Monday, March 24, 2008

Pope John Poul II aonekana katika umbile la moto"Adai aliye piga picha"

Nyota ya the Green Eagles yataka weka daruga za soka muda si mrefu.

London, Uingereza - Mchezaji na nyota ya timu ya taifa ya Nigeria Jay Jay Okacha, amesema ya kuwa msimu wa soka wa 2007-2008, huenda ukawa mwisho wake wa kucheza soka la kulipwa.
Ja Jay Okacha, ambaye kwa sasa anachezea timu ya Hull, amekuwa kivutio kikubwa kila awapo uwanjani kulisakata gozi la ngombe,hasa alipo kuwa amevalia jezi ya timu yake ya taifa ya Nigeria na kufunga magori 59 mpka hapo malipo jiudhuru kuchezea timu hii ya taifa.
Jay Jay Okacha, ambaye ameanzia kucheza timu ya Ujerumani Franfrut, Uturuki Fenebasche,PSG Ufaransa na Bolton ya Uingerea, amekuwa chachandu kwa kila timu aliyo chezea.
Pichani hapo juu anaonekana Jay Jay akiwa nanafanya vitu vyake ndani ya jezi ya the Green Eagles.
Picha ya pili anaonekana,Jay Jay Okacha akiuliza ya kuwa vipi, kwani kila aje kwangu ajue nipo kazini, lazima wawe fiti.
Picha ya tatu anaonekana Jay Jay Okacha, anaonekana akitoa kitu ambacho makipa huwa ni vigumu kutabiri ni jinsi gani wanaweza kuzuia kitu hiki.
Pope John II aonekana katika umbile la moto" adai mpiga picha hii".
Rome, Itali - Picha ambayo ipo katika umbile la moto, imeoneka hivi karibuni wakati wa kuazimisha miaka miwili toka kiongozi wa kanisa Katoriki Duniani hayati Pope John Poul II aiage dunia
Picha hii ilipigwa na polisi mmoja ambaye alipiga picha hii aliseama alikuja kuitambua picha hii baada ya ya muda fulani.
Maadhimisho haya yalifanyika karibu na eneo alilozaliwa Pope John II, kwenye mji wa Beskid Zywiecki.
Pichani hapo juu ni picha ya hayati Pope John II, akitoa salamu na baraka kila alipo kuwa akiwa ziarani, na upande wa pili ni picha ya umbile la moto ambayo ilipigwa siku ya kuadhimisha miaka miwili toka aage dunia.
Miaka mitano ya vita vya Irak, bado utata, " nani zidi".
Baghdad, Iraq - Dunia nzima hivi karibuni imeazimisha miaka mitano tangu vita vya Iraq vianze vikiongozwa na Amerika.
Haki hii imekuwa ya maoni tofauti na mabadiliko makubwa kijamii na kisiasa, aliongea haya , mmoja ya wafanyakazi wa zamani wa shirika la msaraba mwekundu bwana Roland H Benjanin ambaye alikuwa nchini Iraq, wakati wa vita vinaanza.
Shirika la msaraba mwekundu lilitoa wafanayakazi wake wote baada ya jengo lao kulipuliwa na na kusababisha vifo vya wafanayakazi wake. Hata hivyo vita hivi vmeleta maafa ya kupoteza maisha ya watu kutoka jamii tofauti,kuanzia wanajeshi na raia pia
Vita hivi mpaka sasa inasemekana idadi ya wanajeshi 4000, wa Amerika wamepoteza maisha yao, hii ni kwa mujibu wa kituo cha utafiti wa mambo ya kivita nchi Amerika.
Picha hapo juu anaonekana mmoja wa raia wa Iraq akiwa ameshikiliwa na wenzake huku akiwa na uchungu na majonzi baada ya mmoja wa familia yake kuuwawa na bomu hivi karibuni.
Picha pili chini anaonekana mwanajeshi wa jeshi la Amerika akiwa kazini huku raia wa Iraq,wakimwangalia kwa walakini.
Hatuelewi wanamuomba nani msamaha," kwani wanatakiwa kutimiza walicho haidi, mmoja wa wanajeshi waliopigana vita vya Iraq".
New York, Amerika - Harakati za kupata walichokuwa wakipigani imefika hali ya kuwa usumbufu kwa wanajeshi waliopigania nakutetea nchi ambayo walikuwa wanajua ya kuwa wakimaliza kutimiza kazi waliyo tumwa na hawatakuwa na wasiwasi wakuwa raia wa nchi amabyo walipigania na nchi ambayo ilikuwa ndoto yao, haya yalisemwa na mmoja wa wapiganaji ambao walikuwa mstari wa mbele kataika vita vya kumng'oa madarakani rais wa Iraq hayati Saadam Hussein.
Wakiongea kwa nyakati tofauti, wapiganaji hawa, bwana Abdool Habibullah mwenye miaka 27, ambaye ni mzaliwa wa Guyana, alisema yakuwa aliomba urai wa amerika semptemba 2005, baada ya kurudi kwenye mambano ya Iraq,na mpaka sasa 2008, bado anangojea majibu, nas inaelekea alicho ongea rais Bush ya kuwa hali itakuwa nzuri na kila kitu kitakuwa sawa tutakapo rudi kutoka vitani. Sasa hatuelewi nani wanaomba msamaha,kwani wanatakiwa kutimiza hahadi waliohaidi.
Akiongezea yakuwa hali hii ni kuto kuwajibika kwa baadhi ya watu waliopo maofisini, mmoja ya wapiganaji walio rudi kutoka vitani Krzsztof Matejqowasqi mwenya miaka 22, ambaye amekaa Iraq kwa kipindi cha miezi 15 alipo rudi alikuta yakuwa karatasi za maombi yake ya kuwa raia wa Amerika zimepotea.
Picha hapo juu ni moja ya wanajeshi ambao wamepigana vita vya Iraq, na mpaka sasa wanasubiri uraia wao kupitishwa.
Kamati ya Usalama na Ulinzi ya Umoja wa mataifa, inakiuka miiko yake,na Darfur wanateketea.
New York - Amerika -Aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa mataifa bwana Kofi Annan, amesema ya kuwa kamati ya ulinzi na usala ya Umoja wa Mataifa ina kiuka( miiko)wajibu wake kwa kufungia macho matatizo yanayao tokea Darfur.
Akiongea haya wakati alipo kuwa amealikwa kwenye chakula, bwana Kofi alisema ya kuwa dunia nzima imekuwa ikitegemea kamati hii ya ulinzi na usalama kufanya maamuzi ambayo yana manufaa kwa wanadamu wote, lakini sivyo kamati hii inavyo fanya.
Aliongozea ya kuwa kupelekwa kwa jeshi la Umoja wa Afrika Darfur, imekuwa ni kitendawili kwa kamati hii, na wakati huo huo watu wanazidi teketea kwa kipindi kirefu sasa.
Bwana Annan, ingawa hakutaja nchi, lakini inaeleweka ni nchi zipi zipo kwenye kamati hii, aliongea haya mmoja ya wageni walioalikwa kwenye chakula hiki kula pamoja na bwana Annan
Wa Cyprus wataka kuwa kitu kimoja, viongozi wao wasisitiza.
Nicosia, Cyprus - Viongozi wapinzani wa kisiwa cha Cyprus, bwana Mehmet Ali Tarat na Demetris Christofias, walikutana na kuongea chini ya usimamizi wa umoja wa Mataifa.
Mkutano huu ulifanyaiaka kwenye eneo ambalo lipo chini ya Umoja wa mataifa.
hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwa viongozi hawa kukutana baada ya bwana kuwa rais wa Cyprus ambayo ipo upanda wa Greeki.
Viongozi hawa walisema ya kuwa wanataka kufungua kitabu kipya, na kuleta mabadiriko ya kisiasa kisiwani hapo.
Kisiwa cha Cyprus, kimegawanyika sehemu mbili, moja ipo chini ya serikali ya Uturuki na nyingine ipo chnini ya serikali ya Greesi.
Talibani, wasema bado wapo ngangali, waja na mbinu mpya za mapigano.
Kabul, Afghanistani - Kiongozi wa kundi la Talinani bwana Jalaluddini Haqqani, ametangata ya kuwa kundi lake litaanz mashambulizi umpya ya kupigana na wanajeshi wa NATO amabao wapo nchini Afghanistani.
Akiongea katika runinga ambayo ememuonyesha bwana, Jalaluddini Haqqani akiwa amepauka kwa kiasi,aliendelea kusema ya kuwa. kupotea kwao ilikuwa ni moja ya mbinu za kujijenga upya, na hivyo vita hivi hawakuwa wameshindwa, na sasa wamekuja na mbinu mpya ya kushambulia kwa kutumia mbinu za kuvuizia na kushusha.
Picha hapo juu anaonekana kiongozi wa Talibani, bwana Jalaluddini Haqqani akiwa ndani ya gani moja nchini Aghanistani.
Picha nyingine ni picha ambayo inaonyesha jinsi gani Talibani wanavyosumbua vichwa ya jumuia ya kimataifa,kwani hapo katika picha ni moja uaribifu uliotokea baada ya bomu kulipuka na kuuwa baadhi ya wanajeshi wa NATO na wakazi wa eneo hili.
Jeshi la Umoja wa Afrika kuanza kuonyesha misuri yake katika kutatua matatizo ya bara la Afrika?
Njuani, Komoro - Kikosi cha jeshi la Umoja wa Afrika, kimewasili kwenye kisiwa cha Njuani, tayari kupamabana kurudisha kisiwa hicho mikononi mwa serikari.
Inaaminika zaidi ya wanajeshi wasiopungua 1000, kutoka Tanzania, Sudani, na Senegali wapo tayari kukiweka kisiwa hicho mikononi mwa serikali, aliongea haya msemaji wa jeshi hilo la umoja wa Afrika, kamanda Yahaya Abdalhah.
Serikali ya Libya ndiyo itakayo toa kila aina ya misaada ya kiufundi na kitaaluma.
Kisiwa cha Komoro kimekuwa na mgogoro wa kisiasa tangu ulipo fanyika uchaguzi 2002.
Pichani hapo juu wanaonekana wanajeshi wa jeshi la jeshi la Umoja wa Afrika wakiwasili kwenya kisiwa cha Juani nchini Moroko.

Wednesday, March 5, 2008

Polisi atoa siri ya serikali"Serikali ya kanusha" Ushwari kuanza kurejea.

Nyota ya timu ya Barcelona yapata majeraha kwa mara nyingine.

Barcelona, Uispania - Mchezaji nyota wa timu ya Barcelona na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi, hataweza kucheza kwenye mechi au mazoezi kwa kipindi kisicho pungua wiki sita, baada ya kuchanika misuri ya mguu wake wa kushoto.
Messi,amekuwa akisumbuliwa na majeraha tofauti ambayo yamekuwa yakimkuta kila mara.
Akisema haya mganga wa timu ,aongezea yakuwa itambidi apumzike kwa kipindi na siyo vyema kumharakisha kuanza mazoezi.
Akiongezea haya kaptaini wa timu ya Barcelona, Chales Puyol alisema ya kuwa wapenzi wa timu yao wamakuwa wanadai Messi achezeshwe, pindipo akionekana ana nafuu kidogo, na akashauri wawe wavumilivu na kuacha kazi hii iwe ya waganga wa timu.
Pichani hapo juu anaonekana Lionel Messi akiwa na nyota ya soka Diego Armando Maradona.
Picha ya pili anaonekana Messi akiwa anafanya mavitus kabla ya kupata majeraha ya misuri wakati wa pambano la marudiano na timu ya Celtic ya Schotland.
Picha nyingine naonekana Mesi akiwa anagaaga chini, baada ya kupata maumivu,na picha ya chini anaoneka Lionel Messi akiwa anatolewa nje ya uwanja na mmoja wa viongozi wa timu ya Barcelona.
Bi, Madona atoa album mpya, wapenzi wake kukonga roho.
London, Uingereza - Malkia wa muziki wa pop, bi Madonna amezindua rasmi album mpya ijulikanayo kama Hard Candy.
Album hiyo ambayo imekuwa ikingojewa kwa hamu saana, imeanza rasmi kupataikana tangu tarehe, 29/april/2008.
Madonna ambaye kila anapotoa album yake huwa ana kujas na kitu kipya, hivyo kwenye album hii, amesema ya kuwa hii albumu ni kwa ajili ya wale wanaopenda lawalawa.
Picha hapo juu anaonekana bi Madonna , akiwa ame mwaga tabasamu ya hali ya juu, kuashiria ya kuwa wapenzi msiwe na shaka album hii ita konga roho zenu.
Picha ya pili na ya tatu anaonekana bi Madonna anapo kuwa kazini hataki mchezo, huwa anafanya kweli kwa kila zana za muziki.
Picha ya bhapo chini anonekana bi Madonna akiwatumbwiza wapenzi wake huku akiwa amavalia vazi lenye rangi ya mapenzi.
Mafuriko yaleta madhara makubwa kwa wakazi wa Kusini mwa Afrika.
Windhoek, Namibia - Mvua kubwa ambayo inaendelea kunyesha maeneo ya Kusini mwa Afrika, inasababisha uharibifu mkubwa na kuleta madhala makubwa kwa wakazi wamaeneo haya,haya ni kwa mujibu wa msemaji wa msemaji wa kamati ya uokoji na kusaidia kwenye maeneo yaliyo dhurika na mvua hizi bwana Gabriel Kangowa.
Kwa mijibu wa msemaji wa UN, kwa upande wa kusaidia watoto alisema kunazaidi ya watoto wapatao 15000, ambao wanahitaji msaada wa haraka zaidi kwenye maeneo haya..
Mafuriko haya yameleta madhara maeneo tofauti ya nchi za Namibia, Zambia,Zimbabwe, Mozambiki na Malawi.
Picha hapo juu zinaonekana sehemu tofauti amabazo zimekumbwa na mafuriko na kuleta madhara makubwa kwa wakazi wa maeneo ya kusini mwa Afrika.
Polisi atoa siri ya serikali "Serikali yakanusha" ushwari kuanza kurejea.
Nairobi, Kenya - Serikali ya Kenya imekanusha ya kuwa haijawahi kuwa na mkutano wa siri na kundi la Mungiki, kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi.
Akiongea, msemaji wa serikali alikanusha ya kuwa hakukuwepo na mkutano waina yoyote kati ya serikali na kundi hilo.
Inasadikiwa mkutano huo ulifanyika kwa siri, ili kuweza kupanga ni jinsigani kundi hili linaweza kulinda watu wa kabila la Wakikuyu na mali zao hasa maeneo ya Lift Valley.
Siri hii imefichuka baada ya moja wa askari wa polisi kuongea na shirika moja la habari,na kueleza ni kwanini kwenye baadhi ya maeneo, watu wenye siraha waliruhusiwa kuvivuka vizuizi vya polisi bila kuzuiliwa kuelekea maeneo yaliyo tokea fujo.
Picha hapo juu, wanaonekana polisi wa Kenya wakipambana na moja ya watu amabo wanashutumiwa kuleta vurugu na machafuko.
Picha nyingine wanaonekana wananchi wenye huruma wakimsaidia mmoja wa majeruhi, aliye pata majeraha kutokana na vurugu hizi.
Picha ya chini anaonekana, aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa Matifa bwana Kofi Annan, akiongea na waandishi wa habari baada ya viongozi wa pinzani wa Kenya, bwana Mwai Kibaki na Laila Odinga kukubaliana kuongoza nchi kwa pamoja.

Ukanda wa Gaza, bado waleta kichwa kuuma kwa serikali ya Amerika.
Gaza, Palestina - Rais wa Palestina bwana Mahmoud Abbas, ameseama ya kuwa hataendelea na mazungumzo ya kuleta amani kati ya Israeli na Palestina.
Rais Mahamoud Abbas aliyasema haya wakati alipo kuatana na waziri wa mambo ya nje ya nchi wa Amerika bi, Condoleeze Rice, wakati alipo kwenda kumuona kujadili ni jinsigani utulivu unaweza kurudi, baada ya machafuko yaliyo tokea siku za karibu, kati ya kundi la Hamas na na Jeshi la Israel.
Waziri wa mambo ya nje wa Amerika, yupo ziarani kwenye maeneo haya, kuendeleza mazungumzo ya amani katai ya Israeli na Palestina.
Machafuko haya ambayo yameanza tena kwenye ukanda wa Gaza yamekuwa ya kuwa, yakivuruga upatikanaji wa amani katika eneo hili kwa muda mrefu.
Picha hapo juu anaoneka arais Mahamoud Abbas, akimkaribisha bi, Condoleeze Ricealipo kwenda kumtembelea hivi karibuni.
Picha chini anaonekana bi,akikaribishwa na mmoja wa viongozi wa Israeli, alipokwenda kuongea na viongozi wa Israeli
Viongozi wa dini zote kukutana mjini Rome, kuunga dalaja la imani kwa waumini wao.
Rome Itali - Kiongozi wa Kanisa Katoliki diniani Pop Benedict,ataongoza mkutano kati ya Waumini wa Kikristu na Waumuni wa Kiislamu utakao fanyika mwezi wa November mwaka huu.
Akiongea haya msemaji wa wa Vatican alisema ya kuwa mkutano wa kwanza utafanyika november 4 mpaka 6 mjini Rome.
Mkutano huu utaudhuliwa na viongozi wa dini wa wapatao 24 na walimu wa dini zote.
Moja ya mazungumzo yatakayo watakayo zingatia na kujadili kwa undani ni Upendo wa Mungu,n upendo kwa jirani , utu na kuheshimiana kwa watu na imani zao.
Picha hapo juu ni alama inaonekana alama ya mwezi na nyota kama alama ya Uislamu, kati ni alama ya Msalaba ikiwa ni ishara ya kuamini Ukristu
Chini ni picha ya Pop Benedict, akiwa ameshikilia na kukinyanyua kitabu kitakatifu juu.
Rais,Hugo Chavez aionya, serikali ya Kolombia kaeni chonjo, kazi mbaya si mchezo mwema.
Cucuta,Vanezuela - Serikali ya Venezuela, imeaanza kupeleka majeshi yake pamoja na vifaru kwenye mpaka na nchi ya Kolombia,haya ni kwa mujibu wa msemaji wiraza ya ulinzi.
Kupelekwa kwa wanajeshi hawa mpakani, kuna kuja baada ya jeshi la Kolombia, kuingia kinyume cha sheria nchini Ekuado na kumua kiongozi wa kundi la FARC,bwana Raul reyes.
Kuwepo kwa majeshi haya mpakani mwa Kolombia na Venezuela, ni kuwa seriakli ya Venezuela inajiandaa kuzuia uwezekano wa majeshi ya Kolombia kuvuka mpaka na kuingia nchini Venezuela, ambapo inadaiwa ya kuwa, mipakani humo ndipo wapinzani wa serikali ya Kolombia FARC, wanaishi.
Picha ya juu, anaonekana rais Hugo Chavez, akiongea na waandishi wa habari kuhusu maswala ya ulinzi nchini Venezuela.
Picha nyingine anaonekana, rais Hugo Chavez, akijaribu siraha amabyo ni moja ya siraha zitakazo tumika, pindipo vita vikianza kati ya Venezuela na Kolombia.
Picha ya chini wanaonekana wanajeshi wa Venezuela wakiealeka mpakani mwa Venezuela na Kolombia.