Friday, August 17, 2012

Bingwa wa Marathon 2012Londoon apokelewa kwa shangwe nchini.


Bingwa wa Marathon 2012Londoon apokelewa kwa shangwe nchini.

Kampala, Uganda - 16/08/2012. Mwanariadha aliyeshinda mbio za Marathon za michezo ya Olympics London alikalibishwa kwa shangwe na kupewa heshima ya kupata kuonana rais Yoweri Museven.
Stephen Kiprotich aliyeshinda medali ya dhahabu katika mashindo ya michezo Olympics iliyofanyika London, alikaribishwa na rais Yoweri Museven katika chakula ambacho aliandaa kwa ajili ya mwanariadha huyo kwenye Ikulu ya rais ya Entebe.
Rais Yoweri Museven akimkaribisha Kiprotich, alisema' "ningependa kumpongeza kwa ushindi huu, na wale wote ambao wamehusika katika kumsaidia Stephen Kiprotich kuiletea ushindi Uganda."
Stephen Kiprotich  alipewa $800,000 na rais Museven na ameiwezesha Uganda kupata medali ya dhahabu baada ya miaka 40 ambapo marehemu Akii-Bua aliipatia Uganda medali ya dhahabu katika mchezo wa mbio za kuruka viunzi 400 meta.

1 comment:

Anonymous said...

I'm truly enjoying the design and layout of your site. It's
a very easy on the eyes which makes it much more pleasant for me to come here and visit
more often. Did you hire out a designer to create your theme?

Superb work!
my site :: funnymariogames