Obama alaani mauaji ya Polisi.
New York, Marekani - 21/12/2014. Rais wa Marekani Barack Obama amelaani mauaji ya polisi wawili katika jiji la New York, ambao walikuwa wakishika doria ndani ya gari lao.
Kamishna wa polisi wa New York Bill Bratton,
amesema "Ismaaiyl Brinsley, mwenye umri wa miaka 28, aliwapiga risasi kichwani
polisi hao bila kuwepo onyo lolote. Na kabla ya hapo Brinsley ambaye anaasili ya
kiafrika, alimpiga risasi mchumba wake wazami kabla ya kuwauwa polisi hayo wa mji wa Brookyl."
Mauaji ya polisi hao wawili, yametoke, wiki chache baada ya maandamano ya watu wenye hasira, kupinga
vitendo vya polisi kuhusika na matukio ya polisi kuwauwa watu weusi ambao
hawakuwa na silaha.
Ismail Brinsley alijiua mwenyewe kwa risasi baada
ya kukimbilia kwenye kituo cha treni zinazopita chini ya ardhi.
Polisi imesema alikuwa ameweka ujumbe kwenye
mtandao wa wake kuwa alipanga kuwauwa "nguruwe" wawili kama hatua ya
kulipiza kisasi kifo cha Eric Garner, Mmarekani mweusi aliyeuawa kwa kukabwa
koo na polisi.
Rais wa Misri amfuta kazi Mkuu wa ujasusi
Kairo Misri - 21/12/2014. Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi leo amemfukuza kazi mkuu wa upelelezi Jenerali Mohamed Farid el- Tohamy aliyeteuliwa siku chache tu baada ya kuondolewa madarakani rais wa zamani Mohamed Mursi mwezi Julai mwaka jana.Jenerali Khaled Mahmoud Fuad Fawzy ambaye alikuwa msaidizi wa Farid el Tohany ndiye aliyeteuliwa kuchukua nafasi yake.
Hata hivyo hakuna sababu zozote zilizo elezwa za kufukuzwa kazi kwa Jenera Farid el
Tohan.
Wakati huo huo, Misri leo imekifungua mpaka wa Rafah, ambao utawawezesha wakazi wa Ukanda wa Gaza, kwa mara ya kwanza katika kipindi cha karibu miwezi miwili kuweza kuingia na kutoka Misri.
Misri ilifunga mpaka wa kuingia Gaza, Oktoba 25 baada ya wanamgambo wenye itikadi kali za Kiislamu katika eneo la Sinai kuwauwa wanajeshi wake 33.
Marekani ,Washington -21/12/2014 Rais wa Marekani Mabaka Obama, amesema kuwa
Marekani inachunguza ili kuweza kujua kama Korea ya Kaskazini inahusika na
ushambuliaji wa mtandao wa Sony, na kama ikigundulika ilihusika, basi hatua za
kisheria zitachukuliwa.
Obama alisema, "tunalianagalia hili suala la kushambuliwa kwa Kampuni ya Sony kwa
makini, nakuwa kila sheria ya kukabiliana na jambo hili zipo tiyari.
"Kwani hatufanyi maamuzi kwa kupitia vyombo vya habari, bali ukweli utakapo patikana basi sheria zitafuata."
"Kwani hatufanyi maamuzi kwa kupitia vyombo vya habari, bali ukweli utakapo patikana basi sheria zitafuata."
Mazungumzo hayo ya rais Obama yamekuja baada ya Korea ya Kaskazini kukanusha kuhusika na mashambulizi ya kimtandao kwa kampuni ya Sony, na kuitaka Marekani kuonyesha ushirikino ili kulitafutia ukweli suala la uvamiaji wa mtandao wa kampuni ya Sony.
Muhammad Ali alazwa hospitalini.
Kentaki, Marekani - 21/12/2014. Aliyekuwa bingwa ndondi kwa uzito wa juu duniani Muhammad Ali mwenye miaka 72, amelazwa katika hospitali ya mji wa Loiseville ili kutibiwa homa ya mapafu.
Bob Gunnell, ambaye ni msemaji wa Ali, alisema " Ali anatibiwa na kundi la madaktari wake na yuko anaendelea vyema.
Mohammed Ali, ameshakuwa hospitali kwa siku moja na anatarajiwa kuruhusuhusiwa kutoka hopitalini baada ya Madaktari kulidhika na mwenendo wa afya yake .
No comments:
Post a Comment