Thursday, October 30, 2008

Papa John Paul II alijeruhiwa na kisu, asema katibu wake"Ilikuwa siri".

Papa John Paul II alijeruhiwa na kisu, asema katibu wake" Ilikuwa siri".

Vatican,Vatican City - 26/10/08. Aliyekuwa katibu mkuu wa hayati Papa, John Paul II, Kadinali Staninislaw Dziwisz, amesema ya kuwa, hayati Papa John Paul II, alichomwa kisu mwaka 1982, lakini haikutangazwa. Tukio la kuchomwa kisu Papa John Paul II,lili tokea nchini Ureno, wakati wa ziara ya Papa, kutembelea hekalu la Fatima kwa ajili ya kutoa shukurani kwa kupona, baada ya kupigwa risasi na raia wa Uturuki Mehmet Ali Agca.
Katibu huyo, ambaye kwa sasa ni Kadinali wa Krakow nchini Poland, alisema ya kuwa, tukio hilo lilitokea wakati mmoja wa padri kutoka Uispani Juan Fernandez Krohn huku akiwa na kisu alimsogealea,Papa John Paul II,ali kumbusu na kumchoma, lakini walinzi wa Papa, walimuwahi kabla ya kumjeruhi vibaya.
Hata hivyo kisu likimchoma lakini hakikuleta mazara makubwa sana na Papa John Paul aliendelea na ziara yake kama kawaida.
Kadinali, Stanislaw Dziwisz, aliongeza kusema ya kuwa Papa John Paul II, alisema "Itakapo fikia wakati sitaweza sema au kuongea basi muda wangu utakua umefika wa kuondoka"Papa John Paul, aliaga dunia tarehe 2/4/2005.
Cadinali, Stanislaw Dziwsz, amekuwa katibu wa hayati Papa John Paul II kwa kipindi cha miaka 40.
Picha ya hapo juu anaonekan Papa John Paul II, akiwabariki watu wakati wa moja ya ziara zake enzi za uhai wake na chini wanaonekan maelfu ya watu wakiwa wamekuja kuomba Mungu pamoja naye.
Picha ya pili anaonekana Papa John Paul II, akiwa hospitalini kwa matibabu baada ya kupigwa risasi na Mehmet Ali Agca tarehe 13/05/1981, aliruhusiwa kutoka hospitalini baada ya wiki tatu.
Picha ya chini anaonekana hayati Papa John II, akiwa anamwangalia jiwa, anejaribu kutua kwenye mabega yake.
Makubaliano ya kuwa na biashara huru kuingiza mabilioni ya pesa.
Kampala, Uganda - 26/10/08. Viongozi wa bara la Afrika, wametiliana mkataba ili kushirikiana kibiashara hivi karibuni mjini Kampala.
Mkataba huo, ulioshirikisha nchi 26, unatarajiwa kuingiza mapato kwa kiasi cha $US 624 billion kila mwaka.
Mkataba huu ambao umekutanisha jumuiya zote za barala Afrika, ambazo zimekuwa zikijumuisha nchi zilizopo katika bara la Afrika kijografia.
Jumuiya hizo, ni SADC ( Southern Africa Development Community), EAC ( East African Community),COMESA (Common Market for Eastern and Southern Africa)
Picha hapo juu, zinaonekana baadhi ya nchi zitakazo faidika na mkataba huo.
Picha ya chini wanaonekana, viongozi wa nchi za Rwanda, Tanzania Uganda, Burundi na Kenya, ambao nchi zao zitafaniwa kutokana na mkataba huo.
Tofauti za siasa ndani ya Izrael zashindwa kupata atakaye kuwa waziri kuu" Uchaguzi kufanyika mkuu njiani"
Jerusalem,Izrael - 27/10/08. Kiongozi wa chama cha Kadima bi, Tzipi Livni, ambaye alitarajiwa kuwa waziri mkuu wa Izrael, ili kushika uongozi ulioachwa na aliye kuwa waziri mkuu wa Izrael, Ehud Olmert, ambaye alijiuzuru kutokana na kashfa ya kuhusika rushwa, amesema atamwomba rais wa nchi hiyo Shomon Peres kuitisha uchaguzi mapema iwezekanavyo.
Uamuzi hu wa kumwomba, rais, Shomon Peres kuitisha uchaguzi mapema, umekuja baada ya bi, Tzipi Livni, kushindwa kuunda serikali ya mseto.
Hata hivyo wachunguzi wa siasa nchini Izrael, wanasema ya kuwa mpinzani mkubwa wa bi Tzipi Livni, atakuwa aliyewahi kuwa waziri kuu wa Izrael, Benjamin Netanyahu ambaye ni kiongozi wa chama cha Likud.
Picha hapo juu anaonekana, Tzipi Livni , akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.
Mvutano wa imani waleta utata,waumini wa dini tofauti kutoaminiana.
Borepang,India - 23/10/08. Mvutano wa kidini kati ya waumini wa dini ya Hindu na wale waumini ya dini ya Kikristu wamekuwa na wakati mgumu, kufuatia mvutano na ghasia zinazo letwa na waumini mwenye msimamo mkali kutoka pande zote za waumini wa dini hizi"Haya yalisemwa na mmoja wa mchunguzi wa maswala ya dini nchini India.
Kufuatia mvutano huu, kumeleta baadhi ya maeneo ambayo waumuni wa pande wa dini kutoka pande zote wamakuwa wanashindwa kwenda kusikia mahubiri, baada ya baadhi ya maadhi ya mahekalu na makanisa kuchomwa moto au kubomolewa.
Hata hivyo , msemaji wa serikali ya India, amesema yakuwa serikali ya India, inafanya kila jitihada kutatua matatizo haya.
Picha hapo juu,lianaonekana moja ya jengo la kanisa likiwa limeungua vibaya huku picha ya Yesu Kristu ikiwa imebakia imeninginia,baada ya kuchomwa moto na waumini wa dini nyingine ambao wanapinga kuwepo kwa dini ya Kikristu kwenywe eneo hilo.
Picha ya pili ni ya hekalu la waumini wa dini ya Hindu,likiwa lime aribiwa vibaya na moto mara baada ya kuungua na moto, ambao inasadikiwa waumini wa dini wapinzani ndiyo walio choma kanisa hilo.
Kesi ya Thomas Lubanga, bado yagonganisha vichwa vya sheria.
Hague,Uholanzi - 23/10/08. Mahakama ya kimataifa inayo shughulikia makosa ya jinai, ambayo inasikiliza kesi inayo mkabili aliyekuwa askari aliye ongoza vita zidi ya serikali ya Congo, hasa katika sehemu za Ituri bwana, Thomas Lubanga, imesema ya kuwa kuyumba kwa kesi yake kumeleta hali ya utata na kusababisha kusimamishwa kwa kesi hii.
Hata hivyo, Thomas Lubanga, ambaye anashutumiwa kuwatumia vijana wadogo kama askari wakati wa vita, ameamriwa na maakama kubaki kizuizini baada ya mahakama kukataa kuachiwa kwake huru.
Picha hapo juu anaonekana,Thomas Lubanga, akiwa ndani ya mahakama akisililiza kesi yake inayo mkabili.
Colin Powell's, asema atampigia kura, Baraka Obama"Sera za wagombea ndizo zilizo mpa uamuzi huu".
Washington, Amerika - 22/10/08. Aliyekuwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, Colin Powell's, amempitisha mgombea wa urais wa Amerika, Baraka Obama kwa kusema atampigia kura katika uchaguzi wa rais utakaofanyika mapema mwezi wa 11/2008.
Bwana, Baraka Obama, ambaye ndiye mgombea pekee wa urais kwa kupitia chama cha Demokratiki.
Colen Powell's, ambaye ni mwanachama wa chama cha Repablikani, na amefanya kazi na serikali iliyopo ya rais, George Bush kabla ya kujiuzuru.
Akiongea haya, Colin Powell's, alisema ya kuwa msimamo na mwelekeo wa baadhi ya viongozi waliomo ndani ya chama cha Repamblikani, na mwelekeo wa wagombea wote wanao gombea urais nchini Amerika, bwana, Baraka Obama na John MacCain's ndiyo zilizo mfanya achukue uamuzi huo wa kuamua kumpigia kura yake Baraka Obama.
Picha hapo juu, anaonekana, Colin Powell's akiongea kuidhinisha nia yake yakuwa atampigia kura Baraka Obama.
Picha ya pili wanaonekana, Baraka Obama mgombea urais kupitia chama cha Demokratiki kushoto na John MacCain's ambaye ni mgombea urais kupitia chama cha Repablikan kulia, wote wakiwa wanaeleza sera zao wakati walipo wekwa kiti moto mbele ya wananchi wa Amerika ili waweze kuchaguliwa kuiongoza nchi hiyo.

No comments: