Wednesday, August 1, 2012

Sweden yaweka ngumu kwenda ubalozi wa Ekuado.
London, Uingereza - 31/07/2012. Serikali ya Sweden imekata ombi la serikali ya Ekuado la kutaka serikali hiyo kuja kumuhoji mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks ambaye yupo ukimbizini kwenye ubalozi wa Ekuado uliopo London.
Julian Assange ambaye ndiye mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks alikimbilia katika ubalozi wa Ekuado baada ya siku zake za rufaa kukaribia kuisha, jambo ambalo linge mfanya arudi jela na huenda angesafirishwa nchi Sweden ili kujibu mashitaka yanayo mkabili ya uubakaji, jambo ambalo Assange analikataa na kulikanusha.
Assange aliamua kuomba ukimbizi ubalozi wa Ekuado uliopo London, baada ya kuhisi ya kuwa kama angerudishwa Sweden, basi angepelekwa nchi Marekani ili kujibu mashitaka ya kuchapisha nyaraka za siri za nchi ya Marekani.

Rais w Syria atakiwa kuachia madaraka.

Tunis - Tunisia - 31/07/2012.Waziri wa ulinzi wa Marekani amemtaka rais wa Syria kuachia madaraka kama anataka kuilinda familia yake.
Leon Panetta alisema " Marekani na jumuiya ya kimataifa hawatavumilia, na inabidi Asad atoke madarakani kwa kuiokoa nchi yake."
"Pia hatutafanya makosa kama tuliyo yafanya nchini Irak, na nia yetu n kuleta amani na uimara wa eneo zima kwa ujumla."
Agizo la waziri Panetta liomekuja wakati akiwa ziarani nchini Tunisia na huku vita kati ya jeshi la serikali la Syria lililo chini ya rais Asad linapambana vikali na jeshi la upinza linalo pata misaada toka nchi za nje.

No comments: