Monday, October 6, 2008

Chama tawala nchini Afrika ya Kusini kina mvutano" Hali si shwali"

Mkuu wa Polisi ajuuzulu baada ya msukumo wa meya wa jiji.

London, Uingereza-02/10/2008.Mkuu wa jeshi la Polisi nchini Uingereza, amejiuzulu kazi yake,baada ya meya wa jiji la London kumtaka afanya hivyo
Kwa mujibu wa msemaji wa polisi, alisema , bwna Ian Brair, amjiuzulu nafasi hii kwa manufaa ya jeshi la polisi.
Hata hivyo kwa mujibu wa msemaji wa ofisi ya meya wa jiji la London,alisema ya kuwa meya wa jiji hilo hakuwa na imani na mkuu huyo wa polisi, uenda wangeitisha kura ya maoni kuhusu uongozi bwana, Ian Brair.
Kujiuzuru kwa bwana, Ian Brair, kumekuja , baada ya mvutano mkubwa uliotokea kati ya jeshi la polisi na familia ya hayati Charles de Manezes.Ambapo jeeshi la polisi, lilimua kwa kumpiga risasi, hayati Charles de Manezes kwa makosa kwa kumfananisha na mmoja ya watu wanao shukiwa ni magaidi katika kituo kimoja cha treni(Metro) jijini London.
Izrael yatakiwa iyaachie baadhi ya maeneo" Asema Ehud Olmet".
Jerusalemu, Izrael-29/09/1008.Aliyekuwa waziri mkuu wa Izrael, Ehud Olmert, amesema yakuwa ina bidi Izrael ijitoe kwenye maeneo ya Ukingo wa Magharibi, Jerusalemu Mashariki ili kufanikisha mpango wa amani kati ya Izrael na Palestina.
Bwana , Olmert alisistiza kwa kusema, yeye sikiongozi wakwanza kutaha amani iwepo kwenye ukingo huo,basi umefikia wakati wa kusema hali hii kwa jamii na kuwafahaimisha vizuri.
Makomandoo wawakomboa watekwa nyara" Wote wazima"
Kairo, Misri-29/09/2008. Makomandoo wa kutoka serikali ya Sudani na Misri walifanikiwa kuwakomboa mateka waliokuwa wametekwa nyara na kundi la watu wasiojulikana.
Watu waliotekwa nyara walikuwa raia wa Misri 8 , raia wa Ulaya 11.
Kundi hilo lililo wateka nyara, lilikuwa likidai pesa ili watu hao waachiwe huru.
Watu hao waliokuwa ni watalii, walitekwa nyara karibu na mpaka na nchi ya Libya, Sudan na Misri, waliokolewa na wote ni wazima, kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya Misri.
Picha hapo juu ni picha ya watu walio tekwa nyara wakiwasili kwenye uwanja wa ndege wa kijeshi mjini Kairo.
India na Amerika zakubaliana kushirikiana katika nguvu za kinyuklia.
Washington, Amerika- 02/10/2008. Serikali ya India na serikali ya Amerika, zimetiliana makubaliano ya kuwa serikali ya Amerika na India kusaidiana katika kuimarisha nguvu za kinyuklia.
Katika makubaliano hayo, serikali ya India itawajibika kuruhusu, wakaguzi wa umoja wa mataifa kukagua shughuli zote za kinyuklia nchini India, na Amerika itatoa misaada ya kiufundi na maarifa kwa India.
Picha hapo juu wanaonekana,waziri mkuu wa India kushoto,bwana Manmohan Singh,akiwa na rais wa Amerika George Bush,wakati walipokutana mjini Washington.
Wateka nyara watishia kulipua meli" Wadai lazima masharti yao yatimizwe.
Mogadishu, Somalia-02/010/2008.Kikundi kimoja kinacho shikilia meli moja yenye shehena ya mizigo ambayo waliiteka nyara, wamedai yakuwa watailipua meli hiyo ikiwa hawata timiziwa masharti yao, kikundi hicho kinacho julikana kama (Somalia Islamist Militants).
Mmoja wa viongozi hawa alisema" meli hiyo ilikuwa imebeba siraha, zinazo elekea nchini Ethiopia, na kwamba hawataiachia meli hii, kwani siraha hizi zitatumika katika kuwashambulia wao".
Picha hapo juu ni ya meli ambayo imetekwanyara na mmoja ya kundi linalo pigana na serikali ya Somalia.
Chama tawala nchini Afrika ya Kusini kina mvutano,"hali si shwali".
Johannesburg,Afrika ya Kusini-03/10/2008.Viongozi kadhaa wanachama hai wa chama tawala cha ANC- African National Congress, wamesema kuna mgawanyiko ndani ya chama hicho, na hali hii inatishia mshikamano katika chama hicho.
Haya yalielezwa, baada ya aliyekuwa waziri na mwenyekiti wa ANC, Mosiuoa Lekota, kusema ya kuwa haina haja kuwa kimya kwani,kwani viongozi wa juu wa chama hicho cha ANC ni wa kulaumiwa kwa kukiuka misingi, mila na desturi ya chama hicho cha ANC.
Picha hapo juu anaonekana,Mosiuoa Lekota,alipo kuwa akiongea hivi karibuni katika moja ya mkutano.
Chini ni ya picha ya bendera ya chama cha ANC-African National Congress, chama ambacho kinatawala nchi Afrika ya Kusini.
Bolivia na Venezuela, zawekwa katika nchi zinazo pinga kushirika katika vita zidi ya madawa ya kulevya.
Washington, Amerika- 23/09/08. Serikali ya Amerika imetangaza rasmi yas kuwa imeiweka nchi za Bolivia , Burma na Venezuela katika nchi ambazo hazisirikiani na jumuia ya kimataifa kupinga au kuzuia uuzaji wa mada ya kulevya.
Hata hivyo serikali za Bolivia na Venazuela, zimesema hii inakuja kutokana na kutokuelewana kiserikali kati ya Washington na serikali hizi.
Na wakati huo huo, serikali ya Venezuela imeomba msaada wa kusaidiwa kujengewa mitambo ya kinyuklia kwa ajili ya nguvu za umeme na serikali ya Urusi. Hapo juu anaonekana rais wa Venezuela ,Hugo Chavez, akiwa ameshikilia pesa ya Amerika,wakati alipo kuwa akihutubia katika moja ya mikutano nchini Venezuela.
Picha ya pili ni ya bendera ya Amerika , nchi ambayo ina mvutano serikali ya za Venezuela na Bolivia.

No comments: