Tuesday, May 13, 2014

Msuruhishi wa machafuko ya Syria atundika madaruga juu.

Waumini wa dini waajiliwa kupigana na ugaidi nchi Marekani.


New York, Marekani - 13/05/2014. Polisi katika jiji la New York wamekuwa wakiwaajili watu wenye imani na dini Kislaam tangu kutokea mashambulizi ya Septemba 11.

Likilipoti habari hizi, gazeti la New York Times  limeandika "Kamati ya usalama iliamua kuwaa ajili waumini hao wa dini ya Kiislaam katika hotel na kwenye Miskitiili kuweza kujua na kupata habari mapema kabla, kwani  maeneo hayo yamekuwa yakitumika katika mikutano na pia kuajili watu kujiunga na makundi ya kigadi."

Likiongeza katika ripoti hiyo limeandika kuwa " wengi wa waajiliwa wamekuwa wale wanao toka nje ya Marekani."

Akithibitisha kwa kuwepo kwa uajili huo, mkuu wa kitengo cha kupamana na ugaidi John Miller alisema " Tunaangalia watu ambao wanaweza kutupatia undani wa ugaidi kutoka sehemu tofauti duniani jambo ambalo litasaidia kupambana na ugaidi kwa urahisi."

Hata hivyo kufuatia uamuzi wa polisi kuajili watu wenye imani na dini ya Kiislaam, malalamiko yamekuwa yakitolewa na wahusika kwa kudai inabidi washirikiane na polisi kwani hawana njia nyingine.

Gazeti la New York Times limelipoti habari hizi kufuatia sheria ya uhuru wa habari.

Msuruhishi wa machafuko ya Syria atundika madaruga juu.


New York, Marekani 13/05/2014.Lakhdar Ibrahimi ambaye  aliyeteuliwa na umoja wa mataifa kuwa mkuu katika kusuruhisha suala la uleteji wa amani na mapatano katika myumbo wa kisiasa na vita kati ya Wasyria ametangaza kujiudhuru ifikapo mwisho wa tarehe 31/05/2014.

Akitangaza kutaka kujiudhuru huko katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema "Lakhdar Ibrahimi atajiudhuru"

Hata hivyo Ban Ki-moon haueleza ni nini kilicho mfanya msuruhishi huyo kutaagaza kujiudhuru wakati hali ya Syria bado ni tete.

Akiongea baada ya habari kutangazwa Lakhdar Ibrahimi alisema " nimekuwa nafikirika kujiudhuru  kila kukicha na sasa muda umefika wa kutangaza rasmi siku ya kujiudhuru kwangu."

Lakhdar Ibrahimi toka kuteuliwa kwake kushughulikia suala la machafuko ya Syria amaekuwa na wakati mgumu wa kuwapatanisha wapinzani wa serikali na serikali ya rais Assad, jambo ambalo lilimfanya akili na kuomba radhi kwa wananchi wa Syria kuwa hali bado ni tete katika kufikia makubaliano kwa pande zote mbili.

Kujiudhuru kwa Ibrahimi kumekuja wakati serikali ya rais Bashaar Assad imekuwana nguvu zaidi kuliko wapinzani na kufanikiwa kuuchukua mji wa Alepo ambao ulikuwa makao makuu ya wapinzani wa serikali na huku rais Bashar Asaad akiwa katika kampeni ya kugombea tena kiti cha urais kwa miaka saba ijayo, ambapo anatarajiwa kushinda kwa wingi wa kura.

Matokeo ya kura za maoni nchini Ukraine yawa kitendawili.


Moscow, Urusi - 13/05/2014. Matokeo ya kura ya maoni ya kutaka kujitawala kwa majimbo ya  Donitsk na Lugansk yamezidi kuleta kicha kuuma kwa uongozi wa nchi za jumuiya ya Ulaya na Marekani na huku Urusi ikiwa inachukua muda kutathmini nini kitatokea.

Kufuatia matokeo ya kura za maoni katika majimbo hayo,  serikali za majimbo hayo yameitaka Urusi kukubali kuziunganisha katika serikali ya shirikisho na kuwa sehemu ya Urusi.
Naye msemaji  wa rais Dmitry Peskov akjibu kuhusu maombi ya majimbo hayo amesema "Urusi Urusi bado natafakali kwa makini juu ya maombi hayo."

Matokeo ya kura katika majimbo hayo ya Donietsk na Lugansk yame pelekea viongozi wa majimbo hayo kutangaza kusimamisha maandalizi ya uchaguzi mkuu ambao ulitarajiwa kufanyika hivi karibuni jambo
ambalo Marekani imetishia kuwa " ikiwa hakutafanyika uchaguzi mkuu, vikwazo zidi ya Urusi vitazidishwa."

Kura zamaoni ambazo  zilipigwa siku ya Jumapili na  kwa wingi wa kura za asilimia 90 za kuunga mkono kwa majimbo ya Donetsk na Lugansk kujitenga na serikali ya Kiev,yameleta mitazamo tofauti.

Urusi imeshiria msimamo wake kuwa machafuko na mauaji yanayo endelea nchi Ukraine ni sababu ya serikali ya Kiev kushindwa kujua la kufanya, kwani imekuwa ikiongozwa na nguvu za nje badala ya kukaa na kufanya mazungumzo na wapinzani wa serikali na wakati huo huo Marekani na washiriki wake wakuu jumuiya ya Ulaya, kupinga na kulaani matokeo pia kutanganza kutoyatambua,

No comments: