Sunday, December 27, 2009

Ulinzi waongezwa kwenye viwanja vya ndege.

Maelfu wakumbuka waliopoteaza maisha wakati wa Tsunami. Aceh, Sri Lanka - 27/12/09. Maelfu ywa watu diniani wamekusanyika kwenye nchi ambazo zilipata maafa makubwa kutokana na Tsunami yaliyo tokea mnamo mwaka 2004. Maafa hayo ta Tsunami yalipoteza maisha ya watu wapato 226,000 na watu wengine kuachwa bila makazi na kuleta uaribifu mkubwa katika jamii. Kwa mujibu wa shirika linalo shughulikia utoaji wa misaada la umoja wa Matifa Red Cross, limesema maafa ya Tsunami bado yapo katika maeneo yote na hasa kwa familia zilizo athirika na na janga hili. Picha hapo juu ni picha ya boti, ambayo ilibakizwa baada ya janga la Tsunami,na anaonekana mama mmoja akiangalia kwa uchungu janga lililoletwa na Tsunami katika eneo lao.

Gaza waadhimisha mwaka mmoja tangu kuisha vita.
Gaza, Palestina-27/12/09. Wapalestina wakazi wa Gaza wameandamana kukumbuka siku ya kuanza kwa mashambulizi yaliyo fanywa na jeshi la Izrael kwa muda wa siku 22.
Mashambulizi hayo ambayo yalisababisha vifo vya watu 1600 na uaribifu mkubwa wa makazi ya Wapalestina.
Vita hivyo ambavyo vilileta maafa katika eneo la Gaza, vilikuwa kati ya Hamas na jeshi la Izrael.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya waandamanaji wakiwa wakiaandamana kuadhimisha siku ya kuanza kwa vita vya Gaza.
Ulinzi waongezwa kwenye viwanja vya ndege.
Michigan, Amerika- 27/12/09. Raia wa Nigeria ameshitakiwa kwa kosa la kutaka kulipua ndege ya abiria iliyo kuwa ikitokea Schiphol Asterdam.
Hakimu alimsomea kesi mshitakiwa akiwa hospital katika hospitali ya Ann Arbor iliyopo Michigan.
Mshitakiwa huyo kwa jina Umar Abdulmutallab 23, alianzia safari yake nchini Nigeria siku moja kabla ya siku ya tukio.
"Kufuatia tukio hilo , ulinzi umeongezwa katika viwanja vya ndege vyote nchin Amerika" alisema msemaji wa mwaswala ya ualama wa anga wa taifa nchin Amerika.
Picha hapo juu wanaonekana maafisa wa usalama wa moja ya kiwanja cha ndege wakiangali kwa makini wasafiri wanavyo jiandaa kukaguliwa.
Siku ya Ashura yaingia dosari nchini Iran.
Tehran, Iran - 27/12/09. Wapinzani wa serikali nchini Iran, wamepambana na polisi wa serikali wakati wa kusherekea kumbulumbu ya siku ya Ashura na watu kupoteza maisha na wengi kujeruhiwa.
Siku hii ilikuwa ni kwa ajili ya kumbukumbu ya kifo cha mjuukuu wa Mtume Muhammad, Ashura, kilichotokea karne ya 7th
Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Iran, watu wanne walipoteza maisha katika maandamano hayo.
Msaidizi wa jeshi la polisi la Iran,Ahmad Reza Radan, alisema " watu wapatao 300,walikamatwa kwa kusababisha vurugu wakati wa sherhe ya kumbukumbu ya Ashura.
Hata hivyo, viongozi wa vyam vya upinzani walisema kun zaid ya watu wanne waliopoteza maisha yao.
Picha hapo juu, anaonekana mmoja ya mwanadamaji akisaidiwa na wenzake mara maada ya kujeruhiwa vibaya na moto.

Friday, December 25, 2009

Ulinzi wa Papa waingia dosali.

Ulinzi wa Papa waingia dosali Vatican city, Vatican - 25/12/09. Waumini wa madhehebu ya Kikatoriki waliokuja kuhudhuria misa ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu katika kanisa kuu la Vatikani,walishikwa na mshituko baada ya mmoja ya waumini wa kike kuruka kizuizi na kumkaba Papa Benedikt wa XVI na kuanguka nae chini. Mwanamke huyo jina limehifadhiwa, anaulaia wa Itali na Swis,alikamatwa na walinzi wa Papa na baadaye kuwekwa chini ya ulinzi kwa mahojiano. Hata hivyo, Papa , 83 aliweza kuendelea na misa ya usiku wa Krismas, baada ya kuthibitisha hakupat madhara ya aina yoyote. Picha hapo juu anaonekana Papa Benedikt wa XVI akiwasalimia na kuwabaliki waumini waliokuja kuudhulia misa ya Krismas. Waathirika wa nguvu za kinyuklia kulipwa fidia. Paris, Ufaransa - 25/12/09. Serikali ya Ufaransa imekubali kulipa fidia kwa wanachi wa Algeria walio athirika kutokana na mazara ya kujaribiwa nguvu za kinyuklia mnamo kati ya miaka ya 1960-67. Kukubali kwa serikali kumekuja baada ya bunge la Ufaransa kupitisha mswada huo wa malipo kwa waathirika wa nguvu hizo za nyuklia. Hata hivto malipo yatalipwa kutokana na kesi ya kila mwathirika atakapo wakilisha kesi yake. Waziri wa ulinzi wa Ufaransa, Herve Morin alisema " Kupitishwa kwa seria hiyo kumeleta usawa." Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wafanyakazi wa moja ya mitambo inayoongoza nguvu za kinyuklia wakiwa wanaangalia kwa makini mitambo hiyo.

Mwanjeshi aliye kamatwa na Taliban bado yuhai.

Kabul, Afghanistan - 25/12/09. Viongozi wa jeshi la NATO lililopo Afghanistan limethibitisha ya kuwa picha ya video ya mmoja ya mwanajeshi wa Kiamerika aliyekamtwa miezi mitano iliyo pita na kundi la Taliban.

Mwanajeshi huyo, Bowe Bergdahl alitekwa nyara mara baada ya kuwasili Afghanistan katika moja kambi moja ya kijeshi iliyopo Paktika.

Video hiyo ilionyeshwa kwa dakika 36, huku mwanajeshi huyo, akiongea ya kuwa kuwepo kwa majeshi ya NATO nchini Afghanistan ni kimyume cha wananchi wa Afghanistan.

Katika video hiyo, kiongozi mmoja wa Taliban,Zabihullah Mujahid, alisema "Itabidi kuwepo na kubadilishana wafungwa ikiwa NATO inataka Bowe Bergdahl aachiwe na kundi hilo."

Picha hapo juu ni ya Bowe Bergdahl, akiongea katika picha ya video iliyo tolewa na kundi la Taliban hivi karibubi.

Thursday, December 24, 2009

Wakristu duniani wakumbuka kuzaliwa kwa Mkombozi.

Wakristu duniani wakumbuka kuzaliwa kwa Mkombozi. Usiku wa Krismas- 24/12/09. Mamilion ya waumini wa dini ya Kikristu duniani leo usiku wanasherekea siku ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu,akiongea kwa furaha, mmoja wa waumini wa dini ya kikristu alisema "Sisi wakristu tunaamini ya kuwa alikuja kuikomboa dunia na kupitia yeye kila mtu atakombolewa akimfuata Yesu Kristu. icha hapo juu, wanaonekana waumini wa dini ya Kikristu, wakiwa kanisani kuhudhulia misa ikiwa ni siku muhimu ya kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu Kristu.

Iretrea yawekewa vikwazo na UN.
New York, Amerika - 24/12/09.Kamati ya usalama ya umoja wa Matifa, imeiwekea vikwazo serikali ya Iritrea kwa kushirikiana na kuwasaidia magaidi wa Kisomalia wa Al Shabaab na kukataa kutoa jeshi lake karibu na mpaka na Djibuti. Azimio hilo lilipitishwa kwa pamoja kwa kura 13,lakini China na Libya hazikupiga kura. Hata hivyo serikali ya Iritrea, imekuwa ikikanusha ya kuwa inashirikiana na kundi la Al Shabaab ambalo lina pigana na jeshi la serikali ya Somalia. Picha hapo juu anaonekana mmoja wa mwanajeshi wa Iritrea,akiwa kazini kulinda mpaka kati yake Iretrea na Djibuti. Mwana sayansi akubali kutolewa kwa viungo vya mwili.
Tel-Aviv, Izrael- 24/12/09.Mwanasayansi na mchiunguzi wa miili ya binadamu, Jehud Hiss amekubali yakuwa Izrael ilikuwa ikitoa baadhi ya viungo vya binadamu bila ruhusa ya watu walio aga dunia au ruhusa za ndugu zao.
Jehud Hiss, ambaye alikuwa akifanya kazi katika moja ya maabara ambazo zilikuwa zikitumika katika kupima na kuangalia nini nyanzo vya vifo vya watu hao.
Jehus Hiss alisema "viungo kama mioyo ngozi na baadhi ya mifupa ilikuwa ikitolewa kwa ajili ya matumizi binafsi na viungo hivyo vilikuwa vikitolewa katika miili ya wafanyakazi wageni na Wapalestina."
Kukubali kwa habari hizo kunakuja baada ya moja ya gazeti la nchini Sweden, kutoa habari yakuwa Izrael ilikuwa ikitoa baadhi ya viungo vya miili kwa watu walioag dunia bila makubaliano ya watu hao au ndugu zao, habari ambayo Izrael ilikanusha.
Picha hapo juu ni moyo kiungo muhimu katika mwili wa binadamu.
Urussi kuimarisha nguvu zake za kinyuklia.
Moscow, Urussi - 24/12/09. Rais wa Urussi, Dmitry Medveded, amesema Urussi itaendeleza nguvu zake za kinyuklia kufuatina na wakati.
Akiongea na waandishi wa habari, rais Medvedev alisema" Ili kulinda nchi yetu ni lazima kuendeleza na kufanyia marekebisho siraha zetu za kinyuklia na Amerika wanaelewa swala hilo."
Rais Medvedev, aliongezea kwa kusema ya kuwa kukua kwa uchumi wa Urussi, umeanza na utachukua muda kufikia hali nzuri.
Picha hapo juu, anaonekana mmoja ya raia wa Urussi, akiangali runinga,wakati rais wa Russia , Dmitry Medvedev akiongea na waandishi wa habari.
Volkano yatishia maisha ya wakazi.
Mlima Mayon, Philipinsi- 24/12/09 . Hali ya hatari imetangazwa kwa wakazi wanao kaa karibu mlima Mayon kufuatia mlipuko wa volkano uliotokea katika mlima huo.
Akionga kwa msisitizo, mkurugenzi wa maswala ya sayansi ya volkano, Renato Solidu malisema"Mlipuko huo ulionza mwamzoni mwa wiki iliyo pita na hadi kufikia sasa unaelekea kuleta madhara makubwa kwa jamii na mzingira ya karibu na mlima huo." Majivu ya moto yaliotokana na mlipuko huo, yalionekana kuruka kuelekea hewani kiasi cha umbali wa zaidi ya mita miatano.
Picha hapo juu, majivu ya moto yanaonekana yakiruka juu, hali ambayo wakazi karibu na maeneo hayo wamekuwa na wasiwasi mkubwa.
Urussi yafungua mpaka na Georgia.
Moscow,Urussi- 24/12/09 . Serikali ya Georgia na Urussi, zimekubaliana kufungua mpaka nchi zao, tangu kusimama kwa vita vilivtotokea mwaka mmoja uliopita.
Kwa mujinu wa wasemaji wa serikali zote mbili, ufunguzi wa mipaka hiyo utawasaidia wanachi wa Georgia kusafirisha mizigo yao.
Urussi, ilifunga mpaka na Georgia tangu mwaka 2006,kutokana na mvutano wa kisiasa uliotokea kati ya nchi hizo.
Picha hapo juu, kinaonekana moja ya kifaru cha kijeshi kikiwa katika ulinzi wa mpaka kati ya Urussi na Georgia.

Saturday, December 19, 2009

Uchumi wa China kuonyesha mabadiliko.

Uchumi wa China kuonyesha mabadiliko. Beijing,China - 19/12/09. Serikali ya China, imetangaza ya kuwa uchumi wa umekuwa kwa kiasi cha asilimia 0.6 hadi kufikia mwisho wa mwezi wa Novembea. Kwa mujibu wa habari zilizo tolewa na serikali ya China, zinasema kukua huku kwa uchumi kwa kipindi cha miezi kumi iliyo pita , kuanatokana na kuongezeka na ununuzi na uzalishaji na kuwekwezwa kwa vitega uchumi kuliko ongezeka. Picha hapo juu ni bendera ya China nchi ambayo uchumi wake umeanza kuku kwa kulinganisha na nchi zinanzo endelea dunia.

Taliban yawa na mbinu mpya za mashambulizi.
Kabul Afghanistan - 19/12/09. Kiongozi mmoja wa kundi la Taliban,amesema ya kuwa kundi la Taliban litabigana na jeshi la Amerika na NATO hadi mtu wa mwisho, hata kama wakileta zaidi ya wanajeshi 200,000.
Kwa mujibu wa maelezo ya wataalamu wa mambo ya kivita wamesema ya kuwa Taliban, wamebadilisha mbinu ya kupigana hasa kwa kipindi cha baridi, wameongeza mashambulizi tofauti na miaka ya nyuma.
Picha hapo juu wanaonekana wapiganaji wa Taliban, wakiwa mafichoni tayari kwa kuanza mashambulizi.
Jibu la kutunza na kulinda mazingira bado kitendawili kwa jumuia za kimataifa.

Copenhagen,Denmark-19/12/09.Umoja wa mataifa umekubaliana kimsingi uamuzi uliochukuliwa nchini Denmark na viongozi na marais walioudhulia mkutano wa kujadili jinsi ya kukabiliana kuaribika kwa maziangira na hali ya hewa.

Akiongea mbele ya waandishi wa habari katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban ki Moon, alisema" Nchi zote zimekubaliana kimsingi kukubaliana ni kwa jinsi gani zitashiriki kupunguza uharibufu wa masingira na hali ya hewa, muda muafaka utakapo fika miswaada iliyo kubalika itakuwa sheria."

Hata hivyo Amerika, Brazil, China na Afrika ya Kusini, zimekubaliana kwa kiwango kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa kutokana na nchi hizo kuwa na viwanda vingi.

Picha hapo juu, wanaonekana baadhi ya wanachama wa chama cha Kijana na wananchi wengine wakiwa wanapinga na kusema ni aibu kwa uamuzi uliofanywa wa kutokuwa kubaliana kwa pamoja kupambana na uharibifu wa mazingira.

Picha ya pili wanaonekana waandamaji wakiwa wamebeba maelezo yenye ujumbe kwa wajumbe walioudhulia mkutano wa kukabiliana na uharibifu wa mazingiza jijini Copenhagen Denmark.

Monday, December 14, 2009

Evo Morales aongoza kwa kura nchini Bolivia.

Evo Morales, aongoza kwa kura nchini Bolivia.. La Paz, Bolivia - 14/12/09. Matokeo ya uchaguzi uliofanyika nchini Bolivia, yanaonyesha rais wa sasa wa nchi hiyo Evo Morales, ameshinda kwa asilimia 60%. Kwa mujibu wa ripoti za kamati inayo simamia uchaguzi, mpinzani wa Evo, Manfred Reyes Villa, inasemekana amepata kura kwa asilimia 23%. Hata hivyo matokeo ya uchaguzi yanatarajiwa kutangazwa wiki hii rasmi. Picha hapo juu anaonekana, rais wa Bolivia, Evo Morales,akihutubia kwa makini wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Bolivia. Rais wa Kuba Raul Castro, ailaumu Amerika. Havana, KUba 14/12/09. Rais wa Kuba ,Raul Castro, ameilaumu serikali ya Amerika kwa kuunga mkono uchaguzi wa Honduras, ambao hakuwa wa haki na inastahili rais wa zamani Manuel Zelaya arudishwe madarakani. Rais, Raul Castro, aliyasema haya wakati wa mkutano unao zikutanisha nchi za Latini Amerika Hata hivyo msemaji wa serikali ya Amerika, alisema " Raul Castro inabidi aanze demokrasi nchini mwake, kwani wakati wakuchaguliwa kwakwe kura zilikuwa za mtu mmoja." Picha hapo juu anaonekana rais wa Kuba,Raul Castro akiongea wakati wa mkutano wa viongozi wa Latini Amerika uliofanyika jijini Havana nchini Kuba kujadili maendeleo ya nchi zao kiuchumi na kijamii na kutafuta njia ya kukuza uchumi. Waandamanaji wakumbana na nguvu za dola. Copenhagen,Denmark - 14/012/09.Watu zaid ya 200, wamekamtwa na polisi wakati wa maandamano ya kupinga kuongezeka kwa machafuzi ya hali ya hwe na mazingira. Waaanamanaji hao, wanaanandamana kuwataka viongozi wa dunia ambao wapo kwenye mkutano nchini Denmark kujadili kila njia ya kupunguza machafuzi na kuharibu hali ya hewa duniani. Kufuatia maandamano hayo, polisi wamekuwa wanasimamisha watu na kuwakagua kama wana zana za hatari. Picha hapo juu anaonekana mmoja ya waaandamaji akikabiriana na polisi wanao linda mkutanao huo unaoendelea. Waziri mkuu wa Itali ashambuliwa. Roma. Itali - 14/12/09.Waziri mkuu wa Itali, Silvio Berlusconi,amejeruhiwa kwenye paji la uso baada ya mtu mmoja kumrushia kigae usoni. Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, alisema "Mtu mmoja 42 ambaye anamatatizo ya akili ndiye aliyemrushia kigae hicho", mtu huyo alikamatwa na polisi mara moja. Waziri mkuu, Berlusconi, alijeruhiwa pua na baadhi ya meno kukuvunjika. Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Itali, Silvio Berlusconi, akiwa njiani kuelekea hospitali, baaada ya kushambuliwa na kigae.

Thursday, December 3, 2009

NATO kuongeza wapiganaji Afgahinstan.

NATO kuongeza wanajeshi Afghanistan.

Washington, Amerika - 03/12/09. Rais wa Amerika Baraka Obama, ametanganza ya kuwa wanajeshi wapatao 30,000 watakwanda nchini Afghanistan.
Akiongea mbele ya wanajeshi waliomaliza mafunzo ya kijeshi, rais Obama alisema "Vita hivi ni kwajili ya usalama na ulinzi wa Amerika na nchi wanachama wa NATO".
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana zinamsema kabla ya kutangaza hatua hiyo, rais Obama, aliwasiliana na viongozi wa bara la Ulaya wanachama wa NATO,ili kuzihimiza nchi hizo kushirikiana kikamilifu kushinda vita dhidi ya Taliban na kundi la Alqaeda.
Picha hapo juu anaonekana rai wa Amerika, Baraka Obama, akihutubia mbele ya viongozi wa serikali na wanajeshi,kuhusu kuongeza idadi ya wanajeshi watakaokwnda nchini Afghanistan.
Picha ya pili, wanaonekana wanajeshi wakiwa katika doria nchini Afghanistan, katika harakati za kupambana na Taliban na Alqaeda.
Rwanda mwamachama mpya wa Commonwealth.
Kigali, Rwanda - 03/12/09 . Jumuiya ya nchi wanachama wa ambazo zilitawaliwa na Mwingereza - Commonwealth group- zimeikaribisha rasmi nchi ya Rwanda kuwa manachama wa 54. Kwa mujibu wa waziri wa habari wa Rwanda, Louise Mushikiwabo, aliseama nchi yake imepiga hatua kubwa kimaendeleo tangu kutokea vita vya kikabila vya mwaka 1994.
Picha hapo juu, anaonekana rais wa Rwanda, Paul Kagame, ambaye tangu kuwa kiongozi wa Rwanda, nchi yake imeendelea kiuchumi na kijamii kwa kiasi kikubwa.
Picha ya pili, ni ya rais wa Ufaransa, Nikolas Sarkozy, ambye nchi yake imekuwa mtawala wa Rwanda wakati wa kipindi cha ukoloni, na sasa Rwanda imejiunga na jumuia ya nchi zinazo sema kiingereza.