Thursday, October 9, 2008

Angola yaitaka Ufaransa kufuta kesi inayo wakabili ya viongozi wake.

Aliyetaka kuzindua kitabu kumuelezea ,Baraka Obama, arudishwa kwao. Nairobi, Kenya-07/10/2008.Raia mmoja wa Amerika, bwana Jarome Corsi, amerudishwa kinguvu nchini Amerika, baada ya kuingia nchini bila kutimiza sheria. Bwana, Corsi, ambaye alikuwa nchini Kenya, kuzindua kitabu chake (The Obama Nation), ambacho kilikuwa na makusudio ya kumuelezea kiundani, kimaisha na maisha ya kisiasa ,mgombea pekee wa kiti cha urais wa Marekani,kwa kupitia cham chama cha Demokratiki, bwana Baraka Obama, alikutwa kwenya hotel na kupelekwa kiwanja cha ndege. Picha hapo juu ni ya bwana Jarome Corsi, akisindikizwa kiwanja cha ndege, tayari kurudi kwao Amerika kabla ya kuzindua kitabu chake( the Obama Nation ). Askofu Mkuu, Ameritus Desmond Tutu,awapa kitendawili wananchi wa Afrika ya Kusini.

Cape Town,Afrika ya Kusini-08/10/2008. Askofu mkuu wa Kanisa la Kianglikana nchi Afrika ya Kusini, Askofu Desmond Tutu, ameseama wananchi wa Afrika ya Kusini, wamekuwa kama isemavyo bibilia, ya kuwa wale waliovuka mto Jordani, na kusahahu ya kuwa mahali walipo sasa, wamefika baada ya kuvuka mto huo wa Jordan.
Askofu, Desmond Tutu ambaye mshindi wa nobeli ya zawadi ya utetezi wa amani duniani ,aliyaongea haya wakati wa kusherehekea miaka 77 ya tangu kuzaliwa kwake,mapema mwanzo mwa wiki hii mjini Cape Town.
Picha hapo juu ni kitabu Kitakatifu ambacho katika moja ya maandiko ya ke matakatifu, wana Israel walivuka mto Jordan, na baadaye walianza kuuliza maswali mengi na kufikia hata kukorofishana.
Picha ya pili anaonekana, Askofu Desmond Tutu, akiongea hivi karibuni. Picha ya chini, wanaonekana baadhi ya wananchi, wakimuunga mkono rais Thabo Mbeki, aliyekuwa rais wa Afrika ya Kusini, ambaye amejiuzuru kutokana ma mgogoro ndani ya chama tawala cha ANC - ( African national Congress )
Matumizi ya makaa ya mawe, kupunguzwa katika jumuia ya Ulaya.
Brusells, Belgium-09/10/2008.Jumuia ya Ulaya imepanga mkakakati wa kupunguza matumizi ya makaa ya mawe na mitambo yote inayo chafua hali yahewa kupunguzwa ifikapo mwaka 2013.
Kwa mujibu, wa msemaji wa jumuia hiyo, upunguzwaji wa matumizi hayo ya makaa ya mawe,kutakuja baada ya makampuni kutakiwa kulipa kwa kila kiasi cha hewa chafu kiwanda kitakacho chafua.
Kufuatia hali hii, viwanda vinavyo tumia makaa ya mawe, vitalipa kiasi cha $ million 56 kwa mwaka, na huenda kukaongeza bei ya umeme.
Picha hapo juu ina onyesha moja ya kiwanda kinacho tumia makaa ya mawe, katika moja ya nchi wanachama wa jumuia ya Ulaya, inaonyesha ni jinsi gani hali ya hewa inavyo anavyo chafuka.
Angola yaitaka Ufaransa, kufuta kesi inayo wakabili ya viongozi wake.
Paris,Ufaransa-07/10/2008.Serikali ya Angola, imeitaka serikali ya Ufaransa, kusimamisha kesi inayo wakabili baadhi ya viongozi wa Angola,kwa kuhusika na rushwa wakati wa ununuzi wa siraha mnomo miaka ya 90.
Kwa kufatia kufunguliwa kwa kesi hiyo,serikali ya Angola, imesema kuendelea kwa kesi hiyo, kutahatarisha ulinzi na usalama wa Angola.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Ufaransa, nchi ambayo kesi imefunguliwa kuwashitaki baadhi ya viongozi walio husika katika ununuzi wa siraha mapema miaka ya 90.
Chini ni bendera ya nchi ya Angola, nchi ambayo viongozi wake wana tuhumiwa kwa rushwa wakati wa kununua siraha.
Mkuu wa jeshi , asema ipo haja ya Taliban kushirikishwa kuleta amani nchini Afghanistan.
London,Uingereza-06/10/2008.Brigedia Mark Carleton-Smith, ambaye ni mkuu jeshi,amesema yakuwa ushindi vita zidi ya kikundi cha Taliban, utakuwa ni mgumu na kuna haja ya kushirikisha kikundi hiki katika kuleta amani nchini Afghanistan.
Alisisitiza ya kuwa, ikiwa Taliban watakuwa tayari kukaa na kuzungumza, basi ipo haja ya wao kushirikishwa kisiasa, na hii ita leta kusimamisha vita nchini humo.
Kwani kuijenga Afghanistan kunahitajika kufanya kazi ya ziada,kisiasa,uchumi na kijeshi pia.
Picha hapo juu ni ya moja ya wapiganaji wakiwa wanapiga doria, katika moja ya miji nchini Afghanistan,ambapo wamekuwa wanapambana na kikundi cha Taliban.
Mlipuko wa bomu watokea karibu na makazi ya Mfalme wa Swaziland.
Mbabane,Swaziland-07/10/2008.Watu wawili walifariki dunia hivi karibuni, baada ya bomu kuripuka karibu na makazi ya mfalme wa Swaziland.
Msemaji wa serikali, alisema ya kuwa watu hao walisadikiwa kufanya uhaini, lakini bomu lililipuka kabla ya matakwa yao kutimia.
Nchini Swaziland, kumekuwa na mvutano wa kisiasa, na kusababisha baadhi ya viongozi wa siasa kuwekwa chini ya ulinzi wa serikali.
Mfalme Muswati III ametawala Swaziland tangu mwaka 1986, chini ya uongozi wake amekuwa akilaumiwa kwa kutofatilia maswala ya nchi hasa ugonjwa wa ukimwi.
Picha hapo juu ni picha ya Mfalme wa Swaziland , Mfalme Mswati III, ambaye bomu lililipuka karibu na makazi yake.

1 comment:

Anonymous said...

very nice! hahahahaha