Wakaribbean waomba rais mteule wa Amerika, Baraka Obama, kuondoa vikwazo kwa serikali ya Kuba.
Saint John's,Barbuda - 09/12/08.Jumua ya nchi za Karibbien, zimemwomba rais mchaguliwa wa Amerika, Baraka Obama, kuondoa vikwazo vilivyo wekwa kwa serikali ya Kuba.
Akiongea hayo, waziri mkuu wa Antigua na Barbuda, W Baldwin Spencer,ambaye ni mwenyekiti wa jumuia ya nchi za Karibbien, amesema hayo wakati wa mkutana wa viongozi wa nchi hizo ulio fanyika Santiago de Kuba.
Hata hivyo , rais mteule wa Amerika, Baraka Obama, alisema yakuwa serikali yake itapunguza baadhi ya vikwazo kwa wananchi wa Kuba,lakini vikwazo vitabakia mpaka hapo serikali ya Kuba itakapo badilisha msingi wake wa kisiasa.
Picha hapo juu, anaonekana rais mtuele wa Amerika, Baraka Obama, akisikiliza kwa makini wakati alipo udhulia moja ya mikutano ya kampeni ya kugombania urais wa Amerika,na aliahaidi mabadiliko makubwa katika serikali yake ikiwa atachaguliwa kuwa rais wa Amerika na kukuza ushirikiano na jumuia ya kimataifa ili kurudisha hazi ya Amerika na wanachi wake.
Mamia ya waumini wa dini ya Kiislaam, wamaliza kutimiza moja ya nguzo za dini.
Mecca,Saudi Arabia - 09/12/08.Maelfu ya waumini wa dini Kiislaamu,wametiza wajibu na nguzo za dini ya Kiislaamu, baada ya kukamilisha hija kwa kufuata njia zote alizo fanya Mtume Muhammad ( S . A . W).
Kwenda Hija, ni muhimu kwa kila Muislaamu, endapo atajaliwa kufanya Hija wakati uzima wake, alisema, mmoja ya Mahujaji.
Picha hapo, juu wanaonekana baadhi ya waumuni wa dini ya Kiislaamu wakiwa wamepumzika karibu na mlima Arafat.
Picha ya pili wanaoneka, baba na mtoto wake wa wakitupa mawe, ikiwa ni ishara ya kumpiga shetani na mambo yake yote.
Picha ya tatu,wanaonekana mamia ya waumini, wakizunguka mnara wa Kabba, ambao nu moja ya jiwe ambalo limebakiwa ambalo lilijengwa na Mtume Abraham( Ibrahim), na nimuhimu kwa kila Muislaamu akijaliwa kulitenda na kutimiza katika uzima wake.
Pakistan yaweka ngumu kuwapeleka raia wake nchini India.
Islamabad,Pakistan - 08/12/08. Serikali ya Pakistan, imesema ya kuwa haita wapeleka washukiwa wa maafa ya ulipuaji wa mabomu na kusababisha mauaji ya watu 172 na zaidi ya 300, walijeruhiwa.
Serikali ya Pakistan,imesema yakuwa imeamua hivyo ,baada ya kupatikana habari yakuwa serikali ya India,ilikuwa nampango wa kubomu baazi ya maeneo yalipo ndani ya Pakistan, ambapo inasadikiwa ni makazi ya kundi la kigaidi la Lashkae -e-Taiba, ambalo linasadikiwa kuhusika na mlipuko ulio tokea hivi karibuni nchini India.
Hata hivyo, waziri wa mambo ya nje wa Pakistan, Shah Mehmood Qureshi,amesema ya kuwa hawakufanya hivyo,kwa vitisho bali wapo kwa ajili ya kuleta amani kati ya nchi hizi mbili siyo kuleta vita.
India na Pakistan, zote zina nguvu za kijeshi zenye uwezo wa kinyuklia na zimekuwa zikitazamwa kwa karibu na jumuia ya kimataifa na kuagiza lazima zishirikiane katika kupiga vita ugaidi waaina yoyote..
Jumuia ya Ulaya yakubali kuwapa hifazi wakimbizi wa Irak.
Brussels, Belgium - 2/12/08.Jumuia ya Ulaya, imekubaliana kwa pamoja kuwapokea na kuwapa hifazi wakimbizi, 10,000 kutoka nchini Irak, waliopo kwenya makambi ya kikimbizi nchini Syria na Jordan.
Uamuzi huo umekuja baada ya kikao cha mawaziri wa mambo ya ndani ya jumuia hii, walipo kutana mapema tarehe, 28/11, mjini Brussel.
Uamuzi huu umekuja , baada ya shirika la kuudumia wakimbizi la umoja wa mataifa ,kuziomba nchi wanachama wa jumia hiyo kuwapa hifazi wakimbizi hao wa kutoka Irak
Hata hivyo, nchi kama Greesi na Cyprus, zilipinga makubaliano hayo kwa kudai, zina wakimbizi wengi katika nchi zao.
Picha hapo juu, anaonekana nyota ya Holly Wood, mcheza sinema na balozi wa kujitolea wa unoja wa mataifa, bi, Angelina Jolie, akiangalia kwa uchungu, jinsi gani, mama mmoja wa Kiirak, akingojea kupewa posho, wakati balozo huyo alipokwenda kuwatembelea wakimbizi hao mwaka, 2007.
Picha ya pili , ni moja ya makazi ya wakimbizi,mbele ya anaonekan binti, mdogo akiwa amembeba mtoto,hatima yake mtoto huyu na dada yake watapa mahali pazuri na kuweza kwenda shule kama watoto wengine.
Kutovaa kitamba cha kichwa sio kukiuka haki za binadamu"Mahakama ya sema".
Brussels, Ubeligiji - 6/12/08. Mahakama ya haki za binadamu ya jumuia ya Ulaya - European Court of Human Rights (ECHR), imesema kufukuzwa kwa wanafunzi wa kike wawili waliokataa kufua vitambaa vya kichwa, halikuwa tendo la kukiuka haki za binadamu.
Kesi ya wasichana hao, iliyo wakilishwa na jumuia za kutetea haki za binadamu kutokea nchini Uturuki, ambao walifukuzwa shule nchini Ufaransa,baada ya kukataa kuvua vitambaa hivyo vya kichwa wakati wa kipindi cha kufanya mazoezi ya viungo.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wasichana wakiwa wamevalia vitamba vya kichwa ikiwa ndiyo moja ya mtindo wa mavazi ya wakaazi wengi wanaotokea katika jamii ya nchi jumuia za kiarabu na baadhi ya maeneo duniani kote, ikiwa ni ishara ya kutunza heshima ya mwanamke mbele ya jamii.
Picha ya pili, ananonekana mwana mama, akiwa amevalia kitamba kichwani na kufunika uso wake, lakini mavazi kama haya yamekuwa vigumu, kukubalika katika jumuia za nchi za Ulaya na baadhi ya maeneo mengina duniani.
No comments:
Post a Comment