Thursday, February 12, 2009

Hakuna kesi zidi ya rais wa Sudan"Mahakama ya kataa"

Sheyi Emanuel Adebayo, achaguliwa kuwa mchezaji bora wa Afrika kwa msimu wa 2008 - 2009.

Lagos,Nigria-10/02/09.Shirikisho la chama cha mpira la Afrika.,limemchagua mchezaji wa timu ya taifa ya Togo na Arsenal, Sheyi Emanuel Abebayo kuwa mchezaji bora wa bara la Afrika wa ,baadaya kuwashinda kwa kura wachezaji wengini walioshirikishwa katika uchaguzi huo.
Picha hapo juu anaonekana Emanuel Adebayo,akiwa ameshikilia zawadi aliyo pewa baada ya kushinda kuwa mchezaji bora wa Afrika.
Picha ya pili anaonekana Solmon Kalou akiwa ameshikilia zawadi aliyo pewa baada ya kuchaguliwa kuwa mchezai bora mwenye umri mdogo.
Kadima ya shinda uchaguzi nchini Israel "Bi Tzipi Livni huenda akawa waziri mkuu mpya".
Jerusalem,Israel - 12/02/09.Waziri wa mambo yanchi za nje wa Israel, Tzipi Livni,ameshinda uchaguzi mkuu ulio fanyika nchini Israel kwa kuranyingi zaidi kuliko vyama vyote vilivyo shiriki katika uchaguzi huo kwa chama chake kupata viti 28.
Bi, Tzipi Livni ambaye aligombani kupitia chama cha Kadima, aliweza kuwashinda wapinzani wake, hasa mpinzani wake mkuu Benjamini Netanyahu, ambaye aligombani kupitia chama cha Likud.
Hata hivyo kwa mujibu wa katiba ya Israel, itakuwa vigumu kwa Kazima kuongoza nchi kwani ni lazima kishilikiliane na vyama vingine ili kuweza kufikisha idadi kamili ya viti katika bunge ili kuweza kuongoza nchi.
Picha hapo juu anaonekna waziri wa mambo ya nchi za nje Tzipi Livni, akionyesha mikono yake miwili kuonyesha ishara ya ushindi kwa wanachama na wakereketwa wa chama chake cha Kadima.
Picha ya pili, ni ya Benjamini Netanyahu, ambaye chamchake cha Likud,kimekuwa cha pili kwa kimepata viti vingi, hivyo huenda kikashirikishwa kuunda serikali mpya ya Israel.
Moto mkubwa waleta maafa nchini Australia."Wawili wakamatwa"
Sydney,Australia-12/02/09. Polosi nchini Australia wamawakamatwa watu wawili, kwa kushukiwa kuanzisha moto ambao umeleta maafa makubwa na kupoteaz maisha ya watu wapatao 200.
Kwa mujibu wa msemaji wa polisi,Christine Nixon, alisema yakuwa uchunguzi bado unaendelea.
Kufuatia moto huo, serikali ya Australia imetangaza siku moja ya maombelezi kwa maafa yaliyo letwa na moto huo.
Picha hapo juu, anaoneknana polisi akiangalia ni kiasi gani gari lilivyo ungua kutokana na moto ambao umeshutua mamilioni ya wa Australia.
Meli yenye siraha yaachiwa na wateka nyara wa Kisomalia.
Nairobi, Kenya- 12/02/09.Kundi lililo kuwa likishikilia meli ya Ukraine kwa muda wa miezi mitano, wameiachia na sasa ipo mikononi mwa serikali ya Kenya.
Meli hiyo MV Faina, mabayo ilikuwa imebeba zana za kijeshi, iliwasili katika bandali ya Mombasa na wafanyakazi wake wote.
Picha hapo juu, wanaonekna baazi ya watu wakiangali kwa mbali meli iliyo kuwa imetekwa ikiwa imepiga nanga katika bandari ya Mombasa.
Hakukua na kesi zidi ya rais wa Sudan"Mahakama yakataa".
The Hague,Netherland - 11/02/09.Mahakama ya Kimataifa inayoshughulikia kesi za makosa ya jinai iliyopo mjini the Hague, imesema yakuwa hakukua na kibali cha kukamatwa kwa rais wa Sudan, Omar Al Bashir.
Kwa mujibu wa mujibu wa masemaji wa mahakama hiyo iliyopo nchini Netherland,Sonia Robla, alisema hakuna kibali kilichotolewa kwa kukamtwa kwa rais, Omar Al bashir, msemaji huyo,alisema haya alipo kuwa akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.
Picha hapo juu anaonekna rais wa Sudan,akiongea na wandishi wahabari, kuhusu hali halisi ya nchi yake.
Picha ya pili anaonekana raia Omar Al bashir, wa Sudan akiwasili katika moja ya mikoa iliyopo nchini Sudan, ili kukagua maendeleo.
Zimbabwe yapata Waziri Mkuu Mpya.Morgan Tsvangirai awa Waziri Mkuu .
Harare, Zimbabwe - 12/02/09.Waziri mkuu wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai, amaehaidi kurudisha hali ya uchumi na jamii katika hali yake ya kawaida, baada ya kuapishwa kuchukua ofisi kama waziri mkuu mpya wa Zimbabwe.
Waziri Mkuu, Morgani Tsvangirai, ambaye ni kiongozi wa chama cha MDC (Movement of Democratic Change), amekuwa akivutana na rais Robert Mugabe, baada ya uchaguzi mkuu ulio fanyika mapema mwaka 2008.
Picha hapo juu anaonekana, kiongozi wa MDC, Morgan Tsvangirai, akiapishwa kuwa waziri mkuu, na rais wa Zimbabwe,rais Robert Mugabe 11/02/09.
Picha ya chini wanaonekana,kutoka kushoto ni rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, kati ni Morgan Tsvangirai na aliyekuwa rais wa Afrika ya Kusini Thabo Mbeki,wakipeana mikono mara baada ya kumaliza kukubaliana kutia sahii mkataba wa kuongoza serikali pamoja.

No comments: