Friday, June 13, 2014

Mashindano ya kombe la dunia yaanza kwa vishindo.

Mashindano ya kombe la dunia yaanza kwa vishindo.

Sao Paulo, Brazil - 13/06/2014. Mashindano ya kugombea kombe la dunia kwa mchezo wa soka  yameeanza rasmi huku timu wenyeji kiondoka na ushindi.

Wenyeji Brazili ilibidi wafanye kazi ya ziaada na huku bahati kuwaangukia kwa kushinda magoli matutu kwa moja zidi ya timu ya Croatia katika mechi ya ufunguzi wa mashindano hayo. Magoli ya Brazili yalifungwa na Neymar aliye pachika mabao mawili, moja la penati na Oscar alifunga bao la tatu na Croatia walipata goli baada ya beki wa Brazil Marcelo kujifunga katika harakati za kuokoa mpira usiingie golini

Mashindano ya kombe la dunia yanazishirikisha timu 32 kutoka mabara yote yaliyopo duniani na yanafanyika kwa mara ya ishirini tangu kuanzishwa mwaka 1930.

Mashindano ya kombe la dunia kwa mchezo wa kandanda yanatarajiwa kuwa na msisimko mkubwa na huku baadhi ya washabiki wakitoa matumanini kwa timu mwenyeji Brazil kuibuka na ushindi kwa kubeba kombe hilo tena kwa mara ya sita.


2 comments:

Murni Rosa said...

Haha.. which one do you choose? Germany? Argentina? :))

cahaya cinta said...

hello friend,,,,mampir ke blog cahaya juga ya
www.cahayacintablog.blogspot.com
makasih