Wednesday, June 4, 2014

Marekani yahaidi kuwa karibu na Ukraine.

John Kerry afanya ziara ya kustukiza nchini Lebanoni.


Beiruti, Lebanoni - 04/06/2014. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani amewasili nchi Lebanoni ili kujua ni kwakiasi gani Marekani itasaidiana na viongozi wa Lebanoni ili kutatua suala la wakimbizi.

Akiongea mara baada ya kufika Lebanoni na kujionea mwenyewe ni kwa jinsi gani serikali ya Lebanoni inavyo kabiliana na  hali ya wingi wa wakimbizi, waziri John Kerry alisema '' nimuhimu kwa serikali ya Lebanoni ikasaidiwa katika swala zima la kusaidia wakimbizi kwani hili nijukumu la kimataifa''

Kufatia zira hiyo ya John Kerry, Lebanoni inatarajiwa kupata msaada wa dola $51million ili kuweza kukabiliana na wimbi la wakimbizi wanaoingia nchi humo toka Syria ambapo bado vita vya kutaka kuing'oa serikali ya rais bashar al Assad.

Lebanon imekuwa katika myumbo wa kisiasa kwa muda mrefu, na tatizo la ongezeko la wakimbizi kukimbilia nchini humo limefanya jamii ya Walebanoni kuwa na upinzani mkubwa kwa kuwepo kwa wakimbizi wanao ingia nchini humo wengi wao kutoka Syria.

Marekani yahaidi kuwa karibu na Ukraine.

Warsaw, Poland - 04/06/2014. Serikali ya Marekani imehaidi kuongeza misaada kwa serikali ya Ukraine, ili kuweza kupambana na wapinzani wanaotaka kuigawa nchi hiyo.

Haadi hiyo ilitolewa na rais wa Marekani Baraka Obama wakati alipo kutana na rais wa Ukraine Petro Poroshenko jiji Warsaw.

Rais Obama alisema '' kitendo cha wanachi wa Ukraine kumchagua Petro Poroshenko ni cha busara kwani  ni mtu atakaye waongoza kwa bora zaidi.''

'' Na serikali ya Marekani itatoa pesa kiasi cha dola billion 5$ ili kusaidia Uikraine kutokana na hali iliyopo ili kulinda usalama wake''  Tangu mwezi Machi serikali ya Marekani imesha toa dola $23million kwa Ukraine.

Kabla ya kuchaguliwa kuwa rais katika uchaguzi uliyofanyika May 25, Petro Poroshenko, alikuwa mfanya biashara ambaye alikuwa akishughulika na uuzaji wa vyakula hasa chololati na bidhaa zinazo endana na mikate na kupewa jina la Mfalme Chokolati.

No comments: