Saturday, April 5, 2014

Rwanda yatimiza miaka 20 tangu mauaji ya kimbari.

Rwanda yatimiza miaka 20 tangu mauaji ya kimbari.


Rwanda chini ya Uongozi wa rais Paul Kagame imekuwa na amani na maendeleo.

Kigali Rwanda - 05/04/2014. Wananchi wa Rwanda wameadhimisha miaka ishirini tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari ambapo zaidi ya watu 800,000 waliuwawa kutokana na chuki za kijamii zilizo zilizo sambazwa na kukuzwa katika jamii nzima ya Wanyarwanda.

Mauahi hayo yalitokea wakati watu wa jamiii ya Kihutu walipowauwaa watu wa jamiii ya Kitutsi jambo ambalo lilifanya dunia nzima kushikwa na butwaa kwa kuto kuamini na huku maelfu ya Wanyarwanda wakikimbia nchi yao katika kipindi chote cha mauaji hayo.

Akiongea katika kuadhimisha miaka 20 tangu kutokea mauaji haya, rais wa Rwanda Paul Kagame amesema " jumuiya ya kimataifa na hasa Ufaransa zinatakiwa kulaumiwa kwa kuachia mauaji hayo kutokea."

Serikali ya rais Kagame imekuwa imara katika kuhakikisha kuwa historia hii haitarudia tena nchi Rwanda kwa kupitisha sheria kali ambazo zinazuia chuki katika jamii ya Wanyarwanda. na vile vile serikali ya Rwanda imehakikisha kuwa huduma za elimu. afya na nyingine muhimu zinapatikana kwa kila mtu aishiye katika nchi hiyo.

Mauaji ya Rwanda yalitokea mwaka 1994 na kuwa ya kihistoria katika bara la Afrika kwa jamiii moja ya wwtu kutaka kuifuta jamii nyingine ya watu kwa kuwauwa kwa sababu za chuki za kihistoria.

Askofu mkuu wa Anglikani atahadhalisha kuhusu ushoga.

London, Uingereza - 05/04/2014. Askofu mkuu wa kanisa la Anglika ameonya kuwa  ikiwa kanisa hilo litaruhusu ndoa za mashoga huenda likawa na wakati mgumu na idadi kubwa  waumini wake.

Askofu Justin Welby alisema " Kwa kiasi kikubwa waumini wa kanisa la Anglikani wapo katika bara la Afrika  na wakristu  ambao wamekuwa wakidhurika ni wale ambao wanaunga mkono maswala ya kishoga."

" Na hii inaweza kutokea ikiwa kanisa litapitisha sheria ya kuruhusu mashoga."

Akiongezea Askofu Welby amesema kuwa  wakuu wa kanisa hilo  nchi Sudani ya Kusini wamemwomba kutokubadirisha misingi ya kanisa, kwani "kiwa itatokea kubadirishwa basi waumini wa Sudani ya Kusini hawata kuwa na ushirikiano na kanisa la England."

Askofu Justin Welby aliyasema haya baada ya kumaliza ziara yake kutembelea bara la Afrika ili kujione nini kinatakiwa kifanyike ili kukuza imani ya waumini wa kanisa la Anglikani katika bara hilo.

No comments: