Iran na Zimbabwe zakubaliana kushirikiana.
Harare,Zimbabwe - 24/04/2010. Rais wa Iran Mahmoud Ahmadinejad amemaliza ziara yake nchi Zimbabwe.
Katika ziara hiyo rais wa Iran, alifungua maonyesho ya biashara katika mji wa Bulawayo baada ya kumaliza kusaini mkataba wa kiuchumi kati ya Zimbabwe na Iran.
Picha hapo juu wanaonekana rais wa Iran kushoto akiwa na mwenyeji wake rais wa Zimbabwe mara baada ya rais wa Iran kuwasili nchini Zimbabwe.
G-20 bado ya simama njia panda.


Talinn, Estonia 24/04/2010. Viongozi wa NATO wamekutana nchini Estonia kujadili kwa undani jinjia gani watafanya kujiandaa kuondoa majeshi nchini Afghanistan.
Mkutano huo ulioudhuliwa na viongozi wa nchi 28, walikubaliana kwa misingi ya kuimarisha jeshi na polisi la nchi ya Afghanistan ili washike madaraka na kusimamia ulinzi wa nchi.
Akiongea mbele ya wajumbe, katibu mkuu wa NATO, Anders Fogh Rasmussen, alisema"Serikali ya Afghanistani ina endelea vizuri katika ulinzi wa nchi na hivyo kuna haja madaraka yote yawe chini ya uongozi wa serikali ya Afghanistan."
NATO inatarajia kuanza kupunguza majeshi yake nchini Afghanistan kuanzia mwaka 2011.
Vita vya Afghanistan vilinza kwa ajili ya kupambana na makundi ya ugaidi ya Taliban na Al-qaeda.
Picha hapo juu wanaonekana viongozi wa nchi za NATO wakiwa katika mkutano kujadili mbinu mbada kuhusu Afghanistan.
No comments:
Post a Comment