Monday, June 30, 2014

Waasi wa Irak wajitangazia utawala.

Wataalamu wasema Oscar Pistorius ni mzima wa akili.

Pretoria, Afrika ya Kusini - 30/06/2014. Ripoti ya upimaji wa akili ya mwanariadha  maafuru wa Afrika ya Kusini  imetolewa na kukabidhiwa jaji anaye sikiliza kesi hiyo tayari kwa kesi kuendelea.


Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na wataalamu wa kupima akili na utashi, wamesema kuwa " Pitorius ni mzima wa akili."

Akiongea kuhusu ripoti hiyo, jaji anaye sikiliza kesi hiyo, Jaji  Thokozile Masipa amesema, " nimepata ripoti hii leo Jumatatu hasubuhi na bado sijaisoma."

Jaji Masipa, alitoa ruksa kupimwa akili kwa Pistorius, baada ya mwanasheria wake, kudai kuwa mteja wake anamatatizo ya akili kutokana na historia ya maisha yake.

Ripoti hiyo ambayo ina muhusu mwanariadha Osca Pistorius 27,  ambaye alipelekwa kwenye nyumba ya kuangalia mwenendo wa tabia na akili yake ili ilikuweza kufahamu kuwa wakati alipo kuwa akifanya kitendo cha mauaji alikuwa hali ya uzima wa akili au la.
 
Oscar Pistorius akikutwa na hatia ya kuua, huenda hakaukumiwa kwende jela si chini ya miaka 15 au kifungo cha maiasha.

Waasi wa Irak wajitangazia utawala.


Diyala , Irak - 30/06/2014. Kundi linalo julikana kama ISIS lilipo nchini Irak, limetangaza kuwa maeneo ambayo imefanikiwa kuyatwaa yatabadilishwa majina na kuitwa kwa ujumla  kama  majimbo ya nchi za Kiislaam.

Likitoa uthibitisho wa kubadilishwa kwa majina haya, kundi hili lilisema " kuanzia sasa, maeneo ya Diyala  na  jombo la Aleppo yataitwa  kwa pamoja nchi ya Kiislaam na yataongozwa Kiislaam."

Pia kundi hilo liliongeza kuwa " Abu Bakar al Baghdad, ndiye kiongozi wa kundi hilo kwenye eneo hilo zima."
Kundi la ISIS limetangaza hivyo, baada ya miaka kumi kupita tangu jeshi la Marekani na washiriki wake kuiangusha  serikali ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Saadam Hussein.

Kundi hilo limeshutumiwa hivi karibuni kwa kufanya mauaji ya kinyama ambayo yamelaaniwa na mashirika ya haki za binadamu na ya kutetea haki za binadamu, kwa kusema kuwa lazima hatua za kisheria zichukuliwe mapema ili kuhakikisha kuwa mauaji kama hayo yasitokee tena.

Kufuatia kuwa na nguvu kwa kundi hilo ISIS na kufanikiwa kutwaa maeneo inayo yashikilia, waziri mkuu wa Irak Nour al Marik kuomba msaada katika kupambana na kundi hilo, ambalo kwa sasa jeshi la serikali ya Irak linapambana na kundi hilo katika jimbo la Tikrit, ambapo ndiko aliko zaliwa Saadam Hussein.  

No comments: