Viongozi wa Wapalestina na Izrael wakutana Vatican.
Ibada hiyo ambayo ilikuwa na nia ya kuombea amani kati ya Waizrael na Wapalestina, ilidhuriwa na rais wa Izrael Shimon Peres na kiongozi wa Wapalestina Mahamoud Abbas.
Kukutana huko kwa viongozi wa juuu wa jijini Vatican kumekuja baada ya mwaliko uliofanywa na Papa Fransis baadanya kufanya ziara katika eneo la nchi za Mashariki ya Kati za Izreal na maeneo ya Wapalestina ilikutafuta njiaa ya kuleta amani katika eneo hilo.
Akiongea baada ya ibada ya misa na kukutana kwa viongozi hao wa kuu wa Wapalestina na Waizrael, Padri Pierbattista Pizzaballa ambaye ni mkuu wa kitengo kinacho simamia masuala ya amani ya Mashariki ya Kati alisema "hatuwezi jidanganya kuwa amani ya Mashariki ya Kati italetwa bila mazungumzo, na ndoyo maaana Papa Fransis ameweka mkakati katika suala hili, na kwa sara na maombi basi mafanikiyo yataonekana."
Viongozi hao wa Palesestina, Izrael na ongozi wa Vatican kwa pamoja walikaa na kuongea ili kutafuta suruhu ya amani katika eneo zima la Mashariki ya kati na kuwa na ujumbe kuwa eneo la Ardhi takatifu lazima liwe na amani.
Hatimaye Wamisri wapata rais.
Kairo, Misri - 08/06/2014. Aliyekuwa wa majeshi ya Misri, Abdel Fattah al Sisi ameapishwa rasmi kuwa rais wa nchi ya M,isri mwaka mmoja baada ya kuongoza mapinduzi ya kuipindua serikali ya kiongozi wa Muslim Brotherhoods Mohammed Mosri
Akiongea mara baada ya kuapishwa kuwa rias Abdel Fattah Sisi alisema" mafanikio ya Wamisri ya po wazi, hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunajenga Misri bora ambayo inaweza zalisha makate, yenye kufuata sheria na haki za binadamu ambazo zinafuata haki"
Hata hivyo wapinzani wa Sisi, wameeleza wasiwasi wao kuwa "huenda rais huyu mpya wa Misri akafuata nyayo Hosni Mubaraka"
Rais Abdel Fattah al Sisi aliapishwa kwenye jengo ambalo aliapishiwa rais aliyempindua Mohammed Mosri na kuudhuliwa na badhi ya viongozi wa serikali na huku watu wanao mmuunga mkono wakishangilia kwa kupeperusha bendera ya Misri.
Abdel Fattah al Sisi amekuwa rais wa nne kutoka kuwa mkuu wa jeshi hadi kushika nafasi ya uongozi wa juu wa kiti cha urais.
Uongozi wa Kifalme nchi Uhispania wakubwa na mthiani.
Madrid, Uhispania - 08/06/2014. Mamia ya watu wameaandamana katika jiji la Madrid kwa madai ya kuupinga utawala wa kifalme siku chache baada ya mfalme wa sasa wa Uhispania Juan Carlos 74 kutangaza kuwa anamwachia kiti cha ufalme mwanae wa kiume Prince Filipe
.
Maandamano hayo ambayo yalikuwa na nia ya kutaka Uhispania kuwa na serikali ya Jamuhuri, badala ya sasa ambayo inatawaliwa na mfalme.
Mmoja wa waandaaji wa maandamano hayo ana amabaye pia ni mkuu wa chama cha Pademos Pablo Igresias amesema " tunataka suala hili likabidhiwe kwa wananchi, tunaka kura ya maoni ipigwe, na siyo tatizo kama Waispania wakipewa nafasi ya kuamua kwa aajili ya maisha ya baadae ya kila Mspania."
Maandamano hayo yamefanyika ikiwa zimebakia siku 11 kabla ya mwana wa mfalme Prince Filipe kuapishwa rasmi ili kukabidhiwa kiti cha ufalme wa Uispania.
Uongozi wa kifalme unaungwa na chama kilichopo madarakani na baadhi ya vyama vikuu vya upinzani, na Prince Filipe anatarajiwa kukukabidhiwa kiti cha Ufalme Juni 19- 2014 ambapo sherehe hiyo itakuwa ikiendena na shughuli za kibunge katika siku hiyo ya kuapishwa kwa mwana huyo wa mfalme.
1 comment:
Helloo
Post a Comment