Tuesday, August 21, 2012

Waziri mkuu wa Ethiopia aaga dunia.

Waziri mkuu wa Ethiopia aaga dunia.

Addis Ababa, Ethiopia - 21/08/2012. Wananchi wa Ethiopia wameaanza maombelezi baada  ya waziri mkuu wa nchi hiyo Meles Zanawi kufariki nchini Belgium kwa matibabu.
Msemaji wa serikali   Simon Bereket  akiongea baada ya habari za kifo cha Meles Zanawi alisema " makamu wa waziri mkuu Hailemariam Desalegn ataogoza hadi hapo uchaguzi mwingne mwaka  2015."
Waziri mkuu Meles Zanawi  alifariki dunia alipokuwa katika matibabu nchini Belgium na alichukua madaraka ya uongozi baada mapinduzi yaliyopelekea kuangushwa kwa Haile Mariam mwaka 1991.

 Sergie Lavrov aonya mashambulizi zidi ya serikali ya Syria.

Moscow, Urussi - 21/08/2012. Urussi imeonya na kusema kitendo chochote cha kufanya mashambulizi nchini Syria hakitakubalika.
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Urussi Sergie Lavrov aalionya kwa kusema " haitakiwi kuingilia maswala ya ndani ya nchi huru yoyote ikiwemo Syria, na nikinyume na sheria za kimatafa na nimekuwa nasisitiza hilo kila wakati na naonya ya kuwa kitendo chochote cha kuishambuli Syria kitaleta maafa katika jamii nzima ya maeneo hayo."
Waziri Sergie Lavrov aliyasema hayo baada ya kauli ya rais Baraka Obama kudai kuwa upo uwezekano wa nguvu za kijeshi kutumika ikiwa serikali ya Syiria itatumia siraha za sumu zidi ya wapinzani wanaopigana vita na serikali ya rais Bashar al Assad.

Waliotenda makosa ya jinai kunyongwa hivi karibuni asema rais wa Gambia.

Banjul, Gambia - 21/08/2012. Rais wa Gambia ametangaza kuwa watu wote waliukumiwa kunyonwa nchini humu watapata adhabu hiyo ufika mwezi wa Septemba.
Rais Yahya Jammen akiongea katika siku kuu ya kuadhimisha mwisho wa mfungo wa mwezi wa Ramadhani alisema." ningependa kuthibitisha  ya kuwa wale watu waliohukumiwa vifo baada ya kukutwa na makosa kama ya uuaji, ubebajiwa wa madawa ya kulevya, ushoga, na makosa mengine ya jinai basi adhabu zao zitatekelezwa kwa mujibu wa sheria za nchi inavyo eleza.
""Serikali inabidi kuonyesha makali yake kwa wale wote ambao wanakiuka sheria na kuvuruga amani ya nchi  kwa njia moja au nyingine."
Rais Jammen ambaye alichukuwa madaraka mwaka 1994 baada yamapinduzi ya kijeshi na amekuwa akilaumiwa kwa kuongoza nchi kwa vitisho jambo ambalo serikali yake imekuwa ikilikana.

No comments: