Thursday, April 3, 2008

Waziri mkuu wa zamani wa Kosovo,hanahatia, mahakama ya mwachia huru.

Bi, Naomi awa matatani na polisi uwanja wa ndege mjini London.

London,Uingereza - Mwana dada, Naomi Campbell amekamatwa na polisi kwenye kiwanja cha ndege Heathrow.
Bi, Naomi, amekamatwa na polisi,baada ya kukorofishishana na polisi wakiwanja cha ndege.
Bi, Naomi aligombana na polisi, baada ya kupishana lugha na na polisi hawa kuhusu mizigo yake kwenye termimal 5.
Pichani za hapo juu anaonekana bi Naomi, akiwa amepozi wakati wa moja ya maonyesho ya sanii.
Umoja wa mataifa upo kwa ajili yakuleta amani na utuilivu duniani kote"asema katibu mkuu"
Bucharest, Romania - Katibu mkuu wa umoja wa mataifa bwana, Ban Ki moo, amesema ya kuwa umoja huu haupingi Uislam.
Bwana Ki moo, aliyaongea haya kwenye kikao cha NATO kinacho fanyika mjini Bucharest, na kupinga maneno ambayo ya meongewa na kiongozi na mbili wa Alqaida, bwana Ayman Al- Zawahir, ambaye amedai yakuwa umoja huu wa mataifa unashiriki katika kupiga vita Uislamu.
Aliongezea yakuwa umoja huu upo kwa ajili ya kuleta amani na utulivu duniani kote.
Bwana Ki moo, amealikwa katika kikao hiki kuongea na viongozi wa NATO, kuhusu maswala ya amani duniani,kwanai NATO , ni shirikisho lenye nguvu duniani.
Picha hapo juu anaonekana bwana, Ban Ki moo, akongea na waziri mkuuwa Uingereza kuhusu maswala fulani, huku akonyesha kwa vitendo kutumia mkono wake.
Chini ni picha ya kiongozi namba mbili wa kundi la Aqaida, bwana Ayman Al Zawahiri, akiongea kupitia mtandao.
Waziri mkuu wa zamani wa Kosovo, hanahatia, mahakama ya mwachia huru.
The Hague, Holland - Mmoja ya watuhumiwa wa vita vya Kosovo,bwana Ramush Haradinaj,ameachiliwa huru baada ya kesi dhidi yake kukusa ushaidi kamili.
Bwana, Ramush Haradinaj, ambaye alishawahi kuwa waziri mkuu wa Kosovo, aliachiwa huru , baada ya baadhi ya mashahidi kushindwa kutoa ushahidi dhidi yake kwa kuhusika katika viata vya wenyewekwa wenyewe ambavyo vilifanyika nchin Kosovo 1998.
Akiongea mbele ya koti , jaji Alphonss Orie, alisema ya kuwa imekuwa ni vigumu kumtia hatiani mtuhumiwa kwani ushahidi haukuwa wakutosha.
Kabla ya hapo wakili wa mahakama hiyo waliomba mahakama imuhukumu bwana Ramush Haradinaj kifungo cha miaka 25 jela, laki hata hivyo kutokana na ukosefu wa ushahidi imekuwa ni vigumu , alimalizia mmoja ya wanasheria wa mahakama hiyo.
Picha hapo juu kulia ni picha ya bwana Ramush Haradinaj, akitabasamu baada ya jaji kusema yakuwa hakuna ushahidi na hivyo hayupo hataiani.
Picha ya pili naonekana bwana Ramush Haradinaj,akiingia mahakamani wakati wa mwazo wa kuanza kesi dhidi yake.
Mtetezi wa haki za binadamu awekwa ndani na Pilato kwa kuongea.
Beijing, China - Mmoja wa watetezi wa haki za binadamu nchini China bwana Hu Jia, amehukumiwa kwenda jela kwa kipindi cha miaka mitatatu na nusu, kwa kosa la kuongea mambo amabyo serikali ya China haikufurahishwa nayo.
Bwana Hu Jia, amekutwa na hatia baada ya habari alizo ongea na waandishi wa habari, kuonekana kwenye (internet) au mtandao.
Bwana Hu Jia ,amekuwa mtetezi wa haki za binadamu nchini China ,na amekuwa akiongelea hasa swala la wagojwa wa ukimwi na matatizo yanayo wakuta wagonjwa hao nchini China.
Hata hivyo shirika la kuteteta haki za binadamu na mataifa ya magharibi yameiomba serikali ya Chnia kumwachia huru, bwana Hi Jia, kwani wanakiuka haki zabinadamu na haki za kila mtu kueleza au kutoa maoni yake.
Pichani hapo juu ni picha ya bwana Hu Jia kabala yakukamatwa kwake. Na picha nyingine anaonekana bwana Hu Jia alipo kuwa amewekwa kifungo cha ndani siku za nyuma
Imani za dini inapogongana na sheria alizo weka binadamu nani mkweli?
New-York, Umoja wa mataifa - Katibu mkuu wa umoja wa mataifa bwana Ba Ki- moo, siku ya ijumaa ya 28/3/ 2008, ameonya na kulani kitendo cha mmoja wa wabunge na kiongozi wa chama cha siasa bwana Geert Wilders kwa kitendo chake chakutaka kuonyesha picha za sinema ambazo zinahusisha Uislam.
Bwana, Ban Kim-moo, alisema yakuwa hali hii inahatarisha na inaleta mgongano wa kiimani katika jamiii. Na alieleza ya kuwa anafahamu ni kwa jinsi gani, serikali ya Holland ,inavyo jitahidi kuzuia sinema hii isionyeshwe.
Katibu mkuu huyu alisema hakuna sheria ambayo inayo ruhusu mtu kueleza maoni yake ambayo yanaweza leta maafa katika jamii, na hivyo lazima tuwe wangalifu na sheria hizi.
Bwana Geert Wilders, ametengeneza picha ya sinema ijulikanayo kama FITNA, ambayo imeleta mzozo mkubwa katika jamii ya wananchi wa Holland na Jamii ya waumini wa dini ya Kiislaam duniani.
Pichani hapo juu wanaonekana baadhi ya wananchi wakianadamana kupinga kuonyeshwa picha ya sinema ijulikanayo kama FITNA.
Picha ya pili anaonakana katibu mkuu wa umoja wa mataifa bwana Ban Ki moo, akiongea na wandishi wa habari hivi karibuni.
Picha ya tatu , ni picha ya bwana Geert Wilders, ambaye picha yake ya sinema ijulikanayo kama FITNA inagonganisha vichwa vaya watu.

No comments: