Thursday, July 24, 2014

China ya wekeza nchini Kuba kwa vishindo.

Mkuu wa upelelezi enzi ya rais Muammar Gadaffi akataliwa rufaa yake.

Tripo, Libya - 24/07/2014. Mahakama ya kimataifa inayo shughulikia makosa ya jinai na ukiukwajai wa haki za binadamu imetupilia mbali rufaa ya aliyekuwa mkuu wa maswala ya usalama nchini Libya

Abdullah Senoussi ambaye alikuwa mkuu wa maswala ya usalama wakati wa utawala wa rais Muammar gadaffi , alikata rufaa kwa kutaka kesi yake isikilizwe  nchini Uhollanzi katika mji wa Hague kwani  anahofia kuwa mahakama ya Libya haitakuwa na usawa katika uendeshaji wa kwsi nzima kwa kuzingatia kazi aliyokuwa aliifanya.

Katika uamuzi wake huo, mahakama hiyo imesema kuwa " Libya ipo na uwezo wa kuendesha kesi hiyo  baada ya kumaliza kufanya uchunguzi na kwani kesi hiiyo ilisha anzishwa nchini Libya."

Abdullah Sonoussi alishitakiwa mwaka 2011kwa makosa ya mauaji, utesaji na kuhusika katika kupinga kuangushwa kwa serikali ya Muammar Gadaffi 2011. 

China ya wekeza nchini Kuba kwa vishindo.

Havana, Kuba - 24/07/2014.China na Kuba zimesaini mikataba ya kimaendeleo kati ya nchi hizo, kufuatia ziara ya rais wa Chini nchini humo.

Rais Xi Jinping ambaye hii ni ziara yake ya kwanza, tangu kuwa rais wa Chinaa  alikutana na viongozi wa serikali ya Kuba  na kuzungumzia  ni kwa jinsi gani  nchi hizi mbili zitaendelea kudumisha uhusiano.

Ziara hiyo ya rais wa China kwa nchi  Kuba imefanyika, akiwa katika moja ya mpango wa China kutaka kuimarisha uhusiano wakaribu  na nchi zilizopo katika nchi za Karibiani.

Mikataba iliyo sainiwa kati ya  China na Kuba itahusisha sekta ya kilimo ambapo itaghalimu kiasi cha $115 millioni za Kimarekani na pesa nyingine za Kimarekani $600million zitatumika kwa kununulia madini  ya aina ya chuma ya nikele kutoka Kuba na vile vile kujenga bandari nchi Kuba.

 Mikataba ya China na Kuba imekuja siku chache baada ya rais wa Urusi Vladmir Putin kumaliza kufanya ziara nchini Kuba na kusaini mikataba katika sekta tofauti za kiuchumi.


No comments: