Friday, August 1, 2008

Umoja wa Mataifa waidhinisha kuondoa majeshi yake mpakani"Katibu mkuu aonya"

Madona na mumewe Guy Ritchie, wasema hizo ni tetesi tu na siyo kweli.

Hollywood ,Amerika - 28/07/08. Mwanamusiki na nyota ya musiki wa pop, Madona pamoja na mume wake Guy Ritchie, wamesema, tetesi zinazo vuma kuhusu maisha yao ya ndoa, yakuwa ipo njia panda ni za uzushi tu.
Wapendanao hawa, walisema yakuwa uvumishi wa vyombo vya habari ni vya uongo na vyombo vya habari
Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa famulia ya Madona na Ritchie, mcheza sinema Vinnie Jonnes,alisema yakuwa Madona na Guy huwa hawapendi kusoma habari za magazeti.
Na Madona na Guy, wanacho tilia maanani ni kulea watoto wao watatu, Lourdes,Rocco and David, na nimfano wa kuigwa kwani huwawananifurahisha kila tukutanapo, alimalizia kwa hayo.
Pichani wanaonekan Madona na Guy Ritchie wakiwa pamoja hivi karibuni katika moja ya sherehe zilizo fanyika Hollywood hivi karibuni.
Picha ya pili anaonekana Madona, akiwa anaelekea mbele ya jukwaa, kabla ya kuingizwa kuwa mmoja ya wanamusiki maarufu duniani na kutambuliwa rasmi katika kundi la wanamuziki wa rock en roll.
Darfur yapata baraka za Umoja wa Mataifa"Sudani yahidi ushirikiano".
Umoja wa Mataifa, New York - 01/08/08. Kamati ya usalama ya umoja wa mataifa,imepitisha kuongezewa muda kwa kuwepo kwa wanajeshi wa umoja huo nchini Sudani katika eneo la Darfur kwa kipindi ingine cha mwaka mmoja.
Katika makubaliano hayo, ni Amerika peke, haikuwe katika maamuzi hayo, kwa kudai yakuwa kungepeleka maoni tofauti kwa wale wote wanaohusika na maafa katika eneo la Darfur, kwa kuzingatia yakuwa rais wa Sudani bwana Omar Hassan El Bashir na baadhi ya viongozi wa serikali yake walishitakiwa na mahakama ya kimataifa mjini Hague.
Kupitishwa kwa muswada huo kumepokelewa vizuri na serikali ya Sudani na kuhaidi kushirikiana na kikosi hicho.
Hata hivyo, wasemaji wa kikosi hiki wamekuwa waki taka umoja wa matifa kuwapa nyenzo za kufanyia kazi katika eneo hili ambalo limekuwakatika hali ngumu kiamani.
Picha ya juu anaonekana, rais wa Sudani, Omar Hassan El Bashir, akihutubia wananchi wa eneo la Darfur hivi karibuni alipo tembelea eneo hili.
Picha ya pili, ni ya baadhi ya magari yaliyo aribiwa kutokana na mapigano yano endelea katika eno hili la Darfur.
Picha ya tatu anaonekana mmoja ya wapiganaji wa (NAMID - UN - Afrika Union Mission in Darfur), akiwa katika doria nje ya makazi yao.
Picha ya nne anaonekana mwanajeshi wa Umoja wa mataifa, akiwa amesimamama mbele ya ofisi iliyopo katika moja majengo yaliyopo na Afrika.
DRC na makundi ya nayopinga serikali wapo njia panda kwa kuvita"Amani ipo tete, jumuia ya kimataifa wadai".
Kinshasa, DRC - 1/08/08. Serikali ya Kinshasa imeanza kukusanya wanajeshi wake tayari kupambana na makundi yanayo pingana na serikali mashariki mwa nchi hiyo.
Hata hivyo kujikusanya kwa kwa wanjeshi wa serikali kumepelekea hata vikundi vinavyo pinga serikali kuanza kujiandaa na mapambano , kwa mujibu wa msemaji mmoja wa shirika la utoaji wa misaada katika eneo hilo
Mmoja wa wafanyakzi wanaoshugulikia haki za binadamu, Anneke van Waudenberg akisema kuna hali isiyo nzuri kiamani katika eneo hili na kuhatarisha maisha ya jamii.
Kufuati hali hiyo, jumuia za kimataifa zikiongozwa na Umoja wa Ulaya, wameonya ya kuwa hali hii itaongeza utete wa amani katika eneo hili na kupelekea kuvunjika mkatba wa amni ulio kubalika mwezi wa januari.
Picha hapo juu ni picha ya bendera ya DRC, mashariki mwanchi hii kumekuwa katika hali ya utete kwa kipindi kirefu.
Picha chini wanaonekana baadhi ya wanajshi wa DRC, ambo muda si mrefu watakuwa mstari wa mbele kupambana na makundi yanayo pinga serikali ya Kinshasa.
Umoja wa mataifa waidhini kuondoa majeshi yake mpakani"Katibu mkuu aonya".
UN, New York - 31/07/08 . Umoja wa mataifa umepiga kura na kupitisha mswaada wa kusimamisha kuwepo kwa majeshi ya umoja wa mataifa katika mpaka kati ya Ethiopia na Eritrea.
Wanajeshi wapatao 1,700 ambao walikuwepo huko kwa kipindi cha miaka minane, kulinda amani katika mpaka unao tenganisha Eritria na Ethiopia wenye urefu wa zaidi ya maili 15 upana na maili 620 urefu.
Hata hivyo katibu mkuu wa umoja wa mataifa, bwana Ban Ki- Moon, ameonya yakuwa kushindwa kukubaliana kuwepo kwa amani katika eneo hilo na kutokuwepo kwa jeshi la umoja wa mataifa, huenda kukasababisha kuzuka kwa vita tena.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Umoja wa Mataifa, ambapo kupitia umoja huu maswala mengi ya nchi wanachama huamuliwa.
Picha ya lipi wanaonekana wanajeshi wa Ethiopia wakiwa ndani ya lori huku wakiwa wamshikilia baadhi ya siraha mikononi mwao.
Picha ya tatu ni ya wanajeshi wa Kieritrea wakiwa wamesimama pembeni ya kifaru na huku risasi zikiwa wamezining'iza katika mtutu wa kifaru.
Picha ya mwisho ni ya ramani inayoonyesha mpaka kati ya Ethiopia na Eritrea , juu ni ramani nchi ya Eritrea na chini Ethiopia.
Mwenyekiti wa ANC, apata pigo la kisiasa"Ndoto ya Urais ya ingia Ukungu".
Johannesburg, Afrika ya Kusini - 31/07/08. Mwenyekiti wa chama tawala nchini Afrika ya Kusini, bwana Jacob Zuma, amekumbwa na wakati mgumu katika kampeni yake ya kutaka kuwa rais wa nchini hiyo, baada ya mahakama kukataa kuzuia ushaidi unao sadikiwa kuwa unaweza kutumika katika kesi inayao mkabili dhidi yake.
Katika uvamizi huo uliofanyika katika ofisi za bwana, Zuma, kulipelekea kupatikana kwa zaidi ya mafaili yenye makaratasi 93,000.
Kesi inayo mkabili bwana, Jacob Zuma, inahusika na rushwa na utumiaji wa fedha na kuepuka malipo ya kodi katika biashara ya ununuzi wa ndege za kivita.
Picha hapo juu anaonekana bwana, Jacob Zuma akiongea katika moja ya mikutano hivi karibuni.
Picha ya pili, mwenyekiti wa chama tawala ANC, bwana, Jacob Zuma akihutubia katika mkutano wa chama hicho wakati wa kampeni ya kutaka achaguliwe kuwa mwenyekiti wa chama hicho cha ANC.
Chama na serikali za waziri mkuu wa Uturuki bwana , Recep Tayyip Edrogan zaokolea na mahakama.
Ankara, Uturuki - 30/07/08. Chama kinachotawala nchini Uturuki AKP kinacho ongozwa na waziri mkuu bwana, Recep Tayyip Erdogan kimepata hafueni, baada ya mahakama kuu nchini humo kupinga kufutwa kwa chama hicho.
Majaji kumi na moja waliotoa uamuzi huo,baada ya kikao kilicho chukua masaa, na hatimayake waliamua kupiga kura, ndipo matokeo yakaelemea kwa wale majiji walio kuwa wanataka chama cha AKP, kubaki madarakani kushinda kwa kura 6 dhidi ya 5 za majaji.
Hata hivyo majaji hao walitoa onyo kwa chama cha AKP, kwa kushutumiwa kuleta mgawanyiko katika jamii na kuagiziwa kutoingiza maswala ya dini katika serikali.
Kuruhusiwa kuendelea kwa chama cha AKP, kumefikia mwisho wa mgogoro wa kisiasa nchini humo.
Picha hapo juu anaonekana waziri mku wa Uturuki, bwana Recep Tayyip Erdogan, akihutubia katika moja ya mikutano nchini humo.
Picha ya pili anaonekana waziri mkuu wa Uturuki bwana, Recep Tayyip Erdogan akiwa katika kikao cha maswala ya kiuchumi mapema hivi karibuni nchini Uswisi.
Picha ya mwisho, wanaonekana, waziri mkuu wa Uturuki bwana, Recep Tayyip Erdogan akiongea na rais wa Amerika George Bush, wakati walipo kutana, kwani kutulia kwa siasa nchini Uturuki ni habari njema kwa NATO, Uturuki ni mshiriki mkuu wa wa umoja huu.

No comments: