Monday, April 5, 2010

Rais Raul Castro"Kuba haitatetereka kamwe."

Kiongozi wa mlango wa kulia nchini Afrika ya Kusini auwawa.

Ventersdorp, Afrika ya Kusini - 05/04/2010. Serikali ya Afrika ya Kusini imewataka wanchi wawe watulivu baada ya aliyekuwa kiongozi wa wa Wazungu wenye itikadi za mlango wa kulia kuuwawa na wafanyakazi wake baada ya mabishano kuhusu malipo ya kazi. Kwa mujibu wa mama wa mmoja wa watuhumiwa walio husika katika mauaji ya kiongozi huyo Eugene Terreblance, alisema "mwanae alimpiga chuma kiongozi huyo baada ya mabishano kuhusu malio ya kazi walioifanya tangu mwezi wa Desemba." Kufuatia tukio hilo wanancha na wapenzi wa Terreblance wamehaidi kulipa kisasi na pia wameitaka serikali kufuatilia na kuchunguza kwa makini chanzo cha kifao cha kiongozi wao. Eugen Terreblance, alikuwa mmoja wa viongozi ambao wakati wa utawala wa wazungu walio wachache nchini Afrika ya Kusini alikuwa anafanya kazi na serikali hiyo kwa ukaribu sana na hata kushukiwa kuhusika katika matukio makubwa ya kutishia amani ya wazalendo wa Afrika ya Kusini kwa ujumla. Picha hapo juu anaonekana Eugene Terreblance, enzi za uhai wake akiwa juu ya farasi kuzunguka mji ambao watu wengi watamkumbuka kwa mambo yake aliyo yafanya wakati wa uhai wake. Rais Raul Castro"Kuba haita tetereka kamwe."
Havana Kuba - 05/04/2010. Rais wa Kuba amesema ya kuwa serikali na wanchi wa Kuba hawata kubali kuyumbishwa wala kutetereka kwa njama za watu amabo wanaacha kula kwa sababu fulani. Rais Raul Castro, aliyasema haya wakati alipokuwa akiwahutubiwa wanachi wa Kuba siku ya Jumapili kwa kusema "nchi za Ulaya na Amerika zina jitahidi kwa kwakila njia kuleta matatizo ndani ya nchi," "Kuba" "kwa kuwawashawisha wapinzani wa serikali kufanya mambo yasiyo ya kawaida." Wakati huo huo mwandishi wa habari Guillermo Firinas amegoma kula kwa kudai wafungwa wa kisiasa waachiwe huru Kwa mujibu wa shirika la kutetea haki za binadamu, zinasema "Kuba inawafungwa wapatao 55 ambao wapo jela." Picha hapo juu anaonekana Guillermo Firinas, akipelekwa hospital ili kupata matibabu baada ya kugoma kula mpaka madi yake yatimizwe. Wananchi wa China wajawa na furaha kubwa. Shanxi, China - 05/04/2010. Watu wapata 110 wameokolewa kutaka ndania ya machimbo ( migodi) ambayo ilipasuka na kujaa maji kwa kipindi cha wiki moja iliyo pita. Watu hao walichukuliwa na kupelekwa hospitali kwa ajili ya kuangaliwa afya zao zaidi. Kwa mujibu wa msemaji wa serikali Liu Dezheng alisema, " maajabu na ni kweli na imetokea kama tulivyo kuwa tunaamini na hatimaye tume fanikiwa kuwaokoa wenzetu" Viongozi na wanchi wa China wamewapongeza waokoaji wote kwa kazi nzuri waliyoifanya na nifuraha kubwa kwa wanchi wote wa China. Picha hapo juu wanaonekana wakiwa wamembeba mmoja ya wafanyakzai waliokuwa wamekwama ndani ya mgodi baada ya kumtoa ndani ya mgodi.

No comments: