Saturday, May 1, 2010

Nchi ya Chad kukumbwa na janga la ukame na njaa.

Omar al Bashir ahaidi kutumikia Wasudani wote. Khatoum, Sudan - 01/05/2010. Rais mchaguliwa wa Sudan, Omar al Bashir, amwataka wananchi wa Sudan kushirikiana katika kukabiliana matatizo ambayo yanaikabili nchi hiyo.Omar al Bashir aliyasema hayo baada ya kushinda uchaguzi mkuu wa kugombea kiti cha urais uliofanyika mapema mwezi uliopita nchini Sudan. Uchaguzi huo wa kushirikisha vyama vingi ulifanyika huku baadhi ya vya kususia uchaguzi huo Kwa upande wake Omar al Bashir, alisema " mmenichagua kuwa kiongozi wenu na hivyo nitaingoza nchi yangu kwa manufaa ya wananchi wote wa Sudan." Picha hapo juu ni picha kubwa ya rais Omar al Bashir, aliyechaguliwa kuiongoza tena Sudan huku chini ya picha wanaonekana wanchi ambao wanamuunga mkono rais Omar al Bashir wakishangilia baada ya ushindi kura kutangazwa. Nchi ya Chad kukumbwa na janga la ukame na njaa. N'djamena,Chad-01/05/2010. Shirika moja la kimataifa linalo shughulika na kutoa misaada limedai nchi ya Chad inahali mbaya kutokana na ukame ambao unendelea kuikumba nchi hiyo. Hata hivyo shirika hilo limesema " Wanachi wa Chad, wanakabiliwa na hali hiyo ikichangiwa na vita ambavyo vimechangia kuwepo na wakimbizi wengi wa ndani ya nchi na kusababisha hali ya uzalishaji kuwa mgumu hasa kwenye sehemu zile ambazo kuna unafuu wa hali ya ukame." Picha hapo juu anaonekana mama akiwa na mtoto wake ambaye anaonekana kutokuwa na afya nzuri kutokana na utapia mlo. Madawa yatakiwa kurudishwa" Hayakufikia kiwango"

New York. Amerika - 01/05/2-10. Kampuni ya kutengeneza madawa imeitisha madawa ambayo yalikuwa tayari kutumika kutibu, baada ya kufahamika yahakuwa yamefikia kiwango cha bora.
Kwa mujibu wa msemaji wa McNEil, " imebidi dawa zote za aina ya,Tylenol,Zyrtec, Motrian na Benadryl zirudishwe ili kutathmini na kuzihakiki."
Nchi zitakazo athirika ni Amerika-US,Canada,Jamuhuri ya Dominika, Guan, Guatemala,Jamaika, Puerto Rico, Panama, Trinida & Tobago,Kuwait na Fiji.
Picha hapo juu zinaonekana baadhi ya madawa ambayo yanatakiwa yarudishwe kwaajili ya kutathminiwa upya na wataalamu wa madawa.

No comments: