Wednesday, May 21, 2014

China na Urusi zasaini mkataba wa karne.

China na Urusi zasaini mkataba wa karne.

Beijing, China - 21/05/2014. Urusi na China zimesainia mkataba wa biashara wa malighafi mafuta ambao utatudu kwamuda wa miaka 30.

Makubaliano hayo  kufanya biashara pamoja katika sekta ya malighafi mafuta yamechukua miaka kumi ya majadiriano na hatimaye  kufikia makubaliano, ambapo kuanzi sasa  shirika la uzalishaji wa malighafi mafuta la Urusi Gazprom na la China CNPC kwa pamoja yatafanya bishara ambayo itagharimu $ 400 billion.

Mkurugenzi mkuu wa Gazprom Aleksey Miller lisema " mkataba wa makubaliano na matumzi yatakavo fanyika itabaki ni kati ya Gazprom na CNPC katika makubaliano ya kibiashara."

Mkataba wa Urusi na China umeitwa mkataba wa karne, kwani utasaidia nchi hizi mbili kuwa karibu zaidi jambo ambalo nchi za muungano wa Ulaya na Marekani zitauchunguza na kuwa makini na nchi  hizi mbili.

Kitendo cha Urusi kusaini mkataba na China  kibiashara ya malighafi mafuta kimetafsiliwa kuwa  ni ushindi mkubwa kwa rais Vladmir Putin, kwani kutokana na mgogoro wa Ukraine, Urusi imejikuta ikivutana na nchi za muungano wa jumuiya ya Ulaya na Marekani na hata kufikiwa Urusi kuwekewa vikwazo vya kiuchumi.

No comments: