Monday, July 7, 2014

Papa Francis aomba msamaha.

Rais Uhuru Kenyatta kichwa kuuma kwa Raila Odinga  

Nairobi, Kenya - 07/07/2014. Mamia ya watu wameandamana katika jiji la Nairobi, baada ya vyama vya upinzani kuandaa maandamano hayo ili kuishawishi serikali kubadili mwelekeo.

Huku wakiwa wanaimba na kuwa na mabango ambayo yanataka rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kujiudhuru, kwa madai kuwa ameshindwa kuimarisha maisha ya wananchi wa Kenya na pia kuimarisha usalama wao.

Mmoja wa viongozi kutoka kambi ya upinzani na muhusika katika maandalizi ya maandamano hayo Seneta Bonny Khalwale alisema " Leo tuna sema kuwa rais ameshindwa hivyo lazima aondoke madarakanani."

Hata maandamano hayo yalikkwisha salama, na polisni wapatao 15,000 walikuwa katika ulinzi ilikuwa tayari kupambana na watu watakao leta vurugu.

 Hata hivyo kabla ya maandamano hayo, CORD ambacho ni muungano wa vyama pinzani nchini Kenya, wameitaka pia serikali ya Kenya iyaondoe majeshi yake nchini Somali. Baada ya kundi la Al-shabab kuongeza mashambuliz yake tangu majeshi ya Kenya kuingilia kazi vita vinavyo endelea nchini Somalia.

 Naye msemaji wa Raila Odinga ambaye ni mkuuwa vyama vya upinzani amesema kuwa maandamano yaliyofanyika leo ni mwanzo tu, kwani yapo mengi yatafuata.

Raila Odinga ambaye alikuwa waziri mkuu wakati wa serikali ya rais Mwai Kibaki, alirudi hivi karibuni Kenya, baada ya kutokuwepo kwa muda wa nchini Kenya  na kudai anataka kukutana na rais Uhuru Kenyatta ili  wafanye zungumzo yanayo husu usalama wa Kenya.

Papa Francis  aomba msamahaa.

Vatican City, Vatican - 07/07/2014. Mkuu wa kanisa Katoliki dunia amelitaka kanisa kujutia makosa iliyo yafanya na kuwa tayari kujirekebisha.

Papa Francis, aliyasema hayo wakati alipo kutana na watu waliofanyiwa matendo  ya kubakwa kimapenzi na baadhi ya wafanyakazi na wahubiri wa dini hasa kutoka kanisa la Katoliki.

Akisema Papa Francis "Upendo  wa kanisa uliingiliwa na uchafu na sumu ambayo watu ambao walikuwa wanatakiwa kufanya kazi ya kanisa na kuhubiri neno la Mungu wamekuwa wanakwenda kunyume."

"Watu hao walimeli tia sumu kanisa na wanatakiwa watubu."

"Napenda kuomba msaamahaa kwani niaba ya kanisaa, kwani vijana wakiume na wasichana walio  bakwa wakati walikopokuwa na imani na watu wakanisa ili kuwasaidia kiroho na kimahitaji na matokro yake haikuwa hivyo. Hivyo naomba watusamehee."

"Na nahaidi kupambana na wale wote wanao haribu huduma za kanisa kwa jamii."

Papa Francis aliyaongea haya baada ya kukutana na watu waliobakwa na wafanyakazi wa kanisa Katoliki wakati alipo kutana nao mjini Vatican City.