Wednesday, February 25, 2009

Ajari ya ndege yatokea nchini Uhollanzi.

Amani ya Somalia ni mthiani mgumu kwa Jamii ya kimataifa.

Mogadishu, Somalia - 25/02/09.Watu wapatao 48, wameuwawa,huku vita vikendelea katika maeneo ya jiji Somalia kati ya makundi ya kijeshi kwa kushirikiana na jeshi la Muungano la Afrika na kundi kubwa la Al Shabab.
Katika vita hivyo wanajeshi wa muungano wa jeshi la Afrika, pia limewapoteza wanajeshi wake sita ambao wanatokea nchini Burundi.
Kufuatia hali hii, inampa wakati mgumu, rais mpya wa Somalia, Sharif Ahmed, kuweza kuunda serikali ya muungano.
Picha ya hapo juu wanonekana, baadhi ya wanajeshi wa wa muungano wa Afrika, wakiwa katika doria.
Picha ya pili wanonekana baadhi ya wapiganaji wa moja ya kikundi kinacho pinga serikali ya ya Somalia wakiwa katika moja ya maeneo yao,huku wakiwa wamebeba siraha tayari kwa vita pindipo vikitokea.
Ajari ya ndege yatokea nchini Uhollanzi.
Amsterdam,Uhollanzi-2/02/09.Watu wapatao tisa, wamepoteza maisha baada ya ndege ya shirika la Usafiri la Uturuki kuanguka,nchini Uhollanzi karibu na kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Amsterdam.
Katika ajari hiyo, watu wengine wapatao 50, wamajeruhiwa vibaya kati ya abiria 135 walio kuwemo kwenye ndege hiyo.
Ndenge hiyo namba TK1951, iliyo kuwa ikitokea jijini Instambul kuelekea Amsterdam, ilipotea njia ya kutulia na kuanguka na kukatika vipande vitatu.
Hata hivyo, wataalaam wa mambo ya usalama wa ndege wanaendelea na uchunguzi kujua nini chanzo cha ajali hiyo.
Picha hapo juu, inaonekana ndege ya shirika la ndege la Uturuki, ikiwa imeharibika vibaya sehemu za nyuma ya ndege hiyo.
Picha ya pili ineonesha, ndege ikiwa imeanguka karibu na maeneo ya makazi ya wanachini

No comments: