Laurent Gbagbo akutana na viongozi wa ECOWAS.
Abidjan, Ivory Coast- 28/12/2010. Marais watatu wa jumuia ya kiuchumi ya nchi za Afrika ya Magharibi wamekutana na rais wa Ivoty Coast ili kujadili hali ya kisiasa nchini humo na kumtaka aachie madaraka. Marais hao ni Boni Yayi wa Benin, Ernest Bai wa Sierra Leone, na Pedro Pires wa Kape Verde walikutana na rais wa sasa Laurant Gbagbo kuzungumzia hali halisi ya myumbo wa kisiasa uliopo katika nchi hiyo. Marais hao kabla ya kuonana na Gbagbo, waliongea na Alassane Ouattara ambaye jumuia ya kimataifa inamtambua kama ndiye mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika hivi karibuni. Hata hivyo hakuna habari zilizo tolewa kwa undani ili kwa pamoja walisema mkutano ulikuwa wa mafanikio. Picha hapo juu wanaonekana marais wa Laurent Gbagbo kushoto, Ernest Bai Koroma wa Sierra Leone na Boni Yayi wa Benin wakiongea na waandishi wahabari mara baada ya kukutana kwao.Tuesday, December 28, 2010
Laurent Gbagbo akutana na viongozi wa ECOWAS.
Posted by Kibatala at Tuesday, December 28, 2010 0 comments
Friday, December 24, 2010
Korea ya Kusini na Kaskazini wasiwasi wazidi kukuwa.
Makampuni ya Amerika yafanya biashara za kijamii na Iran.
Posted by Kibatala at Friday, December 24, 2010 0 comments
Tuesday, December 21, 2010
Irak yapata serikali mpya.
India na Urussi kushirikiana kwa ukaribu zaidi. New Delhi, India - 21/12/2010. Serikali ya India na Urussi zimekubaliana kwa pamoja kushirikiana katika nyanja za kiusalama na kutiliana mikataba ya kibiashara uchumi na sayansi. Rais wa Urussi Dmirty Medvedev na waziri mkuu wa India Manmohan Singh walikubaliana mikataba hiyo wakati walipo kutana na kuzungumza ili kudumisha uhusiano zaidi. Ziara hiyo wa rais wa Urussi imekuja baada ya ziara za kufuatana za viongozi wa Uingereza, Amerika, China na Ufaransa kufanya ziarani nchini India ili kudumisha ushirikiano wakaribu. Picha hapo juu wanaonekana rais wa Urussi Dmirty Medvedev kushoto akipeana mkono na waziri mkuu wa India Manmouhan Singh mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao. Irak yapata serikali mpya.
Posted by Kibatala at Tuesday, December 21, 2010 0 comments
Thursday, December 16, 2010
Baraka Obama atangaza hali halisi ya Afghanistan.
Baraka Obama atangaza hali halisi ya Afghanistan. Washington, Amerika 15/12/2010 - Serikali na washiriki wake wanafanya kazi nzuri katika kuijengaAfghanistan na kuwaanda wananchi wa Afghanistan kuijenga nchi yao. Rais Baraka Obama, alisema "ingawaje hali ni ngumu lakini hii siyo kikwazo kwani, na nashukuru wale wote waliojitolea na kuendelea kujitolea pamoja na wapiganaji wetu ambao wanafanya kazi usiku na mchana ili kuijenga Aghanistan." Akiongezea rais alisema, "maendeleo yanaonekana na maendeleo haya ndiyo msingi mkubwa wa kuwafanya wananchi wa Afghanistan kuamini yakuwa kazi iliyo fanywa na jumuiya ya kimataifa ilikuwa ni kwa ajili ya wanachi wa Afghanistan." Baraka Obama, ameongea hayo ili kuwahakikishia wanachi wa Afghanistan ya kuwa Amerika ipo pamoja nao. Picha hapo juu anaonekana rais Baraka Obama, akiongea na waandishi wa habari ili kuzungumzia hali halisi ya Afghanistan na mipango ya kuisadia nchi hiyo kimaendeleo. Hatimaye mwanzilishi wa Wiki Leaks akubaliwa dhamana
Posted by Kibatala at Thursday, December 16, 2010 0 comments
Wednesday, December 15, 2010
Ghana kuanza kuzalisha mafuta.
Irak yaondolewa vikwazo na Umoja wa Mataifa. New York, Amerika - 15/12/2010.Kamati ya usalama ya umoja wa Mataifa imeiondolea vikwaza nchi ya Irak iliyo kuwa imeviweka kwa muda wa zaidi ya miaka 19. Akiongea katika mjadala wa kutaka kuiondolea vikwazo Irak, makamu wa rais wa Amerika Joe Biden alisema "Irak inahitaji kuwa katika kiwango cha kimataifa kwa kujitegemea yenyewe na demokrasi ndiyo msingi mkubwa ambo utifanya nchi hiyo imeze kuendelea na Wairak wameonyesha uwezo huo. Pia ni muhimu kwa Irak kuwa na uhusiano mzuri na majirani zake kwani bado Wairak wanamthian mkubwa mbeleni." Katika kikao hicho, kamati ya usalama iliondo vikwazo vyote ilivyoviweka kwa Irak na kupitisha mswada ambao umeiruhusu Irak kuweza kujenga mtambo wa nyuklia kwa matumizi ya kawaida. Vikwazo kwa Irak viliwekwa mwaka 1991 na umoja wa Mataifa mara baada ya Irak kuivamia Kuwait mwaka 1990 enzi ya utawala wa rais Saddam Huissen ambaye alitolewa madarakani na serikali ya Amerika mwaka 2003 baada ya kushukiwa kuwa na siraha za kuangamiza jamii. Ghana kuanza kuzalisha mafuta. Akrah, Ghana - 15/12/2010.Wananchi wa Ghana kwa mara ya kwanza wameungana na nchi nyingine dunia katika kuzalisha mafuta kutoka kwenye Ghuba ya Guinea. Akifungua kuanza kwa uzalishaji huo rais wa Ghana John Atta Mills alisema "kuzalishwa kwa mafuta hayo ni baraka na siyo laaana kwa wananchi wa Ghana, na mafuta yatakayo patikana yataisaidia Ghana kuinua uchumi wake zaidi kulio ilivyo sasa." Kiasi cha mapipa 55.000 yanatarajiwa kuzalishwa kwa siku. Eneo hilo liligunduliwa kuwa linamafuta miaka mitatu iliyo pita na kampuni moja ya Uingreza Tullow Oil PLC. Picha hapo juu ni ya ramani ya nchi ya Ghana ikiwa imefunikwa na rangi za bendera ya nchi hiyo ambayo kwa sasa inatambulika rasmi kuwa mzalishaji wa mafuta na kujiungana na nchi nyingine zilizopo katika bara la Afrika. Wanasiasa maarufu Kenya wahusishwa katika machafuko ya 2007
Posted by Kibatala at Wednesday, December 15, 2010 0 comments
Tuesday, December 14, 2010
Dunia ya mpoteza mtetezi wa amani.
Mahakama ya kubali maombi ya dhamana ya Julian Assange. London, Uingereza - 14/12/2010. Mahakama jijini London imekubali kumwachia kwa masharti mwanzilishi wa mtandao wa Wiki Leaks kwa dhamana ya dola za Kiamerika $ 317,400.
Julian Assange 39,ambaye anashitakiwa nchini Sweden kwa kosa la kufanya mapenzi ya kustukiza ambayo nimakosa nchini Sweden. Assange alijipeleka mwenyewe polisi mara ya karatasi ya kutaka kukamatwa kwake kutolewa na Interpol baada ya serikali ya Sweden kumfungulia mashitaka. Hata hivyo upo uwezekano wa serikali ya Sweden kupinga rufaaa hiyo. Picha hapo juu anaonekana Julian Assange ambaye anashukiwa na makosa ya kufanya mapenzi ya kushtukiza na moja ya mwanadada hivi karibuni nchini Sweden. Wanasheria wa Kenya wafikiria mara mbili mkataba wa Roma. Nairobi,Kenya - 14/12/2010. Kundi la wanasheria nchni Kenya wametishia kuandika barua kwa bunge la Kenya kufuta uanachama wake katika Mahakama ya Kimataifa (International Criminal Court-ICC). Kundi hilo la wanasheria walisema " tulitaka haki itendeke na mahakama ya kimataifa lakini haikuwa hivyo kutokana na uchunguzi wao. Na tunaangalia ni njia gani tutatumia kupitia bunge kujitoa katika matakaba wa Roma ( RomeStatute)." Mjadara huo umekuja baada ya ICC kusema inamajina sita ya watu waliohusika kuleta machafuko ya kisiasa kabla na baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika 2007. Machafuko hayo yalisababisha vifo vya watu zaidi ya 1500 na wengine 300,000 kuachwa bila makazi. Picha hapo juu anaonekana mmoja wa kijana akikimbia kuepusha maisha yake kutokana na machafuko yaliyo tokea kabla na baada ya uchaguzi nchini Kenya 2007 ambapo hali ya kiusalama ilikuwa imechafuka, kutisha kwa kilahali. Waziri mkuu wa Itali ashinda kura za maoni kwa mara nyingine. Roma, Itali - 14/12/2010. Waziri mkuu wa Itali ameshinda kura za maoni ambazo zilikuwa zimeitishwa zidi yake kutokana na baadhi ya wabunge na viongozi wa serikali kutokwa na imani naye. Silvio Berlusconi,ameshida kura hizo za maoni kwa kiasi cha uchache wa kura dhidi ya wale wanaopinga uongozi wake. Ushindi huo aliopata Berlusconi, siyo wa mara ya kwanza kwani alishida kura kama hiyo siku za nyuma. Hata hivyo wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema Berlusconi atakuwa na wakati mgumu kuongoza serikali kutokana na upinzani mkubwa katika bunge na serikalini. Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Itali,Silvio Berlusconi akionyesha dole baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa kuwa ameshinda tena kura za maoni ambazo ziliitishwa na vyama vya upinzani hivi karibuni. Dunia ya mpoteza mtetezi wa amani.Posted by Kibatala at Tuesday, December 14, 2010 0 comments
Sunday, December 12, 2010
Waziri mkuu wa Itali kuwekwa kwenye boksi la maoni na wabunge.
Waziri mkuu wa Itali kuwekwa kenye boksi la maoni na wabunge. Roma, Itali - 12/12/2010. Wachunguzi wa serikali wameanza uchunguzi kufuatia kuwepo na habari ya kuwa waziri mkuu wa Itali ametoa milungula ili ashinde kura za maoni kuuhusu uongozi wake. Malalamiko hayo yalifunguliwa na kiongozi wa upinzani Antonia Di Puerto ambaye akikosoa uongozi wa waziri mkuu wa sasa Silvio Berluscon. Naye kiongozi mwingine wa chama cha upinzani Luigi De Magistris alisema "tumeona rushwa inatumika kati ya wabunge ili kumuunga mkono Berluscon." Hata hivyo Berluscon alisema "sidhani kama kutakuwa na wasaliti wengi na naimani serikali itashinda." Uamuzi wa kutaka kura za maoni zipigwe kumekuja kutokana na baadhi ya wabunge hasa wa upande wa upinzani kutokuwa na inami na waziri mkuu kutokana na habari za matukio ambayo yanamuhusisha moja kwa moja. Picha hapo juu ni picha waziri mkuu wa Itali, Silvio Berluscon ambaye serikali yake imekuwa na mvutano sana na vyama pinzani na kutaka kura za maoni zipigwe zidi ya uongozi wake.
Uchaguzi wa wabunge Misri waleta mvutano upya.Posted by Kibatala at Sunday, December 12, 2010 0 comments
Friday, December 10, 2010
Ujerumani na Ufaransa zasema tutailinda sarafu ya Euro.
Ujeruman na Ufaransa zasema tutailinda sarafu ya Euro.
Freiburg, Ujerumani -10/12/2010. Kansela wa Ujerumani na rais wa Ufaransa wamekuta mjini Freiburg kujadili njia mbadala za kuimarisha sarafu ya Ulaya (EURO). Kansela Angela Markel na Nikolas Sarkozy walikutana na kuangalia kiundani njia ambazo zitaifanya sarafu ya Euro kuimarika zaidi hasa katika wakati uhu mgumu wa myumbo wa uchumi duniani. Viongozi hao kwapamoja walisema "tuta ilinda Eoro, kwani ni sarafu ya Euro ndiyo Ulaya yenyewe."
Kukutana kwa viongozi hao kunakuja kabla ya mkutan wa viongozi wa nchi wanachama wa jumuiya ya Ulaya kufanyika siku chache zijazo. Picha hapo juu anaonekana rais wa Ufaransa Nikolas Sarkozy kushoto akiongea huku Kansela Angela Markel akimsikiliza kwa makini sana na kutathmini nini hasa anaongea wakati walipo kutana hivi karibuni kujadili nini la kufanya ili sarafu ya Euro kuwa imara zaidi kimataifa. Zawadi ya Nobel yawekwa kwenye kiti cha mtarajiwa.
Oslo, Norway -10/12/2010. Sherehe za kumzawadia mshindi wa zawadi ya amani ya Nobel mwaka 2010 imefanyika jijini Oslo bila ya mzawadiwa kuwepo. Liu Xiaobo ambaye ni raia na mazaliwa wa China ndiye aliyekuwa mshindi wa zawadi ya amani ya mwaka 2010, lakini hakuweza kuudhulia sherehe hiyokwani anatunikia kifungo cha miaka 11 jela kwa kosa la uhani kwa mujibu wa sheria za China. Hata hivyo zawadi yake iliwekwa kwenye kiti ambacho alitarajiwa kukalia wakati wa kupokea zawadi hiyo. Thorbjoern Jagland ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo ya kutoa zawadi alisema " Liu hajafanya kitu au jambo baya yeye ni mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu." Msemaji wa serikali ya Chini Jiang Yu, alimesema "kutolewa kwa zawadi hiyo kwa Liu ni siasa iliyo shinikiza, ambayo ni zao la wakati wa vita vita vya baridi, na hivyo China haitakukubali kuingiliwa katika maamuzi yake." Picha hapo juu wanaonekana wageni waalikwa wakiangalia picha ya Liu Xiaobo aliye tunikiwa zawadi ya amani ya Nobel 2010 lakini hauwepo kwenye sherehe hizo na zawadi yake kuwekwa kwenye kiti alicho tarajiwa kukikalia.Posted by Kibatala at Friday, December 10, 2010 0 comments
Tuesday, December 7, 2010
Urussi kuwa mwanachama wa World Trade Organazations
Mwanzilishi wa mtandao wa Wiki Leaks awekwa kizuizini
Posted by Kibatala at Tuesday, December 07, 2010 1 comments
Monday, December 6, 2010
Mazungumzo ya Iran na Umoja wa Matifa yaanza nchini Uswisi.
Mazungumzo ya Iran na Umoja wa Mataifa yaanza nchini Uswisi.
Posted by Kibatala at Monday, December 06, 2010 2 comments
Sunday, December 5, 2010
Umoja wa Afrika watuma mjumbe kuleta suruhu za kisiasa nchini Ivory Coast
Umoja wa Afrika watuma mjumbe kuleta suruhu za kisiasa nchini Ivory Coast. Abidjan,Ivory Coast - 05/12/2010. Rais wa pili wa Afrika ya Kusini tangu kushindwa kwa utawala wa kibaguzi wa rangi, Thabo Mbeki amewasili jijini Abidjan ili kuleta suruhisho la matokeo ya uchaguzi wa rais. Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema "Thabo Mbeki ameteuliwa na Umoja wa Afrika (UA) kushughulikia swala la matokeo ya uchaguzi wa Ivory Coast, ambapo rais mtetezi Laurent Gbagbo waliapishwa kuwa rais, ingawaje apo awali kamati ya uchaguzi ilimtangaza mpizani wake Allasane Ouattara kuwa mshindi kwa kupata kura nyingi zaidi." Kuwasili huko kwa Thabo Mbeki kunatarajiwa kuleta suruhisho ili kuepuka mvutano wa kisiasa. Uchaguzi nchini Ivory Coast uliwahi kuhairishwa zaidi ya mara tano kutokana na mvutano wa kisiasa. Picha hapo juu ni ya aliyekuwa rais wa Afrika ya Kusini Thabo mbeki, ambaye anatarajiwa kuleta suruhisho la kisiasa nchini Ivory Coast.
Posted by Kibatala at Sunday, December 05, 2010 0 comments
Friday, December 3, 2010
Baraka Obama afanya ziara ya ghafla nchini Afghanistan.
Baraka Obama afanya ziara ya ghafla nchini Afghanistan. Kabul, Afghanistan - 03/12/2010. Rais wa Amerika amefanya ziara ya ghafla nchini Afghanistan na kuongea na wanajeshi na raia wa Amerika wanaoshiriki kwa katika vita zidi ya Taliban na washirkia wake. Akiongea katika hotuba hiyo rais Baraka Obama alisema "Amerika itaendelea na kupambana na wale wote ambao wanapinga maendeleo ya Amerika au kutishia usalama wa Amerika na watu wake, na hatutashindwa kamwe kuwasaka popote walipo." Hata hivyo katika ziara hiyo rais Baraka Obama, hakuweza kukutana na rais wa Afghanistan kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya. Picha hapo anaonekana rais wa Amerika Baraka Obama akishuka kutoka kwenye ndenge mara baada ya kuwasili nchini Afghanistan kwa mara ya pili akiwa kama rais wa Amerika ili kuwapa salamu za sikuku wanajeshi na kuelezea ni kwa jinsi gani Waamerika wote wapo pamoja nao. Ulaya ya kumbwa na mporomoko wa barafu. London, Uingereza - 03/12/2011. Bara la Ulaya limekumbwa na mporomoko wa barafu ambao umesababisha hali ya utoaji wa huduma kuyumba. Barafu hizo ambazo zinaendelea kugubika karibuni Ulaya kote tokea Urussi hadi Spain limekuwa gumzo kwa wakazi wengi wa eneo hili. Siku ya Jumanne barafu nyingi ilipolomoka na kusababisha hali ya hewa kuwa barisi hadi kufikia kati ya hasi 20 na 22. Picha hapo juu linaonekana moja ya gari la kusafisha njia likijaribu kutoa barafu ili huduma ziweze kuendelea zilishindikana kutokana na wingi wa barafu iliyo poromoka toka angani
Posted by Kibatala at Friday, December 03, 2010 0 comments
Thursday, December 2, 2010
Kombe la dunia mwenyeji ni Urussi 2018 na Katar 2022.
Kombe la Dunia wenyeji ni Urussi 2018 na Katar 2022.
Posted by Kibatala at Thursday, December 02, 2010 0 comments
Tuesday, November 30, 2010
Mkutano wa utunzaji wa mazingira waanza kwa mashaka.
Google kufanyiwa uchunguzi na jumuia ya Ulaya. Brussel, Umoja wa Ulaya - 30/11/2010. Kitengo cha uchunguzi cha jumuia ya muungano wa umoja wa Ulaya kinachunguza malalamiko yaliyo tolewa dhidi ya Google kwa kukutumia vibaya umezo wake. Kwa mujibu wa makampuni mengine ya kimtando yamsema "google inavunja ushindani wa kiimtandao dhidi ya makampuni washindani." PIcha hapo juu inaonekana picha ya mtandao wa Google ambao unalalamikiwa na washindani wake kwa kuvunja ushindani. Mkutano wa kutunza mazingira waanza kwa mashaka. Cancun,Mexico - 30/11/2010. Mkutano wa kutunza mazingira unaofanyika nchini Mexico umeamza kwa vishindo huku kila nchi muhusika akitaka matakwa yake yatimizwe. Akiongea katika mkutano huo mwakilishi wa serikali ya Amerik Jonathan Pershinga alisema " tunataka kuwepo na makubaliano ya pamoja katika kudhibiti uaribifu wa mazingira duniani" Hata hivyo msimamo huo wa Amerika umeonekana kutiliwa mashaka na baadhi ya washiriki kwa kudai kuwa hakutaleta matokeo mazuri. Pichani hapo juu aanonekana mmoja ya washiriki wa mkutano wa mazingira unaofanyika Mexico akichora kapicha kuashiria ishara kuhusu matokeo ya mikutano iliyo fanyika hapo awali kabla wa sasa unaofanyika Cancun Mexico ambapo wajumbe wa nchi tofauti wanakutana kujadili mazingira. Venezuela yapewa mkopo na Urussi kwa ajili ya kuimarisha maswala ya kiulinzi. Carakas, Venezuela 30/11/2010. Serikali ya Venezuela imesema ya kuwa serikali ya Urussi itaipa mkopo wa $4 billion ambazo zitaiwezesha nchi hiyo kukuawa siraha ili kuimarisha maswala ya kijeshi na ulinzi. Akiongea katika sherehe ya miaka 90 ya jeshi la anga rais wa Venezuela Hugo Chavez alisema " Tumeamua kufanya hivyo ili kuendelea kulinda nchi yetu na maadui." Picha hapo anaonekana rais wa Venezuela Hugo Chavez wakati wa kuadhimisha sherehe za maiaka 90 ya jeshi la anga ambalo ilitaongezewa nguvu. Radi yaleta maafa na vifo ya watu nchi Afrika ya Kusini. Kwa Zulu Natali, Afrika ya Kusini - 30/11/2010.Watu wapatao saba na wengine kujeruhiwa baada ya radi kuwashambulia wakati wakiangali jengo lilijenge kwa turubai kwaajili ya Krismas. Kwa mujibu wa msemaji wa serikali anayeshughulikia maafa Mthokozisi Duza alisema "watu walio jeruhiwa apo hospitali kwa matibabu." Picha hapo juu inaonyesha miali ya moto iliyo tokana na radi ikishambulia Kwa zulu Natal na kusababisha maafa ya kijamii na kwa mazingira. Rais wa Urussi atoa onyo ikiwa hakuna makubaliano na NATO.
Posted by Kibatala at Tuesday, November 30, 2010 1 comments