Tuesday, January 22, 2013

Baraka Hussein Obama achukua ofisi kwa mara ya pili.

Washington Marekani - 22/01/2013. Wananchi na wakazi wa Marekani kwa mara nyingine tena walikusanyika ili kushuhudia kuapishwa kwa Baraka Hussein Obama kuchukua kiti cha urais kwa mara ya pili baada yab kushinda uchaguzi mkuu uliyofanyika Marekani mwaka jana.
Baraka Hussein Obama mara baada ya kuapishwa kuwa rais wa Marekani kwa mara ya pili alihutubia taifa  na kusema"Safari yetu haijakamilika mpaka hapo mama zetu, wake zetu, mabinti wentu wataka;po kuwa na haki sawa katika jamii na pia haki kwa kila mtu inatimizwa na kulifanya taifa hili la Marekani kuwa taifa lenye kutoa nafasi kwa kila mtu aishiye nadani ya nchi hii."
Kabla ya kuapishwa mbele ya kadamnasi ya Wamarekani rais Baraka Obama aliapishwa katika Ikulu kwani kisheria siku ya kushika ofisi iliangukia siku jumapili na ikabidi aapishwe ili kukamilisha sheria ya nchi.

Wajerumani na Wafaransa wakumbuka siku mkataba wa ushirikiano kwa nchi zao.


Berlin, Ujerumani - 22/01/1213.Wananchi wa Ufaransa na Ujerumani wanasherekea mkataba uliyowekwa na  uliyo wekwa kati ya viongozi wa nchi hiyo miaka 50 iliyopita.
Mkataba huo unao julikana kama mkataba wa Elysee ambapo ulisainiwa kati ya  rais wa Ufaransa Charles de Gaulle na Kansela wa Ujerumani Konrad Adenauer siku ya tarehe 22 Januari 1963.
Wakiongea katika kuadhimisha sherehe hiyo  viongozi wa Ufaransa na  Ujerumani walisisitiza kuendeleza uhusiano huo na kuhakikisha ya kuwa wanajenga msingi imara kwa kizazi kijapo cha nchi hizo.                         

No comments: