Saturday, December 20, 2014

Liberia yasifiwa na Ban Ki-moon zidi vita vya Ebola.


Nchi za Africa zatakiwa kushirikiana na mahakama ya ICC.



Mahakama kimataifa inayo shugulikia makosa ya jina (ICC)  imeanza mkutano wake wa siku tatu, jiji New York,Marekani,  ambapo umeghubikwa na mfukuto wa kwanini mahakama hiyo imekuwa ikiiandama bara la Afrika tangu kuanzishwa kwa mahakama hiyo mwaka 2002.

Akiongea katika ufunguzi huo rais mpya wa Baraza la mataifa wanachama wa ICC, Sidiki Kaba, ambaye ni Waziri wa sheria wa Senegal,Alisema " Naomba kuwepo na ushirikiano barani  Afrika, ili kubadili mawazo potofu yanayo haribu mahakama hiyo ya ICC.

"Nana penda  kusisitiza kwamba malalamiko ya nchi wanachama  yanapaswa kusikilizwa, na kutafutiwa ufumbuzi." Aliongeza Kaba.


Mkutano huo ambao unajumuisha nchi wanachama 122, Pia uliudhuliwa na wajumbe kutoka Palestina ambapo walikubaliwa rasmi kuwa waangalizi katika mkutano.

 Na kwa mujibu wa Mahakamaya ICC  uamuzi huo wa kuruhusu kuwepo kwa Wapalestina ni hatua moja muhimu ambayo inafungua njia kwa Wapalestina  kujiunga kama mwanachama kamili wa mahaka hiyo ya uhalifu ya kimataifa.



Liberia yasifiwa na Ban Ki-moon zidi vita vya Ebola.


Serikali ya Liberia, imepongezwa kwa juhudi zake katika kupambana na ugonjwa wa Ebola, Pongezi hizo zilitolewa na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban KI-moon, ambaye yupo nchini humo ili kuona ni hatua gani zimefikiwa katika kupambana ugonjwa wa Ebola.


Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Ban Ki-moon kutembelea Liberia, tangu ugonjwa wa Ebola ulipozuka ambao hadi sasa umeshaua watu zaidi ya 7000 katika eneo zima la Afrika ya Magharibi.

Mkuu wa masuala ya kigeni wa Umoja wa Ulaya kuiuzuru Irak. 

Mkuu wa  kitengo kinacho  shughuli masuala ya  kigeni ya Umoja wa Ulaya  Federica Mogherini anatazamiwa kuizuru  Iraq  wiki ijayo  kwaajili ya kufanya  mazungumzo na  viongozi wa serikali na pia kukutana na viongozi wa  serikali ya Kikurdi.

Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema  kuwa Mogherini  atakutana na kufanya mazungumzo na Waziri mkuu Haider Al-Abadi,  na baadaye  siku ya Jumanne atakuwa na mazungumzo na rais wa jimbo la Kurdi, Masoud Barzani katika mji wa Irbil.

Ziara hiyo za Mogherini itakuwa na madhumuni ya kuona ni kwa jinsi gani  Umoja wa Ulaya, utasaidia katika kupambana na kundi na dola la Kiislaam ,  ambapo hadi sasa Umoja wa Ulaya  umeshatoa  euro milioni 20 kusaidia kutatua matatizo ya kiutu ambayo yamesababishwa na kundi hilo wapiganaji wa IS wanaoshikiria maeneo kadhaa nchini  Iraq.


Waziri Frank Walter Steinmeier aonya kuhusu Urusi.


Waziri wa mambo ya nje ya nchi  wa  Ujerumani Frank Walter Steinmeier,ameleezea wasiwasi wake kuhusu msukumo uliyopo wa  vikwazo kutoka kwa nchi wanachama wa nchi za umoja wa Ulaya kuwa  hutahatarisha na kuiyumbisha Urusi, ambapo wimbi lake litaleta mtikiso katika bara la Ulaya.

Walter Steinmeier alisema kuwa, kushuka kwa tahamni ya Lubo, fedha inayo tumika Urusi, hakutakuwa na faida kwa nchi za Ulaya, hivyo ni bora kuwepo na uangalizi katika sheria za kuweka vikwazo kwa Urusi.

Mazungumzo hayo ya Steinmeier, yamekuja baada kikao cha wakuu wanchi za jumuiya ya Ulaya, kuionya Urusi kuwa kama haitabadiri msimamo wake dhidi ya Ukraine, nchi za Umoja wa Ulaya hazita sita kuongeza  vikwazo zidi ya Urusi.




No comments: