Sunday, May 11, 2008

Morgan Tsvangarai kupigania kiti cha urais tena,"Hii ni kwaajili ya watu wa Zimbabwe"Tsvangarai.

Harare,Zimbabwe - Kiongozi mpinzani wa chama MDC nchini Zimbabwe, kinacho ongozwa na bwana Morgan Tsvangarai, kimetangaza ya kuwa kitashiriki katika uchaguzi mwingine wa kuchagua rais atakaye ongoza Zimbabwe katika kipindi cha miaka mitano itakayo fuata.
Akiongea na waandishi wa habari mjini Pretoria, bwana, Morgan Tsvangarai, alisema yakuwa
marudio ya uchaguzi huu ni kwa ajili ya wananchi, wananchi walisha zungumza kutumia kura zao na sasa watasema tena kutumia kura zao.
Hata hivyo alipo ulizwa kuhusu ,mpatanishi wa sakata hilo la kisiasa nchi Zimbabwe, ambaye ni rais wa Afrika ya Kusini bwana Thabo Mbeki,bwana Tsvangarai, alisema ya kuwa hana imani na mpatanishi huyo ,a kuiomba jumuia ya kimataifa iliangalie kwa undani swala hilo.
Picha ya hapo ju, anaonekana bwana Morgan Tsvangari akiongea na waandishi wa habari mjini Pretoria siki ya jumamosi
Picha nyingine ni picha ya marais wa Zimbabwe bwana Robert Mugabe Kulia, na bwana Thabo Mbeki alipokutani siku ya ijumaa kwa ajili ya mazunfumzo.

No comments: