Thursday, September 18, 2014

Rais wa Ukraine aililia Marekani kimsaada.

Leo ni siku ya Waingereza wasimama njia panda.

Glasgow, Scotland - 18/09/2014. Wananchi wa Uingereza wapo katika mtazamo tofuti na kutokujua nini kitatokea, kwani leo hii raia wakazi wa Scotland wanapiga kura ili kuamua kama wataendelea kuwa katika muungano wa Uingereza au kujitenga na muungano huo na kuanza kujitawala, jambo ambalo limeleta tumbo joto kwa Waingereza walio wengi.

Kura hizo ambazo zimeaanza kupigwa leo hasubuhi, huku  wanasiasa wa pande zote, wanao unga mkono kujitenga  na wale wanao pinga kujitenga, watakuwa wanasubiria kuona kama kampeni walizo fanya zimeleta matokeo waliyo tarajia.

Matokeo ya kura hizo yatangazwa siku ya Ijumaa 19/09/2014.
Ikiwa wananchi wa Scotland watapiga kura kujitenga, kutavunja muunganao ulidumu  miaka 307, jambo ambalo litaleta mabadiriko makubwa ya kisiasa, kiuchumi,kijamii na pia kiutawala wa kifalme.

Rais wa Ukraine aililia Marekani kimsaada.

Washington, Marekani - 18/09/2014. Rais wa Ukraine, ameitaka Marekani kuipatia nchi yake siraha na vifaa vya kivita ili serikali yake iweze kuzitumia kuleta amani Mashariki mwa Ukraine.

Akihutubia bunge la Kongresi la Marekani, rais Petro Poroshenko alisema "Blangeti na vifaa vya kuangazia usiku wa giza ni muhimu, lakini hata hivyo blanketi haziwezi kusaidia kushinda vita na kuleta amani, hivyo tunaomba mtupe vifaa vya kivita ambavyo vitasaidia kuleta amani."

Akipigiwa makofi na wabunge wa  Kongresi, rais Poroshenko aliongezea "Naiomba Marekani kutupatia msaada ya kiulinzi ambao utaambatana na ushirikiano wa jumuhia ya NATO, kwa Ukraine haitaweza kusimama peke yake katika mapambano haya."

Vile vile katika hotuba yake, rais Porocshenko, aliitupia lawama Urusi kwa kuhusika katika kuvuruga amani nchini Ukraine kwa kuwaunga mkono wapinzani wa serikali yake.

Na pia rais Poroshenko alifananisha hali iliyopo nchini Ukraine ni sawa na ile iliyotokea Georgia, na hivyo Marekani ni muhimu kutoruhusu hali kama hiyo kutokea tena.

No comments: