Thursday, October 23, 2008

Matunda ya uongozi bora wa nchi ya mpa nishani ya heshima"Rais wa zamani wa Botswana."

Matunda ya uongozi bora wa nchi ya mpa nishani ya heshima''Rais wa zamani wa Botswana."

Gaberone, Botswana-23/10/08. Rais wa zamani wa Botswana, Festus Mogae, ametunukiwa nishani ya kuwa kiongozi aliye tumikia taifa lake vizuri hasa kwa kupiga vita ugonjwa wa ukimwi wakati wa utawala wake.
Nishani hii iliyo anzishwa na mfanya biashara maarufu wa Afrika Mo Ibrahim, kwa madhumuni kuwafanya viongozi wa nchi za Afrika kufanya kazi vizuri na kwa uadililifu wanapo kuwa madarakani.
Nishani hiiyo itaambatana na donge nono la fedha zipatazo US$ Million 5, ambazo atazipa kwa kipindi cha miaka kumi.
Hapo juu anaonekana, Mo Ibrahim, akipiga makofi kumshangilia rais wa zamani wa Botswana, Festus Mogae, wakati wa kutinikiwa nishani
Picha pili, anaonekana rais, Festus Mogae, ambaye wakati wa uongozi wake nchini Botswana, serikali yake ilijitahidi kupapambana na ugonjwa wa ukimwi.
Umwagaji wa madawa yenye sumu yaleta madhara nchini Ivory Coast.
Abidja, Ivory Coast- 23/10/08. Watu wawili wafanyakazi ya kampuni ya Tommy, wamehukumiwa kwenda jela kwa kosa la kuruhusu madawa ya sumu kumwagwa maeneo ya wazi nchini Ivory Coast.
Akiongea mara baada ya hukumu hiyo, wakili wa serikali, alisema ya kuwa alikuwa ameomba washitakiwa wahukumiwe vifungo vya maisha, lakini mahama imewahukumu watuhumiwa jumla ya miaka 25 jela.
Watuhumiwa hao bwana, Salomon Ugborugbo, ambaye alikuwa mkurugenzi wa kampuni wa kampuni ya Tommy, amehukumiwa kwenda jela miaka 20 na bwana Desire Kouao amehukumiwa miaka 5 jela.
Picha hapo juu wanaonekana wachunguzi wa mazingira wakiangalia kwa makini ni kiasi gani sumu imeathiri mazingira.
Picha yapili wanaonekana wataalamu wa kusafisha mazingira, wakimwagia dawa kusafisha na sumu iliyo mwagwa sumu ambayo imeleta mazara kwa jamii na mimea.
Picha ya tatu anaonekana mwanamke mmoja , ambaye inasemekana aliathirika kutokana na kumwagwa kwa sumu karibu na maeneo aliyokuwa akiishi.
Meya wa mji ajiunga na taliban.
Herat, Afghanistan-18/10/08. Aliyekuwa meya wa mji wa Herat, Ghullamu Yahya Akbari, amejiunga tena na kundi la Taliban.
Ghullamu Yahya Akbari, ambaye ni mmoja wa viongozi na wapiganaji wa Taliban, ambaye alikuwa mstari wa mbele kupigana na wanajeshi wa Shirikisho la jumuia za nchi za Urusi ya zamani, alisema ya kuwa atarudi katika mazungumzo ikiwa majeshi ya kigeni yatatoka ndani ya nchi yake.
Picha hapo juu kushoto, anaonekana akiwa amezungukwa na wapiganaji wake.
Waingereza wawili wahukumiwa jela kwa kukiuka sheria za nchi.
Dubai,Jumuia ya Nchi za Kiarabu- 16/10/08. Raia wawili wa Uingereza, wameukumiwa kifungo cha miezi mitatu na kulipa faini yaUs $ 272 kwa kila mmoja wao baada ya kukutwa wakifanya mapenzi kwenye maeneo ya wazi.
Raia hao majina yao yamehifaziwa, walifunguliwa kesi, kwa kosa la kuvunja sheria ya kufanya mapenzi nje ya ndoa na kulewa hadharani.
Akizungumza hukumu hiyo, hakimu Hamdi Mustafa Abu el Khair, alisema ya kuwa watuhumiwa hao wakimaliza hukumu yao, wanatakiwa warudishwe nchini kwao Uingereza.
Hata hivyo, raia hao wa Uingereza, walikanusha mashitaka yao na walitolewa nje kwa dhamana.
Uingereza kupanga mkakati mpya wa kulinda usalama wa nchi.
London,Uingereza-18/10/08. Serikali ya Uingereza inafikiria kuanzisha muundo mpya wa kuwa na mtambo ambao utajumuisha mawasiliano ya kutumia simu na mtandao ili kudhibiti ualifu na ugaidi.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana katika ofisi ya mambo ya ndani ya Uingereza iliyo chini ya Jacqui Smith, zilisema hii itawasaidia polisi katika kazi zao.
Hata hivyo, wazo la serikali kuwa na mitambo hiyo, ilipingwa na Lord Carle, kwa kusema yakuwa serikali isiruhusiwe kuwa na stoo ya kulundikia habari za watu.
Picha ya hapo juu ni ya serikali ya Uingereza, nchi ambayo inafikilia mbinu mpya ya kupambana na ualifu na ugaidi.
Jumuia ya Ulaya yazidi kukuna kichwa na hali halisi ya Bulgaria.
Sofia,Bulgaria-19/10/08. Jumuia ya Ulaya imeitaka serikali ya Bulgalia, kufanya jitihada ili kukomesha uraji rushwa, ambao matokeo yake huwa inaatarisha hali ya usalama kwa wana siasa na wafanya biashara.
Kwa mujibu wa wa jumuia ya Ulaya,Bulgaria ni moja ya nchi katika jumuia ya Ulaya, ambayo uraji wa rushwa umefika kiwango cha hali ya juu,na kuifanya jumuia hiyo kukuna kichwa kila wakati kwa kuangalia ni jinsi gani watakomesha ulaji huu wa rushwa ambao umeota mizizi kwa muda mrefu.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya walinzi,wakiwa nje ya jengo moja ,kulinda hali ya usalama kwa viongozi na wafanya biashara,walipo kutana hivi karibuni.

No comments: