Tuesday, October 14, 2008

Syiria kufungua uhusiano wa kiserikali na serikali ya Lebanon.

Nigeria kubadirisha majina ya mitaa,na kuyapa majina mapya."Malcos Garvey jina lake kutumika"

Abuja,Nigeria-10/10/2008. Serikali ya Nigeria, imepanga kuyapa majini mapya baadhi ya mitaa na barabara kubwa nchini humu na majina mengine kubadirishwa.
Akiongea hayo, waziri wa serikali mitaa Aliyu Umar, yakuwa baadhi ya mitaa ilipewa majina kinyume,namatakwa , mila na utamaduni wa nchi.
Msemaji wa serikali, alisema baadhi ya mitaa itapewa majina ya wanamichezo na watu mashuhuri waliochangia kwa njia moja katika kuinua uchumi wa nchi na kutetea haki za binadamu.
Kati ya watu, ambo majina yao yatatumika kama majina ya mitaa, hayati Bob Marley, Fela Anikulapo Kuti, Martin Luther King, Malcom X na Malcus Garvey.
Kwa upande wa michezo majina ya wanasoka, JJ Okacha, Kanu Nwankwo na Mery Onyali, majina yao yatatumika kama majina ya mitaa.
Picha hapo juu , ni mwanamuziki maarufu wa muziki wa raggae, hayati Bob Marley, ambaye muziki wake umekuwa kama mshawasha wahisia za kutete haki za wanyonge duniani duniani.
Picha ya pili, ni ya hayati , Fela Anikulapo Kuti, mwanamiziki ambaye musiki wake, ulikuwa unaelezea kinaga ubaga hali halisi ya maisha ya watu katika kupambana na maisha ya kila siku.
Picha ya tatu, anaone mtetezi wa haki za binadamu na usawa kwa wote nchini Amerika, Martin Luther King,akihutubia mamia mnamo miaka ya sitini.
Picha ya mwisho, anaonekana mwana harakati wa usawa wa binadamu nchini Amerika, Malcom X, akiongea katika moja ya mikutano wakati wa harakati za kutetea haki za binadamu.
Bunge la Uingereza la pinga, "Waziri mkuu asisitiza msimamo wake mpaka ufanikiwe".
London,Uingereza-14/10/2008. Waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brawn, amesema atahakikisha yakuwa siku za kuwekwa kizuizini kwa watu wale wanao shukiwa wanajihusisha na ugaidi nchini Uingereza zina ongezwa hadi kufikia siku 42.
Waziri mkuu, Brawn, alisisitiza hayo mara baada ya matokea ya kura zilizo pigwa katika bunge la Uingereza kukataa mswaada wa kuongeza siku za watu kukaa kizuizini kwa washukiwa wanao jihusisha na ugaidi nchini Uingereza.
Kura za kukubaliana na mswaada ambazo zilikuwa 118 na zile zinazo pinga mswaada huo kuwa 308, hivyo kuweka mswada huo katika wakati mgumu, hasa kwa serikali ya waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brawn.
Picha hapo juu ni ya bunge la Uingereza, ambalo limekataa mswaada wa kuongeza siku toka siku 28 hadi 42, baada ya kura kupigwa.
Picha ya pili anaonekana waziri mkuu wa wa Uingereza Gordon Brawn, akionyesha kwa ishara yakuwa kunahaja ya kufungua macho zaidi na kuona kwa makini nini ugaidi unafanya katika jamii.
Syiria kufungua uhusuiano wa kiserikali na serikali ya Lebanon.
Damascus, Syiria-14/10/2008.Rai wa Syiria, Bashar Al- Assad, ametandaza rasmi yakuwa serikali yake itafungua ofisi za kibalozi nchini Lebanon.
Ufunguzi wa ofisi za ubalozi wa Syiria nchini Lebanon, kumekuja tangu mwaka 1948, wakati Lebanon ilipo pata uhuru kutoka kwa Ufaransa.
Uhusiano wa nchi hizi mbili, umekuja baada ya rais wa Lebanon Michel Sleiman, kutembela Syiria mapema mwezi wa nane mwaka huu.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya Lebanon, amesema ya kuwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Lebanon, Fawzi Salloukh, atafanya ziara ya kiserikali nchini Syiria hivi karibuni.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya Syiria, ofisi za kibalozi kati ya nchi hizi mbili funguliwa kabla ya mwisho wa mwaka.
Picha hapo juu wanaonekana, marais wa Lenbanon Michel Sleiman na rais Bashar Al Asaad wakieleka kwenya kukagua gwaride la heshima wakati rais wa Lebano alipo tembelea Syiria.
Picha ya chini wanaonekana rais Bashar Al Saad wa Syiria na rais wa Lebanon Michel Sleiman wakikagua gwaride la heshima wakati wa ziara ya kiserikali ya rais wa Lebanon mapema mwezi wa nane mwaka huu.
Fedha zilizo tolewa na serikali ya Jumuia ya Ulaya na Amerika zainua hali ya masoko.
Brussel, Belgium-14/10/2008. Masoko ya hisa karibu kote duniani yame anza kurudi katika hali yake ya kawaida, baada ya serika ri za jumuia hii ya Ulaya kutoa pesa ili kuzisaidia benki, ambazo zimepata mtikiso kutokana na mporomoko wa biashara wa kifedha.
Na wakati huo huo, rais wa Amerika George Bush, amatangaza rasmi yakuwa serikali itatoa pesa zipatazo dola billion 250,ili kuinua masoko ya nchi hiyo.
Mtikisiko na mporomoko wa hisa ulitokea siku za nyuma, baada baadhi ya mabenki makubwa kushindwa kuhimiri mzunguko wa hisa hizo katika masoko ya dunia kwa kuanzia jijini Tokyo hadi New York.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Amerika nchi ambayo kuporomoka kwa soko la hisa, kulisababisha tikisiko na mporormoko wa masoko duniani kote.
Picha ya pili ni ya bendera ya jumuia ya Ulaya, jumuia ambayo imekuwa ya kwanza kutoa fedha ili kuchangia fedha kusaidia kuinia mabenki na soko la hisa katika jumuia hiyo, na matokeo yake kusaidia kuimasoko kurudi katika hali yake yakawaida.
Mgogoro wa ardhi mpakani huenda ukaleta mvutano mkubwa.
San Pedro,Paraguai-14/10/2008.Uchaguzi uliofanyika mwezi wa april nchini Paraguai umekuwa ni kinyume na matarajio ya wakulima hao.
Kwa mujibu wa msemaji wa wakulima hao,alisema' yakuwa maeneo yao ya asili yamekuwa yakikaliwa na wanchi wakulima kutoka nchi ya Brazil.
Mvutano huo wa kugombea ardhi kati ya wananchi wa nchi hizi mbili, umekuwa ukijadiliwa na viongozi wa serikali zote mbili kwa kipindi kirefu, na mpaka sasa bado mvutano huo haujapatiwa uvumbuzi".
Mgogoro huu wa kugombea ardhi,katika maeneo yanayo pakana nchi hizi mbili, umekuwa ni mkubwa na sasa ni sisi wananchi tunazidi nyanyaswa.
Msemaji huyo alisema kuchaguliwa kwa rais, Fernando Lugo, kulikuwa ndiyo matumaini yao, lakini matumaini haya yamekuwa ni ndoto.
Picha hapo juu ni baadhi ya wakulima wakiwa wameweka kambi karibu na barabara ili kuonyesha kutorizika kwao na serikali ya rais Fernando Lugo kwa kuto timiza haadi yake.

No comments: