Sunday, November 27, 2016

Rais Fidel Castro hatupo naye tena

Rais wa kwanza wa Kuba aaga dunia.


Havana, Kuba - 26/11/2016. Fidel Castro 90 rais wa kwanza wa Kuba na mwana mapinduzi amaefariki dunia.
Akitangaza kupitia luninga ya nchi hiyo, rais was sasa wa Kuba Raul Castro, alisema kuwa "rais wetu wa kwanza na kiongozi na mwanamapinduzi Komrade Fidel Castro amefariki leo 25/11/2016."
Kufuatia kifo cha rais Castro, Kuba itakuwa katika maombelezo ya siku tisa. Mazishi ya rais huyo wa Kuba yanatarajiwa kuudhuliwa na viongozi mbalimbali wa dunia.
Fidel Castro alikuwa mpinzani wa siasa za kibepari na alikuwa akipenda kusema "Uwanamapinduzi ni ni mapambano mpaka kufa ya wakati uliyo pita na wakati ujao."
"Wanaongea kushindwa kwa ujamaaa, lakini yapo wapi mafanikio ya siasa za kibepari katika bara la Afrika Asia na Latin Amerika?
" Sikubaliani na ubepari, ni mbaya auvutii na unatenganisha unaleta vita vitna na mashindano yasiyo na tija katika jamii."
Marehemu rais mstaafu wa Kuba Fidel Castro alizaliwa mwaka 31/08/1926 mjini Biran Kuba.

Wednesday, November 9, 2016

Donald John Trump ashangaza ulimwengu wa Siasa, Achaguliwa kuwa rais wa Marekani

Donaldo John Trump achaguliwa kuwa rais wa 45 wa Marekani

New York, Marekani - 09/10/2016.  Donald John Trump, amechaguliwa kuwa rais wa 45 Marekani baada ya kupata vit vya kura 289 zidi ya mpinzani wake Hillary Clinton aliyepata viti vya kura 218.

Donald Trump akiongea mbele ya wapenzi na washabiki wake walikuwa katika hotel yake inayo julikana kama The Trump alisema. " Hillary Clinton amenipigia simu na kutupongeza na ninampongeza kwa jitihada zake wakati wa harakati wa uchaguzi huu."

"Ushindi wa leo, ni harakati na hazikuwa kampeni za uchaguzi, hivyo hizi harakati ndio sasa zimeanza kazi."

Vilevile rais mteule Donald Trup, aliwaomba watu wote kuwa wamoja na kwa kusema kuwa wale waliomchagua na wasionipigia kura wote wawe kitu kimoja na kuwa atakuwa rais wa Wamarekani wote.  "Nawaomba wote walio umia kutokana na uchaguzi tuwe wamoja ili kujenga Marekani mpya."

Rais mteule, Donald Trump, alikumbana na vikwazo vya kila namna katika kampeni za kuwania urais wa Marekani, kwa kudaiwa kuwa mbaguzi, msemaji wa vitu na mambo ambayo si yakiutu an pia kudaiwa kuwa alikuwa anadhalilisha wanawake.

Ushindi wa Donald Trup unatafsiliwa kuwa ni jibu kwa wanasiasa kwamba wabadirike kwa kuwa wa watu wamechoka na siasa zisizo eleweka na haadi wazizotimiza.