Tuesday, January 29, 2013

Iran yafanikwa kutuma nyani mwezini.

Hali ya amani nchini Misri yazidi kuwa tete.

 Ismailia, Misri - 29/01/2013. Waelfu ya wakazi wa mji wa Ismalia  wamekiuka amri ya serikali iliyo wataka kukaa majumbani kwao ili serikali iweze kukabiliana na vurugu zinazo endelea nchi Misri.
Wakazi hao wa mji wa Ismailia na mji wa Suez Kanal walipinga na kuvunja amri hiyo huku wakidai ya kuwa wanacho taka ni haki zao kwani " wamesha tuonea vya kutosha wameua watoto zetu, wake zetu na hali inazidi kuwa mbaya kila kukicha"
Navyo vyama vya upinzani nchini humo vipepinga vikali hatua hizo za serikali za kuweka dharula yakiusalama katika miji hiyo. 
Rais wa Misri Mohammed Musri alitangaza hali ya dharula ya liusalama katika miji yote ambapo vurugu zinaendelea.
Nchi ya Misri imekuwa na wakati mgumu kiamani tangu kufanyaka maandamano ya liyo mtoa rais Husni Mubaraka.

Waethiopia wapigwa sindano za kuzuia kuzaa kwa wingi  chini Izrael.


 Jerusalemu, Izrael - 29/01/2013. Waziri wa afya wa Izrael amekubali ya kuwa serikali ya Izrael imekuwa ikiwachoma sindano za uzazi wa majira wageni wa Kiithiopia ikiwa ni katika harakati za kudhibiti ongezeko la wahamiaji.
 Kukubali huku kwa serikali ya Izrael kumekuja baada ya gazeti la Haaretz kuandika habari hizo kufuatia maelezo na malalamiko yaliyo tolewa na shirika la kufuatilia haki za binadamu likujulikanalo kama Association for Civil Right in Izrael (ACRI) kuitaka sererikali isimamishe mara moja zoezi hilo, kwa kudai ya kuwa wakinamama wanako pigwa sindano hizo hawajui madhara yake hya hapo baadaye.
Sindano hiyo inayo julikana kwa jina la Depo-Provera imekuwa ikitumika kuwadunga wakina mama wa Kiithiopia na wakina mama wanao tumia dawa hiyo huwa wanatakiwa kupiga sindano hiyo kila baada ya miezi mitatu.
Kwa mujibu wa wachunguzi wa kisayansi dawa hiyo aina ya Depo- Provera huwa inaleta madhara ya  kuumwa na kichwa, kupoteza nywele, mzunguko wa kike kutokuwa wa kawaida, kupungukiwa uzito  na ngozi kuwa na madhara.

 Iran yafanikwa kutuma nyani mwezini. 

  Tehran, Iran - 29/01/2013. Wana sayansi wa Iran wamefanikwa kutuma nyani mwezini ikiwa ni moja ya matayarisho ya kutuma binadamu kwenda mwezini ifikipo 2019.
Msemaji wa kisayansi wa Iran alisema " hii ni atuha muhimu katika maendeleo ya kisanyansi nchini Iran na kila tukifanyacho ni kwaa ajili ya matumizi ya Wairan na binadamu wate kwa ujumla na tunashukuru nyani huyo amewasili bila matatizo yoyote."
Kufuatia kitende hicho, baadhi ya mashirika ya kimataifa yametilia wasiwasi kwa kudai ya kuwa ni kitendo kilicho kiuka sheria za kimataifa.
Marekani na washiriki wake wamekuwa wakitilia mashaka kuhusu mpango mzima wa Iran katika maswala ya kinyuklia kwa kudai "Iran inampango wa kutengeneza bomu la nyuklia."

Malkia wa Netherlands kujiudhulu wadhifa wake.

 The Hague, Netherlands - 29/01/2012. Wananchi na wazalendo waishio Netherlands wamepatwa na mishituko  yenye mawazo na maoni tofauti baada ya Malkia Beatrix kutangaza kuachia nyazifa zake za kwa mwanaye Prinsi William-Alexander.
Akiongea kupitia luninga ya taifa huku wananchi, wazalendo na wakazi wanao ishi nchini Netherlands, Malkia Beatrix  ambaye anatimiza miaka 75 siku ya Alkhamisi 31/01/2013 alisema " Nawashukuru kwa kuwa pamoja nami katika kila hali, na leo imefikia wakati wa kuachia kizazi kipya kuiendeleza nchi."
Napenda kuwatangazia ya kuwa tarehe 30/4/2013 mwanangu William-Alexander atachukua kiti cha kifalme.
Netherlands imekuwa na utamaduni wa wafalme kujiudhuru tofauti na nchi nyingine zenye uongozi wa kifalme.







No comments: