Saturday, May 24, 2014

Papa Francis aanza ziara nchi za Mashariki ya Kati.

Jacob Zuma ala kiapo kuwa rais kwa mara ya pili mfululizo.

Pretoria, Afrika yaKusini - 24/05/2014. Rais Jacob Zuma  ameaapishwa kwa mara nyingine kuwa rais wa Afrika ya Kusini ikiwa ni muhula wake wa pili kama rais wanchi hiyo.

Baada ya kuapishwa rais Zuma  alisema " kipindi hiki cha uongozi wangu wa miaka mitano tutahakikisha tunainua uchumi na maisha ya jamii kwaujumla."

Katika kipindi chake cha kwanza cha uongozi, rais Jacob Zuma, amelaumiwa kwa kukosa kuinua maisha ya wananchi walio wengi ambao inasadikiwa hali ya umaskini imekuwa ikiongezeka kwa haraka kila kukicha.

Katika sherehe hiyo, marais na viongozi mbali mbali waliudhulia kuapishwa huko wakiwemo, rais Robert Mugabe wa Zimbabwe na Goodluck Jonathan.

Rais Jacob Zuma amechukua kiti cha urais chini ya chama cha ANC ambapo kilishinda uchaguzi mkuu uliyofanyika Mei 7 na kuwa chama pekee kinacho ongoza nchi tangu Afrika ya Kusini tangu kukomeshwa kwa serikali ya ubaguzi wa rangi miaka 20 iliyopita.

ICC Hague yatoa hukumu jela miaka 12 kwa German Katanga

Hague, Uhollanzi - 24/05/2014.Mahakama ya kimataifa ICC, inayo shughurikia makosa ya jina na ukiukwaji wa haki za binadamu imemuhukumu kwenda jela aliyekuwa mkuu wa majaeshi ya upinzani nchi Kongo DRC, German Katanga.

German Katanga 36, ambaye alikutwa na makosa ya kuuza siraha ambazo zimetumiwa katika mauaji ya mamia ya watu manamo  mwaka 2003.

Akitoa hukumu hiyo, Jaji Bruno Cotte alisema " mahakama inakuhukumu miaka 12 kwenda jela kutokana na makosa ambayo umekutwa nayo."

Hata hivyo, baada ya hukumu hiyo, wakili wa Katanga amekata rufaa kupinga uamuzi huo wa mahakama.

German Katanga amekuwa ni kiongozi wa pili kuhukumiwa na mahakama ya ICC baada ya mahakama hiyo kumuhuku jela aliyekuwa mkuu wa majeshi ya upinzani Thomas Lubanga mwaka 2012.

Papa Francis aanza ziara nchi za Mashariki ya Kati.

Amman, Jordan - 24/05/2014. Mkuu wa kanisa Katoli dunia Papa Francis amewasili nchi Jordan ikiwa ni moja ya nia yake ya kukuza uhusiano wa karibu na wakazi wa Mashariki ya kati.

Akiongea mara baada ya kuwasili nchini Jordani na kuongoza ibada katika uwanja mkubwa ulipo Amman  Papa Francis alisema " nimatumaini yangu kuwa amani na utulivu utakuwepo kwa wakazi wa eneo zima la Mashariki ya Kati na dunia nzima, na nawashukuru wananchi wa Jordani kuwa mstari wa mbele katika kuleta amani na kutoa msaada na vile vile kuwa weka kilauhudi ili kumaliza mzozo wa Waizrael na Wapalestina."

Papa Francis alipokelewa na  Mfalme wa Jordan Abdullah II wakati alipo wasili nchi Jordani na baadaye alitembelea katika hekalu la waumini wa Orthodox na vile vile kutembelea kambi ya wakimbizi kutoka  Syria.

Papa Francis katika ziara yake hiyo, ameambatana na wakuu wa dini ya Kiislam na Kiyahudi kutoka  Argentinana ikiwa ni katika jitihada zake za kutaka kuwepo na uhusiano wa karibu na waumini wa dini nyingine.

Siku ya Jumapili atatembelea mji wa Bethlehem - West Bank na kuongoza ibada katika eneo ambalo inaaminika ni mahali alipo zaliwa Yesu Kristu.

No comments: