Vita ukanda wa Gaza hatari kwa afya ya baaadaye.
Akiongelea hali halisi inayosababishwa na mapigano hayo, muuguzi kutoka Norway Dr Erick Fosse ambaye yupo katika mji wa Gaza amesema " siraha zinazo tumika zinahathari kubwa kwani madini yaliyo tumika kutengenezea siraha hizo huwa yanasababisha ugonjwa wa saratani ( kansa)."
"Na madhara yake yatakuwa ni kwa kizazi kijacho" Aliongezea Dr Fosse.
Mauaji na uharibifu wa mali ambao unazidi kutokea kwa pande zote mbili, huku uongozi wa Izrael ukidai ni kulinda nchi yao dhizi ya ugaidi na huku makundi ya Kipalestina yanayo ongozwa na kundi la Hamas kudai kuwa yanatete haki za Wapalestina zidi ya Waizrael ambao wamechukua adhi yao kinguvu, jambo ambalo hadi sasa jumuiya ya kimataifa imeshindwa kupatia usuruhisho.
Ujerumani ya vunja mwiko kwa kuwa bingwa wa Dunia wa mchezo wa soka.
Rio de Janeiro, Brazil - 14/07/2013. Timu ya taifa ya mpira wa miguu ya ujerumani kwa upande wa wanaume, imetwaa kombe la dunia kwa mara ya kwanza tangu Ujerumani mbili kuungana.
Ushindi huo ulikuja katika dakika 113 ya kipindi cha ziada, baada ya dakika 90 za kawaida kuisha bila kuzaa matunda wakati mchezaji Mario Gotze alipo tuliza mpira kifuani na kwa ustadi baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa mchezaji mwenzake Andre Schurrle na kuupachika kimiani huku kipa wa Argentina, Romero akiwa anaruka kulia na mpira kumpita kushoto.
Ushindi huo wa Ujerumani ndani ya bara la Amerika ya Kusini ni wa kwanza kihistoria tangu kuanzishwa kwa kombe la dunia 1930, kwani haijawai kutokea kwa kombe la dunia kutwaliwa na timu ya bara la Ulaya wakati mwenyeji ni nchi ya Amerika ya Kusini.
Watu wapatao 74,738 waliokuwapo ndani ya uwanja wa Marakana, hii ikiwemo wakuu wa nchi za BRICS ambao wapo nchi Brazili kikazi.
No comments:
Post a Comment