Wednesday, July 16, 2014

Bashar al Assad aapishwa tena kuwa rais wa Syria.

Bashar al Assad aapishwa tena kuwa rais wa Syria.

Dumascus, Syria - 16/07/2014. Wananchi wa Syria wameshuhudia kuapishwa kwa rais Bashar al Assad rais ili kuwa kiongozi wa nchi hiyo.

Rais Bashar al Assad, amechukua madaraka ya urais kwa mara ya tatu baada ya kushinda uchaguzi wa urais, huku wapinzani wake wa ndani na nje ya nchi wakiwa bado vichwa vinawauma jinsi ya kumtoa madarakani.

Akiongea mara baada ya kuapishwa rais Assad alisema " muda si mrefu, mapinduzi halali yatapatikana, na wale wote ambao wanazani kuwa kutumia nguvu ni dawa, basi wajue kuwa haitapita muda watayaona malipo yao."

Kuapishwa kwa rais Bashar al Assad kuridhuriwa na viongozi wa dini zote  waliopo nchi Syria na wageni wengine  rasmi na baadaye kukagua gwaride la heshima.

Rais Bashar al Assad alishinda uchaguzi kwa kupata kura zenye wingi wa asilimia 89 wakati wauchaguzi mkuu uliyofanyika nchi humo 3/June/2014.

No comments: