Thursday, July 3, 2014

Kundi la Al Qaeda lawa na mbinu mpya za kupitisha mabomu viwanja vya ndege.

Polisi wa watawanya waandamanaji nchini Afrika ya Kusini.



Pretoria, Afrika ya Kusini - 03/07/2014. Polisi wamepambana na wafanyakazi na wanachama chama cha wafanyakazi wa viwanda vya chuma NUMSA ambao walikuwa wanadai ongezeko la posho.

 NUMSA chama ambacho kinawafanyakazi wanachama  waapatao 220,000 kiliitisha mgomo kwa wafanyakazi wake ilikiwa ni njia ya kushirikiza ombi lao lakutaka kuongezewa posho toka asilimia 12 hadi 15.

Msemaji wa polisi, Ronel Otto alisema "maandamano hayo yanafuata mgomo ambao umechukuliwa na wanachama wa NUMSA, na pia  ilibidi polisi kutumia mbinu za kiulinzi ili kutuliza ghasia baada ya baadhi ya wafanyakazi kuzuia mlango mkuu wa kuingia katika kampuni ya kufua umeme ya Eskom iliyopo Midupi Kaskazini mwa jimbo la Limpompo."

Maandamano na mgomo wa wafanyakazi wa NUMSA  umelalamikiwa na viongozi wa mashirika yanayo husika na zualishaji wa chuma kwa kudai kuwa lika siku Rand 300 millioni zinapotea na hivyo kuwataka wafanyakazi warudi kazini.

Jonh McCain aja na sera mpya ya Irak na Syria.



Arizona, Marekani - 03/07/2014. Mbunge wa Seneti la Marekani, ameshinikiza na kusisitiza kuwa inatakiwa kuwapa siraha wapiganaji wa wanaopingana na serikali ya Syria ambapo pia watatumia siraha hizo kupambana  na na kundi la ISIL lililopo nchini Irak.

Seneta John McCain aliyasema hayo wakati alipo kutana kiongozi wa mambo ya kigeni wa kundi linalo pingana na serikali ya Syria wakati alipo kuwa  ziarani nchini Uturuki.

Akiongea Seneta McCain alisema " kutokuwepo na niya ya kuwasaidia kisiraha wapinzani wa serikali ya Syria, kunahatarisha maslahi ya Marekani."

" Napia hili kundi la ISIL lililopo Irak lisipo kabiriwa haraka litakuwa ni hatari kwa katika eneo zima la Mashariki ya Kati jambo ambalo litasababisha hali ya usalama na ulinzi kwa Marekani na mafao yake kuwa katika hali tete."

Akiongezea Seneto John McCain alisema kuwa "Iraq na Syria zimekuwa nchi ambazo ni hatari na zitakuwa hatari zaidi hapo baadaye katika manufaa ya Wamarekani kama hazitazibitiwa mapema."

Hata hivyo habari kutoka ndani ya kundi hilo la ISIL zimesema kuwa
"wapiganaji wake wengi walikuwa wakipata mafunzo kwa kipindi cha miaka miwili nchi Jordan, ili kuwan
tayari kupambana na serikali ya Syria, lakini waliamua kubadirika toka kwenye mwelekeo huo."

Vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyo endelea nchini Syria na Irak, vimekuwa vikiwapa vicha kuuma viongozi na wataalamu wa maswala ya ulinzi na usalama, kwani kuna baadhi ya raia kutoka nchi za Magharibi  wapo katika makundi hayo ya kivita na inahofiwa huenda raia hao wakaja kuwa tishio pindipo watakapo rudi makwao.

Kundi la Al Qaeda lawa na mbinu mpya za kupitisha mabomu viwanja vya ndege.

London, Uingereza - 03/07/2014. Serikali ya Uingereza imeweka hali ya tahadhari katika viwanja vyake vya ndege, baada ya kutahadharishwa kuwa kuna uwezekano wa mabomu kupita.

Habari kutoka ofisi ya waziri wa usafiri zinasema kuwa "ulinzi umeimarishwa baaada ya serikali ya Marekani kuitaadharisha Uingereza kuwa mabomu ambayo si chuma cha kuonekana kwa mitambo yameaandaliwa kupita katika viwanja vya Uingereza kuelekea Marekani kwa ajili ya mashambulizi."

Hali ya tahadhari katika viwanja vya ndege nchini Uingereza imekuja, baada ya kuaminika kuwa "raia wa Ulaya ndiyo watakao beba mabomu hayo, kwani hawaitaji visa kuingia nchin Marekani."

Kuthibitisha ukweli huo wa kuwepo kwa aina hiyo ya mabomu, maafisa usalama wa Marekani wamesema kuwa "kundi la Al-Qaeda ambalo linamakao nchini Yemen na Syria ndilo linalo husika katika kutengeneza mabomu hayo."

Akizungumzia kutokana na habari hizi, makamu wa waziri mkuu wa Uingereza Nick Clegg ameonya kuwa Uingereza imejiaandaa kikamilifu katika swala la ulinzi, na hasa katika viwanja vyake vyote.

Kufuatia tahadhari hiyo, abiria wameonekana wakisubiri kwa muda zaidi ili kuweza kukaguliwa  katika viwanja vyote vya ndege nchini humo.



No comments: