Tuesday, April 9, 2013

Uhuru Kenyatta aapishwa kuwa rais Kenya


Uhuru Kenyatta aapishwa kuwa rais Kenya

Nairobi Kenya -  09/04/2013. Uhuru Kenyatta ameapishwa kuwa rais wa nne wa Kenya. Viongozi kutoka mataifa kadhaa ya Afrika wameudhuria kuungana na Wakenya kwenye sherehe za kuapishwa kwa rais  huyo mpya wa Kenya kwenye uwanja wa mpira wa Kasarani.
Kenyatta mwenye umri wa miaka 51 ni mtoto wa rais wa kwanza wa Kenya, Jomo Kenyatta. Ushindi wake wa asilimia 50.07 katika uchaguzi wa tarehe 4 Machi ulihalalishwa na Mahakama ya Juu baada ya pingamizi lililowekwa na Waziri Mkuu anayemaliza muda wake, Raila Odinga, kutupiliwa mbali na mahakama hiyo.

Kenyatta anayekuwa rais wa nne wa taifa hilo la Afrika ya Mashariki tangu lilipopata uhuru wake kutoka Uingereza mwaka 1963, anakuwa rais wa pili barani Afrika kuwa madarakani hali anakabiliwa na mashitaka kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kwa tuhuma za kusaidia kuchochea ghasia za kikabila zilizoukumba uchaguzi wa urais wa Kenya wa mwaka 2007. Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa mwezi Julai, ambapo Kenyatta na naibu wake, William Ruto, wanakabiliwa na mashitaka ya aina moja.

Mtaalamu wa masuala ya Kenya katika Chuo Kikuu cha Warwick, Daniel Branch, amesema "mataifa ya Magharibi yamejikuta kwenye hali ngumu sana, lakini huenda kila nchi ikatafuta njia yake yenyewe na mahusiano na Kenya.
Hata hivyo rais Uhuru Kenyatta amehaidi kushirikiana na yote yanayo husu maswala ya kimataifa atayafuatilia na kuyatekeleza.








2 comments:

Anonymous said...

Τake іn clam the gamеplay that mοrphs іnto social
fundamental intеraсtion a lοt Cаre the Onlinе сommunities of Faceboоk anԁ MуSρаce.
Extraneous of the to ѕurfaces and to рlayers !


My website: game

Anonymous said...

Would it bе oκ if I cite a feω of your агtiсleѕ prοviding
I gіνe сredit аnd ѕources bаck tο blogger.
сom? Μy blog is οn thе exact same fоcus aѕ yοuг site
and mу reаders would definіtelу benеfіt from a lot of the artiсlеs you give here.
Pleaѕe let me know іf thiѕ is
okaу with you.
Rеgаrdѕ

Μу weblog; schering