ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu katika kanisa kuu la Vatikani,walishikwa na mshituko baada ya mmoja ya waumini wa kike kuruka kizuizi na kumkaba Papa Benedikt wa XVI na kuanguka nae chini. Mwanamke huyo jina limehifadhiwa, anaulaia wa Itali na Swis,alikamatwa na walinzi wa Papa na baadaye kuwekwa chini ya ulinzi kwa mahojiano. Hata hivyo, Papa , 83 aliweza kuendelea na misa ya usiku wa Krismas, baada ya kuthibitisha hakupat madhara ya aina yoyote. Picha hapo juu anaonekana Papa Benedikt wa XVI akiwasalimia na kuwabaliki waumini waliokuja kuudhulia misa ya Krismas. Waathirika wa nguvu za kinyuklia kulipwa fidia. Paris, Ufaransa - 25/12/09. Serikali ya Ufaransa imekubali kulipa fidia kwa wanachi wa Algeria walio athirika kutokana na mazara ya kujaribiwa nguvu za kinyuklia mnamo kati ya miaka ya 1960-67. Kukubali kwa serikali kumekuja baada ya bunge la Ufaransa kupitisha mswada huo wa malipo kwa waathirika wa nguvu hizo za nyuklia. Hata hivto malipo yatalipwa kutokana na kesi ya kila mwathirika atakapo wakilisha kesi yake. Waziri wa ulinzi wa Ufaransa, Herve Morin alisema " Kupitishwa kwa seria hiyo kumeleta usawa." Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wafanyakazi wa moja ya mitambo inayoongoza nguvu za kinyuklia wakiwa wanaangalia kwa makini mitambo hiyo.
Kabul, Afghanistan - 25/12/09. Viongozi wa jeshi la NATO lililopo Afghanistan limethibitisha ya kuwa picha ya video ya mmoja ya mwanajeshi wa Kiamerika aliyekamtwa miezi mitano iliyo pita na kundi la Taliban.
Mwanajeshi huyo, Bowe Bergdahl alitekwa nyara mara baada ya kuwasili Afghanistan katika moja kambi moja ya kijeshi iliyopo Paktika.
Video hiyo ilionyeshwa kwa dakika 36, huku mwanajeshi huyo, akiongea ya kuwa kuwepo kwa majeshi ya NATO nchini Afghanistan ni kimyume cha wananchi wa Afghanistan.
Katika video hiyo, kiongozi mmoja wa Taliban,Zabihullah Mujahid, alisema "Itabidi kuwepo na kubadilishana wafungwa ikiwa NATO inataka Bowe Bergdahl aachiwe na kundi hilo."
Picha hapo juu ni ya Bowe Bergdahl, akiongea katika picha ya video iliyo tolewa na kundi la Taliban hivi karibubi.
Posted by Kibatala at Friday, December 25, 2009 0 comments
Thursday, December 24, 2009
Wakristu duniani wakumbuka kuzaliwa kwa Mkombozi.
Wakristu duniani wakumbuka kuzaliwa kwa Mkombozi. Usiku wa Krismas- 24/12/09. Mamilion ya waumini wa dini ya Kikristu duniani leo usiku wanasherekea siku ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu,akiongea kwa furaha, mmoja wa waumini wa dini ya kikristu alisema "Sisi wakristu tunaamini ya kuwa alikuja kuikomboa dunia na kupitia yeye kila mtu atakombolewa akimfuata Yesu Kristu. icha hapo juu, wanaonekana waumini wa dini ya Kikristu, wakiwa kanisani kuhudhulia misa ikiwa ni siku muhimu ya kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu Kristu.
Posted by Kibatala at Thursday, December 24, 2009 0 comments
Saturday, December 19, 2009
Uchumi wa China kuonyesha mabadiliko.
Uchumi wa China kuonyesha mabadiliko. Beijing,China - 19/12/09. Serikali ya China, imetangaza ya kuwa uchumi wa umekuwa kwa kiasi cha asilimia 0.6 hadi kufikia mwisho wa mwezi wa Novembea. Kwa mujibu wa habari zilizo tolewa na serikali ya China, zinasema kukua huku kwa uchumi kwa kipindi cha miezi kumi iliyo pita , kuanatokana na kuongezeka na ununuzi na uzalishaji na kuwekwezwa kwa vitega uchumi kuliko ongezeka. Picha hapo juu ni bendera ya China nchi ambayo uchumi wake umeanza kuku kwa kulinganisha na nchi zinanzo endelea dunia.
Copenhagen,Denmark-19/12/09.Umoja wa mataifa umekubaliana kimsingi uamuzi uliochukuliwa nchini Denmark na viongozi na marais walioudhulia mkutano wa kujadili jinsi ya kukabiliana kuaribika kwa maziangira na hali ya hewa.
Akiongea mbele ya waandishi wa habari katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban ki Moon, alisema" Nchi zote zimekubaliana kimsingi kukubaliana ni kwa jinsi gani zitashiriki kupunguza uharibufu wa masingira na hali ya hewa, muda muafaka utakapo fika miswaada iliyo kubalika itakuwa sheria."
Hata hivyo Amerika, Brazil, China na Afrika ya Kusini, zimekubaliana kwa kiwango kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa kutokana na nchi hizo kuwa na viwanda vingi.
Picha hapo juu, wanaonekana baadhi ya wanachama wa chama cha Kijana na wananchi wengine wakiwa wanapinga na kusema ni aibu kwa uamuzi uliofanywa wa kutokuwa kubaliana kwa pamoja kupambana na uharibifu wa mazingira.
Picha ya pili wanaonekana waandamaji wakiwa wamebeba maelezo yenye ujumbe kwa wajumbe walioudhulia mkutano wa kukabiliana na uharibifu wa mazingiza jijini Copenhagen Denmark.
Posted by Kibatala at Saturday, December 19, 2009 0 comments
Monday, December 14, 2009
Evo Morales aongoza kwa kura nchini Bolivia.
Evo Morales, aongoza kwa kura nchini Bolivia.. La Paz, Bolivia - 14/12/09. Matokeo ya uchaguzi uliofanyika nchini Bolivia, yanaonyesha rais wa sasa wa nchi hiyo Evo Morales, ameshinda kwa asilimia 60%. Kwa mujibu wa ripoti za kamati inayo simamia uchaguzi, mpinzani wa Evo, Manfred Reyes Villa, inasemekana amepata kura kwa asilimia 23%. Hata hivyo matokeo ya uchaguzi yanatarajiwa kutangazwa wiki hii rasmi. Picha hapo juu anaonekana, rais wa Bolivia, Evo Morales,akihutubia kwa makini wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Bolivia. Rais wa Kuba Raul Castro, ailaumu Amerika. Havana, KUba 14/12/09. Rais wa Kuba ,Raul Castro, ameilaumu serikali ya Amerika kwa kuunga mkono uchaguzi wa Honduras, ambao hakuwa wa haki na inastahili rais wa zamani Manuel Zelaya arudishwe madarakani. Rais, Raul Castro, aliyasema haya wakati wa mkutano unao zikutanisha nchi za Latini Amerika Hata hivyo msemaji wa serikali ya Amerika, alisema " Raul Castro inabidi aanze demokrasi nchini mwake, kwani wakati wakuchaguliwa kwakwe kura zilikuwa za mtu mmoja." Picha hapo juu anaonekana rais wa Kuba,Raul Castro akiongea wakati wa mkutano wa viongozi wa Latini Amerika uliofanyika jijini Havana nchini Kuba kujadili maendeleo ya nchi zao kiuchumi na kijamii na kutafuta njia ya kukuza uchumi. Waandamanaji wakumbana na nguvu za dola. Copenhagen,Denmark - 14/012/09.Watu zaid ya 200, wamekamtwa na polisi wakati wa maandamano ya kupinga kuongezeka kwa machafuzi ya hali ya hwe na mazingira. Waaanamanaji hao, wanaanandamana kuwataka viongozi wa dunia ambao wapo kwenye mkutano nchini Denmark kujadili kila njia ya kupunguza machafuzi na kuharibu hali ya hewa duniani. Kufuatia maandamano hayo, polisi wamekuwa wanasimamisha watu na kuwakagua kama wana zana za hatari. Picha hapo juu anaonekana mmoja ya waaandamaji akikabiriana na polisi wanao linda mkutanao huo unaoendelea. Waziri mkuu wa Itali ashambuliwa. Roma. Itali - 14/12/09.Waziri mkuu wa Itali, Silvio Berlusconi,amejeruhiwa kwenye paji la uso baada ya mtu mmoja kumrushia kigae usoni. Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, alisema "Mtu mmoja 42 ambaye anamatatizo ya akili ndiye aliyemrushia kigae hicho", mtu huyo alikamatwa na polisi mara moja. Waziri mkuu, Berlusconi, alijeruhiwa pua na baadhi ya meno kukuvunjika. Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Itali, Silvio Berlusconi, akiwa njiani kuelekea hospitali, baaada ya kushambuliwa na kigae.
Posted by Kibatala at Monday, December 14, 2009 0 comments
Thursday, December 3, 2009
NATO kuongeza wapiganaji Afgahinstan.
NATO kuongeza wanajeshi Afghanistan.
Posted by Kibatala at Thursday, December 03, 2009 0 comments