Monday, August 20, 2012

Machimbo ya madini yafunguliwa baada ya mauaji.

Uchaguzi wa rais wa Somalia wakwama.

Mogadishu, Somalia - 20/8/2012. Uchaguzi wa kumchagua rais wa Somalia umesimapishwa kwa mdai yakuwa wananchi wa Somalia hawakuwa tayari kwa upigaji wa kura.
Uchagu huo ambao ulikiwa kufanyaka leo 20/08/2012 umeesimamishwa kwa madai ya kuwa kuna baadhi ya matakwa ya uchaguzi lazima  yatekelezwe kwanza.
Serikali ya mpito iliyopo  ambayo iliteuliwa kwa msaada wa nchi za Ulaya Magharibi inamaliza leo mnuda wake rasmi kisheria.
Kufuatia umuzi huo, uongozi wa nchi ya Somalia utasimamiwa na viongozi 225 walioteuliwa kwa baraka za viongozi wakiasili na kuapishwa rasmi leo.
Somalia nchi ambayo tangu mwaka 1991 imekuwa ikikumbwa na mvurugiko wa amani na kusabisha vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Machimbo ya madini yafunguliwa baada ya mauaji. 

Johannesburg, Africa ya Kusini - 20/08/2012. Machimbo ya madini ya platinum yaliyopo nchini Africay Kusini yamefunguliwa baada ya kufungwa kutokana na vurugu kati ya polisi na wafanyakazi jambo ambalo lilipekea watu 44 kuuwa kutokana na kupigwa risasi. 
Kampuni inayosima mchimbo hayo Lonmin ilisema" machimbo ya Marikana yamefunguliwa na theruthi moja ya wafanyakazi 28,000 wa machimbo hayo wamerudi kazini."
Machimbo hayo ambayo yamekuwa katika habari baada ya mauaji yaliyotokea kati ya polisi na wafanyakazi wa machimbo hayo kutupiana risasi. 
Kufuatia mauaji hayo rais Jacob Zuma ameteua kamati maalumu ili kuchunguza chanzo cha muaji hayo ambayo yametokea tangu serikal ya kibagu ya Afrika ya Kusini kung'olewa.


Izrael kutumia ujumbe wa siku kwa kutoa tahadhali.

Jerusalem, Izrael - 20/08/2012. Serikali ya Izrael imekamilisha na kufanikiwa kutuma ujumbe kwa kupitia simu za mkono kuwajulisha wanachi wake ikiwa kama kunashambulizi lolote la kijeshi.
Zoezi hili ambalo lilifanyika kwa mudawa siku tano nakjuisha hivi karibuni limefanyika huku kukiwa kuna hali ya utata ya kati ya Izrael na Iran nchi ambazo zimekuwa zikilumbana kwa vitisho vya kivita jambo ambalo serikali ya Marekani ikiingilia kati ili kuituliza Izrael baada  ya kutilia mashaka ya kuwa huenda serikali ya Izrael kaamua kufanya mashambulizi bila kushauriana na washiriki wake.
Lakhadar Brahim adai kazi ni kubwa juu ya amani ya Syria.

Algies, Algeria - 20/08/2012.  Mkuu mpya ambaye ameteuliwa kusimamia uletwaji wa amani nchi Syria amesisitiza yakuwa kazi kubwa iliyopo ni kuhakikisha amani inarudi nchini  Syria.
Lakhdar Brahimi ambaye ni raia wa Algeria alisema "kwa sasa nchini Syria kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe na inahitaji kazi ya ziada ilikuweza kusimisha vita hivyo kwa jirani anamuua jirani yake na wakati mwingine kaka namuua kaka yake."
Hata hivyo waziri wa mambo wa mambo ya nje wa Syria amekanusha madai ya  Lakhdar Brahim
na kusema "serikali ya Syria ina pambana na magaidi ambao wanasaidiwa na nchi zenye kutaka serekali ya iondoke madarakani na kuweka vibaraka wao ambao watatumikia."
Lakhdar Brahim amechukua nafasi ya Kofi Annani ambaye amejiudhulu katika kazi hiyo ya kusimamia kuleta amani nchini Syria.

Nchi za Amerika ya Kusini zaunga mkono uamizi wa Ekwado kwa Julian Assange.

Quito, Ekuado - 20/08/2012. Mawaziri wa mabo ya nchi za nje wa serikali za Amerika  ya Kusini wameagiza kuanzishwa kwa mazungumzo kati ya serikali ya Ekuado na Uingereza ilikutataua mzozo uliotokea kati ya nchi hizo mbili juu mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks Juliane Asange.
Mawaziri hao kwa pamoja walikubaliana na kuiunga mkono Ekuado kwa uamuzi wake wakumpa hifadhi ya kiutu Julian Assange ambaye anakabiliwa na shutuma za ubakaji nchi Swedeni, jambo ambalo anakusha.
Julian Assange ambaye aliongea kwa mara ya kwanza huku akiwa kasimama katika dirisha la ubalozi wa Ekuado iliyopo jiji London Ungereza ambapo alikimbilia kwa madai upo mpango ukiopo wa kumrudisha nchini Swedeni ni wa kutaka apelekwe nchini Marekani ambapo anadai amefunguliwa mashitaka kwa kutoa habari za kisiri za Marekani katika mtandao wake wa Wikileaks.

No comments: