Sunday, March 20, 2016

Rais Jakaya Kikwete


Mwandishi wa Habari na Mtangazaji, Rukundo L Kibatala, anakuletea makala fupi ya historia ya Uongozi wa Rais Mstaafu wa Tanzania ndugu Jakaya M Kikwete.

Wednesday, March 9, 2016

Iran yarusha makombora.


Tehran, Iran 09/03/2016. Jeshi la Iran limefanikiwa kurusha makombora mawili  (Ballist missiles)  Urushaji wa makombora hayo yaliyo pewa majina ya Qadr -H na Qadr F ulifanyika kaskazini mwa nchi hiyo katika eneo lijulikanao Alborz Mashariki. Makombora hayo yanauwezo wa kushambulia umbali wa kilomita 1500 hadi 2000.

Kamanda wa kitengo cha usalama wa anga wa Iran, Brigedia, Amirali Hajizadeh amesema kuwa. "Kombora aina ya Qadr H linuwezo wa kushambulia umbali wa kilomita 1700 na jingine Qadr F linaweza haribu na kuchakaza kabisa kitu chochote kilichopo umbali wa kilomita 2000."

Tamko la Iran kuhusu kurusha makombora yake, limekuja baada ya msemaji  wa serikala ya Marekani Mark Toner kukosoa kitendo hicho nakusema " Kufuatia kitendo hicho cha Iran, Marekani italifikisha suala hilo katika balaza la usalama la umoja wa mataifa."

Hata hivyo waziri wa mambo ya nje wa Iran Javad Zarif, amesema kuwa " Iran haitaji ruhusa yoyote katika masuala yake ya kiulinzi wa nchi, na tulisha sema kuwa hatuta ulizia wala  omba ruhusa katika kushughulikia masuala yetu ya kiulinzi."

Iran nchi ambayo ilikuwa imewekewa  vikwazo vya kiuchumi kwa muda mrefu na Marekani na washiriki wake, imekuwa kwa miaka mingi ikijitengenezea mitambo ya kiulinzi ya kijeshi na pia kuhakikishia jumuia ya kimataifa kuwa utengenezaji wa zana za kiulinzi  ni harakati za kujiimarisha katika suala la ulinzi wa nchi.




Wednesday, March 2, 2016

Osama bin Laden alitaka mirathi yake itumike kundeleza mapambano. 


Aliyekuwa kiongozi wa kundi la Al Qaeda, Osama bin Laden, alikuwa ameandika kuwa mirathi yake  ya kifedha zipatazo $29 millioni, kwa kiasi kikubwa zitumike takika kusaidia kuendeleza "Jihad" mapambano,  na kiasi kidogo kigawiwe kwa ndugu wa familia, ijapokuwa mpaka hazijulikani hizo fedha zipo wapi.

Zikiwa zimeandikwa kwa mkono wa Osama bin Laden, habari hizi, zimetolewa na serikali ya Marekani wiki hii, baada ya kuruhusu mafaili yaliyo kamatwa na kikosi maalumu cha kijeshi cha Marekani wakati walipo kuvamia makazi na  maficho  ya Osama bin Laden yaliyo kuwepo kwenye mji wa Abbottabad  Pakistan siku ya 1. Mai 2011 na kufanikiwa kumua.

"Nivyema kwa jamii kufahamu nini kiongozi wa Al Qaeda alipanga"  Alisema Brian Hale Mkurugenzi wa mambo ya jamii kutoka idara ya upelelezi ya taifa ya Marekani huku akiwa anaonyesha makaratasi yaliyo chukuliwa kutoka katika makazi wa Osama bin Laden

Karatasi hiyo ambayo inaonyesha nini kiongozi wa Al Qaeda alitaka kifanyike katika mirathi yake, ni moja ya makatasi 100 ambayo yameruhusiwa kuwekwa hadharani, baada ya kamati ya ulinzi na usalama kuyapitia kwa uangalifu.