Mkuu namba 2 wa Al-Qaeda auawa.
Kuuawa huko kwa Nasir al- Wahishi, kunasadikiwa ni pigo la pili kubwa kwa kundi la Al-Qaeda, kufuatia pigo la kwanza la kuuawa kwa kiongozi mkuu wa Al-Qaeda Osama bin Laden mwaka 2011.
Kutokana na kuuawa kwa kiongozi huyo namba mbili wa Al-Qaeda, Qassim al Raim, huenda akachukua kiti cha uongozi wa kundi hilo katika maeneo ya Peninsula.
Rais aliyepinduliwa nchini Misri ahukumiwa kifo.
Kairo, Misri - 16/06/2015. Mahakama kuu nchini Misri, imemuhukumu adhabu ya kifo rais aliye pinduliwa Mohamed Mosri.
Mahakama imemkuta na hatia bwana Musri kwa kuhusika katika makosa ya mauaji na makosa mengine ya ukiukwaji wa haki za binadamu. Pia hukumu kama hiyo ilitolewa kwa wanachama 80 wa chama cha Undugu wa Kislaam (Muslim Brotherhood), japokuwa hawakuwepo mahakamani.
Rais Mohamed Mosri,alipinduliwa kijeshi kutoka madarakani mnamo mwaka 2013 July, na toka hapo amekuwa chini ya ulinzi, nahuku mlolongo wa kesi zikimfuta, kutokana naaliyoyafanya wakati alipo kuwa madarakani.
Urusi kuandaa kuwekeza siraha za kinyukia kiulinzi.
Akiongea katika sherehe za kuazimisha maonyesho ya kijeshi, rais Putin alisema "Mizinga 40 yenye uwezo wa kubeba siraha za nyuklia zitakuwa zimekwisha wekezwa ifikapo mwisho wa mwaka wa 2015."
Matamshi hayo ya rais Putin, yamekuja baada ya Marekani kutamka hivi karibuni, itaongeza ulinzi wa kisiraha katika bara la Ulaya ikiwa nji ya kujihami kutokana na vitisho vinavyo wekwa na Urusi.
No comments:
Post a Comment